Nimeshindwa kuelewa formula ya mahesabu ya mikopo ya benki hii

Nimeshindwa kuelewa formula ya mahesabu ya mikopo ya benki hii

kidadari

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2012
Posts
8,647
Reaction score
9,604
Nimeenda benki fulani kwa uhitaji wa mkopo wa 8.4m wakanimbia riba 18%.

Baada ya kupewa makato yakawa 195,820 kwa mwezi kwa miaka 6. Sasa nawauliza mbona kiuhalisia sio 18% kama wanavyotuambia kwenye matangazo yao? Wanajibu kwa mujibu wa calculator yao ipo sahihi, hapa ina maana mpaka marejesho itakua ni 14,099,040 ndani ya miaka 6.

Hawa jamaa wanatumia formula gani kufanya calculations zao, kuna dalili ya wengi kupigwa maana kuna usiri mwingi sana. Ni vizuri ikawekwa wazi ili kabla hujaenda kuchukua mkopo ujue na marejesho yake yatakuwa vipi.
 
Kwa haraka haraka itakuwa 18% kwa mwaka na si 18% kwa muda wote
wa mkopo.

Hapo wakaipeleka miaka 6 na wakapunguza kidogo ili usione unalipa mkopo kwa riba ya 100%.
Yani kihasara hasara wapunguze milioni3 nzima?
 
Acha kabisa.

Wana katabia fulani hivi riba ni 2.8% p.m....
Hawana tofauti na wezi au matapeli..ukiona riba 18% unaandaa mipango yako ukijua unapata hela kwa riba nafuu ukifika kule unapewa marejesho ya tofauti kabisa. Hata kwenye seminar zao hawaweki wazi formula zao ili wateja wazijue
 
Wana aina flani ya uyapeli ndo maana hawaweki wazi mahesabu yao
... halafu msimamizi mkuu wa mabenki yaani BoT yupo tu! Mtunga sera wa sekta ya fedha yaani wizara ya fedha yeye yupo tu anakimbizana na makusanyo kupitia mwanae TRA!
 
Kwa haraka haraka itakuwa 18% kwa mwaka na si 18% kwa muda wote
wa mkopo.

Hapo wakaipeleka miaka 6 na wakapunguza kidogo ili usione unalipa mkopo kwa riba ya 100%.
Amu on the beat
 
Jamani mbona BOT na wizara husika mpo kimya huku mabenki yakifanya utapeli huu. Kwa nini wasitoe angalau mchanganuo ambao unaeleweka kirahisi kwa wateja, mfano. ukikopa milioni 10 utakatwa kiasi gani kila mwezi kwa mwaka, miaka 2, mitatu nk. siyo kuficha ficha mtu anakuja kushangaa makato makubwa kwenye mapato yake ya mwezi kuliko alivyo tarajia.
 
Tumia Excel kufanya mahesabu ya mkopo wako, kwa kutumia loan amortization schedule, Kama ni ngumu unaweza unaweza Google formula ya mkopo. Nimeangalia hiyo iko sawa tu , riba ni 18% kwa mwaka, hakuna wizi hapo
 
Back
Top Bottom