skia hii, jana nilikuwa napewa stori na dada mmoja anakaribiwa kuolewa
nikamwuliza amempataje mpenzi wake
akanijibu
Dada: nimempata kwenye morning and evening glory nilikuwa naenda kila siku kanisani, kumbe huyo kaka akaniona akanipenda akawa anapima frequency ya kuja kanisani kama na beep au namaanisha
basi baada ya mwaka mmoja akani approach asijue kuwa niko singo mimi tena kwa muda wa miaka 3
tuka exchange namba, tukaanza mawasiliano, baada ya mwaka akaomba wazee wake waje akutane na wazazi wangu!
Money Penny: kwahiyo hamjazini mwaka wote huo?
Dada: hatujazini boss hata ku kiss! nilimwambia nimetoka kwenye very painfull relationship, nimekaa miaka 3 sitaki kusikia kuzini mpaka kwenye ndoa....
ni kweli yale maombi ya morning na evening glory yamenisaidia sana, nilikuwa naenda kwa Bwana Yesu, Bwnaa Yesu akanipa Bwana Mume (My Lord)!
Money Penny: Haya haya sasa! nyie wenzetu mnaendaga wapi kupata waume?
jamani muende kanisani, ohooo! Yesu anatoa waume kama mvua huku Morning Glory!, ila usiende kudanga tu!