Nimewaza Ujinga: Kwanini magari yasigome kuwaka mpaka dereva atakapochomeka leseni yake na funguo kwa pamoja?

Nimewaza Ujinga: Kwanini magari yasigome kuwaka mpaka dereva atakapochomeka leseni yake na funguo kwa pamoja?

Idea hii ungeipeleka Ulaya au ukawasiliana na bright Ideas [emoji362] huenda ukafanikiwa kama idea haijafanyiwa kazi bado duniani
Wazo zuri sana
 
Shikamooni wakubwa zangu wote wa hapa jamiiforums.

Ndugu zangu watanzania eti;

Kwanini kusiwe na mfumo ambao utawezesha, licha ya kwamba engine imewashwa kwa funguo, lakini bado gari itagoma kuwaka mpaka utakapochomeka pia leseni yako ya udereva?

Yaaani kunakuwa na direct contact baina ya servers za TRA, Police Traffic pamoja na ignition system ya gari.

(1) Faida yake ya kwanza ni kwamba, hakuna mtu atakayeweza kuendesha gari kama hana leseni (Leseni inakuwa na smartchip kama ya ATM Card)

(2) Faida ya pili ni kwamba, ata ikitokea kuwa gari imeibwa ni rahisi kujua ni leseni ya dereva yupi inatumika kuendesha gari hiyo.

WATAALAM WA ICT, COMPUTER NETWORKING PAMOJA NA MECHANICAL/AUTOMOBILE ENGINEERING msipite bila kusema chochote please.

I STAND TO BE CORRECTED.....!!!!!

Nimelisajili hili wazo langu la kijinga kijinga...!!!!!

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Mimi kama mdau mkubwa upande wa automobile engineering, hii kitu anachotaka kiwe, inawezekana kama wahandisi watarudi kwenye drawing table. Madhala yake yatakuwa mengi hasa upande wa bei. Itakuwa hayanunuliki magari yenye 'state of the art' ya system hiyo na hata huyo mwenye uwezo akiwa nalo akienda sehemu ambayo ni 'utoporoni' mtandao ni wa kusuasua utashindwa kuwasha gari lako.
 
ni kama wazo la kijinga lakini lina mantiki sana.Kuna magari mengine ukipanda umelewa haliwaki hii
 
Vipi kama babako kupatwa na stroke daraja la 1 au 2 wewe mwanae kwa utundu wako unaweza kuendesha gari na kunusuru maisha ya babako, utaacha kuvunja Sheria hiyo au.....?
Ninarudia tena. Sheria ya nchi inakataza mtu asiye na leseni ya udereva kuendesha gari. Zingatia sana hilo.
 
Back
Top Bottom