Nimewasikiliza wabunge wa CHADEMA waliohojiwa na PCCB, yawezekana Lijualikali ni mwongo wa "Kutupwa"

Swala LA pesa za chadema kuhojiwa na takukuru liko kisiasa mno. Shida kubwa walioibua tuhuma sio wanachadema kwa sasa.Haiwezekani tuhuma ndani ya ccm zitolewe na chadema kisha takukuru wafanyie kazi.
 
Mkuu kamati kuu ndo inaamua matumizi,Kama kamati kuu ilikubali kumkopesha Mwenyekiti,Lijuakali anabwabwaja tu otherwise alipaswa kuilalamikia kamati kuu na si mwenyekiti.Lakini la mwisho nadhani kuanza kugombana na kumtukana na hata kuweka mapungufu ya mwajiri wako wa zamani Wala humkomoi mwajiri wako bali unajikomoa mwenyewe maana unamwonesha mwajiri wako mpya namna ulivyo na kwa sababu hii huyo mwajiri wako mpya kukupa nafasi itakuwa muujiza
 
Jibu swali kwanza. Ford ranger za M4C na magari yanayoingizwa kwa jina la Chadema ni mali ya Mbowe?
Inawezekana huo ni utaratibu wa kawaida kabisa kwenye biashara.

Nimewahi kuwakodisha St Marys School gari na ilijulikana ni gari ya shule hadi uende kwenye kadi ndio unamkuta mmiliki kamili.

Kwa taarifa yako hsta makampumi ya simu, Tbl nk magari mengi siyo yao japo kwa nje utambulisho wote ni wao!
 
Kwa kweli kama alikua na nia ya kuhama CHADEMA angehama tu kistaarabu ama kimya kimya. Sidhani kwa mapovu aliyotoa hata huko alikopokelewa watamuamini

Lijuakali ni hopeless kabisa.
Jana ungemsikiliza Lwakatare katika kipindi cha Medani za Siasa kupitia Star tv ungeona jinsi wanasiasa wastaarabu walivyo.

Jamaa anajitambua sana!
 
Jana ungemsikiliza Lwakatare katika kipindi cha Medani za Siasa kupitia Star tv ungeona jinsi wanasiasa wastaarabu walivyo.

Jamaa anajitambua sana!
Juzi kati hapa mlikuwa na nyuzi kibao za kumponda Lwakatare leo unakuja kumsifia kisa aliongea kila unachokipenda, wanasiasa akili zao sio nzuri jamani
 
Mkuu johnthebaptist ,wewe huko unafanya nini? Angalia mashetani yasikupe sumu,maana ukweli kwao ni dhambi. Kongole kwa kuwa mkweli na kuusimamia. Mungu Mwenyezi akubariki sana.
 
Juzi kati hapa mlikuwa na nyuzi kibao za kumponda Lwakatare leo unakuja kumsifia kisa aliongea kila unachokipenda, wanasiasa akili zao sio nzuri jamani
Mimi ni Chadema hadi nimponde Lwakatare?

Siasa siyo uadui bwashee....... Kalagabaho!
 
Unakwepa mishale kishamba kama sio Yohana. Hilo la Vodacom kukodi Hiace ya mtu na kuweka nembo yao hata mtoto mdogo analijua.
Hapa tunauliza mali zinazonunuliwa kwa jina la Chadema,Michango ambayo inachangwa kwa jina la Chadema ni mali ya Mbowe? Na kama aliichukua bila taratibu asishughulikiwe na vyombo vya dola?
 
Yeye na huyo bamkwe wake ni mazero brain
 
Kwa maelezo yako kweli MAENDELEO HAYANA CHAMA!! Waeleze pia wana Lumumba na WAPWA waelewe hili.
 
Kwa hiyo CAG hakuona yote hayo, yaje yafanyiwe kazi na TAKUKURU? Kitu ambacho CCM na Spika wanatakiwa kujilaumu ni kutokumwambia CAG mapema kabla hajaanza kukagua matumizi ili atoe kwa CHADEMA hati chafu kwa makusudi ili waitumie kama fimbo ya kuichapa CHADEMA.

Kwa sasa TAKUKURU wanapoteza muda na fedha bure. Kazi ya TAKUKURU ni kuchunguza jinai na si matumizi ambayo CAG amebariki.
 
TUNAKUSUBIRI ingawa nguvu ya sauti yako yapungua kwa kasi kama ya Yuda Lijualikali Iscariote.
 
Mkuu Huyo jamaa ndiyo nasikia atagombea kilombero Kwa ticket yenu
Mtu mwongo, Mnafiki mtoa Siri za chama
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…