Nimeyakumbuka maisha yangu ya uyatima; Uyatima ni noma sana ndugu zangu

Nimeyakumbuka maisha yangu ya uyatima; Uyatima ni noma sana ndugu zangu

Mkuu pole sana aisee,ila uyatima unaumiza asikwambie mtu. Kuna muda nilikua nasoma story yako huku machozi yakinilenga.

Binafsi nimepitia hali hiyo katika maisha yangu yote mpaka sasa na bado napitia huko. Nahisi kama sijawahi kuipata furaha au faraja ya kweli hapa duniani.

Msoto ulikua ni mkali sana,ndugu wanageuka mashabiki wa shida zako na haters wa mafanikio yako. Na ndipo nilipoamua kuishi bila mawasiliano yoyote na ndugu yoyote mpaka sasa.

"Mama na ndugu zangu ni wale watu ambao kwa namna yoyote walininitia japo moyo pale nilipokua mtaani nikiishi kama chokoraa", period!
Watu wanamazito jamani
 
Hongera na pole mkuu, mwenyewe simjui baba Wala mama na watesi wangu wote nawajua na kuwakumbuka lakini nimesamehe na bado nawaita jomba, zamani Sana tukio nalokumbuka ni kuzoa kinyesi kwa mikono kisa nimejisaidia njiani huku fimbo zinawaka mgongoni na sikumbuki Kama nilinawa ile mikono au kujifuta na nyasi ,Ila mungu wetu ni mwema
Hapo kwenye kinyesi me mwenyewe ilinitokeaga
Nilijisaidia kwenye shamba la jamaa ambaye pale kijijini alikuwa anaogopeka Sana
Basi Kumbe jamaa alikuwepo mle shambani kalala na aliniona
Akaniacha nimalize baada ya dk kadhaa nashangaa jamaa yupo nyuma yangu kashika panga
Akaniambia zoa hayo mavi na mkono
Nilichofanya nikachota kuanzia chini ya udongo kwani udongo ulikuwa mlaini nikaenda kutupa mtoni.
Aisee Kuna watu wanaroho ngumu Sana.
 
Mkuu pole sana aisee,ila uyatima unaumiza asikwambie mtu. Kuna muda nilikua nasoma story yako huku machozi yakinilenga.

Binafsi nimepitia hali hiyo katika maisha yangu yote mpaka sasa na bado napitia huko. Nahisi kama sijawahi kuipata furaha au faraja ya kweli hapa duniani.

Msoto ulikua ni mkali sana,ndugu wanageuka mashabiki wa shida zako na haters wa mafanikio yako. Na ndipo nilipoamua kuishi bila mawasiliano yoyote na ndugu yoyote mpaka sasa.

"Mama na ndugu zangu ni wale watu ambao kwa namna yoyote walininitia japo moyo pale nilipokua mtaani nikiishi kama chokoraa", period!
You must get over it bro, ila usisahau mafundisho ya mapito yako.

We were on the same boat.

Mpaka sasa am living my life ... bila ya msaada wa ndugu ...

life goes on
 
Tatizo kubwa la wazazi hasa wanaume wa Africa huwa hawaandiki wosia wakiwa hai, hii husababisha mitafaruku mikubwa sana baada ya wao kufariki kama mke ni dhaifu.

Pia utamaduni wa kishenzi wa baadhi ya jamii wa kufanya mali za mtu binafsi ni za ndugu wote au ukoo mzima imechangia kukuza hili tatizo la kugombea mali. Ni wakati sasa wa kutunga sheria inayosema mali za familia ni za mke, mume na watoto wao tu.
 
Mkuu pole sana aisee,ila uyatima unaumiza asikwambie mtu. Kuna muda nilikua nasoma story yako huku machozi yakinilenga.

Binafsi nimepitia hali hiyo katika maisha yangu yote mpaka sasa na bado napitia huko. Nahisi kama sijawahi kuipata furaha au faraja ya kweli hapa duniani.

Msoto ulikua ni mkali sana,ndugu wanageuka mashabiki wa shida zako na haters wa mafanikio yako. Na ndipo nilipoamua kuishi bila mawasiliano yoyote na ndugu yoyote mpaka sasa.

"Mama na ndugu zangu ni wale watu ambao kwa namna yoyote walininitia japo moyo pale nilipokua mtaani nikiishi kama chokoraa", period!
Trust me yanapita.
Nilifanya maamuzi magumu ya kwenda kusoma course nisiyoitaka ili tu nitafute nafuu.
Na kweli bana ile course nisiyoitaka na kuipenda ndio ikanipa ajira serikalini...!!
Hiyo ajira ikalipa ada ya kusoma ile course niliyoitaka..!!
Na sasa natumikia ile course niliyoitaka.

Nafuu ipo ila ukipambana huku unamuomba Mungu.

#YNWA
 
Yatima hadeki😁😁😁
Mi4of.jpg
 
Watu wanamazito jamani
Acha tu ndugu yangu, na mbaya zaidi unakuta hao wa kujuita ndugu wakiona unaanza kupata unafuu kidogo wanakupiga hata kipapai.

Mwanzoni nilihangaika sana yani mpaka nikajiona nina mikosi tu hii dunia,kumbe kuna mtu kashaapa kwamba nitatanga tanga miaka yote mpaka siku nakufa bila kufanikiwa hata nikishika pesa kiasi gani.

Mbinu ni moja tu,ilikua ni kukata mawasiliano mazima yani wasijue kama niko hai au lah! Pia nikaamua kuachana na masuala ya kuulizia rasilimali za huyo Mshua.

Mpaka leo niko safe,niko kama mafichoni ila nina amani kiasi.
 
Jana (Ijumaa) nikiwa kazini Kuna saa nilikosa Kazi (zilikua zimeisha). Nikawazaa, ghafla mawazo ya maisha ya UYATIMA niliyopitia yalinijia.

Ni ndefu sanaa we somaa.!

Japo siwezi kuyaandika yotee, maana UYATIMA wangu ulinipitisha kwenye makubwa sanaa..!!

Nilizaliwa kwenye familia ya watoto 3 tukiwa na baba na mama.
Baba alifariki kwa ku palaryze nikiwa mdogo sanaa.

Baba alikuwa ni mfanyabiashara mwenye mali nyingi ila mama alikua ni mama wa nyumbani.

Kwasababu ya kumkosa mumewe, baada ya baba kufariki mama alikuwa anaumwa umwa Sana.

Hii ilisababisha Mali nyingi kuuzwa na bila kusahau nyengine zilidhulumiwa na ndugu.

Ndugu na marafiki wa baba waligawana mali nyingi sanaa tukaachwa na nyumba tu ya kuishi.

Mama alikua anateseka Sana na mawazo ya kumpoteza mpendwa wake, hii ilisababisha kudhoofisha Kinga ya mwili na hatimae malaria kali ilimjia na kumchukua.

Ilikua ni siku ya jumapili nilipoletewa habari kuwa "Mama yako amefariki".
Aisee Ile siku ilikua nomaa, Mimi na mama tulikua na kijiwe chetu..!! Pale nyumbani (Kona ya barazani kwenye ua alilokuwa analipenda).

Aisee nilikaa pale na kulia sanaa, nilikumbuka ule usia wake, vicheko vyake, sura yake, harufu yake, kifupi niliona dunia imefika mwisho.

Wakati huo nikiwa mdogo sanaa (darasa la 4) ila huwezi amini NAKUMBUKA KILA KITU MPAKA LEO.

Nakuonya mwana JF "Usimfanyie mtoto ubaya" kwamaana "Hawezi sahau".
Mimi japo nilifanyiwa ubaya na ndugu tena nikiwa mdogo ila nakumbuka majina, siku, location yaani kila kitu kwa jambo nililyofanyiwa na ndugu.


Siku ya msiba wa baba watu walijaa wengi na waliiba Mali za pale nyumbani na wezi wote nawakumbuka ""wakina Wajomba zangu""

Baba alikua Tajiri hivyo nyumbani kwetu kulijaa ndugu waliokuja kuomba Msaada.

Ila baada ya baba kufa walipungua sana na baada ya mama kufa ndio kabisaa sikuwaona.

Tulianza kulelewa na dada.

Maisha ya ushua yalipotea na kama upepo, tukaanza shida.

Dada majukumu yalimzidi tuka hamishwa kila mtu kwake.

Mimi nikabaki Dar, mdogo angu mkoani na dada angu akabaki nyumbani.

Huko nilikoenda nilienda kwa mshua mmoja hivi taita Dar pale (rafiki wa baba).

Ila huyu "Mkewe hakunipenda kabisa" sababu mpaka leo huwa siijui.
Nilikua sili Sana, nilifanya Sana Kazi na mengine ila sijui kwanini hakunipenda.

Nilikaa pale miaka miwili, mama akaanda staili moja ili niondoke kwake.

Lile zegwe hausi geli alilijua.
Akanitahadharisha.

Nikamuhadithia shangazi
Shangazi alikuja kunichukua fasta.

Shangazi yangu hakua na maisha mazuri ila nilikomaa hivyohivyo.

Nilikomaa sanaa, chakula hakitoshi, Shule kwenda na miguu tena Dar es salaam, halafu mbali sanaa.
Mwaka mzima hununuliwi nguo mpya..!! Unavaa nguo za kushindia hizohizo mpaka mtaa una kukariri.

Ila nilikomaa.

Shangazi yangu hakuwa na room kwa watoto wa kiume, kwahiyo sometimes nilikua nalala kwenye korido na sometimes nje ya nyumba.

Yaani nje kabisa, milango inafungwa mi nafunga net kibarazani nalala.

Hakua ananitesa na nilikua nina amani.

Kwakuwa chakula kilikuwa hakitoshi nilianza kufanya Kazi kwenye nyumba za watu.

Maisha ya zamani ilikua mwenye hela ndio anabomba la maji la Dawasco.

Hivyo mi nilikua nachotea watu maji wananilipa ndoo moja 50.

Hapo nikawa napata nauli ya kwenda Shule (kipindi hicho mwanafunzi nauli 50).

Na nyengine kabla sijala nyumbani nilikua natanguliza kwanza sambusa, hivyo na kile kidogo cha nyumba nakua nashibaa.

Maisha yalienda mara la 7 nikafaulu.

Miaka ile kufaulu la Saba ilikua dili hasaaa.

Shuleni kwetu tulienda secondary Wa3 tu, yaani tulifaulu Wa3 tu..!!!

Mtaa mzima hongera...!!!

Kufika Shule nikaanza kucheza kamali ili nipate pesa ya kujikimu..!!

Nilikua nawala hasa.

200 inazalisha 3000 mpaka 5000.

Bwana eeeh Kuna siku ikapitishwa karatasi waandikwe majina ya wacheza kamali, na Mimi ndani...!!!

Tulipigwa sanaa siku ile, fimbo kama 100 hivi.
Enzi zile tulikua tunapigwa hasaaa.
Unashika chini huku umebongoa, walimu wanapita na fimbo, ukiishika Tako umefutaa.!!!

Tulipigwa sanaa.

Ila Sasa hata nikiacha kucheza nitapata wapi hela ya kujikimu shule..!!
Shangazi ya kunipa hana, hana uwezo wa kunipa nauli, je madaftari na vitabu atanunua?

Dah maisha yaliendelea, tukawa tunacheza nje ya Shule.

Kufika form 2 nikaongoza wastani kwa Shule nzima.

Ikabidi mwalimu wa darasa aniite "wewe una akili sanaa, kwanini unakua mtundu?"

Nikamuhadithia nayopitia nyumbani, huyu mwalimu niliona kabisa machozi yana mlenga.

Tokea siku hiyo alianza kunichukulia tofauti sanaa.

Form 4 nikaongoza kwa kupata Division 1 Kali sanaaa.

Taarifa zikaenea kwa ndugu na jamaaa + mtaani.

Hongera na masifa kama yoteee.

Ila nyumbani hali ilikua tofauti..!!

Binadamu yangu ye alipata 4 Mimi 1.

Mama ake ikawa kila jambo ananipendelea Mimi..!!

Binamu yangu alini mind sanaaa.

Akawa anatanitaka nitoke kwao, hii "Toka kwetu" mwanzo niliiona ya kawaida sanaa ili kufika form 5 ilikolea sanaa.

Kuna siku nilirudi nyumbani nikafungasha nguo na kusepa gheto la masela wapiga misuli.

Shangazi alimind sanaa.

Akaniita tukaongea na kuahidi kila jumapili nikachukue elfu 5 ya matumizi ya wiki.

Yaani kwa wiki utumie elfu 5..!!
Kula mchana, asubuhi, usiku na hela ya pindi mchikichini..!!

Nilikonda hasaa, maana kila siku nashindia miogo ya Shule.
Maana kila siku natakiwa kutumia buku..!!

Maisha yaliendelea taarifa zikamfikia baba mdogo.

Akaniomba niwe naenda kwake kuchukua misaada.

Nilienda kama wiki 4 mfululizo (kila jumamosi).

Nakumbuka Kuna jumamosi nilienda nikamkuta mkewe na baba mdogo hayupo.

Sasa bana Mimi Nina aibu ya kuomba Msaada kwahiyo muda wa kuondoka nikaaga ili niondoke kimya kimya.

Mama mdogo aliniita akanipa maneno makali "Unasababisha sisi tuishi maisha magumu kisa wewe....." aliongea mengi ila mwisho wa siku alinikataza kwenda kwake kuchukua misaada.

Na kama baba mdogo alijua maana hakuwahi kuniuliza lolote juu ya lile jambo.

Nilifika nyumbani siku hiyo nililia sanaa, nilikumbuka maisha ya baba yupo na mama.
Nililia balaaa.

Ghafla mama mdogo (ndugu wa mama) akaniambia niwe naenda kwake.

Huyu nae alinisaidia mara sijui 6 ya 7 nae akanipa dongo "Kwani wengine hawapo" nilibaki mdomo wazi.

Nikarudi gheto nikajisemea "Sitaki tena msaada nitakomaa mpaka nafia humu"

Ile elfu 20 ya mwisho niliyopewa Msaada nikafanya mtaji wa kuuza vitu vidogo vidogo Shule na mitaani.

Nikaacha kwenda mchikichini (tution) NECTA form 6 sikufaulu vizuriiiiii, ila nilipata credit za Degree.

Nilisoma PCB ila nilipenda sanaa mambo ya biashara.
Afya sikuiwaza kabisaa na Wala sikuipenda.

Sasa bana kuomba mkopo na post, post zinatoka chuo UDSM halafu bodi ya mkopo "NO LOAN".

Nani atanisomesha sasa??..!!!!!

Dah nikawazaa, kumbe shangazi yangu anahangaika.

Akanitafutia ufadhili mmoja wa ada.
Chuoni nikawa nalipa 240,000/= ya mambo mengine ya chuo ila ni Diploma.

Nikajisemea "yaani hizi C zangu za PCB naenda kusoma diploma, huku wenye E na D wanaenda degree"
Maisha gani haya...!!!

Nikabeba begi kwenda chuo.

Chuoni sikua na raha Wala amani, nilipenda masomo ya biashara ila nikawa nasomo visivyojulikana na moyo wangu..!!

Nikiwa Diploma 2 mdogo angu akamaliza form 4, akapata ufaulu wa kawaida ila sio wa kwenda advance..!!

Wakumsomesha HAKUNA..!!

UYATIMA nyie, Achana nao kabisaa...!!

Ikabidi nimpe ahadi ya kwamba anisubiri mi mwaka mmoja nimalize Diploma halafu yeye ataingia kwa ada yangu mi nitaishia hapo..!!

Ila kabla ya hapo nikiwa form 4 na 6 nasubiri matokea na post zakuendelea kusoma nilishawahi fanya sehemu tempo.

Kwahiyo lengo langu lilikua ni kumaliza Diploma halafu niende pale kujishikiza, then mdogo angu aingie chuo.

Nikamaliza diploma kufika ile ofisi kuongea na bosi akakubali. Kunipa Kazi.

Nikawa mpiga Kazi pale.

Nilikomaa kuishi maisha magumu hasaa ili tu mdogo angu aingie chuo.

Aisee ni mengi aiseee.

Ile dogo kumaliza Certificate nikamshikiza pale job na kikazi fulani hivi.
Huku Mimi nika apply Kazi serikalini nikapata Mkoani.
Dah hapo ndio ikawa kama nafuu imeanza kuja.

Maisha yalienda, serikalini kazini nikaomba ruhusa ya kwenda Shule kupiga Bachelor nikaunga Masters.

Sikuacha ndoto zangu zife, nilienda kusoma masomo ya biashara.
Ghafla zile ndoto zilizozimwa kisa yatima kakosa ada zikatimia.

Na mwaka huu naingia darasani kusoma PhD yangu..!!!

Na mdogo wangu aliendelea mpaka akapata CPA..!! Na mwaka huu anaingia darasani kusoma Masters.

Mama yetu alikua anatuambia "baba yenu alitaka na kutamani sanaa msome".

Angalau sasa hata tukifa tunaenda kuwaambia wazazi wetu "Tumemaliza yale mlioyatamani kutupa"

Dada yetu yupo na ameolewa na yeye ndio mama yetu.

Huwa tunamlea vizuri ""Japo tunampaga pesa kimya kimya ili shemeji asijue..!!!""

Aisee ni mengi aisee na siwezi kuyaandika yoteee.

Maana pia nilishawahi fukuzwa na shemeji (mke wa kaka - kaka mtoto wa baba mkubwa) bila kujua sababu..!!
Nilikua naendaga kuwasalimia, mkewe sijui akanichoka na kunifukuza ..!!!

Kifupi ndugu walikua wanadhani na hasa wake wa ndugu zangu walikua wanadhani sijui naenda kumaliza hela za waume zao.

Kifupi hakuna aliyenisaidia bila kulalamika, na kunisimanga.
Na wotee waliona Bora kunitimua ili nisiwaletee shida makwao.

Kifupi mpaka leo ndugu huwa siwaelewi.
Huwa wanapiga simu na kiukweli si "save" namba zao.
Na kesho wakipiga Tena na nikiwauliza "nani mwenzangu" huwa wanakata simu na kusema "huyu siku hizi yupo serikalini na kasoma basi anajidai sanaaa"

Na huwa hawaniambii direct ila Wana mwambia dada au shangazi.

Cha ajabu WAMESAHAU YOTEE WALIYOTENDA..!!!

Kifupi sina swaga yoyotee na ndugu YOYOTE.

Siwachukii ila SINA MPANGO NAO KABISAAA.

Ila mdogo angu anamsemo wake "Atavuna aliyepanda kwenye maisha yangu tu, kwani wakati hatuna wazazi na tunateseka walikua wapi"

Kifupi hatuna connection na ndugu wa upande wa mama woteeeeee yaani hata mmoja sijui yuko wapi.

Ila Kwa baba ni shangazi yangu ndio aliyepambana tukafika hapa..!!!
Tupo nae karibu na tunampenda sanaaa.

Baba yangu kwao walizaliwa Wa2 tu.
Yeye na dada ake ambae alitulea.

Nampenda sanaa shangazi yangu na namuheshimu sanaa.

Siwezi kufika Dar bila kumuona Wala kumletea Zawadi ni Mungu wangu aisee hapa duniani.

Ila ndugu wa mama HAPANA KWA KWELI.

Siwachukii ila HATA SIJUI WAKO WAPI NA SINA MPANGO NAO KABISAAA.
Waliamua kunitupa na Mimi nimejitupa mazima.

Dah tuishie hapo.....

YANAYONITAWALA KICHWANI.

1. Natamani kumuuliza yule mama wa mshua, kwanini alipanga kunifanyia lile tukio ili mumewe anifukuze?

2. Natamani kuwauliza wajomba zangu, kwanini mliamua kutudhulumu mali zetu?

3. Natamani kuwauliza mama wadogo, kwanini mliamua kumuacha dada yao (mama yetu) atulee kwa shida wakati wao walikua wanakuja kwake kulia shida?

Kifupi natamani tu nikae na walionifukuza halafu niwahojii kwanini walinifanyia vile.
Yaani tuhojianee weee mpaka moyo ukaridhika.

Natamani nikae na walionipitisha kwenye shida niwahojiiii mpaka niridhike.

KITU NILICHOSHINDWA NI KUWATAFUTA NA KUONGEA NAO.
Najua watakua wanamiliki simu ila hata kutafuta namba zao NIMESHINDWA ..

Na nimepitia mengi siwezi kuyaandika yoteee mengine yanauma na kuumiza.

Tuishie hapa.

Miss you Daddy and Mammy.

UYATIMA ni nyokooooo sanaaaa.
Safari yako hii ngumu ndo iliyokufanya pia uchukie suala la kuoa?
 
Natamani kuishi ndani ya mioyo ya watoto waishio katika mazingira magumu,yatima na wengineo.

Hii ni ndoto yangu kubwa mno katika maisha yangu na ninaamini nitakuja kuitimiza tu.

Maisha ya upweke Kwa mtoto ni magumu sana [emoji3064][emoji3064][emoji3064]


Nakumbuka mwaka fulani nilikwenda kutembelea kituo cha watoto yatima(hii ni kawaida katika maisha yangu kufanya hivi)nikakutana na katoto kakiume kama miaka minne hivi kamekaa pekeyake pembeni ya mlango chini..jamani nililia mnooo (Nina huruma iliyopitiliza Kwa watoto)

Nakumbuka niliishia kutoa mizigo niliyopeleka..nikaongea kidogo nikaondoka..nilishindwa kuendelea kumwangalia zaidi yule mtoto..

Kilio kikaanza kwenye gari sasa[emoji3064][emoji3064][emoji3064]ilibidi dereva apark pembeni aanze kunibembeleza upya.

Picha ya huyu mtoto bado ipo kichwani haijawahi kunitoka kabisa na ndio picha inayonipa msukumo zaidi kutaka kuwa mama wa watoto wengi sana.

Natamani kuwa mbegu iliyo hai mioyoni mwa watoto walioamini kuwa wamekosa tumaini.

Pole sana
Huruma binadamu wengi tunayo pia wapo wwbaya
Ulikuwa na uwezo wa kumchukua na nafsi bado inakusuta kama ulikuwa na uwezo wa kumchukua na kuishi nae

Kusaidia watu ni wajibu wetu na pia kama una uwezo kulea pia ni nzuri zaidi
Umgekachukua tu maskini
 
Trust me yanapita.
Nilifanya maamuzi magumu ya kwenda kusoma course nisiyoitaka ili tu nitafute nafuu.
Na kweli bana ile course nisiyoitaka na kuipenda ndio ikanipa ajira serikalini...!!
Hiyo ajira ikalipa ada ya kusoma ile course niliyoitaka..!!
Na sasa natumikia ile course niliyoitaka.

Nafuu ipo ila ukipambana huku unamuomba Mungu.

#YNWA
Uko sahihi Kaka, kuna muda inabidi tu tukubaliane na hali,ila mimi suala la ndungu hapana aisee!

I swear to God katika kukua kwangu kwote mpaka sasa sijawahi kuishi kwa ndugu wa aina yoyote yule.

Kitu kinachoniuma mpaka leo ni kuniacha niishi nikiwa kama mtoto wa mtaani katika mji na mkoa ule ambao wamejazana na ndio chimbuko letu.
Kwamba hakuna hata mmoja aliekua na huruma na mimi?
Daaaaah wakuu kuna yime naishiwa mpaka nguvu ya kutyp...[emoji22][emoji22][emoji22][emoji22]
 
Acha tu ndugu yangu, na mbaya zaidi unakuta hao wa kujuita ndugu wakiona unaanza kupata unafuu kidogo wanakupiga hata kipapai.

Mwanzoni nilihangaika sana yani mpaka nikajiona nina mikosi tu hii dunia,kumbe kuna mtu kashaapa kwamba nitatanga tanga miaka yote mpaka siku nakufa bila kufanikiwa hata nikishika pesa kiasi gani.

Mbinu ni moja tu,ilikua ni kukata mawasiliano mazima yani wasijue kama niko hai au lah! Pia nikaamua kuachana na masuala ya kuulizia rasilimali za huyo Mshua.

Mpaka leo niko safe,niko kama mafichoni ila nina amani kiasi.
Mungu ni mwaminifu sana.azidi kukutunza na kukulinda kila siku ndugu yangu.wanadamu si watu wema(sio wote)

Tena bora hata mtu baki kuliko hawa ndugu 🥺🥺
 
Huyo Shangazi yenu aliwekeza wema kwenu na sasa anafaidi wema wake
Hao wengine walipandikiza chuki na sasa wanavuna

Binadamu ukitaka uwe na furaha mwisho lazima usaidie na kuwa mwema kwa watu
Hii itakupa furaha milele
Kuna waliotesa wenzao wakiwa wadogo na hata mkiwa wakubwa bado wanawatafuta kwa shari hao ni wa kuwapiga stop [emoji1630] na kuwapa ukweli

Kwa kweli fanya wema na uwe unawasaidia yatima direct isipite kwa mtu

Kama una uwezo wasaidie sana hata kuwapelekea nguo au unapikisha chakula pilau la nguvu siku ya Ijumaa au jumapili wanafurahi sana

Kama ni Xmas au Eid una waalika wote na kuwapikia
Hicho unakiona kidogo ila kwao ni faraja kubwa sana [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
 
Penda sanaa kusoma.


Nina familia.
Nina binti Nampenda sanaa.
Mama ake aliolewa nikamuomba aniachie, akakubali.

Na nikienda kusoma PhD huko duniani NAONDOKA NAE.

Naamini sanaa kwenye familia ila FAMILIA HAINA UHUSIANO WOWOTE NA KUOA.

Yap ilikua ni kipindi cha jasho na damu ila NILITOBOA.

Yap, Majanga kwenye maisha ni mengi huja hili then hili.

Yale ya UYATIMA nishasahau.

#YNWA
How old is she? Kama anasoma ukiondoka si unamsimamisha masomo au?

Tho waweza ona ni sahihi ila unasababisha mtoto ashindwe kuform relationship later on atashindwa kuform na kumaintain relationship. Unapelekea emotional growth kukwama Na namna yake ya kuditch uhusiano will be just to up and leave.

Kusoma napenda.
 
Pole sana
Huruma binadamu wengi tunayo pia wapo wwbaya
Ulikuwa na uwezo wa kumchukua na nafsi bado inakusuta kama ulikuwa na uwezo wa kumchukua na kuishi nae

Kusaidia watu ni wajibu wetu na pia kama una uwezo kulea pia ni nzuri zaidi
Umgekachukua tu maskini
BS ndugu yangu kwa kipindi nisingeweza kabisa maana nilikuwa ninapitia magumu sana.ingawa na magumu yote niliyokuwa nikiyapitia niliamini na Mpaka sasa ninaamini katika kutoa Kwa wahitaji..Imani yangu inaniambia nifanyapo hivyo basi namgusa Mungu moja Kwa moja.

Bado maisha hayajakuwa vile natamani yawe lakini naamin hiki kidogo nikipatacho nitagawana nao.

Kinandoto na malengo..nikishayafanikisha japo kidogo nitatafuta msaada Kwa watu wengine ili kufanikisha ndoto yangu yakuwa mama wa watoto wengi waliokosa mapenzi ya mama Na kupoteza matumani ya kupata upendo wa wazazi.
 
Huyo Shangazi yenu aliwekeza wema kwenu na sasa anafaidi wema wake
Hao wengine walipandikiza chuki na sasa wanavuna

Binadamu ukitaka uwe na furaha mwisho lazima usaidie na kuwa mwema kwa watu
Hii itakupa furaha milele
Kuna waliotesa wenzao wakiwa wadogo na hata mkiwa wakubwa bado wanawatafuta kwa shari hao ni wa kuwapiga stop [emoji1630] na kuwapa ukweli

Kwa kweli fanya wema na uwe unawasaidia yatima direct isipite kwa mtu

Kama una uwezo wasaidie sana hata kuwapelekea nguo au unapikisha chakula pilau la nguvu siku ya Ijumaa au jumapili wanafurahi sana

Kama ni Xmas au Eid una waalika wote na kuwapikia
Hicho unakiona kidogo ila kwao ni faraja kubwa sana [emoji24][emoji24][emoji24][emoji24][emoji24]
Unahuruma sana
 
Penda sanaa kusoma.


Nina familia.
Nina binti Nampenda sanaa.
Mama ake aliolewa nikamuomba aniachie, akakubali.

Na nikienda kusoma PhD huko duniani NAONDOKA NAE.

Naamini sanaa kwenye familia ila FAMILIA HAINA UHUSIANO WOWOTE NA KUOA.

Yap ilikua ni kipindi cha jasho na damu ila NILITOBOA.

Yap, Majanga kwenye maisha ni mengi huja hili then hili.

Yale ya UYATIMA nishasahau.

#YNWA

Magumu uliyopitia wewe umeamua kumpitisha pia mwanao huyu wa kike kwa kumfanya akose upendo wa MAMA! Hivi unajua umemfanya mwanao naye awe 1/2 yatima??

Nakubali umepitia magumu japo kuna wengine wamepitia magumu zaidi, nasikitika kwamba badala ya kuwa mnyenyekevu shauri ya maisha uliyopitia umekuwa na kiburi na kujiona!
 
Uyatima mbaya sana Kaka,tena ni mbaya sanaaaa asikwambie mtu.

Ila licha changamoto mimi nilipenda sana shule,tena sana yani. Mpaka ilifika hatua nikiona watoto wanarudi kutoka shule na mimi niko tu kitaa nauza miwa basi naumia sana so kesho yake lazima niende shule.
Nilikua mtoro sugu.

Kipindi niko O.level walikua wananiita "Man Mawazo",yani muda nilikua najitenga peke yangu nawazaaa,naliiaaa baadae najicheka sana kwasababu hata nikilia niliona haisaidii kitu zaidi ya kupunguza maumivu tu ya kimaisha.

Kitaa wakawa wananiita "Kapipo", kwasababu nilikua nimekondaa ila nimekomaa kama chuma kwasababu ya kazi ngumu.

Daah wakuu acheni tu niishie hapa,ila kaka Liverpool VPN uyatima unatesa.
 
Back
Top Bottom