Nimeishi Moshi, Bukoba, Lushoto aisee watanzania tuna ukarimu sana tofauti na tunavyoshambuliana kwa tofauti zetu

Maendeleo Yana chama.
Katibu wenu mwenyewe amekiri nchi imeharibiwa.
Imeharibiwa wakati viongozi wote ni wenu.
Licha ya hivyo bado maendeleo yatawagusa wote wenye vyama na wasio na vyama.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kusini ipi?mana kusini nimeishi na nawajua vizuri..hawa wa kusema unaenda kununua kwa mtu wa kaskazini kwani atakuzika ukifa.?kuna maeneo machache ambayo hayana ubaguzi wa kikanda kwa kusini kama masasi au mtwara mjini ila kwengine kote ni ubaguzi..hadi maofisi.

#MaendeleoHayanaChama
 
Una uhakika shida ni bukoba au hata mentality yako na jaribu kuangalia hicho kitu hakifanywi na watu wengine kuna watu ni wepesi kuhukumu utafikiri wao hawana dhambi
 
Nimesoma na jamaa wa chuga si fichi ni wabaguzi mno mbaya walikuwa wachache mpaka wakawa wanagombana na watu wa dar makundi daily maisha ya boarding bhana
Wachaga na watu wa wa arusha huwa wanapenda kujitenga na wengine same to muslims..hasa vyuoni na mashuleni..sijui ndivyo wanavyofundishwa huko manyumbani kwao.

Tabia za ajabu sana.

#MaendeleoHayanaChama
 
Kabisa mkuu. Kuna jamaa yangu yuko katavi alikuwa anaishi dar akapata kazi wakamrusha huko. Anakwambia katu harudi dar now mwaka wa pili keshanunua eneo anataka anza kujenga.
Ukabila upo ila sio kiasi hicho.
Correct, ukabila upo kidogo sana. Watu ambao hawajasafiri wanaona Dar ndio kila kitu, wanasahau kwamba kila mkoa una fursa zake. Katavi kuna fursa sana za mazao na uvuvi
 
Nayaona hata Mimi,Kuna fremu za duka kwa mwaka wanapangishwa watu watatu anafugua biashara inamshinda anafunga anarudisha fremu anapanga mwengine ,lakini pembeni unakuta Kuna duka la mangi halifi miaka yote
 
Bakini na ukabila wenu kuwahukumu hata ambao hawajawai kuwakosea kisa kabila ila msisahau siku ya mauti kila nafsi itahukumiwa kutokana na mzigo wake wa dhambi.

Tusisahau hakuna aliveyekua na option ya kuchagua kabila
You are right
 
Kuhusu wairaque ni uongo sijawahi kuona kitu kama hicho
 
Nimekaa wilaya ya Handen kama mwaka,ilifika mahali wazee wakaniambia tafuta binti hapa kijijin tukuozeshe ila sikuwa tayari kuoa
 
mi nimefanya na wachaga ni wabaguzi kiasi fulani haswa mtu hawezi kumtakia mwenzie hbd mpaka aandike mara chugaboy mara chaga boy mtu alifunga tu kuna mechi wanampost eti wanyumbani
πŸ˜€ πŸ˜€ πŸ˜€
Wabaguzi wa kufa yani
 
Watu wa Dar sio kwamba Wana roho mbaya ila maisha ni magumu. Wengi wao wanapambania chakula bado hata ukimuambia unaenda kwake lazima akupige chenga
Mikoani chakula si kitu Cha kumuumiza mtu kichwa kabisa
 
Ha ha ha nimecheka kwa sauti lakini mbona hata wa mikoa huwa wanakuja hivyo hivyo na pumbuh zao tuuuu?
Hakuna kitu kama hicho utoke mkoani usiwabebe hata maharage huyo labda alikuwa mdaslam alienda akakaa kidogo akarudi ndio huwa wanarudi mikono mitupu


Ila watu wa mikoani ni wakarimu sana hawana aiba ya uchoyo kama hapa dar mtu anakubebea mazagazaga kama yote anakuja kwenye mambo yake unamuuliza ataondoka lini ? Mbona tukienda mkoani hawatuulizi hayo maswali ?


Ktk sehem zote Tanzania dar sijui kuna shida gani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…