Nimemwelewa sana Mbowe, usipoteze imani na Rais Samia. Alivyo kwa Kauli na Matendo hawezi kuwa ni yeye!

Nimemwelewa sana Mbowe, usipoteze imani na Rais Samia. Alivyo kwa Kauli na Matendo hawezi kuwa ni yeye!

Aisee! Nimeshangaa sana Mayalla na hizi hoja zake. Eti watu wakapige kura!? Hivi huyu mtu ni mgeni nchi hii!? I'm very disappointed na huyu jamaa. Ni kama amesahau ya Zanzibar na yale aliyofanya Magufuli 2020.
Mama alishasema anafatilia mitandao so wapenda vyeo wanachacharika kuwinda vyeo humu
 
OK nitamtafuta na kukuletea mujibu hapa!.
ITAKUWA VEMA!.........MAKANISA, MISIKITI /VIWETE/VILEMA/VIPOFU /KUKU/NGOMBE/MBUZI/MBWA VYOTE VINASEMA MISWADA MIBOVU, SAMIA HUSIKII LOLOTE HALAFU USEME 4R NI PERFECT ANAZITEKELEZA
ANAOGOPA NINI KUWA NA KATIBA MPYA? ASIONDOKE MADARAKANI MAANA ANAJUA MUZIKI WA CHADEMA/ACT/CUF AND THE LIKE
 
Halafu anayesema haya ni mwandishi wa habari mkongwe na mwanasheria. Sasa yeye kama hili halifahamu, akina mchomvu wao watajua nini!
No one is perfect!, we are all humans born to make mistakes. Kama manguli wabobezi na wabobevu wa sheria wa serikalini, wanatunga muswada batili, kisha Bunge lenye manguli wabobezi na wabobevu wanatunga sheria batili, rais akaisaini, who M' I?.
P
 
No 4R za Rais Samia is real, ila Utekelezaji wake ndio issue!.

Mbona they are working perfectly!.

P
Kama utekelezaji wa 4Rs za huyu mama ni ishu, unawezaje tena kusema they are working perfectly?

Don't you see that, you're contracting yourself?

By the way Mr Pascal Mayalla, hivi wewe na huyu mama mnaelewa maana ya "Reconciliation" kweli?

Hivi hii nchi ni kina nani wana - reconcile? Ni CCM na CHADEMA tu? Really?

Ni kwa sababu gani has hawa wana - reconcile?

Maana kama ni dhidi ya uhalifu wa kiutawala toka utawala wa hayati John P. Magufuli wa kati ya 2015 - 2021, then ni makosa makubwa kudhani kuwa walioathirika na utawala wa mabavu wa hayati John P. Magufuli ni CHADEMA pekee..

Kwa sababu hiyo 👆👆pekee, ni wazi kuwa katika R nne zote (Reconciliation, Reforms, Rebuild & Reconstruction) ya kwanza na muhimu ni Reconciliation..

Huwezi ku - rebuild, ku - reform wala ku - reconstruct iwapo ktk jamii hakuna Reconciliation..

Na mpaka hapa tulipo, Rais Samia Suluhu Hassan aneshafeli big time kuleta mapatano na maelewano (reconciliation) katika taifa hili lililokuwa limevurugwa na utawala wa miaka 5+ ya hayati Rais Magufuli chini ya CCM hii hii kwa kiasi kikubwa..

Na kosa na dhamira mbaya ya Rais Samia Suluhu Hassan na CCM ilianza kwa jinsi tu alivyoanza ku - implement R namba Moja yaani "Reconciliation" kwa ku - intiate mchakato kwa kubagua makundi ya wananchi wengine yaliyokuwa yameathiriwa na utawala wa Magufuli akidhani kuwa reconciliation iliwahusu CHADEMA pekee yao...

Hapa ndipo ulipo ujinga wa Freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla kushindwa kuuona mtego huu..

Ni mtu mmoja tu alishitukia hii kitu na kusema mara nyingi. Mtu huyu ni Makamu Mwenyekiti upande wa Tanganyika ndugu Tundu Lissu...

Jamaa (Tundu Lissu) alikuwa akiwatahadharisha wenzake mara kwa mara kuhusu dhamira na nia ya CCM kwa kilichoitwa maridhiano..

Kwa sababu inaeleweka wazi kuwa maridhiano huwa hayafanyiki kwa namna na mtindo waliokuwa wanautumia CHADEMA na CCM kufanya hicho walichokiita reconciliation..

Kuwa reconcile watu waliogombana au waliofarakana ni lazima awepo mtu wa tatu au mtu wa kati. Na mara zote kwenye mchakato wa reconciliation wowote katika nchi, huwa lazima kiundwe chombo kinachoitwa "Tume ya Ukweli na Maridhiano - Truth and Reconciliation Commission " tena ikiwa chini ya majaji..

Na sambamba na hilo kuwe na maeneo ya kuridhiana kwa kuangalia chanzo cha ugomvi au matatizo yaliyosababisha watu kuumizwa auau kutoelewana na kisha tume hiyo inakuja na mapendekezo ya nini kifanyike Ili mambo hayo mabaya yasijirudie tena..

Na reconciliation kamwe huwa sio jambo la kufanyika gizani. Mashauri husikilizwa waziwazi na kila aliyeonewa na kuumizwa anapeleka malalamiko yake kwenye tume hiyo akiwa na ushahidi na kusikilizwa..

CHADEMA kwenye hili wakiongozwa na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe waliingizwa mkenge na kupotezewa muda wa bure. Bila shaka walikuwa wanatafuta kitu kingine na nafikiri walidhani CCM wanaweza kuwapa nafasi fulani za uongozi ktk serikali hii..

All in all, naweza kusema 4Rs zenyewe wala hazina shida. Ni maneno halisi na yana maana yake isiyo na shaka yoyote. Lakini kwa Rais Samia Suluhu Hassan na CCM yake, maneno haya yanabaki kuwa maneno tu ya midomoni mwao yasiyo na matokeo yoyote katika maisha na siasa za Tanganyika..

Kwa lugha rahisi, nyepesi na ya kueleweka kirahisi ni kuwa, Samia Suluhu Hassan na CCM wameyatumia maneno haya kututapeli na hasahasa kuwatapeli CHADEMA na wame - prove hili..

Retired & JokaKuu Nguruvi3 Mag3 denooJ BAM
 
Na kosa na dhamira mbaya ya Rais Samia Suluhu Hassan na CCM ilianza kwa jinsi tu alivyoanza ku - implement R namba Moja yaani "Reconciliation" kwa ku - intiate mchakato kwa kubagua makundi ya wananchi wengine yaliyokuwa yameathiriwa na utawala wa Magufuli akidhani kuwa reconciliation iliwahusu CHADEMA pekee yao...

Hapa ndipo ulipo ujinga wa Freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla kushindwa kuuona mtego huu..
Hapana, Mbowe alisema tuwe na tume ya Ukweli na upatanishi. Wooooooooooooooooooooooooooooooooooote waiofanyiwa unyama na utawala wa magufuli waje mbele ya tume , na waliofanya unyama waje watubu! hukumwelewa Mbowe, it was not for chadema only to reconcile but all those who were wronged! including you!
 
Hapana, Mbowe alisema tuwe na tume ya Ukweli na upatanishi. Wooooooooooooooooooooooooooooooooooote waiofanyiwa unyama na utawala wa magufuli waje mbele ya tume , na waliofanya unyama waje watubu! hukumwelewa Mbowe, it was not for chadema only to reconcile but all those who were wronged! including you!
Kama alitaka haya kwanini aliendelea kukaa nao huku akijua hatapata chochote?
 
ITAKUWA VEMA!.........MAKANISA, MISIKITI /VIWETE/VILEMA/VIPOFU
True
/KUKU/NGOMBE/MBUZI/MBWA VYOTE VINASEMA MISWADA MIBOVU,
duh hii kali
SAMIA HUSIKII LOLOTE HALAFU USEME 4R NI PERFECT ANAZITEKELEZA
ANAOGOPA NINI KUWA NA KATIBA MPYA? ASIONDOKE MADARAKANI
hili hata akina sisi, tumeshauri Hongera Sana Rais Samia kwa Miaka Miwili Madarakani. Japo Umefanya Mengi, Makubwa, Mazuri, Lakini Bado! Linalowezekana Leo, Lisingoje Kesho!
MAANA ANAJUA MUZIKI WA CHADEMA/ACT/CUF AND THE LIKE
Sasa msianze vitisho na mikwala mbuzi!.
P
 
No one is perfect!, we are all humans born to make mistakes. Kama manguli wabobezi na wabobevu wa sheria wa serikalini, wanatunga muswada batili, kisha Bunge lenye manguli wabobezi na wabobevu wanatunga sheria batili, rais akaisaini, who M' I?.
P
Lakini hayo yote hayafuti makosa. Kosa ni kosa tu halijalishi kalifanya profesa, rais au mfalme
 
Kama alitaka haya kwanini aliendelea kukaa nao huku akijua hatapata chochote?

..hata mimi nakubaliana na wewe kwamba mazungumzo kati ya Cdm na Ccm yalipaswa kuwa na msuluhishi.

..kukosekana kwa msuluhishi ktk mazungumzo hayo ni kosa ambalo pande zote zinastahili lawama.

..Lakini kitendo cha Rais kuteua watu ambao wamekuwa wakilalamikiwa kwamba walishiriki kwa namna mbalimbali ktk ukandamizaji wa haki ktk utawala wa Jpm ilikuwa ni uthibitisho kwamba hakuwa na nia ya dhati na njema kuhusu maridhiano.

..Mwisho, naunga mkono hoja yako kwamba ni lazima maridhiano yaundiwe Tume ya Haki, Ukweli, na Usuluhishi.
 
Mkuu Mayor Quimby , kwanza asante for being mchangiaji most objective kwa kuja na vifungu. Ibara ya 5 inahusu tuu haki ya kupiga kura, the right to vote, the right to choose.
Kiongozi politics can be amoral, as Machiavelli explained. Kwa hivyo kushindwa kwa sababu ya watu kutembeza mkwanja zaidi hizo unaweza ita mbinu za vita tu. Kukatwa na CC ya CCM ni kawaida panapo ushahidi mgombea ana makando-makando ambayo yanaweza kichafua chama na serikali.

Otherwise ukishinda kwenye kura za maoni wewe ndio mgombea. Na kwenye kukata huo sio utaratibu wa Tanzania hata uingereza upo ivyo be it rarely exercised.

Kilichotokea 2020 ni vitu vya ovyo sana kwenye kukata watu bila ya sababu za msingi (ni moja ya blunder kubwa ya uongozi wa Magufuli) na ile ni moja ya sababu kujiongezea chuki kubwa sana na vigogo wa nchi, wakati alikuwa nao tayari wa kutosha katika kupambana na ufisadi huko serikalini.

Back to the principles huko kwenye vipengele vya katiba sitorudia in details zaidi ya kugusia hivyo vipengele tena.

Ibara ya 5 inaelezea uhuru wa kupiga kura kwenye chaguzi (nothing about sifa za mgombea).​
Ibara ya 11 inaelezea individual rights to prosperity such as being educated, being protected by the state and so forth (nothing to do with election).​
Ibara ya 21 inazungumzia right to participate in employment and social issues either kwa kuteuliwa, kugombea nafasi au ku-support ideas/mtu/kikundi. Hizi rights za ibara hii, zimeelezwa bila ya kuingilia ibara ya 5 (haki za ya kupiga kura), 39 (sifa za mgombea uraisi) na 61 (sifa za mgombea ubunge).​
Kwa hivyo ibara unazo quote hazina uhusiano na malalamiko yako. Labda hiyo ya 61 ndio inayosema ili ugombee lazima upitie chama.

Sasa kuna practical logic kwanini watu wanagombea kupitia vyama. Kumbuka nchi inaendeshwa na admin laws na hata mipango ya serikali inahitaji baraka ya sheria. Na sheria ili ipite bungeni inahitaji quorum ya wabunge.

Kupitia vyama vya siasa serikali tawala mara zote kwenye sheria za kuendesha nchi huwa hakuna free vote ya wabunge wake ndio msingi wa ‘whip’ kuhakikisha zile sheria muhimu za serikali wabunge wote wanakumbushwa kufika bungeni na kusema ndiyoo (ipo hivyo duniani, sio Tanzania tu). Kuna maswala machache hasa ya moral issues ndio serikali inaweza toa free vote kwa wabunge.

Vinginevyo bila ya utaratibu huo nchi aiendesheki, imagine 65% ya wabunge ni kutoka ‘indepent’ hawana vyama. Nani ata wa control hawa kwenye kupitisha sheria wakati kila mtu na kichwa chake kwenye maamuzi huo ndio mwanzo wa banana republic. Ndio maana hata ujerumani na nchi nyingi ambazo kupata majority ya chama kimoja ni ngumu, ili kuondoa ‘hang parliament’ vyama vinaingia makubaliano ya kuungana ili kupata majority ya bunge na kuweza kupitisha sheria.

Moreover baada ya chaguzi kama kuna ‘hang parliament’ wanasiasa wanaweza kuchukua hata miezi sita kukubaliana kuungana na kutengeneza serikali. Katika muda huo ambapo hakuna muafaka wa vyama vya siasa shughuli za serikali na huduma za jamii aziwezi lala lazima kuwe na watu wenye uwezo wa kuendesha nchi. Huko kwa wenzetu wana civil services ambayo katibu mkuu ameandaliwa kwa scenario hiyo ya kuendesha nchi, sisi tuna makatibu wakuu mabalozi hadi siku serikali inaundwa hazina kuna kitu na halmashauri hakuna kitu watu washakombe bakshishi zote.

Ni hivi hayo mambo ya mgombea binafsi yana mambo mengi sana ya kuyaangalia zaidi katika government operational na ya kuyachukulia simple tu kama watanzania tunavyodhani.

Mwisho katiba/sheria inapokuwa na lexical ambiguities kwenye tafsiri, unachohitaji ni records za nyuma za mijadala kuonyesha hiko kipengele au ibara kina lenga nini from discussion evidence, sio hadithi za wanasheria tena.
 
Punguza ujinga. Miaka yote ccm inaongoza wameiba fedha kiasi Gani na wamechukuliwa hatua Gani!? Unakuja kulaumu wapinzani waliofanya kazi kubwa ya kuonesha wezi wa ccm wanavyoitafuna nchi.! Akili Yako itakuwa ina matatizo. Kapambane kwanza na wale wanaosema "wema hawafi"
Shida yao upinzani ni kulilia mabadiliko ya sheria na katiba. Halafu ukiwapa hiyo fursa wanaachana na mapendekezo ya msingi wanakuja na mambo ya kipuuzi ambayo in practice hayawezekani na kuanza kupiga kelele tena wasipoyaona.

Hiyo serikali aijajifunza tu na rasimu ya Warioba, huku ni kupoteza muda ku-entertain ujinga na kusikiliza makelele yasiyo na kichwa wala miguu. Wakati watanzania wanashida luluki na zimeongezeka ndani ya muda mfupi.

Yote kwa sababu serikali badala ya kufanyia kazi shida za watanzania inataka kujibizana na porojo za wanasiasa wasiojitambua wanataka nini zaidi ya kuongoza serikali siku moja. Huku umeme shida.
 
Wanabodi,
Nimemsikiliza Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe katika bandiko hili Mbowe: Najutia kumuamini Rais Samia
View: https://youtu.be/Xjao83Ghy04?si=qSQTeSxIx_8B5a-L

Kiukweli kabisa mimi nimemwelewa sana Mwenyekiti Freeman Mbowe hapa, na hata ningekuwa mimi!, I would have felt the same, but not done the same, I would have done something worthwhile but not maandamano!.

Namuomba sana Mhe. Mbowe, please usipoteze imani na Rais Samia!, kwasababu Rais Samia ninaye mfahamu mimi, sio mtu mwenye ndimi mbili!, namfahamu fika Rais Samia kwa kauli na matendo, yeye kama yeye, hawezi kabisa kusema hivi haiafu akaja kutenda vile!. She is straightforward person and firm, tena usikute yeye kwa intellect yake, japo ndie aliyeongoza kikao cha Baraza la Mawaziri kilichopitisha miswada hiyo lazima ukakuta yeye wala hajui kuwa mswada sheria ya uchaguzi una ubatili ulioshabatilishwa na Mahakama Kuu kwasababu yeye sio mwanasheria!.

Japo miswada yote ya serikali, lazima ipite Baraza la Mawaziri ijadiliwe, wakati mswada huu wa sheria ya uchaguzi unajadiliwa, hakuna mtu yeyote mule akiwemo AG, aliyemwambia ukweli Rais Samia kuwa muswada huo una ubatili!, hivyo mtu ambaye sii mwanasheria hawezi kuujua ubatili wa kisheria kwenye vipengele vya miswada mpaka aelezwe na wanasheria!. Hivyo kwa intellect ya Rais Samia, kumlaumu kwa kutoyajua haya ni kumuonea bure!.

Kwa bahati nzuri, mimi ni miongoni wa watu wanaomfahamu Rais Samia sio tuu kwa kauli na matendo, bali kwa kufanya nae mahojiano ya ana kwa ana mara mbili. Mara ya kwanza akiwa Waziri Ofisi ya Makamo wa Rais na mara ya pili akiwa Makamo Mwenyekiti wa Bunge la Katiba.

Wakati akiwa VP nilimfanyia uchambuzi mara mbili
Mara ya kwanza ni hapa Siku ya Wanawake Duniani: VP Samia Suluhu: "Womanly, Genuine, Humble, Simple na Down To Earth!” na mara ya pili ni hapa "Watu waachwe Huru kuujadili Muungano"- VP, Samia Suluhu Hassan. Huyu mama anaongea vizuri kwa Unyenyekevu mpaka raha. Huchoki kumsikiliza

Na baada ya kuwa Rais wa JMT, pia nilimfanyia uchambuzi mara mbili Psychoanalysis Trends za Viongozi Wetu, Humbleness ya Rais Samia ni Bonafide Genuine, ni asili yake, ni nature yake, ndivyo alivyo, Ila... na Ili kupata Viongozi Bora baadae, Watanzania tujifunze kuwasoma watu kwa asili zao. Mjue Samia alivyo kwa asili yake

Hivyo kwa kauli na matendo, ya Rais Samia, hiki kinachofanyika kwenye miswada hii, naamini kabisa sio yeye, bali waonayafanya haya ni wanasheria, waojua fika ubatili wa muswada huu, lakini wametake advantage ya intellect yake Rais Samia kumsokomezea ubatili tena, ikapelekwa Bungeni, itapitishwa, na kutungwa sheria batili, kisha Rais Samia ataisaini kuanza kutumika, kwa excuse kuwa batili hiyo kwa vile iko kwenye katiba yetu!, then ni batili halali!. Kisheria, batili ni batili, hata ikichomekewa kwenye katiba kiubatili, bado inabaki ni batili, na badala ya kuihalalisha haramu kwa kuichomekea kwenye katiba, haramu hiyo inaiharimisha katiba na kuibatilisha katiba kwa kuifanya kuwa na unajisi!.

Mimi naamini kabisa kwa haya yanayofanyika kuhusu Muswada huu, huyu sio Rais Samia ninaye mfahamu mimi, na naamini kabisa yeye wala hajui kuwa muswada wa sheria ya uchaguzi ni muswada wenye ubatili unaokiuka ibara ya 11 ya katiba ya JMT na kuathiri ibara ya 5, ibara ya 21, ibara ya 39 na ibara ya 67.

Kwa vile yeye sio mwanasheria, hajui kuwa katiba yetu ina ubatili, uliochomekewa kiubatili na awamu zilizopita na Bunge lilolopita unakokwenda kinyume cha Ibara ya 5, ibara 21, ibara ya 39 na ibara ya 67 za Katiba ya Tanzania ya mwaka 1977.

Nimesema ninaamini kabisa Rais Samia hayajui haya na hapa niliandika Madudu ya ajabu ya ubatili wa Katiba yetu, mabadiliko "fake" ya sheria na Tume ya Uchaguzi, Rais Samia asilaumiwe kwasababu yeye sio mwanasheria!.

Hivyo kitendo cha Freeman Mbowe Kutomwamini Rais Samia, ni kumuonea bure, niliwahi kushauri Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda, ila kama Freeman Mbowe anaona muda aliompa kwenye vikao vya maridhiano unatosha, sasa ndio aanzishe maandamano, huku sio kumtendea haki, namshauri Mbowe, aichukulie miswada hii kama fursa, afanye uhamasishaji na uelimishaji umma wa kufa mtu kwa Watanzania kwa ku invest in people, grassroot people kuhusu haki zao, ili Watanzania kwa mamilioni wajitokeze wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura, na 2025 wajitokeze kwa wingi wawapumzishe watu kwa amani kupitia sanduku la kura na sii kupitia maandamano!.

Bahati nzuri sana na mimi nimehudhuria vikao vyote vitatu vya kukusanya maoni ya wadau na mara zote 3 nilipata bahati ya kuchangia.

Mchango wangu kikao cha kwanza ni huu
View: https://youtu.be/PBpjDhH2XiA?si=9dtqZ-1-ZkzWo69t

Mkutano wa pili maoni yangu ni haya
View: https://youtu.be/3a4SjkV46JY?si=98HTkiMGNsmlLBGz

Na Mkutano wa tatu wa Kamati ya Bunge pia nilitoa maoni.
Nimeandika makala zifutazo kuhusu sheria hizi

Mbowe kutangaza maandamano nimetoa ushauri issues za kisiasa zitatuliwe kisiasa, halafu issues za kisheria zitatuliwe kisheria, utungaji miswada ni issue ya kisheria, baada ya watu kutoa maoni yetu, Bunge likitutungia sheria batili, this time around, we'll have to do something!.

Tangu Rais Samia ameingia madarakani ile March 21, 2021, mimi tuu mwenyewe, nimelisemea jambo hili la katiba, sheria na haki zaidi ya mara 100!,

Mhe. Freeman, rudisha moyo, applies zile 4R za Rais Samia tulisongeshe mbele kwa mbele.

Mungu Ibariki Tanzania

Paskali.

Maoni mazuri ndg yangu P, ahsante sana.
 
Kama utekelezaji wa 4Rs za huyu mama ni ishu, unawezaje tena kusema they are working perfectly?
Naomba nikupe taarifa kwamba kuna 'outbreak' ya ku-push 4R katika mitandao siku hizi. Kila jambo linaelezwa kwa 4R ili kuiweka slogan katika mjadala wa kitaifa baada ya kudoda. Ilitegemewa kwamba 'slogan' itavuma kama zilizopita lakini Imedoda big time. Kuna watu wamekuwa 'tasked' kuifanya kazi ya 4Rs,
Hivi hii nchi ni kina nani wana - reconcile? Ni CCM na CHADEMA tu? Really?
Ni kwa sababu gani has hawa wana - reconcile?
Huwezi ku - rebuild, ku - reform wala ku - reconstruct iwapo ktk jamii hakuna Reconciliation..
Na mpaka hapa tulipo, Rais Samia Suluhu Hassan aneshafeli big time kuleta mapatano na maelewano (reconciliation).
Kuna watu wameumizwa katika Biashara, katika ajira, watu wamepotea, wameuawa n.k.
Reconciliation ilitakiwa kwa ujumla. Na hapa amefeli kwasababu bado kuna resentment katika jamii.
Na kosa na dhamira mbaya ya Rais Samia Suluhu Hassan na CCM ilianza kwa jinsi tu alivyoanza ku - implement R namba Moja yaani "Reconciliation" kwa ku - intiate mchakato kwa kubagua makundi ya wananchi wengine yaliyokuwa yameathiriwa na utawala wa Magufuli akidhani kuwa reconciliation iliwahusu CHADEMA pekee yao...
Kwa Chadema haikuwa reconciliation, ilikuwa kupoteza muda na kuwapoza ili apate nafuu. Unakumbuka 'Mzee' akiwa Nairobi alisema '' Kikosi kazi kimesaidia kupooza joto la siasa''.. SSH alikuwa 'sahihi' kwa kuwatega Chadema.
Chadema walipaswa kujiuliza kwanini wao na si makundi mengine! 'Naivety'
Hapa ndipo ulipo ujinga wa Freeman Mbowe na CHADEMA kwa ujumla kushindwa kuuona mtego huu..
Ndipo hoja ilipo kwamba kuna sehemu mbili. Kwanza, Mbowe akiwa mzoefu wa siasa alipasw akuliona hili. Pamoja na kushauriwa na watu wengi sana , Mwenyekiti akajaa kiburi akiita wenzake '' Wahafidhina'
Upande wa pili, Kamati kuu ya CDM ilipaswa kumgomea Mwenyekiti wao kwasababu alipotea njai, haikufanya hivyo.

Tangu siku ya kwanza, ilikwua dhahiri hata wasiokuwa Wanachama wa CDM walishangaa na hatua ya Mbowe kukimbilia Ikulu na picha kusambazwa. Alipaswa kuliona hili, na hapa ni feli nyingine ya Mbowe.
Kwa mtirirko wa felia Mbowe hana option iliyobaki isipokuwa kuachia ngazi. Madhara ya maridhiano ni makubwa sana kwa Taifa.
Ni mtu mmoja tu alishitukia hii kitu na kusema mara nyingi. Mtu huyu ni Makamu Mwenyekiti upande wa Tanganyika ndugu Tundu Lissu...
In fact zaidi ya 3/4 ya CC ya Chadema hawakuridhishwa. Ukisikiliza kauli zao utagundua hawakuridhiswa.
Naweza hata kuwataja kwa kutumia kauli zao, lakini sijui wamelishwa limbwata gani Yarabi!
Kwa sababu inaeleweka wazi kuwa maridhiano huwa hayafanyiki kwa namna na mtindo waliokuwa wanautumia CHADEMA na CCM kufanya hicho walichokiita reconciliation..
Huwezi kuingia katika recondiliation bila kutumia 'bragaining chip'. Mbowe alikuwa na Watu nyuma yake na sababu za ku-force CCM wakubali namna mchakato utakavyotekelezwa.
Ilikuwa wazi wala haikuhitaji certificate yoyote kwamba CCM walikuwa wanapoteza muda na Mbowe kwenye Hotel ,, Mbowe sijui hakujua au alijua lakini tunajua leo AMEFELI na ameumiza Chama chake. Hana option bali kujiuzulu
CHADEMA kwenye hili wakiongozwa na Mwenyekiti wao Freeman Mbowe waliingizwa mkenge na kupotezewa muda wa bure. Bila shaka walikuwa wanatafuta kitu kingine na nafikiri walidhani CCM wanaweza kuwapa nafasi fulani za uongozi ktk serikali hii..
Kamati Kuu na Mbowe wanapaswa kujiuzulu, hawakuwatendea Wanachama haki lakini muhimu Mbowe must go !
Ni maneno halisi na yana maana yake isiyo na shaka yoyote. Lakini kwa Rais Samia Suluhu Hassan na CCM yake, maneno haya yanabaki kuwa maneno tu ya midomoni mwao yasiyo na matokeo yoyote katika maisha na siasa za Tanganyika..
Amechukua ulaghai wa Zanzibar akauleta na kwa bahati mbaya akapewa 'pass' na Chadema kwa ujinga tu.
Yes ni ujinga lazima isemwe hivyo.

Tangu Mbowe anakimbilia Ikulu, nilisimama hapa JF na kusema ilikuwa fyongo ya kisiasa.
Kwa lugha rahisi, nyepesi na ya kueleweka kirahisi ni kuwa, Samia Suluhu Hassan na CCM wameyatumia maneno haya kututapeli na hasahasa kuwatapeli CHADEMA na wame - prove hili..
Chadema wametapeliwa mchana , wameuziwa mbuzi katika gunia! Mwenyekiti akizunguka nchi na hata nchi za nje kunadi utapeli leo anarudi na kilio kana kwamba haya yalifanyika gizani.


Mbowe anaweza kurudi Hotelini kuongea na kinana, kitu asichoweza kufanya tena ni kurudisha imani katika jamii kama kiongozi wa upinzania. Hana option, Mbowe must go!
 
Kiongozi politics can be amoral, as Machiavelli explained. Kwa hivyo kushindwa kwa sababu ya watu kutembeza mkwanja zaidi hizo unaweza ita mbinu za vita tu. Kukatwa na CC ya CCM ni kawaida panapo ushahidi mgombea ana makando-makando ambayo yanaweza kichafua chama na serikali.

Otherwise ukishinda kwenye kura za maoni wewe ndio mgombea. Na kwenye kukata huo sio utaratibu wa Tanzania hata uingereza upo ivyo be it rarely exercised.

Kilichotokea 2020 ni vitu vya ovyo sana kwenye kukata watu bila ya sababu za msingi (ni moja ya blunder kubwa ya uongozi wa Magufuli) na ile ni moja ya sababu kujiongezea chuki kubwa sana na vigogo wa nchi, wakati alikuwa nao tayari wa kutosha katika kupambana na ufisadi huko serikalini.

Back to the principles huko kwenye vipengele vya katiba sitorudia in details zaidi ya kugusia hivyo vipengele tena.

Ibara ya 5 inaelezea uhuru wa kupiga kura kwenye chaguzi (nothing about sifa za mgombea).​
Ibara ya 11 inaelezea individual rights to prosperity such as being educated, being protected by the state and so forth (nothing to do with election).​
Ibara ya 21 inazungumzia right to participate in employment and social issues either kwa kuteuliwa, kugombea nafasi au ku-support ideas/mtu/kikundi. Hizi rights za ibara hii, zimeelezwa bila ya kuingilia ibara ya 5 (haki za ya kupiga kura), 39 (sifa za mgombea uraisi) na 61 (sifa za mgombea ubunge).​
Kwa hivyo ibara unazo quote hazina uhusiano na malalamiko yako. Labda hiyo ya 61 ndio inayosema ili ugombee lazima upitie chama.

Sasa kuna practical logic kwanini watu wanagombea kupitia vyama. Kumbuka nchi inaendeshwa na admin laws na hata mipango ya serikali inahitaji baraka ya sheria. Na sheria ili ipite bungeni inahitaji quorum ya wabunge.

Kupitia vyama vya siasa serikali tawala mara zote kwenye sheria za kuendesha nchi huwa hakuna free vote ya wabunge wake ndio msingi wa ‘whip’ kuhakikisha zile sheria muhimu za serikali wabunge wote wanakumbushwa kufika bungeni na kusema ndiyoo (ipo hivyo duniani, sio Tanzania tu). Kuna maswala machache hasa ya moral issues ndio serikali inaweza toa free vote kwa wabunge.

Vinginevyo bila ya utaratibu huo nchi aiendesheki, imagine 65% ya wabunge ni kutoka ‘indepent’ hawana vyama. Nani ata wa control hawa kwenye kupitisha sheria wakati kila mtu na kichwa chake kwenye maamuzi huo ndio mwanzo wa banana republic. Ndio maana hata ujerumani na nchi nyingi ambazo kupata majority ya chama kimoja ni ngumu, ili kuondoa ‘hang parliament’ vyama vinaingia makubaliano ya kuungana ili kupata majority ya bunge na kuweza kupitisha sheria.

Moreover baada ya chaguzi kama kuna ‘hang parliament’ wanasiasa wanaweza kuchukua hata miezi sita kukubaliana kuungana na kutengeneza serikali. Katika muda huo ambapo hakuna muafaka wa vyama vya siasa shughuli za serikali na huduma za jamii aziwezi lala lazima kuwe na watu wenye uwezo wa kuendesha nchi. Huko kwa wenzetu wana civil services ambayo katibu mkuu ameandaliwa kwa scenario hiyo ya kuendesha nchi, sisi tuna makatibu wakuu mabalozi hadi siku serikali inaundwa hazina kuna kitu na halmashauri hakuna kitu watu washakombe bakshishi zote.

Ni hivi hayo mambo ya mgombea binafsi yana mambo mengi sana ya kuyaangalia zaidi katika government operational na ya kuyachukulia simple tu kama watanzania tunavyodhani.

Mwisho katiba/sheria inapokuwa na lexical ambiguities kwenye tafsiri, unachohitaji ni records za nyuma za mijadala kuonyesha hiko kipengele au ibara kina lenga nini from discussion evidence, sio hadithi za wanasheria tena.
Katika yoote, bila shaka hoja hapa ni mgombea binafsi..

Umejitetea kuwa ni hatari kuwa na mgombea binafsi.

Kwamba, ni vyema kuendelea na mfumo wa sasa wa kila atakaye uongozi wa kuchaguliwa ktk nchi yetu apitie kwenye chama cha siasa..

Sababu yako ni kuwa, mgombea binafsi hadhibitiki, hana chama cha kumdhibiti... Na hapa ndipo upogo wa hoja yako ulipo..

Inaelekea wewe ni miongoni mwa wana CCM waoga wa mabadiliko wanaofaidika na mfumo huu mbovu kiasi cha kuutetea kwa sababu za kitoto sana..

Unaandika kana kwamba hatuwezi kujiwekea utaratibu wa checks & balance ktk mambo haya. Na woga, hofu na wasiwasi wako huu unaweza kuondolewa kwa kukaa wote chini na kutengeneza utaratibu kupitia kutengeneza katiba mpya inayoweza ku - harmonize haya yote..

By the way, uzoefu wa nchi zote zilizoruhusu mgombea binafsi unaonesha kuwa it's very rare wagombea binafsi kuingia kwa wingi ktk vyombo vya maamuzi kama bunge au mabaraza ya miji nk nk..

Hata kama ikitokea mgombea fulani asiye na chama (mgombea binafsi) ameshinda ktk nafasi ya u - Rais, lazima katiba ieleze ni kwa namna gani mgombea huyu ataunda serikali yake. Ndivyo ilivyo ktk nchi za wenzetu..

Tatizo ni Moja kuwa, CCM hawataki mwafaka wa kitaifa kupitia katiba mpya na ndiyo maana wana - reject kila kitu hata ambavyo ni vya muhimu na vinavyoweza ku - fast track maendeleo yetu ya kiuchumi na kijamii kwa sababu kama unazotoa wewe..

Haiwezekani eti ktk kupiga kura kuchagua viongozi watu wote wanaweza kupiga kura ktk uchaguzi na wakachagua viongozi wao bila kujali ni wanachama wa vyama vya siasa au la...

Lakini ktk kugombea nafasi za uongozi ili wapigiwe kura, watu haohao wanachama na wasio wanachama wa chama chochote cha siasa eti unawawekea sharti la kuwa wanachama wa vyama vya siasa..!!

This is very ridiculous, right?

Je, baada ya maelezo haya bado tu wewe unaona hili liko sawa ndugu Mayor Quimby?
 
Kwanini mnamlaumu tu Freeman Mbowe?
Mbowe halaumiwi bali anaelezwa ukweli
Nadhani tunahitaji kuwashauri CHADEMA the way forward. Kwamba, maamuzi yao ya sasa yako sahihi?
Hawashauriki, mbona walielezwa mapema kwamba maridhiano ni utapeli?

Aliyekuwa anasema ' South Africa na Ukraine' wanaongea wakati wanapambana si Mbowe.
Aendelee kuongea na Kinana Hotelini, kwa hili anabeba mzigo wa ujinga! yes wa ujinga kwasababu ilikuwa obvious
Hata hivyo, binafsi naweza kusema, kuwa, hata ktk siasa zipo ajali pia a k.a ajali za kisiasa, zipo imperfections za kutosha..
Hii si ajali.Huwezi kulala Ubungo mataa ukagongwa na gari na kusema ni ajali, hiyo ni 'suicide'
Hakuna ajali kuna ujinga uliofanyika. Period
Freeman Mbowe & CHADEMA hawawezi kuwa na maamuzi sahihi siku zote na muda wote. Kwa hili bila shaka ndiyo tunaona wazi kuwa they made wrong decisions..
Hapana, walipaswa kusikiliza Umma '' Vox populi vox dei' wakajitia kiburi Mbowe akiita wanaomkosoa 'Wahafidhina', akasema hatoki katika mazungumzo, akawa msemaji wa CCM kwamba huko pia kuna wahafidhina. Ni FAM huyo
No matter what happened...
No matter ni makosa gani wamefanya..
Kuingia katika maridhiano bila kujua wanaridhiana nini. Kukubali CCM ina nia njema bila kujali historia. Kudharau Wanachama wao na Wananchi waliowaonya. Kuwa na kiburi kisicho na kichwa wala miguu.

Mbowe amefeli, the next is to step down with immediate effect. Mbowe must goi kama CDM wanajaitakia mema

Huwezi kuongozwa na mtu asiyeona hata treni inayokuja mbele! He must go ! hana vote of confidence
The fact remains kuwa CHADEMA bado ndicho chama tegemeo shindani pekee kuliko vingine vyote kuinyang'anya CCM dola..
Ndio maana Mbowe anatakiwa aachie ngazi! amefelisha mamilioni!
Tuwashauri kuangalia mbele badala ya kuangalia wapi wamejikwaa..
Sijui huko katika chama chao, lakini mimi kama raia mwema ninaona rekodi ya Mbowe ni mbaya.
Amefeli sana! kwa wakati huu hana choice, must go! tena alipaswa kujiuzulu jana.
Amepoteza trust . Kwa chama makini , leo angekuwa mwanachama tu.
Ni Ukweli kuwa hata Freeman Mbowe mwenyewe anajuta kwa hili kwa sababu amepoteza miaka zaidi ya miwili kwa ulaghai wa CCM..
Hapana! Alijuta wakati wa Lowassa
Alijuta wakati wa maridhiano na Magufuli Mwanza
Sasa anajuta tena

Ni kiongozi gani anayejuta kila siku! hana washauri! hana cha kujifunza. Hana changuo isipokuwa aondoke

Mbowe must go!
 
Back
Top Bottom