Nimepiga marufuku watoto wangu kwenda kanisani

Nakushukuru baba wa mbingu na nchi kwa kuwa mambo haya umeyaficha kwa wenye akili na ukawafunulia walio kama watoto wadogo, naam, ndiyo ilivyokupendeza🙏
 
Nashukuru Mungu kupata wazazi wenye hekima hebu just imagine huyu ndo baba ako 😆
Umepost shule niliyosoma mimi AZABOY na PUGU nikajua una akili kumbe bado we mtumwa wa hizo historia za uongo za kwenye biblia na misahafu unaambia Yesu alipaa mbinguni mara Mtume alienda na farasi mbinguni kuswali na wewe unaamini huku shule ulijifunza Gravitational force.
 
Wanao watabarikiwa nawe utalaaniwa, na huo uamuzi hakika ndo mwanzo wa laana
 
Akishatumika vibaya itam affect nn huyo mtoto
Na vp akifikisha miaka 18 akaamua kuwa nyumbu utafanya nn
Kumpachika mtoto kwenye minyororo ya dini ni sawa kumchagulia mke akiwa mtoto una mlimit machaguzi na hiyo ni kumbagaza mambo ambayo hakuwa na ufahamu nayo.
 
Wanao watabarikiwa nawe utalaaniwa, na huo uamuzi hakika ndo mwanzo wa laana
Upo brain washed sana mnataka maduka yenu(makanisa) yasikose maokoto(sadaka).
Tumestuka muanze kutafuta mashamba na nyie mlime sio kujiombereza mavuno as if mlichangia hata mbolea
 
Imani pekee niliyo nayo ni Juu ya Familia yangu, Wazazi, Mke na Watoto pengine na ndugu wa karbu maana tangu nizaliwe Dini haijawah nisaidia chochote licha ya kwamba mimi nimeusaidia sana kwa kutenga muda na VIBUNDA vyangu ili isonge mbele.

Ni vyema mtu ajifunze dini kwanza aijue ili aikosoe vizuri kishaa aachane nayo kabisa, so waache wajifunze waujue ujinga wa huko huku nawe ukiwafundisha maisha mwisho wataamua wenyewe kuendelea kua wajinga au waelevu.

Kumbuka huna mbingu ya kumpeleka mtu ko tusilazimishane ili siku ya majuto tusilaumiane🤣
 
Yeye anadhani duniani kote ni wajinga, watu tunaenda makanisani kwa sababu za kijamii, hayo mengine unayoubiliwa kwa sasa hayana nafasi kwa maisha ya leo haina tofauti sana na kuendekeza waganga, majini nk
 
Yeye anadhani duniani kote ni wajinga, watu tunaenda makanisani kwa sababu za kijamii, hayo mengine unayoubiliwa kwa sasa hayana nafasi kwa maisha ya leo haina tofauti sana na kuendekeza waganga, majini nk
Mi pia hua naenda church mara moja moja ku "socialize" tu lakini najua kabisa hamna la maana pale. Ni biashara kama biashara zingine.
 
Kwenye kujifunza huko anaweza tekwa tumewahi kusoma na jamaa yangu alikuwa John kisomo mwenzangu si akampenda Yesu akaokoka aloo balaa lililotokea jamaa akashuka kimasomo akadisco akawa complicator akawa mtu wa kushinda kanisani kama zombie.Mpaka leo hii kawa fukara wa kutupwa na Yesu wake
 
Atakwambia vyote watazidishiwa, anautajiri wa rohoni🤣
 
Atakwambia vyote watazidishiwa, anautajiri wa rohoni🤣
Huo utajiri wa kiroho wa kazi gani kama mwili na sura vimechoka ? Mi namuonea huruma kapotea kwenye ramani ya maisha umri umeenda hata kumsaidia naishia kumtumia vi elf 40 na 50
 
Huo utajiri wa kiroho wa kazi gani kama mwili na sura vimechoka ? Mi namuonea huruma kapotea kwenye ramani ya maisha umri umeenda hata kumsaidia naishia kumtumia vi elf 40 na 50
Cha kufanye we mnyime aendelee kula Gombo tuone kama atatoboa🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…