Baadhi ya watz ni watu wa ajabu. Jamaa alinipigia simu anakuja kwenye interview ya kazi nikasema fresh njoo tu nakupokea hakuna shida. Eeehh naenda stendi kumpokea huyu rafiki yangu "Y" naona yuko na mtu mwingine "x" anatufata nyuma nyuma tunaingia kwenye gari naona "x" anaingia nauliza nani huyu ndo jamaa "Y" anasema huyu ni rafiki yangu. Namuuliza je na yeye "X" kaja kwenye interview? Jamaa anasema hapana yeye kaja kutembea tu.
Kufika home yule mwamba X aliyekuja kutembea kumbe anavuta sigara kama kichaaa. Mimi na moshi wa sigara hatupatani hata kidogo mwamba akiingia ndani nyumba nzima moshi unanuka.
Nikamuambia yule mwamba X mimi na sigara hatupatani naomba usivute sigara nyumbani kwangu mwamba akanielewa. Baada ya kufanya interview yule rafiki yangu Y akasema hawezi kuondoka hadi majibu yatoke nikasema fresh. Baada ya majibu kutoka akawa amekosa nafasi nikajua sasa anasepa heee naona siku na kwanza, ya pili, ya tatu wapo tu.
Nikaona yule mwamba Y mvuta fegi ameanza kufukuzia mwanamke nyumba ya jirani ambao tunaheshimiana sana nikaona wema utaniponza. Mimi nika deal na rafiki yangu tu. Nikamwambia sasa mimi nasafiri rafiki yangu akasema we nenda utatukuta tu mkuu ukirudi. Nikamwambia hapana kubaki mimi nasafiri kesho kutwa nyinyi mnaondoka kesho asubuhi mapema. Ndio ulikua mwisho wa mawasiliano.
Sent from my SM-A025F using
JamiiForums mobile app