Black Sniper
JF-Expert Member
- Dec 10, 2013
- 32,406
- 55,148
Kuna wanaume wakioa wanabadilika mpaka Kwa ndugu zao, utashangaa mpaka mawasiliano na Kwao anayakata,Matumaini yangu mlio wengi humu ndani mlikua na weekend njema.
Ni miaka sita sasa tangu nimeoa na nimebarikiwa kua na watoto wawili. Kabla sijaoa nilikua nna marafiki wengi na bahati nzuri rafiki hao angalau wanajiweza wao wenyewe na familia zao. Namshukuru sana Mungu kwa ajili yao kwa sababu kwa namna moja au nyingine ndio walionifanya nibadili maisha ya kisela ya kibachela na kuamua nami niwaige kua na familia. Niliona kabisa nahitaji kufanya hivyo ili niendane nao.
Huyu mke wangu anawafahamu vizuri rafiki zangu hata kabla sijamuoa, ingawa kuna tabia alikua anaionesha ya kuchukia/kukasirika hasa nnapomwambia nipo na marafiki zangu au la pale anaponiona na marafiki zangu. Wakija kunitembelea nyumbani alikua anawapokea vizuri na anawachangamkia.
Lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya kufunga nae pingu za maisha.
Anaonesha dhahiri kwamba hawataki rafiki zangu. Hataki waje nyumbani wala hataki mimi niende kuonana nao. Anataka nikitoka kazini moja kwa moja nyumbani, weekends anataka tushinde nyumbani tu. Akisikia hodi ya rafiki yangu yoyote atanuna siku nzima. Anasema wananiharibu, amesahau hao hao ndio walionifanya nimenunua kiwanja na kujenga nyumba, nilinunua gari kwa msaada wa rafiki zangu haohao. Vingi nilivyonavyo nimevipata kwa kua inspired nao.
Hata kumchagua yeye nimuoe, ingawa hajui lakini rafiki hao ndio walinishauri kwamba anafaa zaidi yeye kuliko wengine nilio kua nao. Hataki ndugu, hataki mtu yoyote mgeni zaidi ya rafiki zake au ndugu zake tu.
Kwa sasa rafiki zangu hao pamoja na kumtetea sana mke wangu, wameshagundua kwamba wanajibembeleza sana kuja kwangu. Wote wamekata mguu, imebaki mimi kuwatafuta lakini kila mmoja sasa hivi anaonekana anahamsini zake.
Furaha ya mke wangu ni kuniona mimi tu pembeni yake muda wote. Sina mawazo mapya sababu sijumuiki na wenzangu. Nimekua kama msukule sipati marafiki wapya na niliokua nao hawapo tena.
Hivi majuzi nimepata kibarua mkoani, nimepata angalu muda wa kuwapigia, lakini muamko wao si kama wa zamani.
Naombeni ushauri wenu, nyumba yangu kubwa lakini haivutii kabisa wala siipendi kwa sababu inasisi watu wazima wawili na watoto wawili ambao nao wanashinda shule. Muda mwingi ipo kimya kama wanga vile ππ
Ndugu na jamaa wa pande zote mbili wanapaswa kufika kwenu nanyi pia mnapaswa kufika kwaonikuulize mkuu kwahiyo yeye mwanamke kuleta marafiki zake na ndugu zake ni sawa?
Ndicho anachopitia mleta mada.Sasa kama mke atakataa hadi ndugu zako hapo si unaona shida tayari ndani ya nyumba
Mimi kabla sijaoa nilimuweka mkewangu wazi.Kuna wanaume wakioa wanabadilika mpaka Kwa ndugu zao, utashangaa mpaka mawasiliano na Kwao anayakata,
Ndo maana kabla ya kuoa unashauriwa kama ulikuwa hujamaliza kuwasomesha wadogo zako umalize kwanza maana wanawake si watu wazuri sana
Kaa na mkeo umshauri, asipokuelewa mwitie ndugu zake na zako mumkalishe kikao
Shoga baba yako aliyekuzaa wewe shoga. Kagongwe huko.Ushauri wa kishoga huo huwezi kumwambia hivyo mwanaume eti rafiki zake ni mkewe na watoto wake!!!
Familia yake ipi??Mke ambaye mnaweza achana wakati wowote?Familia yako ndio marafiki wa karibu na wa kweli..ni kitu cha kuzingatia
Hadi ameleta nae humu maana yake amisha zungumz mpaka ameshindwa afanyaje,ndio maana anataka mawazo mbadala sasa ww unasema azungumze.Nimekua muoga sana kushauri mambo ya watu hasahasa mahusiano,kaa zungumza na mkeo haya uliyoaandika hapa mwambie kwa upole atakuelewa tu
Acha uongo mwanamke anaona mbali wapi,utafanikiwaje bila marafiki wala ndugu katika Dunia hiii??Hivi mtu asie weza kufanya maamuzi mwenyewe bila kuwa inspired na watu wengine ana uzima kweli?
Mkeo anakujenga uwe baba bora na imara uwe na decision making ya kwako peke yako we uko bize kulilia marafiki.
Kuna marafiki wengine hawapendi ufanikiwe.
Na nikupe siri leo; mwanamke ni kiumbe anaeona mbali sana hivyo akikwambia kitu sidhani kama ni kwa ubaya. Jitegemee
Huyo jamaa sio wewe Mkuu ? π€£ππ€£ au wewe ni Kataa ndoaUmeshayakanyaga amini kwamba mkeo ana roho mbaya yachoyo na ubinafsi uliokubuhu, unajua ni kwanini? Kwa sababu kwake yeye anaona ni sawa kuwa karibu na ndugu na marafiki lakini kwako anaumia, huyo ni zaidi ya mchawi.
Kuna jamaa yangu nae n hivyo hivyo, mkewe ana kiroho kunguni kama hicho lakini wakipata shida mbio kwa marafiki shida ikikata ndio basi, mwanamke saa 12 jion anataka jamaa awe ndani na jamaa anafyata.
Duh!Kama hao marafiki zako ndio walikuchagulia mke huyo basi ni kweli rafiki zako hawafai ππ€£
Wamekupa mke mbovj asiependa marafiki wala ndugu zako.
Mkuu, wanawake tuko hivyo japo mkeo amezidi. Kinachoumiza ni kwamba mkiwa na hao marafiki zenu mnatusahau kwa muda, kwa jinsi tunavyopenda attention hilo linaumiza.Matumaini yangu mlio wengi humu ndani mlikua na weekend njema.
Ni miaka sita sasa tangu nimeoa na nimebarikiwa kua na watoto wawili. Kabla sijaoa nilikua nna marafiki wengi na bahati nzuri rafiki hao angalau wanajiweza wao wenyewe na familia zao. Namshukuru sana Mungu kwa ajili yao kwa sababu kwa namna moja au nyingine ndio walionifanya nibadili maisha ya kisela ya kibachela na kuamua nami niwaige kua na familia. Niliona kabisa nahitaji kufanya hivyo ili niendane nao.
Huyu mke wangu anawafahamu vizuri rafiki zangu hata kabla sijamuoa, ingawa kuna tabia alikua anaionesha ya kuchukia/kukasirika hasa nnapomwambia nipo na marafiki zangu au la pale anaponiona na marafiki zangu. Wakija kunitembelea nyumbani alikua anawapokea vizuri na anawachangamkia.
Lakini mambo yalibadilika ghafla baada ya kufunga nae pingu za maisha.
Anaonesha dhahiri kwamba hawataki rafiki zangu. Hataki waje nyumbani wala hataki mimi niende kuonana nao. Anataka nikitoka kazini moja kwa moja nyumbani, weekends anataka tushinde nyumbani tu. Akisikia hodi ya rafiki yangu yoyote atanuna siku nzima. Anasema wananiharibu, amesahau hao hao ndio walionifanya nimenunua kiwanja na kujenga nyumba, nilinunua gari kwa msaada wa rafiki zangu haohao. Vingi nilivyonavyo nimevipata kwa kua inspired nao.
Hata kumchagua yeye nimuoe, ingawa hajui lakini rafiki hao ndio walinishauri kwamba anafaa zaidi yeye kuliko wengine nilio kua nao. Hataki ndugu, hataki mtu yoyote mgeni zaidi ya rafiki zake au ndugu zake tu.
Kwa sasa rafiki zangu hao pamoja na kumtetea sana mke wangu, wameshagundua kwamba wanajibembeleza sana kuja kwangu. Wote wamekata mguu, imebaki mimi kuwatafuta lakini kila mmoja sasa hivi anaonekana anahamsini zake.
Furaha ya mke wangu ni kuniona mimi tu pembeni yake muda wote. Sina mawazo mapya sababu sijumuiki na wenzangu. Nimekua kama msukule sipati marafiki wapya na niliokua nao hawapo tena.
Hivi majuzi nimepata kibarua mkoani, nimepata angalu muda wa kuwapigia, lakini muamko wao si kama wa zamani.
Naombeni ushauri wenu, nyumba yangu kubwa lakini haivutii kabisa wala siipendi kwa sababu inasisi watu wazima wawili na watoto wawili ambao nao wanashinda shule. Muda mwingi ipo kimya kama wanga vile ππ
Shida ni kuwa mkewe hajavunja cycle za upande wake (marafiki zake na ndugu zake) mke wa namna hiyo ni mbinafsi hafai.Mkuu trust me,utatajirika na huyo mkeo kavunja cycle ya marafiki zako ambao kwake hajawaelewa.
Pambana