Nimehudhuria mkutano wa ukanda kuhusu mkataba wa EPA, Tanzania tumeonesha njia

Nimehudhuria mkutano wa ukanda kuhusu mkataba wa EPA, Tanzania tumeonesha njia

Anna Mghwira,

Ni kweli kwa hili namuunga mkono Magufuli japo sikubaliani na mambo yake mengi. Sasa kwenye hili inabidi atumie nguvu hiyohiyo kuhakikisha anapitia mikataba mingine nchi iliyoingia huko nyuma ili kuona kama ina faida kwa nchi au ilisainiwa na 10%.

Kwa mara ya kwanza nimeona nchi yetu ikisimama kidete dhidi ya mikataba inayotengenezwa ulaya huku ikivalishwa vazi la nia njema.

Sasa tuhakikishe tunapinga mikataba hii lakini tuhakikishe tunajitahidi kujikwamua na hali hii ya kutegemea bidhaa toka nje kwani ninavyojua kuna uwezekano wa nchi hizi za Ulaya kuanza kutupa wakati mgumu.

Ni kweli mkuu lakini kuna siasa ambayo ndiyo fimbo kuu sikuhizi kwa kisingizio cha democracy wanayotumia mabeberu wa dunia; haihitaji haraka kuna mambo ya msingi yanafanyika kwanza kabla ya kufikia huko.

Ukiiona Zim aliko comrade mwenzetu si kuwa hakuwa anajitambua kuna kamba wanazotumia wenzetu kukuvuta mpaka wanakufikisha kwenye corner ambayo utakuwa laughing stock na ndipo hutumia crafted democracy kukuondoa...tupo imara na kunasehemu tunaelekea ambapo dunia itatambua hata nchi za weusi ziliwekwa kwenye dunia hii na Mungu ambaye hugawa vipawa bila upendeleo...nimesema na narudia tena hii yetu bado haijaonekana duniani na wakubwa wanaulizana ilikuaje hata wakafanikiwa mpaka sasa?
 
EPA ni Mkataba mmoja. Mibovu mingine nayo iekwe. Hata hivyo EPA mkataba ndio ulikuwa unakwenda kuwekwa sahihi, haujakamilika bado. Naona tunachanganya mada. Huu mkataba ndio ungesainiwa kwa mara ya kwanza.
Maana yangu ni kwamba Tanzania tupo vizuri kwenye mambo ya mikataba kuliko nchi zingine za Afrika Mashariki hadi tuwe viongozi wa kuongoza mkataba huo? Maana kuwa kiongozi unajua/unaweza kuliko wenzako.
 
maana yangu ni kwamba Tanzania tupo vizuri kwenye mambo ya mikataba kuliko nchi zingine za Afrika Mashariki hadi tuwe viongozi wa kuongoza mkataba huo? Maana kuwa kiongozi unajua/unaweza kuliko wenzako.
Wapiga dili akina Lowasa toka waondoke serikalini mikataba mibovu imepungua sana...Lowasa alitutia hasara sana kwenye mkataba wa RICHMOND.
 
Mwaka 2014 Jumuiya ya Afrika Mashariki ilisaini makubaliano na European Union, wataalamu wa uchumi wa nchi hii hawakutoka na kueleza nini faida au hata kama kuna hasara katika makubaliano hayo.
Hapa ndipo elimu zetu na vyeti vinapopoteza maana, maana anavyoongea mtaalam wa uchumi na biashara na anavyoongea mtu asiye na weredi kwenye maeno haya ni kama sawa tu, wote wanabuni?
Niliwahi kumuuliza afisa mmoja wa serikali anaelewa nini kuhusu EPA? Hakuwa na majibu zaidi ya kutoa hisia zake na mambo aliyoyasikia kwenye magazeti.
Sasa kama maafisa kama hawa ndio wanamshauri rais katika mambo ya kiuchumi bado tuna safari ndefu.
Nisiingie kwenye maamuzi yaliyofanyika hivi karibuni lakini embu tujiulize maswali machache

1. Unaweza kuepuka kufanya biashara na European Union?
2. Wangapi wetu tumesoma makubaliano ya awali kati EAC na EU yaliyofanyika miaka miwili iliyopita? soma hapa http://trade.ec.europa.eu/doclib/docs/2015/october/tradoc_153845.compressed.pdf

3. Bidhaa/ biashara kutoka East African Community kwenda nchi za Umoja wa Ulaya ni kahawa, maua, chai, kahawa, samaki na mbogamboga - Hii ni exports, je nchi yetu ni shindani katika kuzalisha mazao hayo ukilinganisha na nchi nyingine za Africa Mashariki?

4. Bidhaa kutoka EU kuja EAC ni mashine na mitambo, vifaa vya viwandani na ujenzi, magari na vifaa vya tiba na madawa - Je kwenye njozi yetu ya kuwa na uchumi wa viwanda hatuhitaji EPA? Au tutatumia zana za mawe?

Note: Kilimo kinachangia asilimia 24.5 ya GDP
Viwanda na ujenzi asilimia 22.2
Haya ni maeneo ambayo wataalamu wa uchumi wa serikali hii wangeweka focus yao hapo, na kupima kama EPA itakuwa na faida kwa upande wetu.

Nimetimiza wajibu wangu wa kuchangia kwa mustakabali mwema kwa taifa letu.
Wachache sana watakuelewa mkuu, hii nchi tumechagua ujinga kuwa sehemu ya maisha yetu. No wonder tuliowatuma hawakufanya hata huu utafiti kidogo. Sisi tunatakiwa kujijenga na kufanya vizuri sana kwenye potential zetu hasa kilimo, madini na rasilimali za asili kama gesi na mafuta yakija. Kamwe hatutakuja kushindana na Ulaya kutengeneza magari sana sana walete matawi ya viwanda vyao. Wasomi wetu hawajui hata vitu vidogo kabisa
 
Wachache sana watakuelewa mkuu, hii nchi tumechagua ujinga kuwa sehemu ya maisha yetu. No wonder tuliowatuma hawakufanya hata huu utafiti kidogo. Sisi tunatakiwa kujijenga na kufanya vizuri sana kwenye potential zetu hasa kilimo, madini na rasilimali za asili kama gesi na mafuta yakija. Kamwe hatutakuja kushindana na Ulaya kutengeneza magari sana sana walete matawi ya viwanda vyao. Wasomi wetu hawajui hata vitu vidogo kabisa

Upo sahihi sana mkuu, kwenye biashara za kimataifa nchi huwa hazishandani kuzalisha kila kitu bali unazalisha kile ambacho kitakufanya uwe na ''competitive advantage''.
Bado ukizalisha unahitaji mahali pa kwenda kuuza hizo bidhaa.
 
Anna Mghwira,

..mkataba wa EPA umekuwa negotiated kwa miaka zaidi ya 10.

..mkataba huo ulishakuwa tayari toka mwaka 2014 na EAC ikapewa muda mpaka mwaka huu kusaini mkataba huo.

..sasa wewe ulikuwa MGOMBEA URAISI kwa hiyo suala hili lazima ulipaswa kulifahamu. Kama unafuatilia kampeni za Uraisi za Marekani wagombea wote wanajadili na wana uelewa wa masuala ya trade agreements.

..vilevile wewe ni MWENYEKITI WA CHAMA na chama chenu kina sera zinazohusiana na masuala kama haya.

..sasa naomba kujua msimamo wako, na wa chama chako kuhusu suala hili.

..JE UNGECHAGULIWA KUWA RAISI WETU UNGESAINI MKATABA HUU? AU UNGEUKATAA?

Eric Cartman , chige, @Nguruvi3,MsemajiUkweli ,Geza Ulole
Ni vema kufanya hivyo lakini ifike mahala tubadilishe sheria zetu zinazo ongoza michakato ya mikataba yetu ili mikataba hiyo inakuwa wazi na Wananchi wanapewa furusa ya kuijadili ili waweze kunufaika nayo.
Jokakuu: hata sisi kupewa fursa kujua ni sehemu ya kutatua tatizo. Kwa vyovyote ikiwa majadiliano yalikamilika tangu 2014 hakukuwa na sababu ya kuanza kupima tena. Lakini kama wengine hawakujua na sasa wanataka kujua, pengine hii ni nusu shari, na ni bora kuchukua maamuzi baada ya kujua kuliko bila uhakika. Hii ni changamoto kwa uendeshaji nchi kwa usiri.
 
Wewe Joka unauliza
Anna Mghwira,

..mkataba wa EPA umekuwa negotiated kwa miaka zaidi ya 10.

..mkataba huo ulishakuwa tayari toka mwaka 2014 na EAC ikapewa muda mpaka mwaka huu kusaini mkataba huo.

..sasa wewe ulikuwa MGOMBEA URAISI kwa hiyo suala hili lazima ulipaswa kulifahamu. Kama unafuatilia kampeni za Uraisi za Marekani wagombea wote wanajadili na wana uelewa wa masuala ya trade agreements.

..vilevile wewe ni MWENYEKITI WA CHAMA na chama chenu kina sera zinazohusiana na masuala kama haya.

..sasa naomba kujua msimamo wako, na wa chama chako kuhusu suala hili.

..JE UNGECHAGULIWA KUWA RAISI WETU UNGESAINI MKATABA HUU? AU UNGEUKATAA?

Eric Cartman , chige, @Nguruvi3,MsemajiUkweli ,Geza Ulole
swali la kampeni. Mambo ya ingekuwa mimi ilikuwa mwaka jana. Sasa yupo mtu tunapima kulingana na maelekezo yake. Tunaweza kukataa ama kuridhia bila kuingiza kampeni...
 
Mkuu you nailed it...hata huko EU ni mbali kwa vigin land tulionayo inatosha Kabisa kututajirisha kwa kulisha majirani Zetu tu...tatizo hapa ni kutawaliwa na watawala wale wale wenye mawazo na akili zile zile kwa miaka hamsini..

Wananchi wa Kenya nao wanalalamika kuwa watakachouza EU sana sana ni maua na maua yenyewe wanaolima 85% ni kampuni za kigeni..
Kibiashara inaweza kuonekana tunachelewa, lakini pengine bora kuchelewa kiusahihi kuliko kubahatisha
 
Hang'over ya uchaguzi bado inawaathiri wengi ndio maana hawataki kuyaangalia mambo kiuhalisia,kama yalivyo na kutafakari kwa uamuzi sahihi...ni kama watu wanataka serikali ifanye uamuzi wa hovyo bila kupima ili wapata cha kuzungumza...bila kujua kuwa waathirika ni wananchim wote.Uendeshaji wa serikali una changamoto kubwa sana.
Wewe Joka unauliza

swali la kampeni. Mambo ya ingekuwa mimi ilikuwa mwaka jana. Sasa yupo mtu tunapima kulingana na maelekezo yake. Tunaweza kukataa ama kuridhia bila kuingiza kampeni...
 
Zungu Pule: Soma vizuri post yangu utajua sikusema nimehudhuria mkutano wa wakuu wa nchi..wanachama...hilo ukijibiwa hutahitaji kuuliza mengine
 
Sioni kama tuna la kujisifu katika hili. Kama kwa miaka yote tangu kulipoanzishwa mazungumzo ya mkataba wa EPA tumeshindwa kujua kama kuna faida au hakuna faida, tutaweza kutambua hilo kwa hii miezi michache kati ya sasa na mwakani? Inaonekana sisi hatujua tunataka nini au hatutaki nini.
 
Zungu Pule: Somavizuri post yangu utajua sikusema nimehudhuria mkutano wa wakuu wa nchi..wanachama...hilo ukijibiwa hutahitaji kuuliza mengine

Nadhani kama Taifa tuna tatizo kubwa la kufanya maamuzi. Hata biblia husema ni hatari mwanadamu unapokuwa si moto si baridi. Watanzania hatueleweki, tunashindwa kufanya maamuzi. Kwa karibia miaka 10 kumekuwa na mazungumzo ya mkataba wa EPA, mpaka leo hatujui kama una faida au hauna faida. Nilidhani kwa sasa ilitakiwa tuwe na nafasi ya kusema kuwa mkataba huu au una faida ili usainiwe, au hauna faida, na hivyo tutamke kuwa hatutasaini. Kutokuusaini nako bado inaonekana ni kioja maana mkataba huo haukuletwa bali ulikuwa ukijadiliwa na wawakilishi toka pande zote mbili EU na EAC.

Kama mkataba huo ulikuwa unaandaliwa na pande mbili kwa majadiliano, kama kuna mambo yanayohitaji marekebisho, nina imani kulikuwa na nafasi ya kuyajadili. Kama tunaona ulikuwa hauna maana kwa nini tulipoteza muda huo wote kwa kitu ambacho tunajua hakina faida kwa watu wetu? Kwani tulilazimishwa?
 
Pongezi gani anastahili ? Kama hauna vya kuuza kwenye nchi za watu utauza nini ? Kilimo kimekufa,viwanda vya kuchakata malighafi stadi hauna,una maneno tu vya kuuza hauna!
Nani katufikisha hapa!
 
Nakubaliana nawe hili suala la viwanda sio la kukamilika overnight lakini huu mkataba naona utakuza tu viwanda vya huko ulaya kwa kuwawezesha kuleta bidhaa zao huku with tax exemption, sisi hatuwezi kushindana nao kamwe, tutaishia lada kuuza raw materials halafu wataziprocess kwao na ikiwezekana kuzirejesha huku kama finished products kwa faida maradufu.

Kwa hali hiyo hamna kiwanda hapa nchini kitakachoweza kufunguliwa na kuzalisha bidhaa itakayoshindana na hizo zinazotoka Ulaya tutaishia kuwa dependent on importing goods kutoka nje wakati Rais kwa maono yake anataka sisi tuweze kujihudumia kwa bidhaa zinazozalishwa na viwanda vyetu wenyewe mpaka kufikia hatua ya ku-export kwa wengine.

Hayo ni mawazo yangu japo mimi sija-specialize kwenye maswala ya uchumi wenye ujuzi zaidi wanaweza kunirekebisha au kukubaliana nami.
Mpaka sasa tunazaidi ya 50yrs Tangu tupate UHURU bado tunasema hatuwezi kushindana hebu niambie unadhani kama Taifa ..tupate muda gani ndio tuweze
 
Asante sana Mama Anna Mghwira,
  • Je ni faida zipi wao wameainisha kuwa tutapata kama Taifa, na kama Kanda ya EA
  • Je, kwakitendo cha mataifa mawili kusaini na mengine kukata kunatuweka katika nafasi gani kama nchi kwa upande mmoja na kama Jumuiya kwa upande mwingine
  • Ni mambo gani kama taifa tungependekeza yawepo kwenye mkataba ili kuridhia kuusaini
 
Asante sana Mama Anna Mghwira,
  • Je ni faida zipi wao wameainisha kuwa tutapata kama Taifa, na kama Kanda ya EA
  • Je, kwakitendo cha mataifa mawili kusaini na mengine kukata kunatuweka katika nafasi gani kama nchi kwa upande mmoja na kama Jumuiya kwa upande mwingine
  • Ni mambo gani kama taifa tungependekeza yawepo kwenye mkataba ili kuridhia kuusaini
Asante sana Mama Anna Mghwira,
  • Je ni faida zipi wao wameainisha kuwa tutapata kama Taifa, na kama Kanda ya EA
  • Je, kwakitendo cha mataifa mawili kusaini na mengine kukata kunatuweka katika nafasi gani kama nchi kwa upande mmoja na kama Jumuiya kwa upande mwingine
  • Ni mambo gani kama taifa tungependekeza yawepo kwenye mkataba ili kuridhia kuusaini
Haya ni baadhi ya mambo ya kuainisha, kufafanuliwa na wataalam wa uchumi na wa biashara z kimataifa. Asante.
 
Back
Top Bottom