Nimegundua Bahati Ina mchango mkubwa kwenye Maisha yetu

Nimegundua Bahati Ina mchango mkubwa kwenye Maisha yetu

Basi nikaanza kusoma kwa shauku na furaha bashasha kweli nikidhani dogo katoboa kawa taita, kumbe hadi leo bado anajitafuta. Sad.

Atapata tu asikate tamaa.

Nimekulia katika mazingira fulani tough sana hivyo huwa nafurahi sana nikiona mtu katoboa hata kwa kubet, hata kama simfahamu.
 
Mwambie huyo dogo akae mkao wa kutoa na sio kupokea awe giver na sio taker .

Bahati huwa inaambatana na kujitoa kwa wengine.

Mfano wewe hapo unapomsaidia unakuwa unajisogeza na kupokea mambo mazuri Bahati.
Hivi hii inaaply kwa wanyama? Maana ukimtazama ng'ombe asipokamuliwa basi atalima ila mwisho wake ni kisu njoo kwa nyau sasa sijui paka.
 
Huelew nini? Sasa ukiona mtu anabahat jua tayar nyota ipo vzr.
hapana jinsi ya kutumia nyota yako na nini kinataka kupitia nyota yako.kwa leo nimechoka sana nitakuja kukueleza kuhusu hii elimu ndio maana wengine mnabaki kusema yule jamaa ana kismart au ngekewa wakati ufahamu kuhusu nyota na bahati yako
 
Ni kweli watu wa nyuma wanapaswa kupewa heshima yao, wao pia waliishi kwa muda wao, mkate wao na pumzi yao kwa idadi iliyo pangwa na Mungu wao
Sio watu tu pia kuna matukio yalipaswa yatokee nyuma ili kuandaa matokeo yako ya sasa ,unapoishi wewe kwa sasa ni matokea na maamuzi yaliyofanya nyuma mpaka ukawepo apo sasa, yangeweza pia kufanyika maamuzi apo pawe barabara ,ungekuta hauishi apo sasa , pia ilibidi vizazi vya kale vife ili wewe uweze kupata nafasi ya kuishi apo .
 
Ngoja nirejee maandiko yasemavyo kuhusiana na hili

MHUBIRI 9:11

Nikarudi, na kuona chini ya jua, ya kwamba si wenye mbio washindao katika michezo, wala si walio hodari washindao vitani, wala si wenye hekima wapatao chakula, wala si watu wa ufahamu wapatao mali, wala wenye ustadi wapatao upendeleo; lakini wakati na bahati huwapata wote.
Hapa umeupiga mwingi....ubarikiwe
 
Nataka mmoja humu aseme bahati anapanga Mungu aliye juu...

Uone uzi unavyobadilika hapa
mungu hapangi bahati bali kakupa vyote ila kwa vile ujui kuvitumia kupitia jicho la tatu
imagesdddd.jpg

images.png
 
Hizi mambo zina ukweli. Kuna jamaa kila nikimuona naumia sana. Mbunifu, ana akili sana na sio mchoyo wa maarifa. Cha ajabu kilekile anachofanya yeye hafanikiwi naona anapiga tu mark time na maisha, ila kwa mbinu hizohizo akiwapa wengine wanatoboa. Inatafakarisha!
 
Sio watu tu pia kuna matukio yalipaswa yatokee nyuma ili kuandaa matokeo yako ya sasa ,unapoishi wewe kwa sasa ni matokea na maamuzi yaliyofanya nyuma mpaka ukawepo apo sasa, yangeweza pia kufanyika maamuzi apo pawe barabara ,ungekuta hauishi apo sasa , pia ilibidi vizazi vya kale vife ili wewe uweze kupata nafasi ya kuishi apo .
Ni kweli kabisa mkuu, hiyo inathibitisha kwamba maisha yetu hayajatokea kwa bahati, bali ni matokeo ya muunganiko wa matukio mengi yaliyo pita.
 
Nataka mmoja humu aseme bahati anapanga Mungu aliye juu...

Uone uzi unavyobadilika hapa
Mungu anatoa riziki
Hutoa riziki kwa wakati autakaye yeye

Mungu ana rehema mbili hapa duniani humgawia anaye mtii na asiye mtii hapa duniani

Swala la kusema mtu yule ana bahati au mtu huyu Hana ni Ukosefu Wa subra
Tujikite kwenye kusubiri

Hakika mwenye kusubiri yupo karibu na mungu!
coockie monster
 
Back
Top Bottom