Nimemsikiliza Godbless Lema katika The Big Ajenda Star TV, yupo vizuri kichwani kuwazidi wapinzani wote hapa Tanzania

DR HAYA LAND

JF-Expert Member
Joined
Dec 26, 2017
Posts
23,928
Reaction score
63,499
Lema ana akili nyingi Sana Kichwani na pia ana Huwezo mzuri wa kuchambua Mambo ya kiasiasa, kiuchumi, kijamii na kiutamaduni.

Watz Wamefungwa akili na wanaamini umasikini ni mpango wa Mungu kumbe sio kweli.

Nimeshtushwa alipoongelea Mwalimu kulipwa lakitano na Askari police anayeanza Kazi kulipwa laki nee. Sasa kwa huu mshahara huwezi hata kujenga nyumba Wala kusomesha watoto shule za maana zaidi ya kuendelea kuwa masikini wa kutupwa.

Kiufupi Chadema wamuongezee Lema ulinzi mkali maana huyu ndo nabii mbeba maono tuliyekuwa tunamsubiri mwana wa Adam.

Nillikuwa sitaki kupiga kura lakini lazima nipige kura 2025 na ntaajiandikisha Arusha badala ya Bukoba Ahsante Sana Lema.
 
Asante kwa kutambua hilo japo kwa kuchelewa, pia hongera kamasifa hizo ni za kutoka moyoni,na sii zile za akina Nshomile ambazo ni za kimaslahi. Basi kama kweli wasaidie wananshomile kuujua ukweli kama wewe.🤔
 
Lema anazungumza ukweli mchungu ambao unaweza kukigharimu hata chama chake.
Watanzania wengi ni watu wanaopenda kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.
Bora CHADEMA wakose kura kuliko kumkosoa Lema Jamaa anapiga marungu ya ugoko kanipiga moja la mshahara wa Mwalimu daah siwezi tembea hapa lakini ukweli unauma na mzuri unaponya
 
Lema anazungumza ukweli mchungu ambao unaweza kukigharimu hata chama chake.
Watanzania wengi ni watu wanaopenda kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa.

Uko sahihi mni, anachozungumzia Lema ndio ukweli wenyewe, lakini yuko kwenye jamii iliyolemazwa fikra. Ni vyema aangalie namna ya kuwasilisha ukweli wake hasa kwa jamaa ilifubazwa akili na mwenge wa uhuru.

Angalizo kwa Lema awe makini na mdomo wake, maana yeye ni baadhi ya viongozi wa CDM walioongoza kusema Lowassa ni fisadi, kisha uchaguzi wa 2015 wakampokea na kumpa nafasi iliyotaka mtu muadilifu. Hali hiyo inafanya ukweli wa Lema kuonekana ni uropokaji zaidi kuliko msema ukweli.
 
mm namuona ni mlalamikaji zaidi sio problems solver

Maani huwezi kuja laumu watumishi kulipwa pesa ndogo wakati vyanzo vyetu vya mapato vipo very limited.

Angekuja na experience ya huko alipotoka na kushauri tufanye 1, 2, 3 ili kukuza mapato yetu ili years to come tulipe maslai mazuri kwa watumishi wetu.

Tofauti na hapo lema ni mtafuta attention zisizo na maana.
 
Tanzania Kila mtu anaakili sana piga hesabu watu wanavyomshangilia Zumaridi,watu wakiona mtu kashika vitu vya ajabu ajabu watakusanyika kumsikiliza.
 
Wewe na huyo Lema wako wote viraza tu

Chukua idadi walimu + idadi ya polisi alafu zidisha na mshahara wa 1.5 M uone kama nchi itaweza kulipa huo mshahara
 
Ujenzi wa Bwawa wakati tuna makaa ya mawe ya kutosha miaka zaidi ya 100 lilikuwa kosa sana.

Marekani, Ulaya, China wanatumia sana Makaa ya Mawe kuzalisha umeme
 
Lema kaongea point sana. Bwawa la umeme kwa nyakati za sasa kwa nchi kama Tanzania ni upotevu wa pesa.
 
Ipi ni uongo hapo? Ungeweka mtiririko wa hiyo mijadala iliyozaa hizi nukuu zako ili tupime alifikiaje hitimisho hilo.
Milioni 12 wanazolipwa mjengoni ni ndogo saana ni sawa na malipo ya jobless us. Haaaa haaaa. Chezea reshuuu za kanada wewe
 
Yupo vizuri kwenye kuosha vyombo na kubeba box huko Canada. Inaonekana mabeberu walikuwa wanamlea vizuri, arudi tu huko, maana kila siku anaingea upuuzi.
 
Milioni 12 wanazolipwa mjengoni ni ndogo saana ni sawa na malipo ya jobless us. Haaaa haaaa. Chezea reshuuu za kanada wewe
Ni nyingi kama kipimo chake ni dhidi ya watu masikini, lakini sio nyingi kwa mantiki ya kuwa tajiri.
 
Yupo vizuri kwenye kuosha vyombo na kubeba box huko Canada. Inaonekana mabeberu walikuwa wanamlea vizuri, arudi tu huko, maana kila siku anaingea upuuzi.

Ninachokiona kwa Lema ni kupinga uamsikini kwa nguvu zake zote. Yaani hauvumilii umasikini kabisa, ndio maana anaukemea kwa lugha ngumu. Tatizo anakemea umasikini kwenye jamii iliyoridhika na umasikini. Kwenye jamii ambayo umasikini ni ufahari, ni ngumu kidogo Lema kueleweka.
 
Ipi ni uongo hapo? Ungeweka mtiririko wa hiyo mijadala iliyozaa hizi nukuu zako ili tupime alifikiaje hitimisho hilo.
Anza na namba kumi na 11 kwanza kwa maana hayo mengine yametokana na elimu yake ndogo saaana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…