Nimeshuhudia mtu akiwanga, hili limenitisha

Nimeshuhudia mtu akiwanga, hili limenitisha

Haina shida kabisa hiyo na ni dalili kwamba nguvu zako kiroho zilikuwa kubwa kuliko zake.. Na kama angekuwa juu ya ungo angepiga bonge la mweleka
Vibaya ni kama ungewaona paka weusi tii wakifanya matusi.. Lakini pia nao siku hizi hawana madhara kivile kwakuwa nao wanakula kitimoto kiwe roast au hata kile cha kuchoma! Mbichi hawali
Hawezi kunirudia kwa sababu nimemuona ila sijamtambua ni nani.
 
Hayo ndiyo madhara ya kuwekeza kwenye ushirikina haya ona sasa
 
Kwanini unaona mtu anafanya ujinga hapo nje halafu unapiga magoti kusali, hofu imekutawala.

Kwanini usitoke nje umfukuze au kama unamuweza umpige?
Huku Mara tunabonda hao wapuuzi.
 
Bado navuta kumbukumbu ni ndoto gani nilikuwa naota ikanikurupua usingizini hadi nikashuhudia hilo.
Soma hiyo article, You will know what is behind.
 
Cha kufanya hapo ni kutokuwa na wasiwasi wowote ule kwa sababu hayo mambo, kiuhalisia hayapo.

Watu huwa wanadanganywa na kudanganyana tu na kuishia kuogopa mambo yasiyo na uhalisia wowote ule.

Halafu hao wanga naona huwa wanajua kusoma saikolojia za watu.

Kwa nini waje kwako ilhali mtu kama mimi ambaye nawatukana kila kuku ha na kuwakebehi, wakati mwingine hadi naenda huko kwenye makao makuu yao, hawanijaribu?

Kuna ofa yao humu na nje ya humu pia, kwamba atayeweza kunithibitishia uchawi upo kwa kuniroga, kuna dau nono hapa lililokaa tu kwa takriban miaka 16/17 sasa, likimsubiri huyo mtu wa kuniroga afanye vitu vyake.

Well, 2025 imebaki wiki moja tu iwadie na mimi bado nipo nadunda tu utadhani I own the land.

Wacha uoga wa kijinga [kwa maana halisi ya neno ujinga]. Huyo fala akirudi tena mtandike mangumi mpaka aelewe kwamba wewe hutishwi kijinga namna hiyo.
Hahaha, mkuu uchawi upo ngoja nikuthibitishie hapa

Malaki 3:5
[5]Nami nitawakaribieni ili kuhukumu; nami nitakuwa shahidi mwepesi juu ya wachawi, na juu ya wazinzi, na juu yao waapao kwa uongo; na juu yao wamwoneao mwenye kuajiriwa, kwa ajili ya mshahara wake, wamwoneao mjane na yatima, na kumpotosha mgeni asipate haki yake, wala hawaniogopi mimi, asema BWANA wa majeshi.
 
Chief uchaw upo mimi nmeushuhudia zaidi ya mara moja na najikutaga tu nshasali kwa imani yangu
Unakua unatamani hata ureact unashindwa unabaki kupiga fat-ha tu
Sema hapa umeushuhudia kwa namna gani?

Binafsi, sijawahi kushuhudia kinachoitwa “uchawi” toka nimezaliwa. Nyingi story tu ambazo ukichunguza unagundua hazina ushahidi wowote ule zaidi ya nilisikia au niliona hiki.
 
Sema hapa umeushuhudia kwa namna gani?

Binafsi, sijawahi kushuhudia kinachoitwa “uchawi” toka nimezaliwa. Nyingi story tu ambazo ukichunguza unagundua hazina ushahidi wowote ule zaidi ya nilisikia au niliona hiki.
Una hiyari hio lakini mimi nmeona kwa macho yangu ya nyama vitendo vya kichawi
 
Back
Top Bottom