Southern Highland
JF-Expert Member
- Mar 22, 2017
- 14,938
- 25,405
Relax, Amezaliwa mwokozi tumshangilie. Huyu fala anajaribu kukupima imani yako tu ukiogopa yeye ndio anafurahi. Ilipaswa umkemee hapohapo unammaliza nguvu kabisa.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Herini ya sikukuu ya Noeli, kwangu naona ilishakuwa mbaya kwa mfululizo wa yanayoendelea na hili lililonifanya niandike hapa muda huu.
Kwanza nianze kwa kusema sina utulivu kabisa usingizi umekata na hauwezi kuja kwahiyo kama ntakosea kwenye kuandika mnivumilie.
Ipo hivi nilikuwa ndotoni ghafla nikashtuka muda ilikuwa saa 04:24 , nilivyoshtuka naona reflections za mwanga wa moto, nikajua labda n mwanga wa taa za gari lakini moyo ukasita kuliamini hilo kwa kuwa mwanga wa gari huwa ni mkali zaidi, nikiwa bado kitandani nashangaa zile reflections ghafla zikaanza kumove na kupotea, nikasogeza kapazia kidogo nione nje kinachoendelea. Nimeona moshi unafoka na nikapigia mstari majibu yangu kuwa ule ni moto.
Moyo ukapiga paa!! Nikazungusha macho upande wa pili wa dirisha nikaangalia kwa kunata bila kupepesa macho kama sekunde 40 na kushuhudia mtu kwa mbali kama kapigwa na butwaa akitazama uelekeo wangu kama vile ameniona (ni kama mita 10-15 kutoka nyumba ilipo) ila sikumtambua ni nani kutokana na giza. Baada ya kuona vile nikarudishia pazia nimefanya maombi na ninaamini nipo salama ila hili limenishtua kwa kiasi fulani.
Wakuu nifanye nini zaidi?
Kuna madhara yeyote kushuhudia hilo?
Mshana Jr muongozo wako ni muhimu mkuu nna taharuki kwa lililotokea.
Ah wapi. Wasiwasi wako tu. Hayo ni mambo ya kufikirika tu.Binafsi siujui ila hayo mambo yapo mkuu hasa huku kwetu Afrika.
Tokea 2008 huko natoa ofa kwa wachawi wote popote pale walipo, waniroge hata kidogo tu ili wanishikishe adabu na kunifunga mdomo, lakini wapi. Hakuna lolote. Bado nadunda na ngebe zangu.Sawa mkuu kila lakheli...nakuombea ili siku moja uje hapa utoe shuhuda na ujithibitishie kwa macho na u regret hizi kauli zako na sio mbali toka Sasa.....
Amefufuka au kazaliwa?Relax, Amefufuka mwokozi tumshangilie. Huyu fala anajaribu kukupima imani yako tu ukiogopa yeye ndio anafurahi. Ilipaswa umkemee hapohapo unammaliza nguvu kabisa.
😂 nitakaa sawa mkuuUpo safe bwana, ondoa hofu... ungekutana na hawa,.hofu si ndio ingekuua kabisa ?
View attachment 3184413
Hapo ni umesoma je ungeshuhudia kama mimiMwana post Yako imenitisha mpaka sijalala hadi mda huu imebidi nimpigie pusha aniletee kush na nyagi
Sawa mkuu we endelea kuwatafuta kuna siku utakutana naoAh wapi. Wasiwasi wako tu. Hayo ni mambo ya kufikirika tu.
Alafu inakuaje sasa anapojua?Sjui huwa ni kwann,mchawi unapomchungulia anajua pale pale kwamba kuna mtu kamuona
Ah mwenyezi aepushie mbali, hayo mambo yapo ila sitaki kuyashuhudiaHapo ni umesoma je ungeshuhudia kama mimi
Noma mno mkuu unaweza hisi ni mafatakiwatu wanaroga mpaka kwenye birthday ya yesu noma sana
Tahadhari ya kwanza ya mchawi yeyote kwenye jumuiya Yao ni kuhakikisha hajulikani...Sjui huwa ni kwann,mchawi unapomchungulia anajua pale pale kwamba kuna mtu kamuona
Nilitamani hivyo pia ila leo nimeshuhudia kwa macho yangu ya nyama.Ah mwenyezi aepushie mbali, hayo mambo yapo ila sitaki kuyashuhudia
Kufunga pazia na kuanza kusali ni ishara ya kuwa umejawa na hofu kubwa.
Pale pale mkiwa mnakodoleana, ungemkemea kwa imani. Unammaliza nguvu na mngemaliza biashara.
Sasa zidisha maombi. Maana atakurejea.
Ikitokea kaonekana inakuwaje?Tahadhari ya kwanza ya mchawi yeyote kwenye jumuiya Yao ni kuhakikisha hajulikani...
Huo ndo mwiko wao mkuu
Ungeenda church kwenye mkesha wa krismasNilitamani hivyo pia ila leo nimeshuhudia kwa macho yangu ya nyama.
Nizidishe tu maombi sina namnaAchukue hii,
Witches never leave their projects.
Huyo lazima amrudie tu kuhakiki amejua au hajajua yanayoendelea.
Hapo kwa kila mtu atakae mjia kwa story tata ni kujitoa ufahamu tu kama mwehu hajui chochote huku nafsini akinuia na kufanya dua mabaya yasimpate.
Hapo afanye ujasusi wa kiroho.