Nimepata mfadhili wa mradi mmoja mkubwa unaoweza kugharimu Tsh billioni 116. Ni mradi gani unaweza kugharimu hizo pesa?

Nimepata mfadhili wa mradi mmoja mkubwa unaoweza kugharimu Tsh billioni 116. Ni mradi gani unaweza kugharimu hizo pesa?

Peleke Meli kubwa ya Uvuvi ziwa Tanganyika uvune wale samaki na Dagaa, wana Demand kubwa sana Ulaya shida ni dhana hafifu za kuvua kwenye lile ziwa
 
Kwa Tanzania,miradi ni mingi Sana unless wewe umeshindwa kumpa miradi yenye bei nzuri na yenye kulipa.
1: mradi wa umeme wa ardhini, wa jua, wind nk
2: mradi wa mawe hapo mchuchuma na liganga
3: mradi wa ujenzi wa nyumba na kuuza
4: mradi wa ujenzi wa fuel stations mbali mbali za magari ya gas, kiwanda cha kubadilisha magari mbali mbali kutumia gas
5: uwekezaji wa vifaa vya ujenzi wa bara bara.
6: ununuzi wa meli kubwa ya kisasa ya uvuvi katika maziwa yetu haya kwenye kina kikuu cha bahari ambapo kuna samaki wa gharama kubwa. Meli za namna hii huwa na kila kitu, kiwanda cha kuchakata na kufungasha samaki kwa grade tofauti tofauti na kuuza nje ya nchi.
6: uwekezaji katika ujenzi wa maghala makubwa ya utunzaji wa mafuta ya petroli na disel inayoweza fanya nchi kuwa hub ya mafuta kwa nchi za africa mashariki.
7: uwekezaji kwenye madini hasa katika kuyachakata,kuweka grade mbali mbali, na kisha kufanyia purity na kutengeneza mikufu,miche ya dhahabu,na kuuza nje ya nchi.
8: ujenzi wa ghala za chakula,kuchakata na kuuza nje ya nchi.
9: ujenzi wa visima vya samaki,kukuza na kuchakata samaki KWA ajili ya kuuza nje ya nchi.
Nadhani wengine watachangia ila vyote hivyo ni gharama kubwa na inayoendana na gharama ya hyo fedha
Nimependa wazo namba 6.
 
Habarini wakuu,

Nina swali zito naombeni majibu yake.

Nimepata mfadhili mmoja katika tafuta zangu. Ameniambia nitafute mradi mmoja wa kuwekeza unaoweza kugharimu billioni 116.

Je, ni mradi gani mmoja mkubwa ambao unaweza kugharimu Tsh. billioni 116.

Niliandika miradi yangu mitatu. Miwili ya mafuta na gesi. Na mmoja wa mambo ya elimu. Ila imeonekana ni midogo. Imeonekana haifiki hata Tsh billioni 10. Hivyo nimepewa nafasi ya kutafuta mradi mwingine.

Najua hapa kuna wakubwa wenye uwezo wa kuwaza kuliko Mimi.

Nipo hapa kupata mawazo yenu

Ahsanteni sana
Kuwa makini. Wewe hapo ndio mradi...Utalia soon
 
Yaani unajifanya mwekezaji wa miradi mikubwa huna hata mentors wa kuksimamia na kukshauri,
Wenzako huwa wanatafuta mpaka kampuni zenye kutoa ushauri juu ya masuala ya uwekezaji!!
We unatuletea futuhi humu ndani, huna hela na wala hujaahidiwa hela. Na kama kweli basi hizo pesa za serikali ipo siku utakamatwa tu
 
Yaani unajifanya mwekezaji wa miradi mikubwa huna hata mentors wa kuksimamia na kukshauri,
Wenzako huwa wanatafuta mpaka kampuni zenye kutoa ushauri juu ya masuala ya uwekezaji!!
We unatuletea futuhi humu ndani, huna hela na wala hujaahidiwa hela. Na kama kweli basi hizo pesa za serikali ipo siku utakamatwa tu
Ahsante sana kwa ushauri wako mzuri boss.
 
Back
Top Bottom