Nimeshangaa kumuona Profesa mmoja maarufu wa pale UDSM akisali sala ya Bikira Maria

Nimeshangaa kumuona Profesa mmoja maarufu wa pale UDSM akisali sala ya Bikira Maria

Maria hakuwahi wala hatawahi kuwa mama wa Mungu , maria alizaa human flesh ambayo ilitumiwa na mungu mwana Yesu

Hakuna anayekataa Hilo

Aliyezaliwa ni Kristo na Yesu ni Mungu aliyetenda kazi ndani yake
 
Kila neno la Mungu kwenye biblia linatumika kiimani kutufundisha
Madam naona unaepuka swali la muhimu sana. Maria hana uwezo wa kuwepo sehemu mbili kwa wakati mmoja hivyo kusema huyo awaombee ni kukosa ufahamu.

Mungu peke yake ndio anaweza kuwepo maeneo yote ya ulimwengu mzima kwa wakati mmoja huku akifahamu kila kitu.
 
Madam naona unaepuka swali la muhimu sana. Maria hana uwezo wa kuwepo sehemu mbili kwa wakati mmoja hivyo kusema huyo awaombee ni kukosa ufahamu.
Mungu peke yake ndio anaweza kuwepo maeneo yote ya ulimwengu mzima kwa wakati mmoja huku akifahamu kila kitu.

Hakuna kisichoeleweka ila hakuna anayekulazimisha kuamini imani za wengine. Na huna haja ya kuwatusi kwa kile kisichokudhuru.

Wapo wanaoamini hadi wanyama kwamba wanaweza kuwasaidia na wana haki sawa mbele ya sheria kadri ya imani zao

Mimi binafsi naamini Yohana 14:13-14
"Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya."
 
Kwanza huwa nakushangaeni sana watu wa dizaini yako, huwa mnawashwa wapi kufatilia imani za watu?
Kwani lazima uamini anachoamini mtu mwingine?
Tuache tuendeelee kumheshimu Mama wa Mungu,na kwa taarifa yako tu, TZ iliwekwa chini ya ulinzi wa Mama Bikira Maria.
Atawalinda wanaomwamini na kumwabudu. Sitaki kuhusishwa na Nafsi hiyo ya mwanamke wa Ufunuo 12:1....
 
Kwamba kumpelekea Mwamposa Tsh 100,000/= akuombee siyo kosa?

Au kwa sababu anajiita mtume?
Jadili hoja,Je,Mungu ana mama yake?
Tumuombe&kumuabudu mtu badala ya Mungu?
Kuna mahala nimemtaja Mwamposa?
Ny_u mkubwa wewe😂😂
 
Kwa mlinganisho huu nilitegemea nyani ndo wawe na hizi imani kwa hali ya juu ila sijawahi kuona popote nyani anasali
Mkuu, Almost viumbe wote wenye frontal lobe wana exhibit hizi imani.
Sema kadri kiumbe anavyozidi kuwa na frontal lobe kubwa ndio hizi imani zinakuwa complicated zaidi.

Lakini essence ya hizi imani ni moja...Essense ya kuwa nikifanya kitu A kitaniletea kitu B...ambapo unakuta A na B havina uhusiano wowote kabisa(causal relationship).

Mfano in the wild, nyani huko senegal wameshaonekana wakifanya rituals kama kuponda mawe mti, kila nyani ana mti wake wa kuponda nk. So kuna association wanaamini kuponda miti na imani fulan kma kupata chakula etc... Ukisoma Kazi za Jane Goodal ameelezea deeply tabia ritualistic za nyani.

Ukija maabara kuna experiments nyingi zimeshafanywa kwa Kunguru, Panya, dolphins nk.

Mfano, 1948 famous psychologist B.F Skinner alifanya experiment na njiwa waliokuwa half-starved..Aliwaweka bandani halafu akawa anawapa chakula kila baada ya sekunde kadhaa at a constant interval..As long as ile interval ni fupi, wale njiwa wakaanza kutengeneza behaviours kama kugeuza geuza vichwa, kuzunguka clockwise, kujigeuza geuza chini, kupiga mabawa nk. wakiamini hizo tabia ndo zitaleta chakula.
Baada ya hizo tabia kujengeka hata wakiongeza interval ya kuleta chakula wale njiwa wataendelea kufanya hizo behaviours. Ambapo skinner akiacha kuleta chakula njiwa wanaonekana kama wajinga fulan.

Hii experiment Michael wa Vsauce aliifanya mwaka juzi kwa BINADAMU..mtu anawekwa katika chumba chenye tundu.. halafu kila baada ya sekunde 30 hilo tundu linatoa hela..Sasa wale watu walikuwa wakikaa mule kwenye chumba wanaanza kutengeneza behaviours ambazo waliamini wakifanya ndo zinaleta hela, Kuna wengine waliruka ruka, wengine walizunguka zunguka chumba, wengine walicheza na wengine walichuchumaa. Cheki hapa

So wanyama wengi huwa hatupendi kuwa confused au kukosa control ya matokeo katika mazingira yetu..So instead ya kukubali hatuna control ni bora tutengeneze kitabia/matendo fulani ambayo yatatuaminisha tunayo control hata kama hatuna.
Mfano.
-Kucheza ngoma au kusafisha makaburi li mvua inyeshe
-Kuvaa nguo fulan unapoenda interview
-mchezaji kuchimba chini kabla ya mechi
-Kuvaa nguo/viatu fulani ili timu yako unayoshabikia ishinde (Mimi nilishawahi kudevelop ka tabia kuwa nikienda banda fulani barcelona lazima ishinde)
-Kuweka kakifaa upande fulan dukani ili wateja waongezeke
-Kupiga magoti na kuomba kwa invisible man/woman(Maria)in the sky ili akusaidie jambo fulani nk. Nk.


Sasa hii inashangaza kuwa pamoja na kuwa sisi homo sapiens tumedevelop sana sehemu ya ubongo inayodeal na logic na reasoning, bado we fall prey to these archaic beleif systems.
 
Hakuna sehemu nimemtusi mtu yeyote. Nilichofanya ni kushangaa jambo hilo linalofanywa.
tena unamshangaa Profesa! Ina maana haujui pale UDSM ipo parokia kabisa? Utawashangaa wangapi sasa kwa mtindo huo, maana Wakatoliki wapo wa kutosha tu na hadi wakati fulani kuna mapadri wawili walikuwa ni wahadhiri wa UDSM, nahisi ukiendelea kwenda kwenda UDSM kwa muda wa kutosha pale utakuwa unaishia kushangaa shangaa
 
tena unamshangaa Profesa! Ina maana haujui pale UDSM ipo parokia kabisa? Utawashangaa wangapi sasa kwa mtindo huo, maana Wakatoliki wapo wa kutosha tu na hadi wakati fulani kuna mapadri wawili walikuwa ni wahadhiri wa UDSM, nahisi ukiendelea kwenda kwenda UDSM kwa muda wa kutosha pale utakuwa unaishia kushangaa shangaa
Kijana unateseka sana bila sababu. Ni lazima uchague kati ya kufuata neno la Mungu katika biblia au ufuate mapokeo ya hapa na pale ya hao wakatoliki.

Kufuata mapokeo zaidi ya neno la Mungu sio jambo jipya maana hata Yesu mwenyewe alilikuta kwa wayahudi. Lakini mwisho wa yote hukumu inakuja kwa kufuata neno.
 
Kijana unateseka sana bila sababu. Ni lazima uchague kati ya kufuata neno la Mungu katika biblia au ufuate mapokeo ya hapa na pale ya hao wakatoliki.
Usichokijua ni kwamba hata Biblia iliandikwa kutokana na mapokeo (tena ya Wakatoliki). Uwe unafuatilia walau kidogo historia ya Biblia (na hapa ndipo umuhimu wa kusoma Theology kwa wale wanaotaka kuhubiri unapoonekana, na hata kuwa na elimu ya dunia kwa kiwango fulani, walau shahada ya kwanza). Pengine unadhani Biblia iliandikwa instantly wakati matukio yanatokea. Wataalamu wa maandishi wanaeleza kuwa Injili iliandikwa kati ya miaka 70 AD hadi 110 AD. Biblia yenyewe inatamka kuwa yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu lakini hayakuandikwa:

Yohana 21:25
Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.
 
Profesa kwenye eneo lipi. Unaweza ukawa profesa wa siasa kwenye kilimo ukawa sifuri. Au wa uchumi kwenye dini ukawa sifuri kabisa
 
Hili la sisi wakatoliki kumuomba Bikira Maria na watatifu wengine lina ukakasi haieleweki kibiblia. Thus watu wanasali katoliki tuition wanaenda kwa Walokole
 
Usichokijua ni kwamba hata Biblia iliandikwa kutokana na mapokeo (tena ya Wakatoliki). Uwe unafuatilia walau kidogo historia ya Biblia (na hapa ndipo umuhimu wa kusoma Theology kwa wale wanaotaka kuhubiri unapoonekana, na hata kuwa na elimu ya dunia kwa kiwango fulani, walau shahada ya kwanza).
Hata historia ya kanisa huifahamu. Kuna tofauti kati ya catholic (kanisa la ulimwengu) na roman catholic (mkusanyiko wa wapagani wanaojiita kanisa).

Constantine ndio aliyeanzisha roman catholic ambayo ilikuwa corrupt tangu inaanza na kipindi inaanzishwa tayari biblia ilishakuwa iko kamili ikiwa na vitabu 66 alivyovifanyia compilation Jerome.
Pengine unadhani Biblia iliandikwa instantly wakati matukio yanatokea. Wataalamu wa maandishi wanaeleza kuwa Injili iliandikwa kati ya miaka 70 AD hadi 110 AD.
Sio kweli, Marko imeandikwa AD 54 na injili ya mwisho ya Yohana inakadiriwa ilikuwa imeshaandikwa kufikia AD 90.

Nyaraka ndio ziliandikwa mapema zaidi maana Paulo alikufa mwaka 64AD na hapo alikuwa ameshaandika zote zakwake hadi mtume Petro tayari alikuwa amewahi kuzisoma kabla hajaandika nyaraka zake na ukumbuke mtume Petro naye alikufa around AD 64 na 66.
Biblia yenyewe inatamka kuwa yapo mambo mengi aliyoyafanya Yesu lakini hayakuandikwa:

Yohana 21:25
Kuna na mambo mengi aliyoyafanya Yesu; ambayo yakiandikwa moja moja, nadhani hata ulimwengu usingetosha kwa vile vitabu vitakavyoandikwa.
Kwahiyo nyie mmeamua kufuata yale yasiyoandikwa ambayo hayajulikani?,😂 Hebu acheni uasi, mnaongeza maneno na hukumu yenu inaongezeka.
 
Sio kweli, Marko imeandikwa AD 54 na injili ya mwisho ya Yohana inakadiriwa ilikuwa imeshaandikwa kufikia AD 90.
Haya shikilia hapa kwanza. Je, 54 AD na 90 AD zilikuwa bado ni nyakati za Yesu? Kama enzi za Yesu zilikuwa zimeshapita, hayo sio mapokeo?
 
Nilitegemea labda utaleta maandiko ya kibiblia lakini naona umeishia kuweka msimamo wa kidini.

Mimi nilichofanya ni kushangaa tu kwasababu nimeona ni jambo la ajabu na halipo kwenye maandiko.

Naheshimu imani yako, fainali siku ya mauti.
Endelea tu kushangaa...itakusaidia...na huna cha kufanya zaidi ya kushangaa..
 
Back
Top Bottom