Nimehitimisha kwamba watu wasioamini uchawi upo hayajawakuta, na yakiwakuta huteseka bila kupona mpaka kifo

Uchawi ni kutumia uwezo usio wa kibinadamu ama nguvu za giza (supernatural power) katika kuathiri na kubadili matukio, kuwatawala watu, kuteka, kuvuruga na kuhilibu (manipulate), kusumbua, kutisha, kutesa, kudhuru, kuangamiza, au kuua.
 
Ukisoma vizuri hii article yako paragraph ya pili unakili uchawi upo hapo unapo sema" ili ufanye kazi lazima wewe uane rogwa ukubali" ajabu bado una bishi uchawi haupo
Kitu ambacho huwezi kukithibitisha huwezi kusema kipo uchawi ni imani kama vile uislam na nikisema uchawi upo namaanisha upo kiimani lakini hauna nguvu kama wengi wanavyofikiri
 
Mm sifanyi shirki nyinyi mnaesema kuna uchawi ndio wachawi wenywe
Wewe umejuaje kama kuna uchawi kama sio mchawi
Basi sawa. Sema tu kwakuwa name calling kwa issue fulani fulani hairuhusiwi humu, la sivyo ningekutajia jina la Mheshimiwa ambaye aliwahi kuwa DC wa Magu, Mwanza (alikuja kuwa mtu mkubwa nchini, na sasa ni Msaafu) ili ukasikie ushuhuda wake kuhusiana na jambo unalobishia hapa.

Jamaa alikuwa haamini haya mambo na akawa anawaambia wale Wasukuma wa Magu kuwa hawana la kumfanya. Iko siku aliamka amelala kwenye uwanja wa Sabasaba, akiwa na familia yake hawajitambui. Alihama fasta na kama sikosei hakiendelea na u-DC kokote nchini tena.
 
Ivi mazungaombwe ni uchawi
 
😁😁😁😂 mara kadhaa nimeshafikiria kubadili hii ID yangu, na mapema sana nitafanya hivyo.
Itakuwa vyema sana; una hoja zenye mashiko, sasa tukigeukia ujinani tunaulizana kulikoni. Anyways, tuko pamoja kulijenga taifa zuri la Tanzania & ufalme wa nuru.
 
Watu wengi hawajui jinsi Mungu anavyowalinda kila sekunde; wengine badala ya kumshukuru Mungu wao wanamkufuru.
 
Tupe iyo elimu
 
Kitu ambacho huwezi kukithibitisha huwezi kusema kipo uchawi ni imani kama vile uislam na nikisema uchawi upo namaanisha upo kiimani lakini hauna nguvu kama wengi wanavyofikiri
Haha! nmegundua naweza kua nahangaika na mtoto wa shule kwahio Uislamu haupo?
 
Sidhani kama umewahi kugundua kwamba mkuu wa giza anaweza kujipatia lolote analohitaji kutoka kwako kama ikiruhusiwa afanye hivyo!? Kimsingi, hakuna unaloweza kufanya ama unakoweza kwenda, ukajificha au ukakwepa usiathiriwe kwa hila zake endapo tayari "umejitune" ukawa accessible kwenye frequency & anga za kuzimu. It works like magic because it is real magic -- ndiyo maana inaitwa ushirikina (superstition).
 
Bullshit
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…