Mr George Francis
JF-Expert Member
- Jun 27, 2022
- 234
- 376
Habari yako,
Sorry leo nipo hapa katika jukwaa hili naomba ushauri kuhusiana na hili ninalolileta kwako muda huu.
Naitwa Mr George Francis kwa jina maarufu. Kuna dada mmoja anaitwa Latipha niliwahi kusoma nae sekondari. Kipindi hicho tulikuwa na mahusiano lakini tulivyomaliza shule, mahusiano hayo yalipotelea hewani. Yeye alienda Dar es Salaam kwa mama yake, mimi nilibaki hapahapa Singida.
Latipha alizaliwa hapa Sigida lakini mama yake sio mzaliwa wa hapa. Ni mzaliwa wa Tanga lakini alikuja Singida kwasababu ya ndoa. Baba yake ndio Mnyaturu wa hapa. Baada ya kuachana, mama yake aliamua kwenda kujitafutia maisha yake huko Dar es Salaam.
Tangu hapo hatukuwahi kuonana tena kwa zaidi ya miaka kama nane hivi. Mimi sikuwaza kama kuna siku tutakuja kuonana, hata yeye hakuwahi kuwaza. Alikuwa ameamua kuondoka jumla kwasababu aliona ni heri akaishi na mama huko kutakuwa na raha kuliko kubaki na baba yake ambae alikuwa mlevi hana malezi mazuri kwa watoto, yupo bize na mambo yake.
Miaka kadhaa iliyopita, alipata mwanaume hukohuko Dar. Mwanaume huyo ni mwalimu wa shule ya msingi.
Mwaka wa jana mwanzoni mumewe alihamishiwa hapa Singida kikazi ndipo tulipokuja kuonana na Latipha kwa mala nyingine.
Nilijua amekuja tu kumsalimia baba yake kumbe ndio wamehamia jumla. Mimi nilikuwa sijui lakini aliniambia kuwa ameolewa na ana watoto wawili lakini bado ananipenda na miaka yote hiyo alikuwa ananifikiria sana lakini alijua tu labda nilishaoa, hivyo na yeye aliamua kuolewa.
Alivyoniambia kuwa ameolewa, mimi niliamua kumpotezea na kuendelea na maisha yangu. Lakini baada ya miezi michache alinitafuta mwenyewe akaniambia mumewe amebadirika hamuhudumii vizuri kama mwanzo. Siku hizi hamuachii pesa ya matumizi inayotoshereza kwa mahitaji.
Niliamua kumsaidia na kumpa pesa kila alipohitaji msaada wangu. Hata pesa za kubadilisha mavazi ili apendeze nilikuwa nampatia.
Siku moja, aliniambia amemisi penzi langu la zamani hivyo anaomba tukumbushie kidogo. Kusema ukweli sikumkatalia, nilifanya alivyotaka. Tangu hapo tukafufua ule upendo wetu wa zamani.
Nimejikuta nampenda sana Latipha kuliko mwanamke yoyote hapa duniani. Raha anazinipa sijawahi kuzipata popote maishani. Hatakama kwasasa ni mke wa mtu lakini nampenda sana, na yeye pia ananipenda sana. In short, mimi na Latipha tunapendana sana. Hivyo sijali hata kama ameolewa lakini mimi nipo tayari kusimama katika nafasi yangu kama mchepuko wake ninayempenda kwa dhati.
Lakini kuna watu wananionea wivu na kuanza kunitisha eti wanasema mume wake akijua itakuwa msala.
Sasa najiuliza iwe msala kivipi wakati mwanamke kanipenda mwenyewe?
Kwani kuna ubaya gani mimi kupendana na yeye?
Si ni haki yangu, kumpenda mtu yoyote?
Eti jamani? au wewe ndugu msomaji kwa upande wako hili unalionaje?
Naomba ushauri wako tafadhali."
-----------------------
It's me
Mr. George Francis
KWA SIMULIZI NZURI KAMA HII NA STORY KIBAO ZA KUSISIMUA JIUNGE NA GROUP LANGU LA SIMULIZI
JIUNGE HAPA 👇👇
www.facebook.com
Sorry leo nipo hapa katika jukwaa hili naomba ushauri kuhusiana na hili ninalolileta kwako muda huu.
Naitwa Mr George Francis kwa jina maarufu. Kuna dada mmoja anaitwa Latipha niliwahi kusoma nae sekondari. Kipindi hicho tulikuwa na mahusiano lakini tulivyomaliza shule, mahusiano hayo yalipotelea hewani. Yeye alienda Dar es Salaam kwa mama yake, mimi nilibaki hapahapa Singida.
Latipha alizaliwa hapa Sigida lakini mama yake sio mzaliwa wa hapa. Ni mzaliwa wa Tanga lakini alikuja Singida kwasababu ya ndoa. Baba yake ndio Mnyaturu wa hapa. Baada ya kuachana, mama yake aliamua kwenda kujitafutia maisha yake huko Dar es Salaam.
Tangu hapo hatukuwahi kuonana tena kwa zaidi ya miaka kama nane hivi. Mimi sikuwaza kama kuna siku tutakuja kuonana, hata yeye hakuwahi kuwaza. Alikuwa ameamua kuondoka jumla kwasababu aliona ni heri akaishi na mama huko kutakuwa na raha kuliko kubaki na baba yake ambae alikuwa mlevi hana malezi mazuri kwa watoto, yupo bize na mambo yake.
Miaka kadhaa iliyopita, alipata mwanaume hukohuko Dar. Mwanaume huyo ni mwalimu wa shule ya msingi.
Mwaka wa jana mwanzoni mumewe alihamishiwa hapa Singida kikazi ndipo tulipokuja kuonana na Latipha kwa mala nyingine.
Nilijua amekuja tu kumsalimia baba yake kumbe ndio wamehamia jumla. Mimi nilikuwa sijui lakini aliniambia kuwa ameolewa na ana watoto wawili lakini bado ananipenda na miaka yote hiyo alikuwa ananifikiria sana lakini alijua tu labda nilishaoa, hivyo na yeye aliamua kuolewa.
Alivyoniambia kuwa ameolewa, mimi niliamua kumpotezea na kuendelea na maisha yangu. Lakini baada ya miezi michache alinitafuta mwenyewe akaniambia mumewe amebadirika hamuhudumii vizuri kama mwanzo. Siku hizi hamuachii pesa ya matumizi inayotoshereza kwa mahitaji.
Niliamua kumsaidia na kumpa pesa kila alipohitaji msaada wangu. Hata pesa za kubadilisha mavazi ili apendeze nilikuwa nampatia.
Siku moja, aliniambia amemisi penzi langu la zamani hivyo anaomba tukumbushie kidogo. Kusema ukweli sikumkatalia, nilifanya alivyotaka. Tangu hapo tukafufua ule upendo wetu wa zamani.
Nimejikuta nampenda sana Latipha kuliko mwanamke yoyote hapa duniani. Raha anazinipa sijawahi kuzipata popote maishani. Hatakama kwasasa ni mke wa mtu lakini nampenda sana, na yeye pia ananipenda sana. In short, mimi na Latipha tunapendana sana. Hivyo sijali hata kama ameolewa lakini mimi nipo tayari kusimama katika nafasi yangu kama mchepuko wake ninayempenda kwa dhati.
Lakini kuna watu wananionea wivu na kuanza kunitisha eti wanasema mume wake akijua itakuwa msala.
Sasa najiuliza iwe msala kivipi wakati mwanamke kanipenda mwenyewe?
Kwani kuna ubaya gani mimi kupendana na yeye?
Si ni haki yangu, kumpenda mtu yoyote?
Eti jamani? au wewe ndugu msomaji kwa upande wako hili unalionaje?
Naomba ushauri wako tafadhali."
-----------------------
It's me
Mr. George Francis
KWA SIMULIZI NZURI KAMA HII NA STORY KIBAO ZA KUSISIMUA JIUNGE NA GROUP LANGU LA SIMULIZI
JIUNGE HAPA 👇👇
Bei Facebook anmelden
Melde dich bei Facebook an, um dich mit deinen Freunden, deiner Familie und Personen, die du kennst, zu verbinden und Inhalte zu teilen.