Nimetapeliwa zaidi ya Tsh. 45,000,000 kwa kuuziwa kiwanja feki

Nimetapeliwa zaidi ya Tsh. 45,000,000 kwa kuuziwa kiwanja feki

Mkuu kila situation huwa inaamuliwa kwa namna yake. Katika sheria ya mikataba Tanzania kuna kitu kinaitwa 'voidable contract ' hii ni aina ya mkataba ambao ni halali hadi pale mmoja wa pande za mkataba atakapogundua tatizo na kutoendelea na mkataba, ila akiamua kuendelea nao kunakua hakuna tatizo kisheria.

Sasa kwa wewe sijui kama msimamizi wa mirathi ya marehemu baba mwenye nyumba ni nani na kama kiwanja kilikua cha urithi, na kama kila upande wa urithi umepata mgao wake. Nadhani tukipata maelezo ya kutosha tunaweza kuwa na chochote cha kutoa maoni.
Ni hivi huyu mwanamke aliishatarakiana na mumewake (ambaye ni marehemu) na baada ya taraka waligawana nyumba na viwanja....na kabla hajafariki alikuwa ni mstaafu na aliwagawia wanae urithi (fedha) na hivyo kila mmoja ana maisha yake kivyake ila siku ya kuuziana kiwanja walikuwepo watoto wake wawili tu kati ya wanne
 
Mkuu kila situation huwa inaamuliwa kwa namna yake. Katika sheria ya mikataba Tanzania kuna kitu kinaitwa 'voidable contract ' hii ni aina ya mkataba ambao ni halali hadi pale mmoja wa pande za mkataba atakapogundua tatizo na kutoendelea na mkataba, ila akiamua kuendelea nao kunakua hakuna tatizo kisheria.

Sasa kwa wewe sijui kama msimamizi wa mirathi ya marehemu baba mwenye nyumba ni nani na kama kiwanja kilikua cha urithi, na kama kila upande wa urithi umepata mgao wake. Nadhani tukipata maelezo ya kutosha tunaweza kuwa na chochote cha kutoa maoni.
Unatoa maelezo mazuri sana lakini watanzania hawaelewi. Haya mambo ya kuhusisha mabalozi wa nyumba kumi kumi, wenyeviti wa mitaa au vijijini yapo sana. Na mbaya zaidi huwa wanachaji fedha nyingi sana. BTW kuhusu utapeli wa viwanja au nyumba hata serikali haiwezi kukwepa lawama. Nina uhakika wakiweka taratibu nzuri utapeli utapungua kwa kiasi kikubwa.
 
Mkuu kwenye sheria ya ardhi, hao hawatambuliki kabisa kwenye kuuziana , labda kama ni ardhi ya kijiji.
Anayetambulika ni hakimu, na mawakili tu, ndio wanaoweza kusimamia mauziano hayo na yakawa na nguvu ya kisheria.zile hati za serikali za mtaa ni makaratasi tu, ambayo kisheria hayana nguvu kabisa.Ukiwa nalo hilo halafu akaja mtu akauziwa hicho kiwanja chako tena na akawa na hati ya mauziano yaliyosimamiwa na wakili, huwezi kushinda hiyo kesi kwa kuonyesha hizo karatasi.

serikali ya kijiji /mtaa wanakosaje nguvu kwenye kuhalalisha mikataba ya mauziano kama majirani au kama wanahusika na mtaa/kijiji husika
 
Ninaamini kabisa kuwa utapeli upo lakini kuna namna huwa watu tunaweza kuchukua tahadhari na kupunguza visa vya kutapeliwa.
KWA VIWANJA VILIVYOPIMWA:
[emoji91]Baada ya kuwa umeoneshwa kiwanja husika na mmekubaliana bei, hakikisha kuwa unampa wakili kazi ya kusimamia mauzo hayo maana ni lazma atafanya search katika mamlaka husika kujua mmiliki halali ama kama kuna attachment yoyote juu ya kiwanja husika
[emoji91] Hakikisha unajua marital status ya muuza kiwanja, kama atakwambia wameachana hakikisha anakuonesha hati ya talaka ama ya kutengana iliyotolewa na MAHAKAMA na sio vinginevyo.
[emoji91] Endapo ametengana kienyeji na mwenza wake hakikisha huyo mwenza anajaza fomu maalumu (spousal consent) ya kuridhia mauzo ya kiwanja husika yaani hata kama wamenuniana hakikisha mwenza amejaza hiyo form yeye mwenyewe.
[emoji91] Kama kutakua na wasiwasi wowote wa vipimo vya kiwanja husika vile vya kwenye nyaraka na uhalisia hakikisha mnaitumia mamlaka ya ardhi eneo husika kisha kuwakutanisha na majirani wako ili kuweka sawa suala hilo.

KWA VIWANJA/MAENEO AMBAYO HAYAJAPIMWA:
[emoji91]Hakikisha kuwa unawapata watu wote wa pande zote ambazo eneo hilo mnapakana na wakuoneshe na mkubaliane wote mipaka halisi ya eneo unalotaka kununua na hawa ndio watakua mashuhuda wa mjataba wako.
[emoji91]Hakikisha mauziano hayo yanasimamiwa na wakili ambaye atakuongiza katika kufanya search na taratibu sahihi.
[emoji91]Hakikisha mwenza wa anayekuuzia eneo husika anajaza form maalumu ya kuridhia mauzo hayo na kama wameachana hakikisha unapata nyaraka ya mahakama kuthibitisha hili.

KWA MAENEO YA UKOO/FAMILIA/URITHI.
Hapa ndio kuna kivumbi na wanunuzi hupoteza sana pesa hapa.
Kuna wakati ambapo mzazi/mmiliki wa eneo akifariki basi familia haifungui mirathi mahakamani bali hukaa kikao na kuamua kutoaiuza ardhi lakini wakagawanya vyumba ama hisa katika nyumba husika mfano, huweza kugawana vyumba hivyo kila mmoja akawa na mpangaji wake ama wakaipangisha kisha kila kodi ikitolewa basi wanagawana.
Sasa endapo unataka kununua ardhi ya mazingira ya namna hii unatakiwa kuwa makini sanaaa na endapo nyumba ni ya familia hakikisha kuwa wale wanafamilia woooote yaani namaanisha WOTE sio wengi hapana, nasema WANAFAMILIA WOTE wahaohusika na ardhi ama nyumba husika ndipo muweze kuendelea na mauzo. Hii ni kwa sababu endapo ikatokea mmoja ama sehemu ya wanahisa wa hiyo ardhi ya familia hakuridhia basi utakua umepigwaaa(rejea kilichomkuta S. H. Amon hapo Kariakoo)
Iwapo nyumba inamilikiwa na Ukoo yaani vizazi hata viwili ama vitatu yaani nyumba alikua anamiliki babu yangu ambaye alikua na watoto nane na wote hao walikua na familia, wakafariki 4 na watoto wa babu wakazaa tukatokea sisi na baadhi yetu tumeshafariki lakini tumeacha watoto wetu ambao wana haki kupitia baba na babu zao aisee mimi NINAKUSHAURU USINUNUE ARDHI HIYO hakikisha kabla ya kununua au kulipia hata sh mia unawasiliana na wakili wako.


Kiukweli wakuu ukitapeliwa kwenye kiwanja kilichopimwa ni lazma wewe mnunuzi kuna mahali ulizembea kwenye utaratibu mzima wa manunuzi maana kwa upande wa hivi viwanja vilivyopimwa utaratibu upo wazi sana.
Nilichogundua ni kuwa wengi wana mazoea na kukalili taratibu za kizamani zisizotambuliwa kisheria yaani mtu anaona kutoa 2M kwa wakili asimamie mchakato mzima wa mauziano ya 50M anamuamini dalali ambaye atalipwa 10% na mtedaji/mwenyekiti halafu anatoa hela[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

HAKIKISHENI MNAFUATA MIONGOZO YA WANASHERIA KUPUNGUZA KUTAPELIWA
[emoji106]
 
serikali ya kijiji /mtaa wanakosaje nguvu kwenye kuhalalisha mikataba ya mauziano kama majirani au kama wanahusika na mtaa/kijiji husika
Sio suala la kubishana, ila kwa sheria ya ardhi ya Tz, haiwatambui hao kuwa wanaruhusiwa kisheria kusimamia mauziano ya ardhi hasa baina ya mtu na mtu.kama una bishana na sheria sawa.wale ni hiyo sio kazi kazi bali zile 10%tu za mauziano ndio zinawafanya afanye kama ni jukumu lao, lakini utakapo tokea mgogoro wowote ule wa kisheria hawana uwezo wa kukusaidia kwa makaratasi yao hayo.
 
Ni hivi huyu mwanamke aliishatarakiana na mumewake (ambaye ni marehemu) na baada ya taraka waligawana nyumba na viwanja....na kabla hajafariki alikuwa ni mstaafu na aliwagawia wanae urithi (fedha) na hivyo kila mmoja ana maisha yake kivyake ila siku ya kuuziana kiwanja walikuwepo watoto wake wawili tu kati ya wanne
Kama ni hivyo relax, endelea kula maisha. Hapo hata hao wanae wasingekuwepo kabisaaa ni sawa tu maana umeuziwa na mmiliki halali.
 
Hela inatafutwa mkuu poke sana Ila umejifunza
 
Kama hauja ikopa piga moyo konde ili maisha mengine yaendelee
 
Sio suala la kubishana, ila kwa sheria ya ardhi ya Tz, haiwatambui hao kuwa wanaruhusiwa kisheria kusimamia mauziano ya ardhi hasa baina ya mtu na mtu.kama una bishana na sheria sawa.wale ni hiyo sio kazi kazi bali zile 10%tu za mauziano ndio zinawafanya afanye kama ni jukumu lao, lakini utakapo tokea mgogoro wowote ule wa kisheria hawana uwezo wa kukusaidia kwa makaratasi yao hayo.
Mkuu vp kama umetumia mwanasheria na ujumbe wa mtaa bila kuhusisha serikali ya mtaa?
 
Kama ni hivyo relax, endelea kula maisha. Hapo hata hao wanae wasingekuwepo kabisaaa ni sawa tu maana umeuziwa na mmiliki halali.
Daaaah afadhar.....tena kesho napeleka trip mbili za mawe ya msingi
 
Unatoa maelezo mazuri sana lakini watanzania hawaelewi. Haya mambo ya kuhusisha mabalozi wa nyumba kumi kumi, wenyeviti wa mitaa au vijijini yapo sana. Na mbaya zaidi huwa wanachaji fedha nyingi sana. BTW kuhusu utapeli wa viwanja au nyumba hata serikali haiwezi kukwepa lawama. Nina uhakika wakiweka taratibu nzuri utapeli utapungua kwa kiasi kikubwa.
Mkuu mimi hapa ninaamini na nitazidi kuamini kuwa utapeli katika viwanja kwa zaidi ya 85% unachangiwa na sisi wenyewe wanunuzi. Mkuu mimi ni mwanasheria, ila nikwambie ukweli kabisa kuna wateja hamshaurikiiii hamtaki kusikiliza ya wataalamu na mwisho wa siku mnapigwa.
Mfano, mteja anatafuta kiwanja anaona dalali amepost. Baada ya hapo anaenda kuona kiwanja, dalali anatia maneno ya kuonesha kuwa wengi wanahitaji kiwanja hicho, anamleta mtu ambaye anadai kuwa ndiye mmiliki(kumbe ni msimamizi tu wa familia na sio mmiliki). Mnaenda kwa mwenyekiti wa mtaa anakula 10% dalali anakula % yake halafu mnaandikishana pale kisha mnampelekea wakili makaratasi yenu kuwa 'AWAGONGEE MUHURI' mna laki 5😂😂😂😂😂😂 wakili anakuuliza kama umefanya utafiti kuwa hakuna shida yoyote? Unajibu ndioooo na mwenyekiti ametuthibitishia, wakili anakwambia kama umejiridhisha basi hakuna shida(huku akitabasamu) maana hata akikukatalia utaenda kwa mwingine na unaweza kukutana na karani wake akagonga huo muhuri kwa laki 2.
Kinanuka baadae ndio unatambua kuwa dalali na mwenyekiti hawatambuliki kwa namna yoyote katika mikataba ya ardhi binafsi, unamfuata wakili anakukumbusha maswali ya siku hiyo na mwisho wa siku hata kesi yako hawezi kuisimamia mahakamani tena unabaki kumuachia Mungu 😂😂😂😂😂😂😂😂
 
Mkuu vp kama umetumia mwanasheria na ujumbe wa mtaa bila kuhusisha serikali ya mtaa?
Mkuu, kisheria anayetakiwa kusimamia mauziano ya ardhi binafi hapa nchini ni WAKILI na HAKIMU, hao ndio wapo na mandate ya kuweza kuandaa mikataba hiyo na kukuelekeza taratibu sahihi, kuna mauziano ya ardhi yalibatilishwa na mahakama kisa tu stamp duty haikulipwa na hiki huwa hakifanyiki mkiuziana huko kwa mtendaji.
Huyo mtendaji awe kama shahidi wala hulazimishwi chochoteee yeye kuwepo kwenye list ya mashahidi ama yeye kuidhinisha mauziano ya ardhi bali WAKILI ndio mwenye nafasi hiyo mkuu. Kuna mahali kuna uzi niliwahi kueleza haya wakasema tunataka hela na kutangaza biashara na mtu akanusurika kupigwa akanishukuru palepale kwenye uzi.

Tuzingatie taratibu maana siku hizi matapeli wamekua smart kwa hiyo ikitokea upenyo kidogo tu umekwishaa
 
Hivyo ndio waganga hua wanawatapeli ukute mganga mwenyewe choka mbaya balaa kosa ajisaidie yeye atoke kwenye umaskini eti akisaidie wewe ulienshinda uwezo
Mganga sio choka mbaya, na mganga hatoi utajiri mganga Ni Kama dalali anakuunganisha wewe (mteja) na majini (ndo wanatoa utajiri) mganga anahitaji pesa Kama malipo yake lakini majini hayahitaji pesa maana yanazo nyingi tuu!yenyewe yatahitaji ufate masharti ambayo utaelekezwa na mganga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sio suala la kubishana, ila kwa sheria ya ardhi ya Tz, haiwatambui hao kuwa wanaruhusiwa kisheria kusimamia mauziano ya ardhi hasa baina ya mtu na mtu.kama una bishana na sheria sawa.wale ni hiyo sio kazi kazi bali zile 10%tu za mauziano ndio zinawafanya afanye kama ni jukumu lao, lakini utakapo tokea mgogoro wowote ule wa kisheria hawana uwezo wa kukusaidia kwa makaratasi yao hayo.
Wewe ni mwanasheria? Sio kaa tunabishana ukiweka hiyo perception tunakua hatujifunzi, haya swali langu ni hivi nguvu yao ni kwenye ushahidi kwanini useme hawana kitu juu ya sheria ya ardhi? Mauziano bila shahidi mkataba unakuaje hapo sio valid, ila pia mawakili wanaweza pitisha mikataba kisheria lakini hawajui background ya hiyo ardhi
 
Mkuu, kisheria anayetakiwa kusimamia mauziano ya ardhi binafi hapa nchini ni WAKILI na HAKIMU, hao ndio wapo na mandate ya kuweza kuandaa mikataba hiyo na kukuelekeza taratibu sahihi, kuna mauziano ya ardhi yalibatilishwa na mahakama kisa tu stamp duty haikulipwa na hiki huwa hakifanyiki mkiuziana huko kwa mtendaji.
Huyo mtendaji awe kama shahidi wala hulazimishwi chochoteee yeye kuwepo kwenye list ya mashahidi ama yeye kuidhinisha mauziano ya ardhi bali WAKILI ndio mwenye nafasi hiyo mkuu. Kuna mahali kuna uzi niliwahi kueleza haya wakasema tunataka hela na kutangaza biashara na mtu akanusurika kupigwa akanishukuru palepale kwenye uzi.

Tuzingatie taratibu maana siku hizi matapeli wamekua smart kwa hiyo ikitokea upenyo kidogo tu umekwishaa
Ahsante,
 
Back
Top Bottom