Uchaguzi 2020 Nimesikitishwa na ubinafsi wa CHADEMA katika mkakati wa wapinzani kusimamisha mgombea mmoja

Tulia ww
 
Mkuu unatakiwa uwe makini sana , hatuna shaka na Maalim Seif , 2015 Zitto alikuwa nje ya UKAWA , Uliwahi kujiuliza kwanini ? Zitto Kabwe ndio mpinzani pekee aliyebaki ndani ya bunge siku Magufuli analihutubia bunge kwa mara ya kwanza baada ya wapinzani wote kuondoka kupinga Mamluki Dr Shein mtu aliyeshindwa uchaguzi na Maalim Seif kuingia bungeni , umewahi kujiuliza hili ?

Sisemi Zitto yuko vile vile , maana watu hubadilika , bali ni lazima ukafahamu kwamba haya mambo yanahitaji umakini mkubwa sana , kwa jinsi Zitto alivyokuwa si rahisi tena kwa Chadema kujiingiza kichwa kichwa , ni lazima tathmini kubwa ifanyike , mimi ni miongoni mwa wanaoamini katika ushirikiano , tena sana kabisa , lakini ni lazima kushirikiana kwa umakini sana
 
ACT Kigoma ina nguvu, hebu niambie wana majimbo mangapi waliyoshinda huko uchaguzi mkuu uliopita?

Hata ukisema wana nguvu Pwani, niambie wana majimbo mangapi waliyoshinda huko Pwani uchaguzi mkuu uliopita?

Inshort, umeandika mambo mengi ambayo hayapo kabisa.
 
Hivi mzee baba ACT ina wabunge wangapi na madiwani wangapi nchi nzima?
Hapo ndo makosa yalipo na huo ndo ubinafsi.
kama kigezo ni idadi ya wabunge kwa nini Chadema inajaribu kuungana na ACT ambao wana mbunge mmoja?
 
Kipi kilichokusikitisha Ndugu?! kwani mpaka sasa hujaandika chochote kuhusu huo ubinafsi. Anza upya...acha kubwabwaja kaka
 
CCM mnangaika Sana these days... Ngojeni dozi iwaingie
 
Hapo ndo makosa yalipo na huo ndo ubinafsi.
kama kigezo ni idadi ya wabunge kwa nini Chadema inajaribu kuungana na ACT ambao wana mbunge mmoja?
Cdm haina haja ya kuungana na virus wa lumumba, ni heri tukose kabisa kuliko kushirikiana na watu kama kina Mwambe na lowasa amabao nia yao ni kuimaliza cdm.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…