Nimekuta SMS hizi kwenye simu ya zamani ya Mume wangu, sijazielewa naombeni mnisaidie mlioko kwenye Ndoa

Nimekuta SMS hizi kwenye simu ya zamani ya Mume wangu, sijazielewa naombeni mnisaidie mlioko kwenye Ndoa

Habari,

Mimi na mwenzangu tumeishi miaka kama 13 kwenye ndoa yetu na tumebarikiwa na kuwa na watoto 2. Niseme ukweli hatujawahi kukorofishaba au kugombana tunapendana sana.

Sasa wiki mbili zilizopota kuna picha moja nilipigaga na mume wangu na watoto. Niliikumbuka nikamuuliza mume wangu kuhusu picha akaniambia ipo kwenye simu yake ya zamani ambayo ni mbovu kwa kiasi kikubwa.

Aliniambia nikaichukue na nilipoichukua akanipa password ili nichukue picha, kwa vile simu mbovu niliiangaika nikafanikiwa kuzichukua zile picha. Ila siunajua mume nikaamua kupekua kidogo simu nikaenda upande wa sms za kawaida sikukuta lolote baya ila nikakuta anatumiana sms na mtu mmoja anonekana ni mwanaume mwenzie kamsave jina la Doctor.

Kwa sms zile inaonekana alikuwa ni mwanaume nilishidwa kuscreenshoot coz simu ilikuwa mbovu hata kuandika pembeni nilishidwa coz mume alikuwepo palepale na mimi, na wameanzia mbali nafikili kuna zingine amefuta za juu, naamini zile alisahau kuzifuta, Ila ninakumbuka zilikuwa hivi.

Doctor: Kuwa na amani furahia ndoa yako, maana unaonekana wasiwasi ulikuwa nao mkubwa sana, naamini Sasa utakuwa na furaha na kumuamini mke wako.

Mume wangu: Asante sana hofu ilikuwa ni kubwa sana maana hii ishu nilifikisha mpaka kwa baba na baba akanishauri hivyo nilijaribu kufuata utaratibu wa kiserikali ila ulikuwa ni mgumu , na sikutaka nimshirikishe mke wangu. Kwa majibu haya nina amani sasa na furaha. Asante sana kwa ninisaidia.

Doctor: Ni changamoto za ndoa kijana hayo mambo yapo kwa wanaume wenzio wanayakuta hayo pole sana be strong now.

Mume wangu: Asante maana mimi sijawahi hata kucheat hata siku moja, sasa ningepata tofauti sijui ingekuwaje daaa. Maana nilienda mpaka kenya kupata jibu sahihi.

Doctor: Pole sana kwa vile ushajua basi kuwa Safi.

Mume wangu: Asante sana maana hata Baba nimemwambia kasema kama majibu yapo vizuri basi hakuna haja tena na kuwa na wasiwasi na mke wako.

Zipo nyingine sms zinaendea ila hizi zimenitia wasiwasi. Nimefikiria sana alifanya nini mume wangu, nimewauliza watu wengi kwenye magroup yetu ya wanawake na magroup ya ndoa. Wengi wanasema tuu achana nayo kwa vile ushaona kuwa hakuna shida yoyote na mume wako hajawakukucheat so usiwe na wasiwasi.

Ila mimi nahitaji kujua ni nini hicho mpaka kwenda Kenya?

Naombeni mnisaidie.
Kuna mtoto au watoto alikuwa anaona kabisa kapigwa kaibiwa sijajua kwa muonekano wa watoto au tabia zao au tabia zako akamshirikisha baba yake na DNA akapima na watoto kakuta ni wake sasa usichoelewa hapo ni nini.
 
Punguza umalaya

Pengine mumeo anasiri kubwakwako na hujui na ilipelekea akampime mtoto DAN

Lakini wewe umeona hilo tayari unaaza kutusumbua hapa
 
Hapo inaonekana alikuwa na wasi wasi na mtoto au watoto wenu inawezekana kuna mtu alimwambia umalaya unayofanya na kuwa mtoto si wako , jamaa ikabidi akafanye vipimo vya DNA Kenya ili kujua ukweli, Kwa mujibu wa sms vipimo vitakiwa vimesoma vizuri.
 
Hapo inaonekana alikuwa na wasi wasi na mtoto au watoto wenu inawezekana kuna mtu alimwambia umalaya unayofanya na kuwa mtoto si wako , jamaa ikabidi akafanye vipimo vya DNA Kenya ili kujua ukweli, Kwa mujibu wa sms vipimo vitakiwa vimesoma vizuri.
Bila shaka beki za huyu mwanamke hazikabi ndio maana jamaa hamuamini
 
Back
Top Bottom