Nimegombana na Mke wangu leo mpaka nimeshangaa

Nimegombana na Mke wangu leo mpaka nimeshangaa

Habar wana JF,

Nashukuru mungu wote ni wazima
Mtanisamehe mimi sio muandishi mzuri sana wakuu.

Nimetoka kugombana na wife mpaka nimebaki nashangaa na kuwaza kwa maneno alioyasema wife, nikwamba wife ni mjamzito wa miezi 4 sasa anatimiza ikifika tarehe 13 sasa leo nimetoka kazini nikawa nimekaa kwenye gari nawaza sana kutokana na maisha na life style anayoishi wife sio kabsa kiupande mwingine.

Kutokana na maisha yalivyo toka wife amebeba mimba anaishi life style ambayo kwa upande mwingine bado haijanivutia lakin ni kawaida sana yeye ni 24hrs/7days yupo ndani amelala akichoka anafungua insta atashinda mitandaoni akichoka sebleni kuangalia TV tamthilia zake mwenyewe.

Ni vizuri kupata muda wa kupumzika kwa hali yake lakini mimba sio mzigo au mimba sio ugonjwa ukufanye ushinde ndani 24hrs. Nikampigia sim kumjulia hali kashindaje leo then nikamuuliza unafanya nini akajibu yupo kitandani amelala.

Nikamwambia kiupole sana na kiutaarabu kuwa mkewangu em bas uwe unatoka na kuchakarika kuna duka la biashara now yupo kijana uwe hata unakwenda basi kuangalia mambo yanaendaje sio hadi mimi nitoke kazini nimechoka nipitie tena huko wakati wewe upo tu nyumbani umetulia vituvingine ni kuichangamsha akili na kupambana kuliko kushinda tu ndani mamaangu wewe sio mgonjwa.

Kusema kwamba huwez kutembea mbona kuna wanawake wana mimba lakini wanachakalika wengine unakutana nao anatumbo kubwa kabeba beseni lake la mboga anatembeza mitaani wengine wanakimbiza maofisi na matumbo yao tena makubwa lakin wanachakalika asubuh na mapema kashafika ofisi nikamwambia hayo siyo maisha uyaotaka kuishi.

Sijajua nihilo tu au kuna mengine ila Alivimba na kuanza kuongea kwa hasira na kuongea maneno mengi sana ambayo sikutegemea na kusema kuwa namnyanyasa mara kisa kubeba mimba naanza kumuona mjinga so nisimfananishe na hao wajinga ye anaakili zake na anajua anachofanya, mara nimeanza kumuona mzigo kwangu kwakuwa kabeba mimba duuh wakuu nilibaki nimeishiwa nguvu maana sikutegemea kama ndo yangekuwa hayo mara sasa ataondoka ataenda kukaa kwao duuh.

Kiukweli sikumjibu chochote nikaamua kutumia hekima tu maana yeye teali alishapanda kaamua kushuka nakumuacha nikakata simu yangu nikawaza sana huyu skuiz amekuaje kwamba ndo mimba inampeleka hivyo au nikaacha kama yalivyo lakin narud nyumbani njiani ninawaza sana yale maneno Nikafika home nikaingia ndani nikamkuta kakaa sebleni, sikumsemesha chochote nikapitiliza jikoni nikamkuta beki 3 anapika nikamuuliza kuwa dadaako kala akasema ndio alikula na saivi ndio napika chakula cha usiku nikasema powa nikapitiliza chumbani nikaingia bafuni nikaoga nikamaliza nikapanda kitandani nikapumzika.

Dakika 3 akaja chumbani kimya sikumsemesha kakaa nikamwambia jiandae kesho nakupa nauli yakuendea huko kwenu iliuepuke hayo manyanyaso unayosema.

Nikainuka nikavaa nikafungua mlango kabla sijatoka nikamwambia natoka napiga simu kwenu kesho wakupokee nikaondoka zangu now nipo somewhere nimetulia kwanza ila kweli nimewaza huyu kesho namsafirisha kweli sioutani acha aende kwanza kwao akatulie akikaribia kujifungua nitamfata wakuu kwasababu najitahdi sana anapopanda namimi nisipande maana minajijua nina hasira sana.
Mkuu mwanamke mjamzito mchukulie kama mtoto tu yaan ukiwa nae serious kiasi hicho kwa kila kitu anachofanya basi utatia fora mtaani[emoji16][emoji16][emoji16].Yaan hapo ianbid uwe mpole na mbunifu laasivyo utamuona msumbufu,mvivu,mlalamishi na asiyetosheka.Machemical imbalance kunako mwili wake[emoji4][emoji4][emoji4]
 
Mwanamke akiwa na mimba anakuwa kama kichaa flani.
Sio wote na hii sio kawaida. Ninae dada angu yuko kwenye ndoa enzi na enzi. Akaniambia katu usije ukatumia mimba kama fimbo kwa mwenza wako. Hizi drama watoto wa saiv mnazoziletaga hazifai. Tena mkome.

Mimba ni kiumbe cha Mungu. Na Mungu ni mpenda amani. Kamuumba alieko tumboni, kamuumba aliemuweka humo, kakuumba na wewe uliembeba. Iweje kiumbe cha Mungu kikakufanya uwe na visingizio na drama za kipepo namna hiyo. Kwann umtese mwanaume anaehangaika kukulea, kukulisha kuhakikisha unaishi ukiwa salama bila shida. Tena mara nyingi wanawake wakiwa na ujauzito mwanaume anaongeza sana mapenzi maana anajua mtoto wake yuko njiani.

Sasa wewe ndo utake kuitumia kama fimbo. Hizi drama za sijui nataka hiki nataka kile sitaki hiki ni kwa watu wenye pesa. Kimwanafunzi kiko kijijini na kimepewa mimba kina nguvu ya kuchagua? Mihogo twende, magimbi twende, chochote kinapanda. Sitaki kujiapiza mengi lakin kila mara nataman nitembee kwenye ushauri wake. Mimba isiwe chanzo cha kumtesa mtoto wa mtu maana hata yeye kazaliwa na mwanamke kama mimi. Mimba inatakiwa imtukuze Mungu vilevile maana sisi sote ni mali yake. Upendo, umoja, heshima, upole juu yangu na vijacho wangu. Amen.
 
Ushauri huu natoa bure sitaki hata mia yako. Rudi home, tulia, muombe msamaha kabisa!

Kesho wahi kutoka job, Rudi home mchukue nendeni Dukani, mpitishe kwenye ice cream ama pahala penye miti mingi, ama maji, aone ukuu wa Mungu na ajue mimba siyo ugonjwa.

Mkeo ana upweke sana ni vile hujajua tu, suala la ww kwenda job kurudi siyo issue kwa kipindi hiki

Kesho kutwa yake mpeleke akafanyiwe massage nzuri kabisa, atengeneze kucha, nywele ukiwepo, nasisitiza ukiwepo!

taratibu kabisa utashangaa na roho yako, utarudi kushukuru.

Umpeleke kwao ndo wamemtia mimba? em tuliza akili mwanaume
Dah umetisha Mkuu very positive [emoji122][emoji122][emoji122][emoji120]
 
Habar wana JF,

Nashukuru mungu wote ni wazima
Mtanisamehe mimi sio muandishi mzuri sana wakuu.

Nimetoka kugombana na wife mpaka nimebaki nashangaa na kuwaza kwa maneno alioyasema wife, nikwamba wife ni mjamzito wa miezi 4 sasa anatimiza ikifika tarehe 13 sasa leo nimetoka kazini nikawa nimekaa kwenye gari nawaza sana kutokana na maisha na life style anayoishi wife sio kabsa kiupande mwingine.

Kutokana na maisha yalivyo toka wife amebeba mimba anaishi life style ambayo kwa upande mwingine bado haijanivutia lakin ni kawaida sana yeye ni 24hrs/7days yupo ndani amelala akichoka anafungua insta atashinda mitandaoni akichoka sebleni kuangalia TV tamthilia zake mwenyewe.

Ni vizuri kupata muda wa kupumzika kwa hali yake lakini mimba sio mzigo au mimba sio ugonjwa ukufanye ushinde ndani 24hrs. Nikampigia sim kumjulia hali kashindaje leo then nikamuuliza unafanya nini akajibu yupo kitandani amelala.

Nikamwambia kiupole sana na kiutaarabu kuwa mkewangu em bas uwe unatoka na kuchakarika kuna duka la biashara now yupo kijana uwe hata unakwenda basi kuangalia mambo yanaendaje sio hadi mimi nitoke kazini nimechoka nipitie tena huko wakati wewe upo tu nyumbani umetulia vituvingine ni kuichangamsha akili na kupambana kuliko kushinda tu ndani mamaangu wewe sio mgonjwa.

Kusema kwamba huwez kutembea mbona kuna wanawake wana mimba lakini wanachakalika wengine unakutana nao anatumbo kubwa kabeba beseni lake la mboga anatembeza mitaani wengine wanakimbiza maofisi na matumbo yao tena makubwa lakin wanachakalika asubuh na mapema kashafika ofisi nikamwambia hayo siyo maisha uyaotaka kuishi.

Sijajua nihilo tu au kuna mengine ila Alivimba na kuanza kuongea kwa hasira na kuongea maneno mengi sana ambayo sikutegemea na kusema kuwa namnyanyasa mara kisa kubeba mimba naanza kumuona mjinga so nisimfananishe na hao wajinga ye anaakili zake na anajua anachofanya, mara nimeanza kumuona mzigo kwangu kwakuwa kabeba mimba duuh wakuu nilibaki nimeishiwa nguvu maana sikutegemea kama ndo yangekuwa hayo mara sasa ataondoka ataenda kukaa kwao duuh.

Kiukweli sikumjibu chochote nikaamua kutumia hekima tu maana yeye teali alishapanda kaamua kushuka nakumuacha nikakata simu yangu nikawaza sana huyu skuiz amekuaje kwamba ndo mimba inampeleka hivyo au nikaacha kama yalivyo lakin narud nyumbani njiani ninawaza sana yale maneno Nikafika home nikaingia ndani nikamkuta kakaa sebleni, sikumsemesha chochote nikapitiliza jikoni nikamkuta beki 3 anapika nikamuuliza kuwa dadaako kala akasema ndio alikula na saivi ndio napika chakula cha usiku nikasema powa nikapitiliza chumbani nikaingia bafuni nikaoga nikamaliza nikapanda kitandani nikapumzika.

Dakika 3 akaja chumbani kimya sikumsemesha kakaa nikamwambia jiandae kesho nakupa nauli yakuendea huko kwenu iliuepuke hayo manyanyaso unayosema.

Nikainuka nikavaa nikafungua mlango kabla sijatoka nikamwambia natoka napiga simu kwenu kesho wakupokee nikaondoka zangu now nipo somewhere nimetulia kwanza ila kweli nimewaza huyu kesho namsafirisha kweli sioutani acha aende kwanza kwao akatulie akikaribia kujifungua nitamfata wakuu kwasababu najitahdi sana anapopanda namimi nisipande maana minajijua nina hasira sana.
Tatizo lenu, elimu,pesa na vyeo lakini bado mnashindwa kiowa wanawake wa kuwafaeni, ilibidi muowe huyo beki tatu
 
How mkuu maana mimi sijamlinganisha na mtu nimeongeanae tu kwa wema

Unalinganisha mimba ya mkeo na Za watu wengine

Nimebeba mimba mbili Hakuna hata moja iliyofanana na nyingine

Mimba ya kwanza nilikua nabadilisha tu sehemu za kulala
Nahama kitandani nahamia sofani
Nahamia mkekani, mpaka Giza linaingia
Nikisema hata niende kwenye biashara nalala
Nilishapitishwa mpaka mbagala tokea buguruni nimelala zangu kwenye daladala

Ila ya mwisho nilikua napiga Kazi mpaka mwisho kabisa lakini matukio yangu mzee alihama nyumba

Hivyo sikushauri ulinganishe mimba ya mkeo na za watu wengine

Ongeeni tu wenyewe na Kama hawezi mvumilie Kwani miezi Tisa ni mingi?
 
Kosa lako lilianzia hapa.

Hujawahi kufuatilia mambo ambayo mwanaume hapaswi kumuuliza mwanamke.

Hilo swali hukupaswa kumuuliza kwa njia ya simu umeharibu dogo, kosa lingine ni wewe kuzozana na mjamzito.
Nadhani umri wako bado mdogo ktk ndoa.

Nikushauri tu "ahirisha kumpeleka kwao badala yake mtake radhi, jishushe kabisa" utakuja kunishukuru

Kumbuka hasira huzaa hasara.

Inawezekana pia

Mi nakumbuka ilikua nikianza kuwasha moto anasema tu basi mama baadae na simu amekata [emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kama hakuwa na tabia hio kabla ya ujauzito kuwa mpole Acha hasira,
Cheza na mudi yake weka uanaume pembeni, Ili asimstress mtoto tumboni. Mvumilie akishusha kama sio tabia yake ataacha tu
Kwa kweli uko sahihi. Kila mwanamke hormones zake zina'react' kivyake kwa hivyo lazima awe mstahmilivu. Akishajifungua hali itarudi kama kawaida.
 
Kuna mdada alikuwa mwl.kafundisha Leo kesho yake akaenda kujifungua,alivyopata mimba nyingine miezi 2 tu hawezi chochote,akitembea kidogo miguu yote inavimba Hadi huruma

Ni mimi kabisa Yaani mwili unagoma kabisa kabisa
Plus craving ya Vitu ambavyo nikiwa normal haunilishi hata kwa fimbo[emoji30]

I hate being pregnant sema tu baba chanja ashanisoma anaelewa anasolve kiutu uzima


Mwenye anauza iPhone 14 akuje inbox nimfungie zawadi ya Valentines mtoto wa mama mkwe
 
Ila wanawake wengine wanapitia magumu jamani, Ukiachana na kosa alilofanya la kukupandishia sauti, kwanini umemwambia utamrudisha kwako? Hii kurudishwa kwao ni adhabu au maonyo au ni aina nyingine ya unyanyasaji?

Kwao ni kubaya au ni porini?

Mi niliaga kwenda kwetu nikipata likizo sikujibiwa mtu kajifanya hajanisikia kabisa!

Sijui ni kwa nini
Yaani utasikia utarudi kwenu na mabag yako[emoji30]

Wanawake tutafute hela
 
Mpeleke kwao bodaboda wakamchakate huko, sikuhizi wanawapenda sana wanawake wenye mimba
 
Habar wana JF,

Nashukuru mungu wote ni wazima
Mtanisamehe mimi sio muandishi mzuri sana wakuu.

Nimetoka kugombana na wife mpaka nimebaki nashangaa na kuwaza kwa maneno alioyasema wife, nikwamba wife ni mjamzito wa miezi 4 sasa anatimiza ikifika tarehe 13 sasa leo nimetoka kazini nikawa nimekaa kwenye gari nawaza sana kutokana na maisha na life style anayoishi wife sio kabsa kiupande mwingine.

Kutokana na maisha yalivyo toka wife amebeba mimba anaishi life style ambayo kwa upande mwingine bado haijanivutia lakin ni kawaida sana yeye ni 24hrs/7days yupo ndani amelala akichoka anafungua insta atashinda mitandaoni akichoka sebleni kuangalia TV tamthilia zake mwenyewe.

Ni vizuri kupata muda wa kupumzika kwa hali yake lakini mimba sio mzigo au mimba sio ugonjwa ukufanye ushinde ndani 24hrs. Nikampigia sim kumjulia hali kashindaje leo then nikamuuliza unafanya nini akajibu yupo kitandani amelala.

Nikamwambia kiupole sana na kiutaarabu kuwa mkewangu em bas uwe unatoka na kuchakarika kuna duka la biashara now yupo kijana uwe hata unakwenda basi kuangalia mambo yanaendaje sio hadi mimi nitoke kazini nimechoka nipitie tena huko wakati wewe upo tu nyumbani umetulia vituvingine ni kuichangamsha akili na kupambana kuliko kushinda tu ndani mamaangu wewe sio mgonjwa.

Kusema kwamba huwez kutembea mbona kuna wanawake wana mimba lakini wanachakalika wengine unakutana nao anatumbo kubwa kabeba beseni lake la mboga anatembeza mitaani wengine wanakimbiza maofisi na matumbo yao tena makubwa lakin wanachakalika asubuh na mapema kashafika ofisi nikamwambia hayo siyo maisha uyaotaka kuishi.

Sijajua nihilo tu au kuna mengine ila Alivimba na kuanza kuongea kwa hasira na kuongea maneno mengi sana ambayo sikutegemea na kusema kuwa namnyanyasa mara kisa kubeba mimba naanza kumuona mjinga so nisimfananishe na hao wajinga ye anaakili zake na anajua anachofanya, mara nimeanza kumuona mzigo kwangu kwakuwa kabeba mimba duuh wakuu nilibaki nimeishiwa nguvu maana sikutegemea kama ndo yangekuwa hayo mara sasa ataondoka ataenda kukaa kwao duuh.

Kiukweli sikumjibu chochote nikaamua kutumia hekima tu maana yeye teali alishapanda kaamua kushuka nakumuacha nikakata simu yangu nikawaza sana huyu skuiz amekuaje kwamba ndo mimba inampeleka hivyo au nikaacha kama yalivyo lakin narud nyumbani njiani ninawaza sana yale maneno Nikafika home nikaingia ndani nikamkuta kakaa sebleni, sikumsemesha chochote nikapitiliza jikoni nikamkuta beki 3 anapika nikamuuliza kuwa dadaako kala akasema ndio alikula na saivi ndio napika chakula cha usiku nikasema powa nikapitiliza chumbani nikaingia bafuni nikaoga nikamaliza nikapanda kitandani nikapumzika.

Dakika 3 akaja chumbani kimya sikumsemesha kakaa nikamwambia jiandae kesho nakupa nauli yakuendea huko kwenu iliuepuke hayo manyanyaso unayosema.

Nikainuka nikavaa nikafungua mlango kabla sijatoka nikamwambia natoka napiga simu kwenu kesho wakupokee nikaondoka zangu now nipo somewhere nimetulia kwanza ila kweli nimewaza huyu kesho namsafirisha kweli sioutani acha aende kwanza kwao akatulie akikaribia kujifungua nitamfata wakuu kwasababu najitahdi sana anapopanda namimi nisipande maana minajijua nina hasira sana.
Nenda naye taratibu ndio mimba ya Kwanza lazima adeke na uvumilivu ndio unatakiwa kwenye ndoa mkuu, nenda naye taratibu huna haja ya kumpeleka kwao.
 
2:Mimba ya kwanza
3:ndio nafahamu mkuu
4: kwani nikosa kuongea na mkewangu tena kwa upendo lakin nalo kosa?
Kwa nini hukuwa na subira?
Ungesubiri urudi nyumbani uongee naye kuliko kupiga simu,ni muhimu kuwa mwanaume.
Ulivyorudi nyumbani kwa nini ukumsemesha?ila ukawa umepanic?
Jitathmini sana,uanaume si lelemama
 
siku ya kujifungua aanze tena kulalamika, mpe nauli aende akapambane na mama ake mbona atafanya tu mazoezi.
 
Wanaume acheni story za kijiweni kua mimba sio ugonjwa niliwahi beba mimba mapigo ya moyo yanaenda kasi balaa miguu na mikono haina nguvu hata kidogo wee asee mimi mjamzito hata aniambie kitu gani naamini, msiwe wajuaji kwa vitu msivyo vijua, lakini nilibeba mimba nyingine nilikua normal kabisa nilipiga kazi mpaka nikawa najishangaa yaani. Mimba hii na ile hutofautiana jamani au huyu na yule.
 
Umekosea namna ulivyomwambia lazima apanick Yani apo amekusikia kama unamwambia we ni mvivu sana wenzio wote wachapa kazi
 
Back
Top Bottom