Nimetosheka na maisha ya ujana wa ki-bachelor (natangaza nia: jimbo lipo wazi)!

Nimetosheka na maisha ya ujana wa ki-bachelor (natangaza nia: jimbo lipo wazi)!

Atueleze amejipanga vipi ili kumtunza mtoto wa mtu kama mke kwanza.
Kiufupi niwahakikishie kuwa nimekwisha jipanga kwa uwajibikaji wa mahitaji ya familia kwa ujumla, sio tu mkee pekee. Pia kama nilivyoeleza awali; ni shauku yangu kumpata mpenda maendeleo ambaye tutajadiliana sote juu ya yale tutakayofanya pamoja kwa ustawi wa familia yetu.
 
Kwahio aoe tu bila kujiridhisha[emoji28] ili aje kuambiwa mke amechoka ajipikie na kujifulia mwenyewe[emoji28]
Ni muhimu mno kujiridhidha. Nimejifunza mengi kwa walio tangulia kuingia katika taasisi hii ya NDOA.
 
We nae huna vigezo? Ukipata vidoto f4 vikaanza kuomba vicha usituchoshe na uzi wa malalamiko.

Weka vigezo upate size yako mwanamke ambae hata akikupiga mzinga basi unajua anaenda kununua kiwanja.sio vizinga vya vocha.
Mmh, nadhani upo out of context.
 
Hujanielewa vizuri. Huyu jamaa ametangaza kuwa angependa KUOA (Mwanaume) na wala si kuolewa (Wavulana), sasa kama mwanaume amejipangaje kutunza huyo mwanamke. Je, ataweza kumlisha, kumvesha na kumpatia pahala pa kulala? Nikauliza amejipangaje? Asije akaja hapa mwisho wa siku analialia kama (Wale tuliokosea kuoa tukutane hapa) ingawa alitakiwa kusema wale tuliokosea kuoa kabla ya kujipanga tukutane hapa).
Nirudie kusema kuwa: Nimejipanga. Ondoa shaka kabisa juu ya hilo. Umeulizia kuhusu kumtunza mke, Mimi nimejiandaa kutunza familia.
 
Back
Top Bottom