Nimetapeliwa zaidi ya Tsh. 45,000,000 kwa kuuziwa kiwanja feki

Nimetapeliwa zaidi ya Tsh. 45,000,000 kwa kuuziwa kiwanja feki

Mganga sio choka mbaya, na mganga hatoi utajiri mganga Ni Kama dalali anakuunganisha wewe (mteja) na majini (ndo wanatoa utajiri) mganga anahitaji pesa Kama malipo yake lakini majini hayahitaji pesa maana yanazo nyingi tuu!yenyewe yatahitaji ufate masharti ambayo utaelekezwa na mganga.

Sent using Jamii Forums mobile app
True jini anakupa utajiri nawe unampa jini kafara ya damu.
Damu ni chakula cha majini.
Waganga na wachawi ni matajiri Sana wa pesa lakini masharti yao hayawaruhusu kumiliki mali.Pesa zao wanazitumia kununua vifaa vyao vya Kazi
 
hujatapeliwa umebondwa na chuma kizito.
unakua ngangari kuitafuta hela ila kupoteza sasa mzembe.
hao wenzio mliotapeliwa wote walijiandaa kukupa uenyekiti wa kijiji sahii wanakuona boya mwenzao tu.
 
Ninaamini kabisa kuwa utapeli upo lakini kuna namna huwa watu tunaweza kuchukua tahadhari na kupunguza visa vya kutapeliwa.
KWA VIWANJA VILIVYOPIMWA:
[emoji91]Baada ya kuwa umeoneshwa kiwanja husika na mmekubaliana bei, hakikisha kuwa unampa wakili kazi ya kusimamia mauzo hayo maana ni lazma atafanya search katika mamlaka husika kujua mmiliki halali ama kama kuna attachment yoyote juu ya kiwanja husika
[emoji91] Hakikisha unajua marital status ya muuza kiwanja, kama atakwambia wameachana hakikisha anakuonesha hati ya talaka ama ya kutengana iliyotolewa na MAHAKAMA na sio vinginevyo.
[emoji91] Endapo ametengana kienyeji na mwenza wake hakikisha huyo mwenza anajaza fomu maalumu (spousal consent) ya kuridhia mauzo ya kiwanja husika yaani hata kama wamenuniana hakikisha mwenza amejaza hiyo form yeye mwenyewe.
[emoji91] Kama kutakua na wasiwasi wowote wa vipimo vya kiwanja husika vile vya kwenye nyaraka na uhalisia hakikisha mnaitumia mamlaka ya ardhi eneo husika kisha kuwakutanisha na majirani wako ili kuweka sawa suala hilo.

KWA VIWANJA/MAENEO AMBAYO HAYAJAPIMWA:
[emoji91]Hakikisha kuwa unawapata watu wote wa pande zote ambazo eneo hilo mnapakana na wakuoneshe na mkubaliane wote mipaka halisi ya eneo unalotaka kununua na hawa ndio watakua mashuhuda wa mjataba wako.
[emoji91]Hakikisha mauziano hayo yanasimamiwa na wakili ambaye atakuongiza katika kufanya search na taratibu sahihi.
[emoji91]Hakikisha mwenza wa anayekuuzia eneo husika anajaza form maalumu ya kuridhia mauzo hayo na kama wameachana hakikisha unapata nyaraka ya mahakama kuthibitisha hili.

KWA MAENEO YA UKOO/FAMILIA/URITHI.
Hapa ndio kuna kivumbi na wanunuzi hupoteza sana pesa hapa.
Kuna wakati ambapo mzazi/mmiliki wa eneo akifariki basi familia haifungui mirathi mahakamani bali hukaa kikao na kuamua kutoaiuza ardhi lakini wakagawanya vyumba ama hisa katika nyumba husika mfano, huweza kugawana vyumba hivyo kila mmoja akawa na mpangaji wake ama wakaipangisha kisha kila kodi ikitolewa basi wanagawana.
Sasa endapo unataka kununua ardhi ya mazingira ya namna hii unatakiwa kuwa makini sanaaa na endapo nyumba ni ya familia hakikisha kuwa wale wanafamilia woooote yaani namaanisha WOTE sio wengi hapana, nasema WANAFAMILIA WOTE wahaohusika na ardhi ama nyumba husika ndipo muweze kuendelea na mauzo. Hii ni kwa sababu endapo ikatokea mmoja ama sehemu ya wanahisa wa hiyo ardhi ya familia hakuridhia basi utakua umepigwaaa(rejea kilichomkuta S. H. Amon hapo Kariakoo)
Iwapo nyumba inamilikiwa na Ukoo yaani vizazi hata viwili ama vitatu yaani nyumba alikua anamiliki babu yangu ambaye alikua na watoto nane na wote hao walikua na familia, wakafariki 4 na watoto wa babu wakazaa tukatokea sisi na baadhi yetu tumeshafariki lakini tumeacha watoto wetu ambao wana haki kupitia baba na babu zao aisee mimi NINAKUSHAURU USINUNUE ARDHI HIYO hakikisha kabla ya kununua au kulipia hata sh mia unawasiliana na wakili wako.


Kiukweli wakuu ukitapeliwa kwenye kiwanja kilichopimwa ni lazma wewe mnunuzi kuna mahali ulizembea kwenye utaratibu mzima wa manunuzi maana kwa upande wa hivi viwanja vilivyopimwa utaratibu upo wazi sana.
Nilichogundua ni kuwa wengi wana mazoea na kukalili taratibu za kizamani zisizotambuliwa kisheria yaani mtu anaona kutoa 2M kwa wakili asimamie mchakato mzima wa mauziano ya 50M anamuamini dalali ambaye atalipwa 10% na mtedaji/mwenyekiti halafu anatoa hela[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]

HAKIKISHENI MNAFUATA MIONGOZO YA WANASHERIA KUPUNGUZA KUTAPELIWA
Hata mm hapa nais nimepigwa mnk nilinunua eneo la shamba huko mbeya bila kumshirikisha mke wa jamaa aliyeniuuzia Happ kwa kweli nimekozea nimewashirkisha wajomba zake na mwenyekit wa kijij tu bila kwenda offisini eeh mungu wangu nimemwaga pesa zangu buree duh

Ngao popote nakutafuta
 
Haya mambo yasikie tu.

Nina siku ya nne leo tangu nigundue kwamba nimepigwa, hata kula vizuri siwezi, nawaonea wivu wenzangu walionunua maeneo madogo kwa bei za 15m kushuka chini. Naona hasara yao ni ndogo kuliko yangu.
Bwana Mangushi,
Nakupa Pole sana,
Watu hao ni Walaghai eeee,
Wanaitwa Matapeli eeee,

Watu hao wameenea sana, kila pembe hapa mjini, kazi yao ni kuibia watu, jina lao matapeli.
 
Hata mm hapa nais nimepigwa mnk nilinunua eneo la shamba huko mbeya bila kumshirikisha mke wa jamaa aliyeniuuzia Happ kwa kweli nimekozea nimewashirkisha wajomba zake na mwenyekit wa kijij tu bila kwenda offisini eeh mungu wangu nimemwaga pesa zangu buree duh

Ngao popote nakutafuta
Hapana mkuu usikate tamaa, hiyo werevu ndio huwa wanakugeuka ila kwa Mbeya kule ni mfumo dume zaidi hivyo mara nyingi mama anakua ameridhia. Ila kaa ukipiga maombi sana wasivurugane halafu waachane na mama apate wakili mwerevu utajua kwa kupata hela yako😂😂😂😂😂😂. Hii hufanyika zaidi katika mali za ndoa/zilizochumwa pamoja.

Ila kaa kwa machale hiyo ni voidable contract
 
Wewe ni mwanasheria? Sio kaa tunabishana ukiweka hiyo perception tunakua hatujifunzi, haya swali langu ni hivi nguvu yao ni kwenye ushahidi kwanini useme hawana kitu juu ya sheria ya ardhi? Mauziano bila shahidi mkataba unakuaje hapo sio valid, ila pia mawakili wanaweza pitisha mikataba kisheria lakini hawajui background ya hiyo ardhi

Wakili wako anawajibu wakufuatilia taarifa zote kuhusu hiyo aridhi kabla ya mauziano,kwa hiyo lazima ajue background ya hiyo ardhi,mana hata sheria inambana mnunuzi kabla hujanunua aridhi hakikisha una taarifa sahihi vinginevyo utalia na kusaga meno huko mbele.
 
Hapana mkuu usikate tamaa, hiyo werevu ndio huwa wanakugeuka ila kwa Mbeya kule ni mfumo dume zaidi hivyo mara nyingi mama anakua ameridhia. Ila kaa ukipiga maombi sana wasivurugane halafu waachane na mama apate wakili mwerevu utajua kwa kupata hela yako[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]. Hii hufanyika zaidi katika mali za ndoa/zilizochumwa pamoja.

Ila kaa kwa machale hiyo ni voidable contract

Wakivurugana lazima aite maji mma hapo Land Act na The Village land act pamoja na Law of marriage Act lazima imsulubishe[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Sio suala la kubishana, ila kwa sheria ya ardhi ya Tz, haiwatambui hao kuwa wanaruhusiwa kisheria kusimamia mauziano ya ardhi hasa baina ya mtu na mtu.kama una bishana na sheria sawa.wale ni hiyo sio kazi kazi bali zile 10%tu za mauziano ndio zinawafanya afanye kama ni jukumu lao, lakini utakapo tokea mgogoro wowote ule wa kisheria hawana uwezo wa kukusaidia kwa makaratasi yao hayo.
- mwenye masikio na asikie
-Wenyeviti wa serikali za mitaa hawaruhusiwi kujihusisha na Ardhi ya jumla (general Land) hata Waziri wa ardhi (Mhe.Lukuvi Kama alivyokuwa Waziri wa ardhi) alikuwa anawapiga marufuku
- Mwenyekiti wa serikali ya Mtaa sio mtaalam wa Ardhi, Wakili atakuongoza kwenye kufanya utafiti wa Ardhi ili kujua mpango wa matumizi ardhi ya eneo husika kwa Mujibu wa Sheria ya Urban planning Act, ataenda Kwa msajili wa hati za Ardhi (kwa ardhi zilizopimwa na kusajiliwa) kuangalia hiyo ardhi mmiliki halali ni Nani?, Inamilikiwa kwa mfumo gani i.e ya wanandoa, au inamilikiwa na mtu zaidi ya mmoja, kuangalià Kama imekopewa kwenye benki fulani, kuangalia Kama zuio lolote limewekwa kwenye hiyo ardhi na Kama Kuna upangishaji wa muda wa muda mrefu kwa Mujibu wa Sheria ya Land registration act na Land Act, Wakili atakuongoza jinsi ya kuandika mikataba ambayo iko clear isiyo na utata ili kuepuka doctrine of contra proferetem,.
 
Mkuu sio kwamba serikali ya mtaa hawakusaidii ila HAWANA MAMLAKA WALA UWEZO WOWOTE WA KUKUSAIDIA KWA LOLOTE KISHERIA. Labda iwe hiyo ni ardhi ya kijiji, ila kama ni ardhi binafsi aisee hao ni sawa na hakuna. Wakili ama hakimu ndio maafisa pekee wanaoruhusiwa kusimamia mikataba ya mauziano ya ardhi.
Mkuu CAT wametoa decision inayopiga marufuku Mahakimu kujihusisha na Mambo ya mikataba
 
Mkuu mm nikinunua kiwanja kwanza napoteza mda wiki nzima nishawasaidia marafiki kununua viwanja pia na nishawahi waokoa wengi tuu. Ww ukimalizana nao km viwanja visivyo nahati washakuonesha kiwanja kilipo nenda kwa mjumbe ulizia mmiliki nani, pia ulizia eneo lipo kwa ajili ya makazi ama laa, ukitoka hapo nenda kwa majirani hata watatu hakikisha maelezo yanafanana. Km kuna lolote utajua tuu.
 
Wewe ni mwanasheria? Sio kaa tunabishana ukiweka hiyo perception tunakua hatujifunzi, haya swali langu ni hivi nguvu yao ni kwenye ushahidi kwanini useme hawana kitu juu ya sheria ya ardhi? Mauziano bila shahidi mkataba unakuaje hapo sio valid, ila pia mawakili wanaweza pitisha mikataba kisheria lakini hawajui background ya hiyo ardhi
Iko hivi, sheria haiwatambui, ila wao wakisimamia mauziano hayo ni sawa tu kama umemuita mtu yoyote yule kama shahidi tu, na sio kwa cheo chake!!yeye anachokusaidia ni kukuhakikishia kuwa anayeuza ndio mmiliki wa ardhi hiyo, japo naye anaweza kuwa hana uhakika nalo, kwenye mauziano unaweza kuwa na muuzaji , na mashahidi, na biashara ikafanyika, lakini kisheria kuna watu ambao ndio wamepewa jukumu hilo, hiyo document, ichukue ipeleke kwa wakili akuandalie , document, yenyewe ambayo hata huko mbele ukitokea mgogoro ni rahisi kuwa sehemu salama.Tatizo huwa tunakimbia gharama huko.
Inshu sio kujua background ya ardhi, kwani hao wenyeviti huwa wanakuwa na kumbukumbu tena baada ya kuchukua 10%yao?!labda mgogoro utokee baina ya pande mbili na wote muwe na hayo mavifungashio ya serikali za mitaa, , ndio wataangalia, labda muuzaji sahihi ni nani, nani alikuwa wa kwanza kunununua.
 
Iko hivi, sheria haiwatambui, ila wao wakisimamia mauziano hayo ni sawa tu kama umemuita mtu yoyote yule kama shahidi tu, na sio kwa cheo chake!!yeye anachokusaidia ni kukuhakikishia kuwa anayeuza ndio mmiliki wa ardhi hiyo, japo naye anaweza kuwa hana uhakika nalo, kwenye mauziano unaweza kuwa na muuzaji , na mashahidi, na biashara ikafanyika, lakini kisheria kuna watu ambao ndio wamepewa jukumu hilo, hiyo document, ichukue ipeleke kwa wakili akuandalie , document, yenyewe ambayo hata huko mbele ukitokea mgogoro ni rahisi kuwa sehemu salama.Tatizo huwa tunakimbia gharama huko.
Inshu sio kujua background ya ardhi, kwani hao wenyeviti huwa wanakuwa na kumbukumbu tena baada ya kuchukua 10%yao?!labda mgogoro utokee baina ya pande mbili na wote muwe na hayo mavifungashio ya serikali za mitaa, , ndio wataangalia, labda muuzaji sahihi ni nani, nani alikuwa wa kwanza kunununua.
  • yeah nakubaliana na ww Mkuu
  • ndiyo maana mtu akiwa Wakili anakuwa na vyeo vitatu cha Kwanza Ni Wakili hiki Cheo ndiyo kinampa haki ya kuwakilisha Watu Mahakamani, Cheo cha pili ni Notary public Cheo hiki kimpa mamlaka ya kuthibitisha/kushuhudia mauziano, Cheo cha tatu ni Commissioner for Oaths cheo hiki kinampa haki ya kuandaa viapo, na kuthibitisha nyaraka nk
 
Mimi naweza kukuchezeshea hicho ulichotapeliwa na kikawa chako kweli.......
 
Nitafutie mbuzi weusi watatu, ng’ombe mmoja awe wa kisasa jike wa maziwa awe amezaa mara moja ndio dawa itashika, kuku wawili mmoja jogoo na jike, nitafutie na mchele wa kyela ndoo mbili kubwa ili kutoa kafara kwa wazee, na vitenge vitatu was original vya kufunikia dawa halafu hela usinipe yoyote ukifanikiwa utarudi kushukuru.
[emoji23][emoji23] oyaa unataka kuweka stock ya chakula nini
 
Juzi kati hapa nimeponea chupuchupu Mara 2 nikaona tu maneno siyaelewi Mara hivi Mara sijui biashara ifanyike chapchap mtu ana safari sijui nini nikaona huu utapeli live [emoji119][emoji119][emoji119] Dodoma kumekithiri utapeli
 
Back
Top Bottom