Prof Koboko
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 350
- 2,550
Nimemshangaa Mufti Abubakar Zuberi kwa maneno yake baada ya kukutana na Mhe Rais kuhusu Mhe Freeman Mbowe. Yaani kiongozi mkubwa kama mufti unaongea maneno ya uoga uoga na kujipendekeza eti Rais awasamehe kina Mbowe eti wakirudia tena wachukuliwe hatua.
Yaani kiongozi anayewaza adhabu tu wakati wote badala ya huruma na misingi ya tatizo ni mbaya sana. Huyu mufti ana roho mbaya sana pamoja na tunajua ndiyo ni kada wa CCM. Anajivunija tu heshima sana, sijui hajui nini aongee mbele ya macho ya umma. Au yawezekana haya mambo ya kimahakama hajui kitu na hata kesi zinazosemwa hazijui na hana uelewa nazo. Hivi hua hawangalii kina Dr Shoo wanaongeaje?
Unaambiwa mtu ameshtakiwa makosa yote ni kesi ya Kubumba wewe unaropoka tu, hujui kulimbikiza mtu kesi ni dhambi? Asemehewe amekosea kipi wakati hata hukumu bado? Wasubiri Mbowe afungwe jela kwa hukumu ndiyo waniombee msamaha.
Kiongozi mwenye busara angeomba busara zitumike katika kufungua na kuendesha kesi, maana yake kesi zisiendeshwe kisiasa. Eti mtu ananyanyuka bila hata haya wasamehewe, wamekosa nini?
Yaani yeye yupo kimaslahi tu hata delegations za nafasi yake hazijui. Mtu unazungumzia kitu hujui msingi wake wala outcome ya utakachosema unaropoka tu.
Kwakweli Waislam kwa huyu kiongozi tumepigwa. Hakuna kiongozi hapa na huu ndio ukweli. Ifike mahali uchaguaji viongozi wa nafasi uangalie wenye elimu zote, wenye experience kwenye mambo yote.
Siye hawa walimu wa madrassa ambao mtu anapewa nafasi hajui azungumze nini anajikuta anaropoka tu.
Yaani kiongozi anayewaza adhabu tu wakati wote badala ya huruma na misingi ya tatizo ni mbaya sana. Huyu mufti ana roho mbaya sana pamoja na tunajua ndiyo ni kada wa CCM. Anajivunija tu heshima sana, sijui hajui nini aongee mbele ya macho ya umma. Au yawezekana haya mambo ya kimahakama hajui kitu na hata kesi zinazosemwa hazijui na hana uelewa nazo. Hivi hua hawangalii kina Dr Shoo wanaongeaje?
Unaambiwa mtu ameshtakiwa makosa yote ni kesi ya Kubumba wewe unaropoka tu, hujui kulimbikiza mtu kesi ni dhambi? Asemehewe amekosea kipi wakati hata hukumu bado? Wasubiri Mbowe afungwe jela kwa hukumu ndiyo waniombee msamaha.
Kiongozi mwenye busara angeomba busara zitumike katika kufungua na kuendesha kesi, maana yake kesi zisiendeshwe kisiasa. Eti mtu ananyanyuka bila hata haya wasamehewe, wamekosa nini?
Yaani yeye yupo kimaslahi tu hata delegations za nafasi yake hazijui. Mtu unazungumzia kitu hujui msingi wake wala outcome ya utakachosema unaropoka tu.
Kwakweli Waislam kwa huyu kiongozi tumepigwa. Hakuna kiongozi hapa na huu ndio ukweli. Ifike mahali uchaguaji viongozi wa nafasi uangalie wenye elimu zote, wenye experience kwenye mambo yote.
Siye hawa walimu wa madrassa ambao mtu anapewa nafasi hajui azungumze nini anajikuta anaropoka tu.