Nimetafakari sana juu ya uwezo wa Askari Polisi

Nimetafakari sana juu ya uwezo wa Askari Polisi

Nadhani polic wa kwanza walifanyiwa ambush hawakuwa aware. Ndipo marehem alijichukulia advantage. ila wangejiandaa kama wanavyoenda kwenye matukio ya kijambaz sidhan kama angetoboa.
Kwa hiyo unataka kusema wahalifu wakitaka kuvamia,wawe wanawataarifu police dakika 20 kabla ili wajiandae?
 
Kwenye matukio ya ujambazi mara nyingi polisi ndio wanatega mtego, majambazi wanakuwa 'surprised'

Kwa Hamza polisi walivamiwa bila kutarajia wala kujiandaa. Kwenye mazingira hayo hata komando anaweza kuuawa.
Vipi ile kauli maarufu ya "intelijensia ya polisi"??
 
Majuzi lilipotokea tukio la kutupiana risasi baina ya vijana wetu wa jeshi la polisi na bwana Hamza vimenifanya nifikirie saana juu ya uwezo wa polisi katika kulenga shabaha! Hamza alikuwa sehemu ya wazi! Lakini zilitumika risasi nyingi saana na polisi kumshambulia hamza. Mwishowe tulisikia wameuwawa askari 3 (polisi). Huku 6 wakiwa majeruhi!

Mara kadhaa huwa tunapewa taarifa na polisi ya kuuwawa kwa watu wanaosasikika ni majambazi waliokuwa wakijibizana na risasi na polisi. Cha ajabu huwa hakuna polisi anayejeruhiwa au kudhurika. Lkn tukio la hamza linanifanya niwaze mara 2, hawa askari ambao huwauwa wote wanaojaribu kutupiana nao risasi bila ya kudhurika iweje hamza aliweza kuwasumbua vile!? Tena akiwa stationary tena eneo la wazi!

Mtu mmoja tu tena akajeruhi idadi kubwa ya vijana wetu!

Sitegemei eti kuwa watajitetea kuwa walishtukizwa maana kitendo cha askari kwenda armory ukachukua silaha na kuingia doria tafsiri yake ni kuwa upo tayari katika mapambano kwa muda wowote
Hata miongozo ya kazi yao hawaifuati. Wabeba silaha wanakuwa in pairs, kila mmoja anamlinda mwenzake. Kitendo cha polisi wawili kuuawa na mtu mmoja kinaonesha uzembe na udhaifu wa hali ya juu wa polisi wa Tanzania.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Laana za waPemba hizo zinawaandama polisi,polisi ambao nyakati za uchaguzi wao ndio wanaohesabu,wao ndio wanalinda kura,wao ndio wanaokimbia na masanduku ya kura wakiondoka nayo kwenye vituo,hili tukio limewafariji wapemba vibaya sana.

Kati ya chombo kinachopendwa na wananchi polisi walikuwa nambari wani ila upendo huo polisi wenyewe wameutupa.

Na mara nyingi wananchi wamekuwa wakiwanasihi polisi kuwa nyinyi ni kwa ajili ya watu wote aka vyama vyote kuna leo na kesho, msijiweke kuwa nyinyi ni maccm na kila kitu ni lazima CCM ashinde mtawasaidia kwa hali na silaha mnafikia kuwauwa watu ili muwasimike CCM. Polisi ludisheni upndo kwa kuwa fair bila ya kupendelea wazi wazi pasipo kificho, hili litawagalimu bei mbaya,

Japo tukio limetendwa na mwanaccm mjenzi wa ofisi nzima ya chama cha mapinduzi waliofurahia ni wapinzani wananchi waliohujumiwa na vyombo hivi ,Pemba ni sherehe kila nyumba nyuso zimekunjuka.
Hakuna wakati polisi wamewahi kupendwa. Nyumbani kwako akatoka polisi hata kama alipita kukusalimia na hatambuliki kwa majirani, akiondoka tu simu au hodi zinaanza kuliizia kuna nini.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Mi nadhani hivi vipolisi vya sasahivi pia havina nidhamu. Mara kadhaa unavikuta vimeshika silaha mikononi viko lindo lakini havina tahadhari yoyote.

Muda mwingi vinachati na simunkulikonumakininwa kazi. Ningenshauri Siro azuie polisi kuchati akiwa kazini. Hii inawezekana kuwapatia device za mawasiliano zisizoruhusu mtu kuchati.

Hiki kizazi cha polisi wa miaka ya 1985 kuja mpaka juu huku 90 hamna kitu. Maarifa na umakini mdogo sana.
Wazuiwe simu, watumie radio calls. Wanachati bunduki ziko mgongoni au mezani.

Sent from my Infinix X650B using JamiiForums mobile app
 
Kwani si wapewe Bastola kama askari wa marekani jamani hii mitutu saa nyingine kama mamizigo bhana kitambo aiweke sawa akunyooshee Adui kashachomoa bastola kamuwahi ya kichwa then anawapora mitutu yao[emoji23] Mitutu iwekwe kwaajili ya vita iliyopamba moto ila bastola itumike kwenye ulizi huu wa kawaida na doriya.
Hujui lolote kaa kimya, bastola utafanya majibizano na adui mwenye silaha kubwa?
 
UVCCM + form4 division 4 = ?
[/QUOT





Usidharau elimu ya watu wanaojitoa mhanga kwa ajili ya wengine.

Nchi maskini huwezi kuajiri wasomi pekee kwenye majeshi.

Hakuna msomi anayepigania nchi duniani kote.
Wasomi ndio nchi ,hivyo wanapiganiwa ili wafaidi usomi wao.
Wasomi kule Afghanistan wameikimbia nchi na kwenda kula bata Ulaya. Nchi inapiganiwa na mbumbu kisha wanawaita wasomu kuja kutawala.

Darasa la saba wa Tanzania walilikomboa bara la Afrika kusini na maahariki.
Wasomi walikua wanasoma kwenye Seminari za Wazungu na kuiga uzungu wote ili wafaidi usomi wao.

Waheshimu watu wanaoweka nafsi zao mbele ya AK47.
Tena Hamza alikua mstaarabu kwa Sababu ni kada mtiifu wa CCM angeweza kuleta madhara makubwa sana.

Kuna mtu alikua anajiita Carlos alisumbua sana Dunia wakiwemo Makomando.

Binadamu yeyote akiwa jasiri anaweza akafanya chochote akiwa na bomu au Bunduki. Popote anaweza akaingia na akafanya chochote kwa wakati fulani.
Ujasiri ni jambo la ajabu na muujiza mkubwa.
Mungu ndiye anayewapa nguvu walinzi wetu na kulilinda Taifa. Tusilaumu polisi wakati wenzao walipoteza maisha.
Wasomi ni akina siro na mabeyo wamekaa ofisini wanalindwa na darasa la 12 faillure masaa 48.
Hata wewe nyumbani kwako kuna mlinzi asiyejua hata kusoma. Watoto wanalelewa na hausi geli drasa la saba wanakua na kuwadharau walezi wao na kuwaheshimu wazazi waliokuwa bize utumwani au kazini.
Ndivyo dunia ya Gwajima na CCM ilivyo.
 
Ile lugha ya polisi wameua majambazi yaliyokuwa yanarushiana risasi na polisi unaiamini?
 
Back
Top Bottom