Nimempiga mwizi mapanga mawili ya kichwa, akifa Mungu nisamehe

Nimempiga mwizi mapanga mawili ya kichwa, akifa Mungu nisamehe

Hahaahaa Mzee baba Kitoabu Kama nakuona vile,hapo ulicheza Kama pere dadeq bora umeliwahi maana majitu ya Moçambique nasikia yana roho ya chuma lingekutoa roho na hiyo nondo yake Bora umetumia mbinu za Afande Chacha mura piga risasi rikikwepa rusha panga!

Wasaalam hapo Cabo de galdo mkuu!

Dadeq!
Mkuu, hawa jamaa hata kukaba kistaarabu hawajui.
Unaweza sikia wamemuua mtu kisa kisimu cha tochi tu.
 
Serikali ikifanya uchunguzi itagundulika tu ww ndie umemuua (Kama akifa)na sababu ulimtoa nje kwenda kumtupa hapo ndipo ulipofanya kosa kubwa litakalokupeleka kingi
Maisha tu, na maisha ni kama maji, usipo ya oga uta yanywa.
 
Oyah, poa ndugu zangu, wacha nivae nguo za uchizi nielekee maporini nikatafute madola ili siku moja tuje tuishi wote hapo bongo.
Naipenda Tanzania yangu, ila kwa sasa nimejikojolea (sina pesa) niki kutana nazo lazima nirudi tuje kuungana kudai Katiba mpya na kuomba kutolewa kodi za tozo.
Pamoja wadau.
 
Oyah, poa ndugu zangu, wacha nivae nguo za uchizi nielekee maporini nikatafute madola ili siku moja tuje tuishi wote hapo bongo.
Naipenda Tanzania yangu, ila kwa sasa nimejikojolea (sina pesa) niki kutana nazo lazima nirudi tuje kuungana kudai Katiba mpya na kuomba kutolewa kodi za tozo.
Pamoja wadau.
Nimependa spirit yako ya kuwaaga wabongo wenzio kama hivi kabla ya kwenda kujilipua, Mungu akuongoze mpambanaji

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna mtu alifanya uhalifu akajakamatwa kupitia kitabu alichoandika yeye mwenyewe...

Maandishi haya!
 
Mungu anajua sijawahi liua jitu hata siku moja lakini ikitokea lile jamaa likafa shauri yake na familia yake.

Mwaka jana nimeibiwa mara mbili nikahama mtaa.

Wiki iliyopita nimemkosa kidogo tu, ashukuru niliamka usingizini nikiwa na pombe kichwani na kupelekea kupiga kelele akasepa zake. Leo sasa kajikanyaga, asipokufa basi majeraha ya kichwa atayauguza mpaka tutakapo kutana motoni, jinga sana.

Ilikuwa hivi, nimerudi zangu mihangaikoni mida ya jioni kama saa kumi na moja.

Kwa uchovu wa kazi niliokuwa nao (kuchimba jamani sio sawa na kutia sign kwenye makaratasi) nikaamua kuoga na kujipumzisha kidogo, kutokana na uchovu, usingizi ukanipitia na kujikuta nimeamka mida ya tano usiku.

Kwakuwa mida ilishakuwa imeenda na watu walishalala nikaamua wacha itoke tu mpaka kesho.

Lakini kila nilipojaribu tena kulala usingizi ulikuwa haupatikani, nikaamua kutoa simu yangu, cha kwanza nikampigia mke wangu kujua hali zao yeye na watoto, nilipomaliza mazungumzo nikaingia mjengoni (JF) kupata kujua kinachoendelea duniani.

Kipindi naendelea na charting zangu, mara nasikia mtu kama anapushi mlango, nilitulia kidogo, eeh sindio naona kitasa kinavunjwa, hapo nikaifunika simu chini fasta ili asiuone mwanga wa simu, nikainuka na panga langu nikatulia pembezoni na mlango, kwamba akifungua mlango awe amenificha na ule mlango.

Kama aliingia ndani ya akili yangu, jamaa kafosi mpaka akafanikiwa, alivyoingia ndani (mkononi ana nondo) yeye akawa mbele mimi niko nyuma yake na ndani kiza hakuniona.

Mungu anisamehe, nikapeleka la kwanza, sikutaka kungoja fasta nikapeleka la pili mchizi chini kwenye sakafu, alipiga kelele moja tu ya mamaa khinakwa (kwa kimakua maana yake mama nakufa).

Nahisi nje kulikuwa na mwenzie akimpigia saiti mila, maana nilisikia vishindo vya mtu akikimbia.

Nilichofanya niliokota nondo yake na kuishika mkoni, mara jirani yangu tunaekaa chumba jirani akaamka na kuja chumbani kwangu, nikawasha taa, jamaa kafloti analia kwa sauti ya mbali.

Mpangaji mwenzangu nae ni mchimbaji kama mimi, tukashauriana tumbebe tukamtupe nje. Tukalibeba msobe msobe mpaka nje jirani na mitaa hii, tukalitupia huko.

Uzuri wa maeneo haya (mgodini) kila mtu anaangalia lake, hakuna hata alietoka nje, kushabikia.

Hapa nimemaliza kufuta damu chumbani kwangu, na sidhani leo kama nitalala.

Maduka kama yangekuwa hayajafungwa ilibidi nipate kikali (pombe kali) ili kutoa mawenge kichwani.

Akipona safi, akifa shauri yake.
Dah....dadadeki....panga lenyewe hujui kulitumia...kwa taarifa tu ulikuwa mchubuko mdogo tu....nimeosha na mafuta ya taa....Niko vizuri tu....bahati yako uliniotea kutokea nyuma....nitarudi anytime....jiandae 😠
 
Ukamkata (kumbuka hapo ni gizani)akaanguka akadosha nondo alokuwa kashika mkononi na ukaiokota)(bado mpo gizani tuu hapo)alafu ukakata tena panga la pili.....
Ngoja niingie gym kwanza nitarudi badae
 
Umetenda dhambi. Unatakiwa utubu kwa Mungu wako usiku wa saa9.
 
Back
Top Bottom