Nimenusurika kufa usiku huu na ajali

Pole sana mkuu. Mungu ana ishara zake. Mojawapo ni hili somo kwamba tujiandae muda wote. Tunamshukuru Mungu kwa kukunusuru na familia yako
 
Pole sana mkuu. Mungu ana ishara zake. Mojawapo ni hili somo kwamba tujiandae muda wote. Tunamshukuru Mungu kwa kukunusuru na familia yako
Asante nashukuru,ile hadithi ya kusema kabla hujalala unawandika wote kwenye karatasi wanaokudai na unaowadai,nimeikumbuka leo
 
Kuna siku nilikoswa koswa na mnazi chumbani.
Yaani pona yangu ilikuwa umbali uliopo mnazi na kile chumba nilichokuwepo.
 
Kuna jamaa aliuliza majuzi nini faida na hasara za kujenga nyumba karribu na barabara, hii iingefaa akaiona
 
Mleta mada ulikuwa usingizini baada ya kula tunda kimasihara?
Kula mizigo mpaka ikome.
 
Pole sana mkuu.
Wenzako wajanja wanaoishi pembezoni mwa bara bara huchumbia mataruma ama mirunda kuzikinga nyumba zao na ajali kama hizo.
 
Ungekuwa ushajikomboa na hizi tozo..
 
Amakweli KIFO ni FUMBO.

Jana J3 kuna Jamaa kanusirika kama wewe hivyo hivyo na alishajiandaa na Mipango chungu mzima.

Yuko hospitalini anauguzwa lakini uhai anao na nyumba haifai tena maana Lori limeichakaza.

Pole sana na nakushauri ongeza Ibada ndugu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…