Nimesingiziwa mimba isiyo yangu, wanawake tuishi nao kwa akili kweli

Nimesingiziwa mimba isiyo yangu, wanawake tuishi nao kwa akili kweli

Hiyo hali uliyokuw nayo mkuu ,ndo hali inayonisumbua Mimi , japo me nimeamua kutulia tu sijakataa mimba ila kama yangu tutajua baadae.
 
Kuwa makini sana aisee umeshakosea sasa inabidi tu urekebishe makosa, hapa naona kama alikutegeshea mimba makusudi kama alikuuliza hayo maswali, alitaka akwambie ana mimba ili umwoe yeye yan hapo nishaona inaweza kuwa mimba yako ila alikudanganya na cocacola mkuu
Sawa mkuu nisha kubali, lakini siku ile ya Coca Cola ndo mara yetu ya kwanza kukutana naye kimwili
 
Nakwambia ukweli ndoa sio mchezo ebu fikiria kuish na mtu for the rest of your life na huna amani , haifai kabisaa
Kweli mkuu hapa nisha stick kabisa,, yaani amani haipo mkuu nayeye ameamua kukaa kimya sahiz
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] baada ya kula mzigo ndo unasema wanawake wanatamaa sana[emoji23][emoji23], unajaribu kufanya hapo ni kutafuta sapoti ya kukana mimba
Daah nijipange kwa mapambano
 
Kwa hiyo tarehe 24 ilikua siku ya danger,,hiyo tarehe 28 alikua safe.. Kuna uwezekano mkubwa ujauzito ni wako mana ovulation inaweza kuwahi siku mbil kabla au baada..usiikatae mimba, subiri mtoto azaliwe ndo utaujua ukweli
 
Mimba yako hio ..kwa taarifa tu Coca cola haizuii mimba na ukipiga mahesabu alikua siku ya hatari hio tarh 24.Muombe msamaha na anza kujiandaa kua baba
 
Huu ni wizi hakuna kitu kama hicho,, yeye aseme tu ukweli
Hivi unafaham kusoma calendar kweli? Wizi upo waoi kama mzunguko wake ni siku 28_30? Au unataka tu kukimbia majukumu.

Acha kumuumiza kihisia mtoto wa watu jilaumu wewe kwa kuacha kwenda kununua condom ukanunua Coca
 
Naona mjadala hauishi kama vipi nikabidhiwe huyo mwanamke mwenye mimba niendelee kujazia vitu vilivyopungua hadi mtoa mada atapokuwa tayari.
 
Habari za Jumapili njema wapendwa, sifa zote apewe Mungu muumba mbingu na nchi. Amina.

Soma kwa makini kuna fundisho hapa

Jamani nimekuja humu ndani kupata suruhisho la masaibu yanayo nisumbua na kunipa stress zaidi katika wakati huu.

Hii changamoto naona inanilemea tofauti na kupata msaada wenu ntaishia pabaya.

Maada:

Me nimekuwepo na girl friend ambae tumezoeana takriban mwezi mmoja, tumezoeana siku hadi siku baadae mwafaka ukawa baadaye tuoane.

Amekuwa akija kunitembelea kama kawaida geto,, lakini tokana na nguvu ya shetani kutuvaa tulijikuta tumeanguka.

Ilikuwa tarehe 24 ya mwezi wa 4 usiku ndo tulishiriki ngono lakini pia katika kushiriki binti aliniambia nikanunue soda ya Coca Cola kwa ajili ya kutumia kama kinga.

Basi sikuwa na hiana nikafata baada ya kunikazia kuwa yupo kwenye siku za hatari yasije tokea mengine ya mimba.

Nilipoileta basi tukaendelea na mambo mengine baada ya kumaliza alimimina na kuanza kunywa taratibu,,nikamuuliza kazi yake, anadai anapokunywa zile shahawa zinatelemka zenyewe tu.

Basi na kweli zikawa zinatelemka anajifuta.

Baada ya siku hiyo kupita tukakutana tena tarehe 28 mwezi 4 huo huo mchana.

Baada ya kumaliza, siku hiyo akaanza kudai tumbo linamuuma,nikamwambia itakuwa hali tu ya tumbo,, siku ya pili hivyo hivyo basi ikafika tarehe 6 ya mwezi wa 5 akadai haoni siku zake na siku ya pili yake hakuaona ambayo ni tarehe 7,mpaka sasa anasema yupo dry.

Nikamsihi itakuwa mabadiliko ya hali ya hewa lakini ananambia hii itakuwa mimba,, wakati huo sipo nae maana yupo kwao alisafiri hiyo tarehe 6 tokana na changamoto alizokuwa akipata alipo kuwa anaishi.

Mimi nikamsisitiza kapime tuone tatizo nini(yupo kwao mda huu) anasema ntapima tu lakini itakuwa mimba.

Nimemtolea uvivu nikamtega maswali, alidai breed aliingia tarehe 6 mwezi wa nne akatoka tarehe 9 na mimi nilikutana nae tarehe 24 kwa kinga ya soda,tarehe 28 bila kinga,.

Nimefatilia kuhusu mzunguko maana me si kweli alikuwa kwenye hatari ya kupata mimba, na nimemhusisha imekuwa kesi,nikamwambia aniambie ukweli kama hakuwa na mahusiano huko nyuma kabla yangu lakini kakana.kalia sana eti hakutegemea kama ntamwambia mambo kama hayo.

Mara mimi najua hii mimba niyako hata ukikataa,, lakini mimi moyo wangu hauna amani kabisa juu ya swala hili,, nahisi kubambikiwa mzigo usiyo kuwa wangu.

Ilikuwa imebaki kidogo tu tuanze maisha ya ndoa maana wazazi taarifa wanazo kuwa runataka kuoana,,

lakini amani moyoni mwangu haipo nahisi harufu ya usaliti imepita.

Nisiwachoshe sana wakuu swali langu.

Kwa wataalamu wa mzunguko wa hedhi hasa wanawake mnisaidie je nikweli huu mzigo ni wangu?

Maana mimi nikiangalia siku zote tulizo shiriki siyo siku za kushika mimba kufatana na huo mzunguko wake.

Asije ikawa mimba alikuwa nayo halafu kaja kutegesha kwangu.

Nikomee hapo wakuu, msaada wenu ni mhimu sana.

Asanteni.

Kwa uzoefu wangu mdogo mkuu umepiga akiwa kwenye danger zone kama kweli mara ya mwisho aliingia tar 6 naww ukapiga tar 24. Maana safe zone inaisha around 10 days baada ya kuingia bleed say tar 16. Then danger zone inaanza immediately for around 10 days means inaenda mpaka around tar 26 ikiisha hiyo inakuja safe zone for around 10 days from around tar 27 mpaka mzunguko mwingine so kama ulipiga tar 24 hiyo imo ndan ya danger zone mzee kwahyo mzigo unakuhusu huo
 
Ila elimu ni jambo la muhimu sana...

Hivi kweli kuna mtu anaamini kunywa Coke kunazuia ujauzito...!!!

Halafu mtu anadinyana bila condom wakati hata elimu ya uzazi hana, hajui kwamba mimba hiweza kutungwa hata nje ya siku za hatari kutegemeana na mabadiliko ya vichocheo...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom