Nimetapeliwa zaidi ya Tsh. 45,000,000 kwa kuuziwa kiwanja feki

Nimetapeliwa zaidi ya Tsh. 45,000,000 kwa kuuziwa kiwanja feki

Wengine kumuita wakili wanaona gharama.
Hawajui kuwa wakili ndo mtetezi wako hata ikitokea matatizo anayekwenda mahakamani kufuatilia kesi NI yule hakimu .
Wakati wewe unaendelea na Mambo yako
Nakazia...

Hata Serikali za Mitaa siku hizi nao ni wale wale tu...
Wanachojali ni ile asilimia yao.. likikupata janga huko unapambana mwenyewe..
 
Kaka serikali ni kubwa na Ina mkono mrefu.
Kama unachotaka kuuziwa hakijulikani na serikali.
KIMBIA.
Mfano viwanja vilivyopo uko vikindj ndani ndani je wizara ya ardhi inavijua ama inakuwaje apa?
 
Serikali za mitaa wana umuhimu wao.kwanza wanakuwa wanajua historia ya eneo.
Pili ni mashahidi wa karibu kabisa ambao wanaweza kusaidia,tofauti na wakili ambaye wakati mwingine anafanya kazi yake akiwa ofisini.

Kutumia wakili kusikufanye ,usiwashirikishe serikali za mitaa kupata taarifa zaidi kuhusu Hilo eneo.
Mkuu mimi sikubishii unachoamini ila kama umeamua mkataba wako wa kununua ardhi usimamiwe na mwenyekiti wa serikali ya mtaa sawa na ninakutakia kila la kheri maana unaamini kuwa wanajua historia.
Ila ninakupa task, nenda kafuatilie migogoro ya ardhi ambayo mauzo yalisimamiwa na hai unaosema wanajua historia halafu uje hapa utueleze.
Kwamba mwenyekiti akajue taarifa za mirathi, familia, vikao vya familia, kama kuna mikopo, kama mali ilichumwa na wenza, nk? Sawa, kila la kheri mkuu.
 
  • Wana umuhimu wao kwa ardhi ambazo hazijapimwa,
  • Na hao serikali ya Mtaa ndio wameleta mabalaa ya kuuza Ardhi Mara mbili
  • Unasema Wakili amekaa ofisini hivi unajua maana ya neno 'official search'?
Yamkini anaamini kuwa ili uonekane unafanya kazi ni lazma uchafuke na tope ama hadi jasho likutoke😂😂😂😂😂😂. Na ndio maana hawataki kuwafuata mawakili. Lakini naamini gharama nje ya wakili ni kubwa sanaaa tofauyi na wanavyodai; mfano, kwenye kiwanja cha 45M mwenyekiti anakula 4.5M cash, dalali anakula si chini ya 4M jumla 9M. Hapo hapo kazi akipewa wakili unaweza kumlilia kwa hata 3M akamaliza kila kitu
 
Mkuu mimi hapa ninaamini na nitazidi kuamini kuwa utapeli katika viwanja kwa zaidi ya 85% unachangiwa na sisi wenyewe wanunuzi. Mkuu mimi ni mwanasheria, ila nikwambie ukweli kabisa kuna wateja hamshaurikiiii hamtaki kusikiliza ya wataalamu na mwisho wa siku mnapigwa.
Mfano, mteja anatafuta kiwanja anaona dalali amepost. Baada ya hapo anaenda kuona kiwanja, dalali anatia maneno ya kuonesha kuwa wengi wanahitaji kiwanja hicho, anamleta mtu ambaye anadai kuwa ndiye mmiliki(kumbe ni msimamizi tu wa familia na sio mmiliki). Mnaenda kwa mwenyekiti wa mtaa anakula 10% dalali anakula % yake halafu mnaandikishana pale kisha mnampelekea wakili makaratasi yenu kuwa 'AWAGONGEE MUHURI' mna laki 5😂😂😂😂😂😂 wakili anakuuliza kama umefanya utafiti kuwa hakuna shida yoyote? Unajibu ndioooo na mwenyekiti ametuthibitishia, wakili anakwambia kama umejiridhisha basi hakuna shida(huku akitabasamu) maana hata akikukatalia utaenda kwa mwingine na unaweza kukutana na karani wake akagonga huo muhuri kwa laki 2.
Kinanuka baadae ndio unatambua kuwa dalali na mwenyekiti hawatambuliki kwa namna yoyote katika mikataba ya ardhi binafsi, unamfuata wakili anakukumbusha maswali ya siku hiyo na mwisho wa siku hata kesi yako hawezi kuisimamia mahakamani tena unabaki kumuachia Mungu 😂😂😂😂😂😂😂😂
Sasa tufanyeje aisee...upigaji umeanza upyyaaaaa yaani, hizo process wengi wetu tunafanya ivyo ulivyosema
 
Sasa tufanyeje aisee...upigaji umeanza upyyaaaaa yaani, hizo process wengi wetu tunafanya ivyo ulivyosema
Safi, hakikisha ukitaka kununua kiwanja ama eneo sehemu nyingine tumia wakili akusaidie kukuelekeza tahadhali za kuchukua.
Pia, ukiona mtu yeyote anataka kununua mshauri kuwa huo mkataba husika unaandaliwa na wakili pia anampa kazi nzima ya uchunguzi huyo wakili, hii haitaepusha kutapeliwa bali itasaidia kwa zaidi ya 85% kiepusha kutapeliwa, isikaze ubongo kulazimisha utakacho baada ya kushauriwa na wakili maana atakukubalia halafu baadae unaingia kwenye hatari.

Asante.
 
Serikali za mitaa wana umuhimu wao.kwanza wanakuwa wanajua historia ya eneo.
Pili ni mashahidi wa karibu kabisa ambao wanaweza kusaidia,tofauti na wakili ambaye wakati mwingine anafanya kazi yake akiwa ofisini.

Kutumia wakili kusikufanye ,usiwashirikishe serikali za mitaa kupata taarifa zaidi kuhusu Hilo eneo.
Ninyi Serikali za mitaa hamna mamlaka hayo kisheria, HAMTAMBULIKI POPOTE kisheria. Usilazimishe kwaajili ya 10% Mkuu.
 
Wakili wako anawajibu wakufuatilia taarifa zote kuhusu hiyo aridhi kabla ya mauziano,kwa hiyo lazima ajue background ya hiyo ardhi,mana hata sheria inambana mnunuzi kabla hujanunua aridhi hakikisha una taarifa sahihi vinginevyo utalia na kusaga meno huko mbele.
Sawa sawa meku
 
Iko hivi, sheria haiwatambui, ila wao wakisimamia mauziano hayo ni sawa tu kama umemuita mtu yoyote yule kama shahidi tu, na sio kwa cheo chake!!yeye anachokusaidia ni kukuhakikishia kuwa anayeuza ndio mmiliki wa ardhi hiyo, japo naye anaweza kuwa hana uhakika nalo, kwenye mauziano unaweza kuwa na muuzaji , na mashahidi, na biashara ikafanyika, lakini kisheria kuna watu ambao ndio wamepewa jukumu hilo, hiyo document, ichukue ipeleke kwa wakili akuandalie , document, yenyewe ambayo hata huko mbele ukitokea mgogoro ni rahisi kuwa sehemu salama.Tatizo huwa tunakimbia gharama huko.
Inshu sio kujua background ya ardhi, kwani hao wenyeviti huwa wanakuwa na kumbukumbu tena baada ya kuchukua 10%yao?!labda mgogoro utokee baina ya pande mbili na wote muwe na hayo mavifungashio ya serikali za mitaa, , ndio wataangalia, labda muuzaji sahihi ni nani, nani alikuwa wa kwanza kunununua.
[emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122][emoji122]
 
Kiufupi ni kwamba nimetapeli million 45, nimekuja kugundua huu ni mtandao mkubwa unaongozwa na Diwani mstafu ambae alikuwa anajimilikisha maeneo ambayo wenyewe hawayajaendeleza au kutoonekana kwa mda mrefu na baadae anawapa vijana wake wa kazi na madalali wauze.

nimeshangazwa wenyeviti wa mitaa hata watendaji hawajui maeneo yao vizuri nao wamekuwa sehemu ya mgogoro, manunuzi yangu nimefata taratibu zote na zaidi nimeyafanya kupitia mwanasheria.

Tapeli wangu tayari nimemkamata jana usiku Dodoma vijini huko Kibaigwa, nimemrudisha morogoro nimemkabidhi polisi mwenyewe.

Hawa matapeli napelekana nao kimafia, lazima nifidiwe hata kwa kuuza makazi yao
 
Kaka kosa nililofanya ni kutokupitia kwa wenyeviti wa seriklai za mitaa nikamtumia direct mwanasheria lakini wenzangu walionitangulia kununua walipitia huko kwa wenyeviti lakini mambo ndo yamekuwa hivo
Ndio maana imekuwa rahisi kutapeliwa pole sana mkuu
 
Haya mambo yasikie tu.

Nina siku ya nne leo tangu nigundue kwamba nimepigwa, hata kula vizuri siwezi, nawaonea wivu wenzangu walionunua maeneo madogo kwa bei za 15m kushuka chini. Naona hasara yao ni ndogo kuliko yangu.
Hebu weka mkasa mzima mkuu na sisi tujifunze! Ilikuwaje hiyo! Mimi mwenzio nilitapeliwa 2m lakini nilijidharau karibia wiki nzima, nawaza tu nilivyotapeliwa kiboya (ingawa kwangu niliona kuna nguvu za giza zilitumika). Sasa wewe 45m si unaweza kuchizika kabisa?
 
Back
Top Bottom