Nimeshangazwa na kauli ya Rais kudharau msimamo wa Waziri wa Kilimo juu ya kuzuia uagizaji wa sukari nje

Wewe naona haujamwelewa Waziri Mkenda, kasema kama kutakuwa na upungufu vibali watapewa wazalishaji,yahani wenye viwanda,sio wafanyabiashara.
 
FTA au Face Threatening Act proper response yake ni kuapply Positive Face ukikaa kimya unajichoresha, waziri kama ni muungwana ajiudhuru.atajenga haiba yake
 
..Waziri wa kilimo Prof.Mkenda akizungumzia sukari.



..Naibu waziri wa kilimo Hussein Bashe akizungumzia sukari.

 
Elimu elimu elimu
 
Hapa kuna tatizo. Si kawaida Rais, Waziri Mkuu na Waziri kutofautiana wakati wote wanatumikia serikali moja na wana kila fursa ya kuweza kuwasiliana kabla ya kutoa msimamo. Naona hapa Rais amechemsha kweli kweli. Anaonyesha alivyo mtupu kwa kiwango kikubwa. Nadhani ingekuwa vizuri wahusika wote wajiuzulu. Nasema hivi kuepuka mmoja kutumia mamlaka yake kuwaumiza wengine. Hapa kuna tatizo. Rais hata hajui sheria inasema nini! Je anapata faida gani au amepewa kitu au hii biashara ni ya watu wake au ndugu zake?
 
Absolutely!
 
Kwani aliesema Sukari isinunuliwe Nje ni Waziri mkuu au Waziri wa kilimo????
 
Na mimi namshauri Mh. Mkenda kujiuzulu ili kulinda heshima yake.
 
Mpaka akili ziwakae sawa. Twende tu mwendo uwe ni huu huu
 
Waziri hana mamlaka ya kuweka sera kama yake waziri anatekeleza yanayoamuliwa na baraza la mawaziri au sera ya serikali. sasa ajibu aliambiwa na nani hatununui sukari ya Uganda au ilikuwa uamuzi wake yeye
Hakusema hatutanunua, alichosisitiza ni kwamba tutanunua tukiwa na uhitaji yaani patakapotokea upungufu na kwamba kibali kitatolewa kwa wale wazalishaji wa sukari tu na sio kwa mfanyabiashara ambaye hazalishi sukari. Sasa hapo kosa lake lipo wapi?
 
Mwenye kosa ndio alaumiwe. Makosa makubwa ya Prof. Mkenda; Waziri wa Kilimo hadi akaambiwa hoja zake (sio yeye binafsi) ni nonsense yanatokana na:

1. Kuishi kwa Kukariri na kutotambua majira
Hizo sera anazozozitetea za ''Protectionism'' tuliziacha toka March 2021. Kila kiongozi ana falsafa zake na maono yake, na bahati nzuri Rais Samia amekuwa wazi sana kuhusu sera za kuifungua nchi. Huyu mwenzetu alikuwa bado yupo kwenye zama za awamu ya tano.

2. Kuvuka mpaka wa majukumu yake

Waziri wa Kilimo ni nafasi ya ndani ya nchi, hata Zanzabar hapo hana mamlaka. Amepata wapi audacity ya kuzungumzia sera za nchi dhidi ya nchi nyingine. Je yeye ndiye mhimili wa diplomasia ya nchi. Mwenye dhamana ya kwanza linapokuja suala la mahusiano iwe ya kibiashara au vyovyote katika ya nchi na nchi ni RAIS mwenyewe au msaidizi wake Waziri wa Mambo ya nje. Ambaye naye huzungumza kwa niaba ya Rais; hata Waziri Mkuu au Makamu wa Rais hawezi kuzungumza suala la nchi na nchi bila idhini ya Rais wa nchi. Sasa huyu mwenzetu huo ujasiri aliotoa wapi? kama sio kudhani mambo ni kama juzi.

Rais wetu hapati hata muda wa kupumzika kila siku anafanya diplomasia ndani na nje ya nchi. Akirudi Ikulu hakuna kupumzika ni mlolongo wa mikutano kila siku ya kidiplomasia na uchumi ili kuifungua nchi ambayo ki ukweli mahusiano na nchi na taasisi nyingi hayakuwa mazuri. Mama halali usingizi, kutia uzito anaona aende mwenyewe maana ni ngumu mtu mwingine kuaminika maana mambo ya nyuma yaliamuliwa na sitting president. Hivyo, lazima Rais mwenyewe aende ili kujenga imani. Chuma hutolewa na chuma.

Rais anafanya jitihada hizi halafu anatokea mtu anasema '' MIMI SITAFANYA'' wewe ni nani useme hivyo? ni utashi wako au utashi wa nchi?

Tuwe makini sana, nchi sasa hivi iko kwenye paradigm shift mambo makubwa ya kisera ni vyema kufanya consultations na wakuu kabla ya kutoa matamko.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…