Nimeyakumbuka maisha yangu ya uyatima; Uyatima ni noma sana ndugu zangu

Mkuu hakika Mungu akupiganie
 
Uzi huu Kuna vipande vinanihusu, ni kama tumepita njia Moja. Mimi sikuwa yatima ila umaskini WA familia na ukubwa wake.
 
Heri yako umeshakiepuka hicho kikombe japo uliteseka sana, sie wengine bado tupo kwenye mchakato wa mateso sijui mpaka lini. Ndugu wa kweli ni Baba, Mama na kaka/dada mliozaliwa kwenye familia moja tu.
 
Heri yako umeshakiepuka hicho kikombe japo uliteseka sana, sie wengine bado tupo kwenye mchakato wa mateso sijui mpaka lini. Ndugu wa kweli ni Baba, Mama na kaka/dada mliozaliwa kwenye familia moja tu.
Soon, nakuhakikishia bado kidogo tu. Usiache kumuomba Mwenyezi Mungu Mwenye rehema
 
Jamani jamani 😭😭😭😭 mnatuumiza sasa
 
Mmmh roho yako ya fisi kabisa mkuu. Yaani wewe ni mulemule kwenye wanyanyasaji.
 
Aisee Mungu akupiganie utimize dhamira yako.
Wale watoto wanatia imani unapofika pale na kuanza kusema Baaba huyooo...asee una tambua kuwa wanakosa upendo wa wazazi wote ingawa ni wadogo sana ila wana tambua kuwa wale sio wazazi wao bali ni walezi.
 
Pole sana Mkuu [mention]Liverpool VPN [/mention]

Ila pia kulea mtoto asiye wako ni changamoto

Mwanao unaweza kumkaripia na kumwambia neno lolote, hata la kashfa na kipondo juu na pasiwe na tatizo lolote. Ila ukifanya jambo hilo hilo kwa yatima au mwana asiye wako, inatafsiriwa tofauti kabisa. Na yule mtoto anaichukulia tofauti kabisa, anahisi kafanyiwa vile kwa sababu ya hali yake...

Kuna familia naijua waliishi na yatima, ambaye wazazi wake walifariki na kwa bahati nzuri, ile familia walikuwa na mtoto mdogo ana kama miezi mitatu hivi, so ikawa rahisi tu, mama akamchukua yatima wakashare ziwa moja na mwanae. Akawalea vizuri bila hata shida. Na baadaye mama akapata watoto wengine wengi tu. Familia ikawa kubwaa.

So kwenye kukua wale watoto wawili wakaambia kuwa wao ni mapacha. Na jina la ubini wanatumia moja, shuleni wanapangwa darasa moja. Kila kitu swafi.

Kafika umri fulani ndugu wakaja kumwambia ukweli yule yatima, kuwa wewe hapo unapoishi huyo sio baba yako wala Mama yako. Mama yako amefariki na baba yako amefariki.

Nadhani yule binti alipata msongo wa mawazo, Yule binti aliharibikiwa mazima.

Na bahati mbaya sasa yule mzee naye alikuwa ni mkali sana by nature tu, alikuwaga watoto wake wakizingua zinapita bakora za maana.

Sasa yule binti alichezea bakora sana ila wapii.. akawa anauweka uyatima mbele, kila kitu akiambiwa anakimbilia kwenye kivuli cha uyatima.

Ilikuwa tafrani.

Binti Alitanga tanga sana na dunia.

Kumlea ikashindikanika.

Kaja kujitafuta na kujitambua tena baada ya kama miaka 15 au 20 hivi.

Hapo watoto aliowacha kwenye ile familia wameshasoma wengine wapo makazini.

Akarudi tena kwa wale wazee, kawaomba msamaha. Wakamsamehe. Ndo kuanza tena shule pale alipoishia. Akakomaa komaa na shule kwa miaka kadhaa mpaka akapata degree.

Kasoma zile elimu za watu wazima.

Na akaja kupata na ajira mahali.
 
Huu uzi ni mchungu sana kwa sis wazaz vijana ambao bado ni wapambanaji.
NB
sihofii kifo ila naogopa kufa sasa hiv kwasababu ya watoto wangu na mama yao
 
Hizi ndio sadaka zile tunazozisema.

Na Mimi ngoja mambo Fulani yakae njema nitatake responsibility kwa mtoto mmoja wapo.
 
Hii Stori imenikumbusha mbali.
Pumzikeni kwa Amani Wazazi wangu huko mlipo.
 
Itakuwa ngumu kumuelewesha jamaa kuwa anatengeneza season ya kilichomtokea kikatokee kwa huyo binti au mjukuu.

Ni muda sasa a estblish strong family, aoe. Asije akaamini kuwa mdogo wake aliesta nae, atasimamia majukumu yeye ikitokea hayupo duniani ohoo.
 
Kumbuka Maisha ni FUMBO gumu sana. Mafanikio ni MITIHANI migumu sana. Ulikopita usipaangalie kwa uchungu bali kwa furaha, kwasababu umesha vuka huko.

Mafanikio ni mazuri ukiweza kuwasaidia wengi kadri uwezavyo bila kujali walifanya nini wakati ulipokuwa ukihitaji, na bila kujali watakulipa nini au kukukumbuka ulivyo wasaidia. Kwa kifupi tenda wema nenda zako. Usiweke kinyongo kwenye haya maisha, mafanikio ni FUMBO, ulichokipata kwa jasho kinaweza kuondoka kirahisi sana,bila kujali ulivipata kwa jasho la damu au kwa ugumu vipi.

Usikumbuke saana mapito kwa maana ya maumivu, kumbuka mapita kwa maana ya uongeze juhudi kutafuta.
Wasaidie wote bila kubagua, na watafute ndugu ,jamaa na marafiki popote walipo, furahi nao hata kama huwasaidii chochote.

Kuna rafiki yangu tumekuwa pamoja, alikuwa na uwezo mkubwa sana kielimu, lakini hakufanikiwa kusoma sana kwasababu zingine ulizozieleza, hawakuwa na kipato kizuri kuweza kusoma.

Alifanikiwa kwa biashara, alitumbua sana. Ila bahati mbaya alipata ajali akavunjika mikono yote miwili, Mkono mmoja ulikatwa kwa jinsi ulivyokuwa umesagika, mkono wa kushoto waliweza kuuunga unga, upo lakini hauna nguvu sana.

Maisha yalipiga U-Turn, aliishiwa, akakimbiwa na mke, hadi ndugu. Alirudi nyumbani kwao anaishi na mama yake ni mzee sana, lakini ndiye umuhudumia muda mwingi.

Huwa anakumbuka, alivyo kuwa anakula bata, na aliokuwa akila nao, leo hawamkumbuki tena.

Usilipize ubaya kwa ubaya, lipa wema kwa kila baya unalotendewa, na Mungu atakubariki sana.

Ubinadamu mgumu sana, ni hayo tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…