Nimeshangazwa na kauli ya Waziri mwenye dhamana ya mitandao ya kijamii kuwa kura zipo mitaani sio mitandaoni

Idugunde

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2020
Posts
6,404
Reaction score
6,969
Your browser is not able to display this video.

Kauli zingine zinafikirisha sana.

Maana dunia ya leo kila kitu kipo kidijitali.

Maoni ya watu wananapiga kelele kupitia mitandao ya kijamii. Watawala wanaumia.

Hao hao wanaopiga kelele mitandaoni wanaishi mitaani.

Alafu waziri aliye na digrii anasema hawapigi kura.

Inashangaza.
 
Vya kushangaza ni vingi

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usiseme uongo, sema alichokisema, kasema hao ni asilimia 16 tu na kati ya hao 40% wapo nje ya Tanzania.

Nini ambacho hukuelewa hapo au ni lazima u twist?
 
Sasa ikifika uchaguzi wanafungia mitandao ya nini na kwanini? Kikwete 2005 alishinda kwa kishindo kuliko 2010 ambapo kula zilishuka utafiti ukaonyesha kuwa asilimia kubwa ya kushuka kwa kura ni kutokana na hamasa za mitandaoni, juzi tu rais kasema ameunda kikosi cha kuangalia mitandaoni hapo bado mtamuamini Nape?
 
Mkuu
Huko mitaani kwa moto sasa.

Hata mie natumia muda mwingi mtaani kuwaeleza watanzania wenzangu uovu wa CCM
 
Inamaana nayeye hapigi kura sababu yuko mtandaoni miccm akili ya kuku,na kwanini wanakimbilia kufunga mitandao wakati wa uchaguzi kama hakuna wapiga kura humu
 
Hiyo digrii unayoizungumzia ni ya kimchongo kinoma aliipata kule Bangalow, India.
BOngo kupata maendeleo ni ndoto za mchana kwasabb tunaongozwa na wenye akili za kawaida, uwezo wao wa kuwaza na kuja na suluhisho la matatizo ya wananchi ni finyu!.
 
Body language: ukiangalia yule anayeambiwa anajua kabisa anadanganywa. Lakini IQ zao si mbali, huyu anayesema maneno haya hajui kama anadanganya. Hapo ndiyo Tanzania ilipofika, ……… imagine hao wawili uwabadirishe mmoja Nyerere na mwingine Mwakawago

Tanzania kwisney
 
Nilichogundua baada ya kuangalia hii clip ni kwamba body language ya samia haiendani na wimbo anaouimba nape.

Maana yake ni nini..
1. Ameshatambua wanamdanganya sana na wanampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
2. Amegundua wapo kimaslahi zaidi na wanalinda matumbo yao.
3. Anajua huyo nape hamfai ila hakuna namna ya kumtoa..watamuendeshea fitina ambazo hataweza kupambana nazo..maana hilo ni zao la kinana na kikwete.
4. Huyu mama ni muumini wa mitandao toka siku alipotawazwa na anaiamini mitandao kuliko hao watu..kuambiwa apuuze mitandao inamchanganya sana maana anajua mitandao inafika duniani kwa haraka kuliko hao watu wa tandahimba..kuna wakati alipangua watu kwa kusoma mitandaoni tu.
5. Anaona kiza zaidi mbele kwenye safari yake ya kiuongozi kwa kushirikiana na hawa watu ambao mwanzoni alidhani watamfaa. Ni kama mwisho wa siku ama aamue kutogombea au apokee urais wa dhulma kwa maslahi ya kikundi kidogo cha watu fulani.

Kazi ipo..

Sent from my SM-A225F using JamiiForums mobile app
 
Wewe ni mjinga wa statistics....huju what level of confidence & std error of estimate inference is drawn....nyie memorize tuu "anaupiga mwingi"
Wewe bingwa wa statistics, Mbarali jana ni bashraf tu, mziki kamili waja soon.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…