Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,931
- 24,816
- Thread starter
-
- #101
Mkuu we acha mimi kuna mtu yuko hapa kwangu na mwanae mwezi wa tatu ninavumilia mengi, mtoto anaelekea miaka saba akiamua anajikojolea, ikifka muda wa kula eti anaanza kulia, anaweza amgomee kwenda kulala hata saa sita usku.
Yani kuna muda uvumilivu unataka kunishinda. Mwanangu uwa anataka kuiga, namtia kerebu
🤣🤣🤣🤣🤣🤣👏👏👏👏👏👏Naona ndugu wamekuwekea sanctions ila WaTz tupo nyuma yako
Ni kweli na wanaiga ujinga zaidiAtakuharibia mwanao. Watoto wana tabia ya kuigana.
kitoto = mtoto
chake = wake
kina = ana
alikileta = alimleta
kije = aje
shida imeanzia hapo kwa jinsi ulivyomuelezea huyo mtoto wa miaka 6.
Na wewe ukiandika andika uonavyo sahihi kwako. Hicho kitoto kilikuwa kinalelewa kwa mazingira ambayo yangekifanya kikikua kiwe nacho hakielewi matumizi ya lugha.kitoto = mtoto
chake = wake
kina = ana
alikileta = alimleta
kije = aje
shida imeanzia hapo kwa jinsi ulivyomuelezea huyo mtoto wa miaka 6.
Hawaelewi hawa watu. Sababu wamekariri.... Hawakuelewa lugha na matumizi yake.Nafikiri kaandika kulingana na sifa za mtoto alivyo.
Hajakosea.
Anajaribu kuelezea hadhira yake kuwa Mtoto alipitiliza kitabia mbaya
Natumia udogolesho, kukadharau n.k
Kwa mtoto unatakiwa umagufuli 70 na ukikwete 30, Ukitumia ukikwete totally mtoto anakunyea mikononiHuyu ni aina ya kina "junya"(junior)
wana taabu sana
Hawaelewi hawa watu. Sababu wamekariri.... Hawakuelewa lugha na matumizi yake.
🤣🤣🤣 mtoto wa kaka angu anaitwa junior, kwa kweli alivyokuwa mdogo ilikuwa balaa ila kwasasa amekuwa ametulia amekuwa mtoto mzuri sanaHujawahi kuona kitoto kinaitwa junior wewe
Nakuunga mkono, mbwa za aina sitaki hiyo hata zikanyage kwangu, na-mind sana. Nina bahati mbaya kwamba kwangu kumekuwa kama kambi ya wakimbiziHuyu mdogo wangu wa kike wa mwisho ana kitoto chake kina miaka 6. Weekend hii alikileta kije msalimia uncle. Mi sikuona shida kabisa. Wazo lilikuwa jema.
Shida ikawa kwenye utekelezaji. Kile ki uncle kina kera balaa... Kinakera mpaka mwisho. Kimefika home ndani ya muda mfupi kimeshaingia vyumba vyote, kimechafua kwenye friji na kimeshavunja jug la juice.
Mi niliweka pause tu kwanza kuvumilia nikiomba Mungu asaidie wageni waondoke haraka. Kikaanza kulilia remote kiangalie tamthiliya za A**m. Mimi nilishapiga marufuku pale home. Nikakikatalia ...kikaanza kulia. Mama yake anakimbembeleza....
Hakitaki kikamrushia remote usoni. Hapo nilitaka kunyanyuka....malaika akanizuia. Mama yake akawa tu anasema "Jamaani... Amran na hasira kama baba yake....yaani huyu mtoto" huku anajichekesha akifikicha fikicha jicho.
Nikainuka nikaichukua remote nikaijaribu nikaona inafanya kazi. Nikashusha pumzi kumshukuru Mungu maana nilijua pale hali ya hewa ingechafuka.
Kakawa kana mghasi sana mwanangu....uzalendo ulinishinda kalipomwambia "mshenzi weeee" hapo nilijikuta nimeamka nikakamata na kukapeleka uani. Nikavunja ua langu zuri maskini nipate fimbo. Nilikatandika sana... Heeehhh .... Si kanalia kananambia ... "Toka hapa...." Nikaona haka kametumwa kunitafutia kesi na Serikali au ustawi wa jamii....
Nikakacharaza viboko miguuni, mamaa yake akaja ...na kudai inatosha nitamuumiza mwanaye si vizuri kumchapa mtoto, inatakiwa kukaa naye kuongea naye.
Nilimwambia hilo la kukaa naye kuongea naye akafanyie huko kwao. Hapa kwa uncle katulie hasa. Mama yake ali mind. Eti....mtoto anapaswa apewe muda wa kucheza atakavyo. Nilimwambia akacheze huko ila asichezee vitu vyangu na sitaki kabisa uharibifu.
Akasema: "Kaka ndo maana wengi hatupendi kuja kwako ...mkoloni sana na hupendi watoto" alinikwaza....yaani yeye kukilea kitoto chake vile kama kimbwa koko anaona ndo mapenzi. Kitoto kina sugu, vidonda na kimekuwa cheusi, kimekauka kama kinakula cement eti ndo anakipenda nikasema wacha iwe hivyo.
Kimekaa kaa kidogo kwa utulivu kikajisahau tena ...kikajikojolea.... Mtoto wa miaka 6 anajikojoleaje? Mimi wangu ameanza kukojoa mwenyewe akiwa na miaka 2 huyu sita anakojolea carpet?
Mama yake anasema ndo alivyo yaani ...ukichelewa tu kumvua nguo anajikojolea hapendi kukaa na mkojo. NIlimwita mtoto wangu nikamwambia niitie dada. Dada alipokuja nikamwambia kanichumie fimbo.
Sister akaamua akachukue katoto kake akakapeleka kwenye gari kukaepusha na dhahama. Wakaamua kuondoka. Nikasema na iwe hivyo...alaaaah yaani kafanye ujinga nikaogope sababu ya mama yake.....sister kawaambia wadogo zangu wengine kuwa nime mnyanyasa mtoto wake. Ndugu wananisema....mama akapata taarifa.
Akanipigia simu kuwa nimefanya swadakta kile kitoto kinalelewa hovyo. Mama yake anakikiss mpaka ulimi.....anasema ndo mapenzi kwa mtoto. Mama anasema hataki hata kikamtembelee kilimtia hasara nyingi ikiwepo kudumbukiza simu yake majini.
Nimejisemea tu wacha na iwe. Asiyefunzwa na mamaye sisi tutamfunza tu ...
Sawa sawa baba junior!Madikiteta ni weng sana na itachukua mda sana kuisha acha mfumo dume wa kijinga huo
Kla mtu anautaratibu wake wa kulea mtoto wake sasa usitake kla mtu alee mtoto km unavyolea wakwako ww unayoona ni tabia nzuri kwako kwa mingne ni mbaya cha msingi jaribu kueshimu utaratbu wa kla mtu na familia yake
Mwisho wa sku mtatengenezeana mabifu na machuki baina ya ndugu kisa watoto na inavyoonyesha ww sio yan ktk maongezi yako tu unaonesha umentamani kumpiga uyo mtt mda mrefu sana ni chance tu ndo ulikua ujapata
Hoja nzuri tunaingoja.Nakuja na hoja kuwa hivi bora single mother au bibi na babu katika malezi.
Yaani. huyu ni mwenyewe kabisa.Sawa sawa baba junior!
Ujumbe bora kabisa huu tena wa mwaka kwa sisi wahenga...[emoji16]MAKOSA 30 AMBAYO WATOTO WA ZAMANI WALIKUWA WAKILA BAKORA!!
WATOTO WA ZAMANI TULIISHI MAJUMBANI KAMA TUKO MAFUNZO YA JESHI!! UKIKUA NI FULL ADABU KUHESHIMU WATU, UTU, BUSARA NA KUJITETEGEMEA UKIWA NA UMRI MDOGO TU
1: Usiposalimia wakubwa asubuhi unapigwa
2: Usiposalimia wageni unapigwa
3: Ukinawa kabla ya wageni unapigwa
4: Ukilia bila sababu unapigwa
5: Ukinyanyuka wakati wa kula kabla ya wakubwa kuinuka unapigwa
6: Wakubwa wakiwa wamekaa wewe ukaenda kusimana pembeni unapigwa
7: Ukikaa wakubwa wamesimama unapigwa
8: Ukitumwa dukani ukachelewa kurudi unapigwa
9: Ukichelewa kurudi toka shuleni unapigwa
10. Ukiwahi kurudi shuleni unapigwa
11: Ukililia wageni wakati wanaondoka , wakitoka unapigwa
12: Kujipitisha pitisha wageni wakiwa wanakula unapigwa
13: Kujibu ovyo wakubwa unapigwa
14: Kutukana watu wazima, watoto au rika lako unapigwa
15: Ukiwa mbishi bila sababu unapigwa
16: Ukipigwa ukalia unapigwa ili unyamaze
17: Ukipigwa umenyamaza unapigwa ili ulie
18: Ukipigwa shuleni ukaenda kusema nyumbani, unapigwa
19: Ukianza kula nyama kabla ya wakubwa unapigwa
20: Ukila kwa jirani ukabainika unapigwa
21: Ukianza kunawisha wenyeji badala ya wageni mkimaliza kula unaitwa chumbani unapigwa
22: Ukianza kunawisha watoto badala ya wakubwa unapigwa
23. Ukikutana na mtu mzima ana mzigo hujampokea unapigwa
24. Ukienda kusema kama umepigwa unapigwa.
25. Mtu mzima akipita kama mnacheza hamjamshughulikia unapigwa.
26. Ukienda nyumba za watu, ukaona kitu au ukasikia story ukaileta nyumbani unapigwa
27. Ukipewa hela na mtu asiefahamika au hata anaejulikana inategemea mazingira gani unapigwa
28. Ukianza kuchagua chakula hiki nakula hiki sili unapigwa
29. Ukianza kuwa na marafiki wasioleweka makwao unapigwa
30. Mtu mkubwa akija kukuchongea nyumbani hata kama sio cha ukweli unapigwa.
YAANI YALE MAISHA! Acha kabisa.
...... Wahenga, hapo vipi???......[emoji16][emoji16][emoji16][emoji16]
Madikiteta ni weng sana na itachukua mda sana kuisha acha mfumo dume wa kijinga huo
Kla mtu anautaratibu wake wa kulea mtoto wake sasa usitake kla mtu alee mtoto km unavyolea wakwako ww unayoona ni tabia nzuri kwako kwa mingne ni mbaya cha msingi jaribu kueshimu utaratbu wa kla mtu na familia yake
Mwisho wa sku mtatengenezeana mabifu na machuki baina ya ndugu kisa watoto na inavyoonyesha ww sio yan ktk maongezi yako tu unaonesha umentamani kumpiga uyo mtt mda mrefu sana ni chance tu ndo ulikua ujapaata