Nimeibiwa simu na mwizi ametoa pesa tiGO Pesa!

Nimeibiwa simu na mwizi ametoa pesa tiGO Pesa!

Hata mm hiyo imenitokea niliibiwa simu kwenda kurudisha line nakuta pesa hakuna hata Mia kwenda tigo naambiwa mwizi aliomba PIN reset wakampa 0000 akabadili number akatoa pesa sina hamu na tigo
Kwamba mtu yoyote anaweza omba na akapewa, ni hatari.
 
Hata mm hiyo imenitokea niliibiwa simu kwenda kurudisha line nakuta pesa hakuna hata Mia kwenda tigo naambiwa mwizi aliomba PIN reset wakampa 0000 akabadili number akatoa pesa sina hamu na tigo
Kwa hili Tigo watawajibika. Ndiyo kampuni ya kwanza nimekuwa nayo kabla zingine hazijaanza. Haiwezekani pesa zangu zipotee hivi hivi. They are custodians. Siyo niende ofisini wananiambia nikaripoti polisi.
 
Ni rahisi sana kujua nida namba kama namba yako kaijua, mfano naenda kwa wanaosajili lain nawaambia nataka kusajili laini lakin nida namba nmepoteza, msajil atasema unakumbuka namba yeyote ambayo umeisajili kwa nida yako, mm najbu ndio! halaf nataja namba ambayo nimeiba, msajil akiingiza tu hyo namba nida namba zako zote zpo uchi had hapo zoez linalofata had kuiba hela kwenye tgopesa akaunt n kama kumsukuma mlevi tu.
 
Shukrani kwa mchango wako. Wacha nirudi kwenye traditional banking tu. Nimepata hasara but Tigo nust compensate . SIwezi kuwaacha hivihivi.
Ni kampuni ya wahuni sana yaan hata wakala aliyetoa hiyo pesa wanamjua ila hawatakupa ushirikiano hata kumjua tu wakala maana kumjua wakala na wapi alipo na pesa ilipotelewa sometime unaweza kupata clue Fulani pa kuanzia
 
Ukinunua line mpya inakuwa na pin, mara nyingi tunatoa hiyo pin, madhara yake ni mtu akiokota au akiiba simu yako ni rahisi kuingia moja kwa moja.
Kwa nini hakuna security ya kutosha ambayo hata brutforce haiwezi kufanya cracking ya password. I am very disappointed
 
Ni kampuni ya wahuni sana yaan hata wakala aliyetoa hiyo pesa wanamjua ila hawatakupa ushirikiano hata kumjua tu wakala maana kumjua wakala na wapi alipo na pesa ilipotelewa sometime unaweza kupata clue Fulani pa kuanzia
I swear kwa hili watawajibika. We can not trust a company with no security standards.
 
Ni mtu alishakuchungulia ukifanya miamala labda kwenye daladala, akaidaka namba yako ya siri. Akatafuta namna ya kukuibia simu. Unashauriwa uwe unabadili namba yako ya siri mara kwa mara. Kama sivyo tigo wanawajibika.
 
Hata nchi yetu hiyo sheria wameweka. Mitandao kama TTCL na Voda wanajitahidi kuifuata lakini Tigo wao ndo ma-nunda.

Nilipotezaga ki simu na laini zote tatu. Kilichotokea nilirenew laini ya TigO bila shida yoyote kwa wakala tu. Laini ya voDa na TTcl ilinibidi kwenda kwenye 'shop' zao. Ya voda nikafanikiwa hapo lakini ya ttcl ikaongezeka kipengele cha kuwa hadi na loss report.

Wakati ule niliwamaindi kwa mtiririko wa ttcl then voda then wa mwisho hao tigo...... lakini kumbe kiusalama linaanza baba lao ttcl halafu voda then wa mwisho ndio hao tigo😅.
Huu ni ushuhuda binafsi.
Bado hujajua kijana...kwamba TTCL upande wa security ni kubwa kuliko voda..??!! Utakua unatañia
 
Ni mtu alishakuchungulia ukifanya miamala labda kwenye daladala, akaidaka namba yako ya siri. Akatafuta namna ya kukuibia simu. Unashauriwa uwe unabadili namba yako ya siri mara kwa mara. Kama sivyo tigo wanawajibika.
Sikufanya muamala wowote kwenye daladala
 
Back
Top Bottom