Nimenunua pressure cooker, Cha ajabu natumia saa moja na nusu kupika maharage. Nakosea wapi?

Chemsha maji weka na maharage yako kwenye chupa isiyopooza usiku kucha asubuhi ikifika yapike dkk 5 tu maharage unakula, mjini mipango, dkk 40 zote hizo si muda wa kuingiza hela 🤣🤣
 
Chemsha maji weka na maharage yako kwenye chupa isiyopooza usiku kucha asubuhi ikifika yapike dkk 5 tu maharage unakula, mjini mipango, dkk 40 zote hizo si muda wa kuingiza hela 🤣🤣
Umetumia muda Gani kusoma hii threads vipi SI muda wa kuingiza hela huu? Acha usenge na ujuaji mpumbavu wewe
 
Nakumbuka enzi zetu kuwa na pasi ya mkaa tu ilikuwa anasa, mara nyingi ili kunyoosha nguo tulikuwa tunazipeleka kwa dobi.
Kinyume na hapo unazikunja nguo vizui, unaziweka chini ya godoro, unalalia, ukiamka zimenyooka vizuri.

Kuhusu maharage, tulikuwa tunayaloweka ile usiku, asubuhi unaenda kazini, jioni ukirudi unayachemsha kwa muda wa dakika 20 au nusu saa tayari yanakuwa yameshaiva. Ukijisahau ukaendelea kuyaacha yamelowekwa hadi siku ya pii unakuta maji yameshakolea rangi ya mchuzi wa maharage, halafu maharage yenyewe yameshaanza kuota humo kwenye sufuria
 
Chemsha maji weka na maharage yako kwenye chupa isiyopooza usiku kucha asubuhi ikifika yapike dkk 5 tu maharage unakula, mjini mipango, dkk 40 zote hizo si muda wa kuingiza hela 🤣🤣
Hii pia tuliitumia sana miaka ya themanini hadi 90 mwanzoni
 
Maji hayaishi lakini maharage si yanaiva?
 
Hiyo ni Electric Cooker na sio Pressure cooker,
Mfumo wake wa kupika ni kama wa Rice cooker
Electric cooker inakua na muda elekezi na kutokana na uwezo wake inashauriwa kupika vyakula vya kawaida kama Wali, Choroko, Njegere
Nyama na Maharage tafuta “PressCooker”
Ambayo inapika kwa mkandamizo wa hewa bila kutuhusu hewa kutoka kwa muda kadhaa
Pressure cooker za kampuni ya T-Fal au Kenchan zinapika maharage kwa 30min top.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…