Nimeshuhudia mtu akiwanga, hili limenitisha

Nimeshuhudia mtu akiwanga, hili limenitisha

Half american

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
38,283
Reaction score
97,793
Herini ya sikukuu ya Noeli, kwangu naona ilishakuwa mbaya kwa mfululizo wa yanayoendelea na hili lililonifanya niandike hapa muda huu.

Kwanza nianze kwa kusema sina utulivu kabisa usingizi umekata na hauwezi kuja kwahiyo kama ntakosea kwenye kuandika mnivumilie.

Ipo hivi nilikuwa ndotoni ghafla nikashtuka muda ilikuwa saa 04:24 alfajiri, nilivyoshtuka naona reflections za mwanga wa moto, nikajua labda ni mwanga wa taa za gari lakini moyo ukasita kuliamini hilo kwa kuwa mwanga wa gari huwa ni mkali zaidi,

Nikiwa bado kitandani nashangaa zile reflections ghafla zikaanza kumove na kupotea, nikasogeza kapazia kidogo nione nje kinachoendelea. Nimeona moshi unafoka na nikapigia mstari majibu yangu kuwa ule ni moto.

Moyo ukapiga paa!! Nikazungusha macho upande wa pili wa dirisha nikaangalia kwa kunata bila kupepesa macho kama sekunde 40 na kushuhudia mtu kwa mbali kama kapigwa na butwaa akitazama uelekeo wangu kama vile ameniona (ni kama mita 10-15 kutoka nyumba ilipo) ila sikumtambua ni nani kutokana na giza.

Baada ya kuona vile nikarudishia pazia nimefanya maombi na ninaamini nipo salama ila hili limenishtua kwa kiasi fulani.

Wakuu nifanye nini zaidi?

Kuna madhara yeyote kushuhudia hilo?
Mshana Jr muongozo wako ni muhimu mkuu nna taharuki kwa lililotokea.
 
Herini ya sikukuu ya Noeli, kwangu naona ilishakuwa mbaya kwa mfululizo wa yanayoendelea na hili lililonifanya niandike hapa muda huu.

Kwanza nianze kwa kusema sina utulivu kabisa usingizi umekata na hauwezi kuja kwahiyo kama ntakosea kwenye kuandika mnivumilie.

Ipo hivi nilikuwa ndotoni ghafla nikashtuka muda ilikuwa saa 04:24 , nilivyoshtuka naona reflections za mwanga wa moto, nikajua labda n mwanga wa taa za gari lakini moyo ukasita kuliamini hilo kwa kuwa mwanga wa gari huwa ni mkali zaidi, nikiwa bado kitandani nashangaa zile reflections ghafla zikaanza kumove na kupotea, nikasogeza kapazia kidogo nione nje kinachoendelea. Nimeona moshi unafoka na nikapigia mstari majibu yangu kuwa ule ni moto.

Moyo ukapiga paa!! Nikazungusha macho upande wa pili wa dirisha nikaangalia kwa kunata bila kupepesa macho kama sekunde 40 na kushuhudia mtu kwa mbali kama kapigwa na butwaa akitazama uelekeo wangu kama vile ameniona (ni kama mita 10-15 kutoka nyumba ilipo) ila sikumtambua ni nani kutokana na giza. Baada ya kuona vile nikarudishia pazia nimefanya maombi na ninaamini nipo salama ila hili limenishtua kwa kiasi fulani.
Wakuu nifanye nini zaidi?
Kuna madhara yeyote kushuhudia hilo?
Mshana Jr muongozo wako ni muhimu mkuu nna taharuki kwa lililotokea.
Cha kufanya hapo ni kutokuwa na wasiwasi wowote ule kwa sababu hayo mambo, kiuhalisia hayapo.

Watu huwa wanadanganywa na kudanganyana tu na kuishia kuogopa mambo yasiyo na uhalisia wowote ule.

Halafu hao wanga naona huwa wanajua kusoma saikolojia za watu.

Kwa nini waje kwako ilhali mtu kama mimi ambaye nawatukana kila siku na kuwakebehi, wakati mwingine hadi naenda huko kwenye makao makuu yao, hawanijaribu?

Kuna ofa yao humu na nje ya humu pia, kwamba atayeweza kunithibitishia uchawi upo kwa kuniroga, kuna dau nono hapa lililokaa tu kwa takriban miaka 16/17 sasa, likimsubiri huyo mtu wa kuniroga afanye vitu vyake.

Well, 2025 imebaki wiki moja tu iwadie na mimi bado nipo nadunda tu utadhani I own the land.

Wacha uoga wa kijinga [kwa maana halisi ya neno ujinga]. Huyo fala akirudi tena mtandike mangumi mpaka aelewe kwamba wewe hutishwi kijinga namna hiyo.
 
Cha kufanya hapo ni kutokuwa na wasiwasi wowote ule kwa sababu hayo mambo, kiuhalisia hayapo.

Watu huwa wanadanganywa na kudanganyana tu na kuishia kuogopa mambo yasiyo na uhalisia wowote ule.

Halafu hao wanga naona huwa wanajua kusoma saikolojia za watu.

Kwa nini waje kwako ilhali mtu kama mimi ambaye nawatukana kila na kuwakebehi, wakati mwingine hadi naenda huko kwenye makao makuu yao, hawanijaribu?

Kuna ofa yao humu na nje ya humu pia, kwamba atayeweza kunithibitishia uchawi upo kwa kuniroga, kuna dau nono hapa lililokaa tu kwa takriban miaka 16/17 sasa, likimsubiri huyo mtu wa kuniroga afanye vitu vyake.

Well, 2025 imebaki wiki moja tu iwadie na mimi bado nipo nadunda tu utadhani I own the land.

Wacha uoga wa kijinga [kwa maana halisi ya neno ujinga]. Huyo fala akirudi tena mtandike mangumi mpaka aelewe kwamba wewe hutishwi kijinga namna hiyo.
Mzee Mbona umeandika kwa confidence ya SGR 😊☺️

Kuna vizika wazima...Bado hujakua wewe..hii dunia Ina mengi..Kuna kafara...Kuna mizimu...wachawi..majini Kuna mambo mengi SANAA kuliko unavyo fahamu..

Nenda hapo kigoma TU kadharau wazee na kuji mwambafy uone jasho la meno litakutoka..

NB.
Kuna mkuu wa mkoa iringa alijikuta yupo makaburini kalala wakati alikua nyumbani kalala.
 
Cha kufanya hapo ni kutokuwa na wasiwasi wowote ule kwa sababu hayo mambo, kiuhalisia hayapo.

Watu huwa wanadanganywa na kudanganyana tu na kuishia kuogopa mambo yasiyo na uhalisia wowote ule.

Halafu hao wanga naona huwa wanajua kusoma saikolojia za watu.

Kwa nini waje kwako ilhali mtu kama mimi ambaye nawatukana kila na kuwakebehi, wakati mwingine hadi naenda huko kwenye makao makuu yao, hawanijaribu?

Kuna ofa yao humu na nje ya humu pia, kwamba atayeweza kunithibitishia uchawi upo kwa kuniroga, kuna dau nono hapa lililokaa tu kwa takriban miaka 16/17 sasa, likimsubiri huyo mtu wa kuniroga afanye vitu vyake.

Well, 2025 imebaki wiki moja tu iwadie na mimi bado nipo nadunda tu utadhani I own the land.

Wacha uoga wa kijinga [kwa maana halisi ya neno ujinga]. Huyo fala akirudi tena mtandike mangumi mpaka aelewe kwamba wewe hutishwi kijinga namna hiyo.
Uchawi upo mkuu hata kama huamini
 
Mzee Mbona umeandika kwa confidence ya SGR 😊☺️

Kuna vizika wazima...Bado hujakua wewe..hii dunia Ina mengi..Kuna kafara...Kuna mizimu...wachawi..majini Kuna mambo mengi SANAA kuliko unavyo fahamu..

Nenda hapo kigoma TU kadharau wazee na kuji mwambafy uone jasho la meno litakutoka..

NB.
Kuna mkuu wa mkoa iringa alijikuta yupo makaburini kalala wakati alikua nyumbani kalala.
Wadanganye wajinga kwa hizo stori zako.

Hakuna uchawi. Ni fiksi tu.

Wenzenu NASA leo wamepeleka chombo chao kwenda kujivinjari anga za karibu na jua lilipo, nyie bado mnatishana na mambo ya mythology.

Hakuna mchawi yeyote yule dunia hii anayeweza kunifanya chochote.

Fcuk them.
 
Wadanganye wajinga kwa hizo stori zako.

Hakuna uchawi. Ni fiksi tu.

Wenzenu NASA leo wamepeleka chombo chao kwenda kujivinjari anga za karibu na jua lilipo, nyie bado mnatishana na mambo ya mythology.

Hakuna mchawi yeyote yule dunia hii anayeweza kunifanya chochote.

Fcuk them.
Sawa mkuu kila lakheli...nakuombea ili siku moja uje hapa utoe shuhuda na ujithibitishie kwa macho na u regret hizi kauli zako na sio mbali toka Sasa.....
 
Back
Top Bottom