Nimepewa lift nikiwa na mtoto wangu, roho imeniuma sana

Nimepewa lift nikiwa na mtoto wangu, roho imeniuma sana

Wewe ndiyo usome vizuri; kaandika raum nyekundu. Kama kiswahili hadi leo hujakielewa, bora urudi kwenu burundi
Sasa hata kusoma huwezi , unachangia mada nini?? RAUM na Rumion, unaona ni kitu kimoja?? ....
 
Kila la kheri mleta mada, maisha mapambano! 😄

Usikute ana changamoto zake zingine zaidi yako pia.!
 
Mimi nikajua roho imekuuma kwa kuogopa jamaa mwenye Raum angekuteka wewe na huyo madogo, kumbe wivu wa jamaa kumiliki ki-Raum ulikutesa.
Raum ni sh. 8-9m tu
Kamanda! Hiyo bei Kama used ya hapa bongo

Ila zile used za japan raum inaenda 14 million
 
Wazima humu?

Mimi huwa na utaratibu wa kutoka na mwanangu asubuhi kumpeleka shule kila siku na huwa natoka nae kuanzia saa moja huwa tunapanda bajaji au bodaboda, sasa leo tukiwa tunatembea kuona kama tutakutana na bajaji ili tupande ndo akapita jamaa na Rumion nyekundu akaniambia panda nikusogeze mpaka stand na sisi tukapanda.

Wakati tumeshuka mwanangu akaniuliza "baba mbona hujamlipa nauli"? Ikabidi nimuongopee tu nikamwambia nimempa ila wewe hukuona.

Niseme tu ukweli japo jamaa kanisaidia ila roho imeniuma sana, manake mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye nguvu kuliko baba za watu wote, mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye hela kuliko baba za watu wote.

Roho imeniuma sio kwa wivu wa chuki kwanini sina gari bali ni kwa wivu wa maendeleo, itabidi nipambane na mimi ili nimpeleke mwanangu shule na usafiri.
kwakwelii ili watoto wetu waache kusema ningezaliwa kwenye familia Ile au ningekua na baba Kam yulee..

tunapaswaa tupambne na MUNGU atusaidiee
 
Wazima humu?

Mimi huwa na utaratibu wa kutoka na mwanangu asubuhi kumpeleka shule kila siku na huwa natoka nae kuanzia saa moja huwa tunapanda bajaji au bodaboda, sasa leo tukiwa tunatembea kuona kama tutakutana na bajaji ili tupande ndo akapita jamaa na Rumion nyekundu akaniambia panda nikusogeze mpaka stand na sisi tukapanda.

Wakati tumeshuka mwanangu akaniuliza "baba mbona hujamlipa nauli"? Ikabidi nimuongopee tu nikamwambia nimempa ila wewe hukuona.

Niseme tu ukweli japo jamaa kanisaidia ila roho imeniuma sana, manake mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye nguvu kuliko baba za watu wote, mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye hela kuliko baba za watu wote.

Roho imeniuma sio kwa wivu wa chuki kwanini sina gari bali ni kwa wivu wa maendeleo, itabidi nipambane na mimi ili nimpeleke mwanangu shule na usafiri.
Ni vizuri kuwa na wivu wa maendeleo

Ila ukijihisi kila kitu huna utakuwa mwizi..
Kila mtu na vipaumbele vyake

We umejenga gari huna, mwenye gari kapanga
 
Wazima humu?

Mimi huwa na utaratibu wa kutoka na mwanangu asubuhi kumpeleka shule kila siku na huwa natoka nae kuanzia saa moja huwa tunapanda bajaji au bodaboda, sasa leo tukiwa tunatembea kuona kama tutakutana na bajaji ili tupande ndo akapita jamaa na Rumion nyekundu akaniambia panda nikusogeze mpaka stand na sisi tukapanda.

Wakati tumeshuka mwanangu akaniuliza "baba mbona hujamlipa nauli"? Ikabidi nimuongopee tu nikamwambia nimempa ila wewe hukuona.

Niseme tu ukweli japo jamaa kanisaidia ila roho imeniuma sana, manake mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye nguvu kuliko baba za watu wote, mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye hela kuliko baba za watu wote.

Roho imeniuma sio kwa wivu wa chuki kwanini sina gari bali ni kwa wivu wa maendeleo, itabidi nipambane na mimi ili nimpeleke mwanangu shule na usafiri.
Wachawi watu wabaya! Unalogwa mpaka kupata gari ni mbinde! Wengine hata kununua TV! Radio! Friji! Freezer! Jiko! Smartphone! Nk, mpaka uombe na kufunga!
 
Nashangaa sana hii tabia ya kumuamini mtu usiemjua anapokupa lift au unaomba lift
Una mtoto halafu unapanda vya bure
Hapo niemeweka risk zaidi maana hata peke yako sio salama kabisa kupanda vya watu

Kama ni psychopath na anakuuwa
Wengine ndio fantasy zao hizo
Mtoto anaekuona shujaa kwa sasa na ukamdanganya
Hivi kama just kama lingetokea mwanao akaachiwa bado ungekua hero wake

Acheni tabia za kupanda vya bure wakati hela mnazo
 
Kwenye dunia ya sasa ilivyopinduka, msaada unaweza kuleta balaa. Ila usikate tamaa, kama kitu unakipenda na nia ipo. Utakipata, utupe mrejesho tu. Mambo huwa yanabadilika sekunde moja, unakuwa mwingine le millionea...
 
Wazima humu?

Mimi huwa na utaratibu wa kutoka na mwanangu asubuhi kumpeleka shule kila siku na huwa natoka nae kuanzia saa moja huwa tunapanda bajaji au bodaboda, sasa leo tukiwa tunatembea kuona kama tutakutana na bajaji ili tupande ndo akapita jamaa na Rumion nyekundu akaniambia panda nikusogeze mpaka stand na sisi tukapanda.

Wakati tumeshuka mwanangu akaniuliza "baba mbona hujamlipa nauli"? Ikabidi nimuongopee tu nikamwambia nimempa ila wewe hukuona.

Niseme tu ukweli japo jamaa kanisaidia ila roho imeniuma sana, manake mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye nguvu kuliko baba za watu wote, mwanangu anajua baba yake ndo mtu mwenye hela kuliko baba za watu wote.

Roho imeniuma sio kwa wivu wa chuki kwanini sina gari bali ni kwa wivu wa maendeleo, itabidi nipambane na mimi ili nimpeleke mwanangu shule na usafiri.
Utapata inshallah mm hata baiskeli Sina ila Mungu ni mwema
 
Back
Top Bottom