Nimesikitishwa, huzunishwa na kufadhaishwa na uongo wa Kamati ya PAC! Escrow sio fedha za umma!

Nimesikitishwa, huzunishwa na kufadhaishwa na uongo wa Kamati ya PAC! Escrow sio fedha za umma!

Mimi kwa uzoefu nilio nayo na account za ESCROW ni kuwa ile Fedha zilizomo katika ile account bado hazikuwa za IPTL japo kuwa zinatakiwa kulipwa IPTL. Ingelikuwa ni za IPTL zingekuwemo katika account yake ila kwavile kuna mgogoro, Escrow Account (third party holder) ikafunguliwa. Kwahiyo zile Fedha ni bado za Tanesco. Na tusisahau kuwa Mule ndani kuna fedha za TRA.
Sasa Suali linakuja je fedha za tanesco na TRA ni za Umma au sio za Umma?
Sasa ikiwa tanesco na TRA ni Private companies basi fedha sio za Umma ila ikiwa ni Public companies tusidanganyane zile fedha ni za Umma tu.

Sasa kutokana na Taarifa za CAG na PCCB kuwa PAP sio wamiliki halali wa IPTL. Na waziri na timu yake pamoja na Mwanasheria mkuu wamehusika na ruhusa za kutoka zile fedha kwa tapeli ambae anajulikana Duniani kuwa ni mtu wa Fraud.
Kwahiyo PAC hawakutoa uongo ndani ya bunge wao wametoa Report ya uchunguzi uliofanyika kutoka report ya CAG na uchunguzi wa PCCB na TRA.
 
Si kwamba hoyo Pasco hatambui kuwa hizo pesa ni za umma laa...! Bali apenda kuwatweza zenyu akili maana yu kazini.
 
Last edited by a moderator:
Pasco,
Tanesco ni shirika la umma linaloendeshwa na serikali kwa asilimia Mia moja. Tanesco ni kampuni inayoendeshwa kwa ruzuku ya serikali kwa kiwango kikubwa kuliko shirika lingine lolote la umma; tanesco Kama shirika haliendeshwi kwa faida Bali hasara, kwa sababu limekuwa ni Chaka la majizi Kukomba fedha za wananchi. Ruzuku ya serikali inatokana na kodi za wananchi, inakuwaje hoja ijengwe Kwamba zile sio fedha za umma?
Mbunge Laiser Leo Katika uchangiaji wake amehoji: ni Tajiri gani duniani amewahi kugawa hela binafsi Kama hizi? Ni fedha za umma tu Ndio majitu Kama rugamalira na mafisadi Ndio Hawana uchungu nazo.

Msipotoshe Watu.
Mkuu Mchambuzi, with due respect, tubishane kwa hoja tuu na sio kwa emotions, hata uthibitisho ukithibitisha PAP ni mwizi, ameinunua IPTL kwa utapeli, then hizo fedha zilizoibiwa ni fedha za IPTL!, sio fedha za umma!.
  1. Tanesco ni shirika la umma, litatumia fedha za umma kulipia huduma, zile fedha zikiisha change hands na kumfikia service provider, zina change form, from fedha za umma to fedha binafsi.
  2. Escrow ni account iliyofunguliwa katakana na mgogoro wa kiwango cha capacity charges mlalamikaji ni Tanesco na sio IPTL!, hivyo determinant ya fedha kutoka ni Tanesco na sio IPTL!.
  3. jumla ya deni la IPTL kwa Tanesco ni bilioni zaidi ya 300!, ndani ya escrow kulikuwa na bilioni 128!. Hivyo bado Tanesco inadaiwa zaidi ya bilioni 180!.
  4. Tanesco na IPTL walikaa na kukubaliana kwa maandishi, kuwa wamekubali kuwa fedha zote ni za IPTL walioridhia IPTL walipwe!. Hivyo hata kama zingekuwa ni fedha za umma, baada ya fedha hizo kulipia huduma, wajemeni sio fedha za umma tena!.
  5. Kuna swali nimeuliza na sijabahatika kupata jibu lolote la maana kuwa kama account ya escrow ni ya Tanesco na IPTL, na fedha zilikuwa za IPTL, ilikuwaje BOT ikailipa PAP ambaye ni third party?. Sakata la Escrow: Did "BOT Had a Role to Play?, or Just An Innocent Victim?
  6. Alichofanya Singasinga ni kula dili ya kuuibia IPTL na sio serikali, kwa sababu hata ingekuwa kama IPTL na Tanesco wangekubaliana kuipunguza capacity charge to 50%, bado fedha zote zilizomo ndani ya account ya escrow, bado zingekuwa ni za IPTL.
  7. Kwa vile invoices ni za IPTL ambayo inalipa VAT, na hata kama PAP alidai ameinunua IPTL, BOT ilibidi kuzilipa hizo fedha IPTL, kisha IPTL ilipe kodi ya serikali, ndipo imlipe PAP ambaye sio VAT registered!, ilikuwaje invoice za IPTL zenye kodi, akalipwa PAP ambaye hana VAT?!.
  8. Huu mjadala umefika hapa kwa sababu wengi wetu tunajadili kwa kutumia emotions na sio reasoning, tuwewke emotioms pembeni, tendwe kwenye facts tupu, tutakubaliana!.
  9. Hata kama fedha za escrow sio za serikali, haina maana Tanzania hatuibiwi, bali sioni yoyote anayezungumzia hili jinamizi la IPTL lilitokea wapi na majinamizi mengine kibao yaliyopo, watu wameshupalia tuu escrow, huku tunaibiwa mara mia kuliko escrow na watu mmenyamaza!.
  10. Mjadala wa escrow umenifumbua macho how ignorants we are!.Escrow: Jee Watanzania ni Ignorants? au Tumelogwa?!.Tuache Cherry Picking !.
Pasco
 
Pasco unaonaje ukaeleza hio maana ya "fedha za Umma"
Mzee wa Conspiracy, nikieleza itafika mara 100 sasa, ila kwa faida yako na wengine ambao hawakuliona jibu la awali, nitarudia.
  1. Hapa tuko wote, ndani pesa za account ya escrow zimechange forms mara tatu, au zime change hands mara tatu, kuna mtu anaitwa depositor, ambaye yeye ni Tanesco, fedha zilipokuwa mikononi mwa Tanesco, ni fedha za umma, kitendo cha kuzitoa ndani ya account ya Tanesco kuzi deposit kwenye escrow, kitendo cha depositing, kumezichange form hizi fedha from kuwa pesa za umma, into pesa za depository, na zimechange hands from mikono ya Tanesco to mikono ya depositor ambaye yeye ni custodian tuu wa fedha hizo hadi mgogoro utakapokwisha!, hivyo wakati fedha zikiwa kwenye safe custody ya custodian, fedha zile sii za umma wala sii za binafsi, some zingeweza kuwa za umma na kurudishwa Tanesco, some zingeweza kuwa za IPTL with a unique options ya possibility with "uncertainty" that "only some" "could" be Tanesco's, but with definite that some are IPTL's with possibility ya all kuwa ni za IPTL!. Unakijua ni nini kilichotokea kuhusu madai ya Tanesco na ni nini kilikubalika?!. Tanesco wali give in, na kukubali wanadaiwa more than that na wakaweka schedule of repayment na ndipo Tanesco waka authorise pesa zote zilipwe kwa IPTL!, and that is when all the money zili change form kutoka kuwa fedha za wote na kugeuka fedha za binafsi, and during withdrawer by the time fedha zinalipwa IPTL zilikuwa sio fedha za umma!.
 
prof mark mwandosya kaeleza vizuri sana pesa zimeibiwa kutoka ac ya escrow iliyokuwa chini bot na ndiyo maana gavana alikuwa anachukuwa tahadhari kubwa sana kuzitoa lakini pia kaongeza kuwa mabenki yote yako chini ya bot yakiibiwa au kufilisika bot inalipa kama yameshindwa kulipa kwa msingi huo hata hizo pia ni fedha za umma twende kwenye pesa ambazo tanesco walikuwa wanadai kutozwa zaidi kutokana iptl kutotimiza baadhi ya masharti ya mkataba kwa hiyo kwenye ac escrow kwa miaka 12 tanesco kuna pesa yao na wameshinda kesi na kinachotakiwa ni kupiga hesabu upya kwa mujibu wa madai ya tanesco tatizo hauwezi kupiga hesabu wakati pesa zimeshaliwa.
na cheyo kalieleza vizuri aliyelipwa siyo iptl bali pap aliyedai kauziwa shares na piperlink kwa nyaraka za kugushi harakaharaka kalipwa pesa za iptl inatakiwa kama ingelikuwa kweli angebeba na madeni ya iptl iliyokopa benki ya standard chatered ya hongkong lakini tunavyosema pesa zimeshabebwa zote account ya pap imefungwa sasa madeni yote ya iptl tutayalipa sisi kwa kuwa iptl walikopa wakiwa na government guarantee sasa kuna watu wanadhani hatujaibiwa akili nzito kiasi gani cheyo kidogo alie machozi na bora angelilia kabisa nchi hii inaumwa nini?
 
Sawa sio zetu...Na kodi?
Kampuni zinapouziana hisa lazima zilipe Huyo aliegawa kalipa kodi ila huyo mwenye hisa nyingi kaondoka na kodi zetu tafsiri Sahihi ni Mwizi.
 
Mara nyingine watu hutaka kuonyesha usugu wa akili zao na kujifanya kila kitu wanajua,ndio maana Mama Makinda akasema ikiwa wewe si mwanasheria ila unatoa ushauri wa kisheria then wewe ni bush Lawyer.

Hiyo Escrow imeelezwa na wataalam kuzidi Pasco ambaye si mchumi,si muhasibu.......lakini hpa unataka kutuaminisha na tuchukue kile unachosema wewe wakati unajua kabisa si sahihi.Hakuna watu ninawakubali kama Wasira,Zitto Kabwe,na Luhaga Mpina,ninawakubali kwasababu wako fresh sana upstairs,mwanzo sikuilewa kabisa hii ishu ila niliamua kujifunza kutokana na hoja zilizoletwa na nimegundua kuwa humu ndani ya Jukwaa kuna watu kwa makusudi kabisa wanataka kutupotosha.

Labda ni kwa makusudi au vyovyote vile lakini ukweli mioyoni mwao wanaujua.

Tupeni ukweli hata kama unauma.
 
Unajua nyinyi watu. Kuna majamaa wasio viongozi wa serikali pia wamepokea huo mgao. Escrow imegusa sehemu kubwa ya jamii kuanzia dini,serikali na hata tasisi binafsi.

Mpumbavu atajitetea na isitoshe wengi wanakuja hapa kutetea hoja kwamba sio maili ya umma maana wamefaidika nazo kwa namna moja au nyingine.
Kwanza hujui historia ya IPTL mpaka baada ya escrow watu ndio wanajua.
Pili,ni wapi duniani watu wanapeana fedha binafsi kwa mabilioni na serikali isiulize?
Je serikali ya kikwete iliuliza ? Kwanini askofu apewe hela binafsi? Kwanini mawaziri wapewe mabilioni? Kwa lipi hasa? Mana wao wamefanya kazi zaidi ya wengine?
In a simple logic tu,this non sense doesnt add up.
Na ndio maana tumekuwa kizazi cha kishenzi, maana ndio culture tunajeng hii; nipate changu kwanza.

Hii ni laana ya mwafrica toka enzi zile za mababu. Selling out another brother or sister ndio zetu.

We pasco unajifanya hujui waa hutaki kujua na unajua wazi hizo hela sio za watu binafsi.
Hawa watu wote waliopokea hiI fedha wengi na wafaham binafsi.
Wengi walikuwa kwenye uratibu wa deal la IPTL toka huko nyuma 1995.
Kwahiyo usionge ushenzi hapa.
 
Niwapongeze sana wasomi nyie kwani mnatuweka bayana kuhusu sakata hili...Hakika nawachukia wansiasa wanatumia bunge vibaya kwa malengo maovu...naomba sana tuwahukumu ifikapo 2015 kwa kuwanyima kura ili tupate wawakilishi wanaoteta maslahi yetu na siyo yao binafsi..
Wanabodi,

Kwa waliosoma fasihi, kitabu cha "An Enemy of the People" by Henrik Ibsen mnaweza kuniita mimi Pasco wa JF, kuwa ni "an enemy of the people!", Fedha za Escrow, Sio Fedha za Umma!, hizo Bilioni 320 zilizokuwa kwenye account ya Escrow, hazijaibiwa!, bali zimetumika kulipia umeme!.

Inawezekana PAP amenunua kampuni hewa, amefanya utapeli kuinunua IPTL toka kwa wamiliki halali, hayo hayatuhusu, bali malipo ya Tanesco kwenye account ya escrow ni kulipia capacity charges ya mitambo ya IPTL ambayo ni mitambo kweli sio mitambo hewa!, na pia Tanesco inalipia malipo ya huduma za umeme kweli unaokuwa genereted na mitambo ya IPTL, ni umeme kweli na sio umeme hewa!, na imeelezwa kuwa Tanesco bado inadaiwa!.

Ukiwa mkweli sana wa type ya ukweli huu, pia lazima uwe tayari to pay the price!.

Niko tayari to pay the price of expresing my opinion kuwa Nimesikitishwa!, Huzunishwa!, na Kufadhaishwa na Uongo wa Kamati ya PAC!-Escrow Sio Fedha za Umma!.

Pasco.

Ufafanuzi unapatikana hapa kwa Mkuu Ng'wamapalala.
Hoja za Kamati ya PAC zinavyokinzana kuhusu Escrow akaunti kama ni fedha ya umma

[/LIST]
Mkuu Mwalimu, Prof. Kitila, kwanza hongera kupata uprofesa, maana hatujakutana humu jukwaani kwenye thread yangu yoyote tangu umekuwa prof, bado nimekuzoea zaidi kama Dr. Pili nimefarijika sana, kunitembelea kwenye uzi huu, its an honour to me and to my thread, kama nilivyofarijika nilipo tembelewa na Mchambuzi na Nguruvi 3.

Kwenye posti yako ume raise hoja 12 za msingi, mwanafunzi unapoulizwa maswali na mwalimu, unaamini kabisa mwalimu anajua, ila anakuuliza tuu ili kuujua ufahamu wako, inapotokea mwalimu anaomba kueleweshwa na mwanafunzi, then mwanafunzi huyo anakuwa more than gladi kumuelewesha mwalimu, na hapa mwanafunzi atajisikia sasa yeye ndio mwalimu, na mwalimu ndio mwanafunzi wake, hivyo Mwalimu Kitila, karibu katika darasa langu.

  1. Mimi ni mkweli daima hivyo mara kadhaa huanzia kwa kuweka "the end" na kisha ndipo na "justify the means". The end product hapa "pesa ni za nani?!", naanza kwenye kumtaja mwenye pesa ndipo tuje kuhalalisha kwa nini sio pesa za umma!. Kuna hoja za mijadala, na kuna hoja sio za mijadala ni straight conclusive!. Ingekuwa hoja yangu ni mjadala, ningeiliza Jee Fedha za Escrow ni za Umma?, ili watu walete michango, mwisho tufikie hitimisho!. Hapa kuna ukweli na uongo!, kuna kumaninishana kwa kudanganyana kuwa fedha za umma zimeibiwa!, zimechotwa, zimekapuliwa, hivyo wananchi wamehaminika, wakati ukweli ni kuwa fedha hazikuibiwa zimelipwa!. Mtindo wangu wa kutoa conclusiwe sikuanza leo, tulupoanza tuu huu mchakato wa katiba, nilisema tutapata "bora katiba". Kabla kura hazijapigwa kuipitisha nilisema humu "kura zisipotosha, zitatosheshwa!". Sasa watu wanapigia chapuo kura za hapana, nikasema wazi huko ni kujifurahisha kwa sababu kura za ndio "zitatosheshwa!", na kwenye siasa pia mara kibao nimeweka conclusive humu hata "2015 ni CCM tena!" kwa sababu hatuna any serious opposition, Ukawa mimi nauita ni just a "married of convenience!", conveniences zikiisha kila mtu atashika njia yake!. Escrow sio fedha za umma!.
  2. Hapa tuko wote, ndani pesa za account ya escrow zimechange formas mara tatu, au zime change hands mara tatu, kuna mtu anaitwa depositor, ambaye yeye ni Tanesco, fedha zilipokuwa mikononi mwa Tanesco, ni fedha za umma, kitendo cha kuzitoa ndani ya account ya Tanesco kuzi deposit kwenye escrow, kitendo cha depositing, kumezichange form hizi fedha from kuwa pesa za umma, into pesa za depository, na zimechange hands from mikono ya Tanesco to mikono ya depositor ambaye yeye ni custodian tuu wa fedha hizo hadi mgogoro utakapokwisha!, hivyo wakati fedha zikiwa kwenye safe custody ya custodian, fedha zile sii za umma wala sii za binafsi, some zingeweza kuwa za umma na kurudishwa Tanesco, some zingeweza kuwa za IPTL with a unique options ya possibility with "uncertainty" that "only some" "could" be Tanesco's, but with definite that some are IPTL's with possibility ya all kuwa ni za IPTL!. Unakijua ni nini kilichotokea kuhusu madai ya Tanesco na ni nini kilikubalika?!. Tanesco wali give in, na kukubali wanadaiwa more than that na wakaweka schedule of repayment na ndipo Tanesco waka authorise pesa zote zilipwe kwa IPTL!, and that is when all the money zili change form kutoka kuwa fedha za wote na kugeuka fedha za binafsi, and during withdrawer by the time fedha zinalipwa IPTL zilikuwa sio fedha za umma!.
  3. Ni kweli Tanesco ilikuwa overcharged hugely hivyo tulikuwa tunaibiwa!, ila wizi wenyewe ni kwa mujibu wa mkataba na tulikubali, kama tulivyokubali kununua radar, ndege ya rais, vifaa vya kijeshi na sasa bomba la gesi na mikataba ya gesi, nenda kanisome hapa Gesi asili: Is it "day light robbery?!"- watanzania tunaibiwa ...Tetesi: Bomba la Gesi Mtwara:A "20 -Year Grace Period" ni Kiini Macho!. Hivyo kama ni kuwa overcharged, kila siku tunakuwa overcharged, overpriced, na huge kick backs!.
  4. Nashukuru kuwa kumbe unajua tulipewa hii nafasi jee unajua tuliitumiaje?!. Hii ndio conversion process ya kuachia fedha za umma zilizoibiwa na kugeuka fedha binafsi!.
  5. Hatukushindwa!, this is where the deal is!, PCCB ni nothing!, Hosea is nothing!, kitu kinachoitwa usalama wa Taifa is nothing!, tangu mwanzo IPTL ni rushwa mwanzo mwisho, what did we do?!. Bodi ya Tanesco ilipata "ganzi!" ya ajabu!, wakaridhia kwa maandishi pesa zote ni za IPTL!. Ruge na Singasinga ni wapiga dili, kama pesa zilikuwa zetu, then kikulacho kii nguoni mwetu!, tusitafute mchawi!, wala tusimbebeshe msalaba mtoto wa Mkulima, wezi wetu tunawajua na ni wale wale toka Richmond, Dowans hadi Simbioni!. Tungekuwa na akili laiti mgelijua huyo Simba mwenye 50% ya PAP ndipo angalau mngenielewa!.
  6. "Mwenye kisu kikali ndiye anaekula nyama!", "fimbo iliyoko mkononi ndiyo uiwayo nyoka!", "the end justify the means!", "Aliyeshika usukani wa gari ndiye dereva" regardless gari ni la nani!, hivyo as long as pesa iko mikononi mwa JR as private money, what he does with his monies!, is non of our businesses!.
  7. Private money is none of our business!.
  8. Kumbe sasa tatizo ni kugawa?!, Ukimuondoa Bakhresa, please don't talk of Mengi and Rostam, kwao this is "missed opportunity!", masking JR akajivutia na kujinyamazia, haya yote yasinge fumka!. Siku zote wahindi wanapiga dili hizi na kujituliza tuli!, lakini masikini wakipata.... Kuna DCP walipiga wahindi watupu wakatulia haikubumburuka!, EPA wahindi walikuwa wanaipiga long time, huku wametulia, Waswahili walipoingia tuu, wanasafiri 1st class, wananunua Vogue custom made kutoka UK, wanasafirisha kwa air cargo, gari zinafika zina kuwa cleared by cash on the spot!, mtaani mbona tulikomaje?!, si ndio dili ikabumbuluka!, wangejinyamazia tuu kama walivyo wahindi yote haya yasingetokea!.
  9. As long as sio hela ya umma, haijalishi nani amegaiwa na kwa huduma gani, ndio maana nikasema PCCB is nothing!, mnaangalia waliogaiwa pesa, haya ni matokeo tuu!, mnaacha kuangalia chanzo cha jinamizi hili la IPTL na kila kitu kiko wazi!, Rutabanzibwa alikataa hongo ya dola 200 na akahamishwa!, unamjua waziri wake alikuwa nani?, kama KM alimegewa dola laki mbili, jee aliyekuwa waziri alipewa ngapi?, unamjua ni nani?. Pesa zikiisha kuwa zako, you are free kuzigawa utakavyo bila kuvunja sheria yoyote!. Hakuna sheria inayokataza kugawa pesa wala jinai yoyote kupokea pesa yoyote kwa kazi yoyote au hata bila kazi yoyote!. Hata mimi kuna wakati "huwapitia wale" na kukubaliana bei, then nikifika huko, ninachange mind, lakini bado nalipa mtu bila kufanya chochote, its my money!.
  10. When the money is yours, you are free to use it as you please!, kwa winging umasikini ni laana, hivyo badala ya kuwagawia masking unamuomba Mungu, masking wore bora wajifie tuu na umasikini wao, na kumfutilishia Mungu kuwa mwenye nacho, ataongezewa!, asiye nacho atanyang'anywa hata kidogo alichonacho!, mzee wa vijisenti, kapewa katiba, ndiye mwenyekiti wa kamati ya bajeji na ndie mshauri wa JR wa mambo ya kisheria na umeona consultancy fee yake!.
  11. Yes ni saws kabisa na amini usiamini, hata mimi Pasco wa jf, nikiwa nazo, huwa nagawa!, tofauti ni kiwango, kwa uwezo wangu huwa nagawa ten ten, jelo jelo hadi buku buku!, kila nikienda bush, nahakikisha nina kama just 1.M tangu bank naiomba in small denominations, nikitua bush!, kijiji kizima kinajua leo mtoto wa mama fulani ameingia kijijini, kuanzia pombe hadi hizo ten ten, jeero jero na buku buku, its my money, I do with it what it pleases me!. Kwenye ule mgao kuna kick backs, kuna asante, kuna just sadakalawe kuwa "ninazo" kuna genuine charity na kuna sadaka!.
  12. Sio nchi za wenzetu hata sisi tunayo FIU pale BOT, miala yote ya more than 10.m lazima taarifa ziende FIU ndio maana siku hizi hakuna kutoa malipo more than that bila kupitia BOT, the only exception ni same bank transactions ndio maana recipients wote walilazimishwa lazima wafungue account the same bank!. Nawaombeni sana msibabaishwe na huto tujisenti kwenye account za Mkombozi, the real transactions zimefanywa kwenye account yake iliyoko nchi Uholanzi, naamini "wanene" wamepewa asante zao zimehifadhiwa kule "Credit Sussie" transactions zinafanywa kwa "codes" only!, hata bank manageger, hawezi kujua jina la account holders!.
Natumaini mwalimu utakuwa umenielewa!.

Ni wako mwanafunzi mtiifu
Pasco wa jf!.

 
Kwa ugawaji huu wa pesa kwa kiongizi makini lazima ushtuke maana hii nisawa na kupindua nchi
 
Pasco unaweza kuwa sahihi kuwa hizi si fedha za umma lakini uchukuaji wake bank unadhirisha kuwa hizi ni fedha haramu. Uharamu wake unatokana na maelezo waliyotoa wanaotetea hoja kuwa hizi ni fedha za umma. Unachonitisha mimi ni kutuhumu PAC badala ya kutuhumu vyanzo vya PAC.
Na nashawishika kudhani Pasco ni hardcore member wa CCM maslahi. CCM maslahi hampendi mifumo ifanye kazi mnapenda mkubwa ndoo aamue.
 
  1. prof mark mwandosya kaeleza vizuri sana pesa zimeibiwa kutoka ac ya escrow iliyokuwa chini bot na ndiyo maana gavana alikuwa anachukuwa tahadhari kubwa sana kuzitoa lakini pia kaongeza kuwa mabenki yote yako chini ya bot yakiibiwa au kufilisika bot inalipa kama yameshindwa kulipa kwa msingi huo hata hizo pia ni fedha za umma.
  2. twende kwenye pesa ambazo tanesco walikuwa wanadai kutozwa zaidi kutokana iptl kutotimiza baadhi ya masharti ya mkataba kwa hiyo kwenye ac escrow kwa miaka 12 tanesco kuna pesa yao na wameshinda kesi na kinachotakiwa ni kupiga hesabu upya kwa mujibu wa madai ya tanesco tatizo hauwezi kupiga hesabu wakati pesa zimeshaliwa.
  3. cheyo kalieleza vizuri aliyelipwa siyo iptl bali pap aliyedai kauziwa shares na piperlink kwa nyaraka za kugushi harakaharaka kalipwa pesa za iptl inatakiwa kama ingelikuwa kweli angebeba na madeni ya iptl iliyokopa benki ya standard chatered ya hongkong lakini tunavyosema
  4. pesa zimeshabebwa zote account ya pap imefungwa sasa madeni yote ya iptl tutayalipa sisi kwa kuwa iptl walikopa wakiwa na government guarantee sasa kuna watu wanadhani hatujaibiwa akili nzito kiasi gani cheyo kidogo alie machozi na bora angelilia kabisa nchi hii inaumwa nini?
Mkuu Ngozi Mbili, asante kwa hoja zako hizi, nimeziweka kwenye makundi manne.
  1. Kama zilikuwa ni fedha za umma, BOT ilizilipaje kwa PAP wakati mwenye pesa ni IPTL?!, siku zote fedha ni ama za aliyeweka, Tanesco, ama anayepokea IPTL, mwenye pesa za umma Tanesco, ndie aliyeikubalia BOT imlipe PAP, custodian wa fedha za umma hapa ni BOT, aliwezaje kulipa PAP ambao were not part to the contract?!. Ukijikuta umeingiziwa fedha kwenye simu yako ni jukumu la aliyeingiza na sio mpokeaji!.
  2. Nikweli ndani ya escrow kulikuwa na fedha ambayo Tanesco ingepaswa kurudishiwa kutokana na kuibiwa kwa miaka 12. Madai ya Tanesco ni very genuine, wakitaka wapunguziwe capacity charge. Japo mazungumzo ya kupunguziana bado hayafanyika, ila tuseme labda Tanesco wangepunguziwa capacity charge hadi 50 %, bado pesa yote iliyokuwemo ndani ya escrow ni bilioni 128 tuu, jumla ya fedha ambayo Tanesco inadaiwa hadi leo hadi kesho ni zaidi ya bilioni 300!, hivyo hata Tanesco wangepunguziwa vipi, hilo punguzo lisingerudisha hata senti moja back to Tanesco, hivyo ni Tanesco wenyewe kwa ridhaa yao, ndio walioruhusu fedha yote itumike ku ofset hilo deni la bilioni 300!.
  3. Kama ilivyo aliyelipwa ni PAP na sio IPTL, aliyekopeshwa na Standard Charted ni IPTL na sio PAP, PAP kauziwa kampuni bila kuuziwa madeni!. Mkopo wa ujenzi wa IPTL dola milioni 150 ulikopwa na benki ya Sime na Bumuputra za Maleysia, ili fedha zilizofika huku ni dola milioni 80 tuu!. Mechimal ikafilisika huko kwao, deni lake likanunuliwa na benki nyingine ya Maleysia iliyoliuza kwa Stan Chart Bank ya Hong Hong. Hivyo by the time Mechima anaiuza IPTL kwa Piper Link, IPTL original iliisha uzwa kwa Stan Chart, huku IPTL imeuzwa, huku Mechimar inaiuza IPTL kwa bei ya bure kwa Pieper link, wakati PAP ananunua IPTL toka Pieper Link, hakuuziwa deni lolote!, hivyo PAP hajui deni, wala hamjui Stan Chart, yeye kauziwa mitambo, Stan Chart wameuziwa makaratasi!. Hata mahakama yetu imeitambua PAP bila kulitambua deni la IPTL.
  4. Ni kweli mkpo ulikopwa kwa government guarantee, pesa zilizoliwa ni pesa za VAT, na zinalipika!, hata account ya PAP ikifungwa, mitambo ya IPTL bado ipo, na umeme bado unazalishwa!, hivyo kila kitu kinalipika!.
Pasco
 
Pasco unaweza kuwa sahihi kuwa hizi si fedha za umma lakini uchukuaji wake bank unadhirisha kuwa hizi ni fedha haramu. Uharamu wake unatokana na maelezo waliyotoa wanaotetea hoja kuwa hizi ni fedha za umma.
Mkuu Mpitwaga, kwanza asante, pili nakubaliana kuwa hizo fedha zimepigwa!, zimeibiwa!, mwizi ni PAP, ameiba fedha za IPTL zilizokuwa na VAT ndani yake!.

Unachonitisha mimi ni kutuhumu PAC badala ya kutuhumu vyanzo vya PAC.
Na nashawishika kudhani Pasco ni hardcore member wa CCM maslahi. CCM maslahi hampendi mifumo ifanye kazi mnapenda mkubwa ndoo aamue.
Hili la mimi kuwa CCM sina tatizo nalo kabisa!, Pasco wa JF ni Mwana CCM damu ila anajifanya hana chama!.

Hizi ni baadhi ya Threads zangu kutetea chama changu CCM na kumfagilia Mwenyekiti wangu wa chama!.

Mapungufu ya JK: Ni Rais Dhaifu! -

CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga!
Yametimia!, CCM Imechokwa!, Chadema Njia Nyeupe 2015 ...
Mtazamo: Kanda ya kaskazini, ccm imechokwa mpaka basi!
Katiba: Nashauri Bunge Batili Lililopo Livunjwe!, Liundwe Bunge Halali la Katiba!.
Mchakato Huu wa Katiba, ni Umasikini Wetu!, Tujikubali
Ikithibitika ZNZ Haikushirikishwa, P'se JK Simamisha Huu Mchakato Batili!.
Chonde Chonde Rais JK: Msimamo wa Serikali ...
Tahadhari ya hatari: CCM Imepania Kufanya Kinyume cha
Kama Kweli Nia ya Dhati ni Kuimarisha Muungano, Then

Kidumu cha Mapinduzi!.

CCM Oye!.

Pasco
 
Sawa sio zetu...Na kodi?
Kampuni zinapouziana hisa lazima zilipe Huyo aliegawa kalipa kodi ila huyo mwenye hisa nyingi kaondoka na kodi zetu tafsiri Sahihi ni Mwizi.

Kutokua imara kwenye kudai kodi ni uzembe wa TRA angalia nyendo zako usikurupuke kuita watu wezi
 
Mkuu Mpitwaga, kwanza asante, pili nakubaliana kuwa hizo fedha zimepigwa!, zimeibiwa!, mwizi ni PAP, ameiba fedha za IPTL zilizokuwa na VAT ndani yake!.

Hili la mimi kuwa CCM sina tatizo nalo kabisa!, Pasco wa JF ni Mwana CCM damu ila anajifanya hana chama!.

Hizi ni baadhi ya Threads zangu kutetea chama changu CCM na kumfagilia Mwenyekiti wangu wa chama!.

Mapungufu ya JK: Ni Rais Dhaifu! -

CCM Imechokwa; CHADEMA Haijajipanga!
Yametimia!, CCM Imechokwa!, Chadema Njia Nyeupe 2015 ...
Mtazamo: Kanda ya kaskazini, ccm imechokwa mpaka basi!
Katiba: Nashauri Bunge Batili Lililopo Livunjwe!, Liundwe Bunge Halali la Katiba!.
Mchakato Huu wa Katiba, ni Umasikini Wetu!, Tujikubali
Ikithibitika ZNZ Haikushirikishwa, P'se JK Simamisha Huu Mchakato Batili!.
Chonde Chonde Rais JK: Msimamo wa Serikali ...
Tahadhari ya hatari: CCM Imepania Kufanya Kinyume cha
Kama Kweli Nia ya Dhati ni Kuimarisha Muungano, Then

Kidumu cha Mapinduzi!.

CCM Oye!.

Pasco

Thibitisha
 
Wanabodi,
Kwa waliosoma fasihi, kitabu cha "An Enemy of the People" by Henrik Ibsen mnaweza kuniita mimi Pasco wa JF, kuwa ni "an enemy of the people!", Fedha za Escrow, Sio Fedha za Umma!, hizo Bilioni 128 zilizokuwa kwenye account ya Escrow, hazijaibiwa!, bali zimetumika kulipia umeme!.

Inawezekana PAP amenunua kampuni hewa, amefanya utapeli kuinunua IPTL toka kwa wamiliki halali, hayo hayatuhusu, bali malipo ya Tanesco kwenye account ya escrow ni kulipia capacity charges ya mitambo ya IPTL ambayo ni mitambo kweli sio mitambo hewa!, na pia Tanesco inalipia malipo ya huduma za umeme kweli unaokuwa genereted na mitambo ya IPTL, ni umeme kweli na sio umeme hewa!, na imeelezwa kuwa Tanesco bado inadaiwa!.

Ukiwa mkweli sana wa type ya ukweli huu, pia lazima uwe tayari to pay the price!.

Niko tayari to pay the price of expresing my opinion kuwa Nimesikitishwa!, Huzunishwa!, na Kufadhaishwa na Uongo wa Kamati ya PAC!-Escrow Sio Fedha za Umma!.

Pasco.

Nafanya mapitio, kwa ku compare na ku contrast maoni yangu na ya JK!.

Pasco.
 
Back
Top Bottom