Nina changamoto ya usikivu hafifu. Natafuta kazi; ikiwa ya kutengeza sofa itanifaa zaidi

Nina changamoto ya usikivu hafifu. Natafuta kazi; ikiwa ya kutengeza sofa itanifaa zaidi

Hilo jina nipe yote lina maana gani?
Mkuu hili jina lilikuja tu wakati nafungua id hii kwani id yangu ya mwanzo nilifungua mda wakati nipo shule ina jina majina yangu mawili halisi inakuwa rahisi mtu kunifahamu. Sasa ikawa kila nikiotea jina bandia likakataa mwisho nikabahatisha hili ndo likakubali. Kwangu halina maana yoyote mkuu
 
mimi nina tatizo kama la mtoa post icho kifaa hakisaidii kwani tatizo lake sio masikio bali ni kichwa ukimuongelesha anakisikia ila haluelewi kama tunavyojua sauti hutoka kwa mfumo wa mawimbi na kazi ya ubongo ni kuyachakata mawimbi kuwa kitu kinachoeleweka ila ufanisi wetu ni hafifu mfano mtu anakuita jumaa unamgeukia alafu anakuambia mama kasema fusgajsjksjbska hapo kwenye fusgajsjksjbska ndio kimbembe lazima umuombe arudie na anaweza kurudia na bado ikawa changamoto kingine bila kumuangalia usoni mdomoni huelewi asemacho hata ukiongea kwa sauti nyuma yale haelewi ila anasikia unaongea.
Sahihi sana mkuu, pole pia changamoto ni nyingi
 
Mkuu hili jina lilikuja tu wakati nafungua id hii kwani id yangu ya mwanzo nilifungua mda wakati nipo shule ina jina majina yangu mawili halisi inakuwa rahisi mtu kunifahamu. Sasa ikawa kila nikiotea jina bandia likakataa mwisho nikabahatisha hili ndo likakubali. Kwangu halina maana yoyote mkuu
Haina noma mkuu nikajua lina maana
 
Habari zenu wakuu,

Mimi ni kijana wamiaka 24 kwasasa, elimu yangu ni kidato cha nne ambapo nilifaulu vizuri ila nilishindwa kuendelea na masomo kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kutosikia vizuri.

Baada ya kumaliza shule mwakav2015, kuanzia 2017 nilianza rasmi kujifunza kutengeneza sofa katika ofisi za ndugu zangu ambapo mpaka sasa nilipofika nina ujuzi wa kutosha kutengeza sofa na vitanda vya sofa.

Changamoto ni kwamba hapa nilipo nakosa kazi zangu binafsi kutokana na hali yangu niliyonayo naishia mara moja moja kufanya kazi za mafundi wenzangu kwa malipo kiduchu ambayo kiukweli yanashindwa kunitoa hapa nilipo kwani bado nakaa nyumbani kwa ndungu zangu.

Naandika uzi huu kuwaomba wana jamiiforums wenye uwezo kunisaidia kupata kazi iwe kama hii niliyo na ujuzi nayo ama yoyote nipo tayari kwani nahitaji nijikwamue nijitegemee na mimi.

Mawasiliano yangu 0788362088 itapendeza ukinitumia sms maana hatutoweza kusikilizana vizuri kwa simu, nipo Dar.
Si ununue kifaa cha kukusaidia kukusikia earing aid...hata cha kichina tu
 
mimi nina tatizo kama la mtoa post icho kifaa hakisaidii kwani tatizo lake sio masikio bali ni kichwa ukimuongelesha anakisikia ila haluelewi kama tunavyojua sauti hutoka kwa mfumo wa mawimbi na kazi ya ubongo ni kuyachakata mawimbi kuwa kitu kinachoeleweka ila ufanisi wetu ni hafifu mfano mtu anakuita jumaa unamgeukia alafu anakuambia mama kasema fusgajsjksjbska hapo kwenye fusgajsjksjbska ndio kimbembe lazima umuombe arudie na anaweza kurudia na bado ikawa changamoto kingine bila kumuangalia usoni mdomoni huelewi asemacho hata ukiongea kwa sauti nyuma yale haelewi ila anasikia unaongea.
Ila samahani kidogo hii ishu imekuwa serious sana .Nyuzi kibao zimerindima kuhusu huu ulemavu wa kupoteza kusikia sijui tatizo ni nn!?
Wengi hawakuzaliwa na tatizo hilo , changamoto mbalimbali wanapata katika kuendea fursa mbalimbali .

Cc Mheshimiwa Dkt. Gwajima D
 
Si ununue kifaa cha kukusaidia kukusikia earing aid...hata cha kichina tu
Mkuu asante kwa ushauri, swali kama hili nilishajibu 👇
Asante mkuu, vile vifaa vinaitwa hearing aid nimeshatumia hasa wakati nipo shule, bahati mbaya havijawahi kunisaidia wala sidhani kama vimeshamsaidia mtu mwenye tatizo kama langu kwani kazi yake ni kuongeza tu sauti
Pia na hii👇
mimi nina tatizo kama la mtoa post icho kifaa hakisaidii kwani tatizo lake sio masikio bali ni kichwa ukimuongelesha anakisikia ila haluelewi kama tunavyojua sauti hutoka kwa mfumo wa mawimbi na kazi ya ubongo ni kuyachakata mawimbi kuwa kitu kinachoeleweka ila ufanisi wetu ni hafifu mfano mtu anakuita jumaa unamgeukia alafu anakuambia mama kasema fusgajsjksjbska hapo kwenye fusgajsjksjbska ndio kimbembe lazima umuombe arudie na anaweza kurudia na bado ikawa changamoto kingine bila kumuangalia usoni mdomoni huelewi asemacho hata ukiongea kwa sauti nyuma yale haelewi ila anasikia unaongea.
 
Ila samahani kidogo hii ishu imekuwa serious sana .Nyuzi kibao zimerindima kuhusu huu ulemavu wa kupoteza kusikia sijui tatizo ni nn!?
Wengi hawakuzaliwa na tatizo hilo , changamoto mbalimbali wanapata katika kuendea fursa mbalimbali .

Cc Mheshimiwa Dkt. Gwajima D
Ni kweli tatizo sio la kuzaliwa binafsi limenianza nikiwa shule ya msingi sikumbuki ni mwaka gani na kadri siku zinavyokwenda ndo linazidi kuongezeka kwani uwezo wangu wa kusikia sasa sio kama wa miaka miwili au mitatu nyuma, na hospitali zetu kila nikienda solution yao ni hiyo hearing aid
 
Habari zenu wakuu,

Mimi ni kijana wamiaka 24 kwasasa, elimu yangu ni kidato cha nne ambapo nilifaulu vizuri ila nilishindwa kuendelea na masomo kutokana na changamoto mbalimbali ikiwemo kutosikia vizuri.

Baada ya kumaliza shule mwakav2015, kuanzia 2017 nilianza rasmi kujifunza kutengeneza sofa katika ofisi za ndugu zangu ambapo mpaka sasa nilipofika nina ujuzi wa kutosha kutengeza sofa na vitanda vya sofa.

Changamoto ni kwamba hapa nilipo nakosa kazi zangu binafsi kutokana na hali yangu niliyonayo naishia mara moja moja kufanya kazi za mafundi wenzangu kwa malipo kiduchu ambayo kiukweli yanashindwa kunitoa hapa nilipo kwani bado nakaa nyumbani kwa ndungu zangu.

Naandika uzi huu kuwaomba wana jamiiforums wenye uwezo kunisaidia kupata kazi iwe kama hii niliyo na ujuzi nayo ama yoyote nipo tayari kwani nahitaji nijikwamue nijitegemee na mimi.

Mawasiliano yangu 0788362088 itapendeza ukinitumia sms maana hatutoweza kusikilizana vizuri kwa simu, nipo Dar.
Pole sana mkuu, usikate tamaa mimi ni mwenzako pia, japo sijui kiwango chako cha usikivu.

Ushauri wangu ni endelea kupambana na hiyohiyo kazi ulio na ujuzi nayo,kwetu wenye shida za hearing inshu za kuajiriwa tofauti na serikalini ni shida sana.

Kama uwezo upo kasome ualimu, waalimu wanasjiriwa sana serikalini.
 
nimesikitika. tuliwahi kumuajiri mdada wa kazi ana hiyo hali. tulimvumilia na kuishi naye kwa upendo mwingi.
bahati mbaya sana nchi uliyopo ndio mtihani zaidi. ila nadhani kuna vifaa vile huwa mnawekewa kwa lengo la kuongeza usikivu. umewahi kufuatilia hilo?
Vile vifaa havisaidii, na vikisaidia msaada wake mi mdogo sana.
 
Ila samahani kidogo hii ishu imekuwa serious sana .Nyuzi kibao zimerindima kuhusu huu ulemavu wa kupoteza kusikia sijui tatizo ni nn!?
Wengi hawakuzaliwa na tatizo hilo , changamoto mbalimbali wanapata katika kuendea fursa mbalimbali .

Cc Mheshimiwa Dkt. Gwajima D
binafsi sijazaliwa nalo na lilianza baada ya kumaliza darasa la 7
 
Pole Sana .
Naimani MUNGU atakuvusha katika hii changamoto nothing impossible. Keep GOD first.
 
Kuwa strong na Hali iyo Ni maisha yetu wanadamu,hapa duaniani tunapita tu.
Ila nilivyokuona ujuzi wako nikawaza kuwa mtu anaweza akafungua ofisi wewe ukawa fundi mkuu. Mnaelewana malipo mnalipanaje kwa kila kazi inavyopatiakana
Sema saivi mfuko hauko vizuri mie nimekuwazia ivyo
 
Kuwa strong na Hali iyo Ni maisha yetu wanadamu,hapa duaniani tunapita tu.
Ila nilivyokuona ujuzi wako nikawaza kuwa mtu anaweza akafungua ofisi wewe ukawa fundi mkuu. Mnaelewana malipo mnalipanaje kwa kila kazi inavyopatiakana
Sema saivi mfuko hauko vizuri mie nimekuwazia ivyo
Asante sana, binafsi nahitaji sana kitu kama hicho ila namna ya kumpata mtu awekeze kwako nayo mtihani
 
I feel you brother pole sana. Daaah. Naelewa ushajaribu mengi kuwa sawa. Sema kipande cha kazi. Nikuombe pambana online. Tena ukiweza una simu nzuri fungua insta account tangaza biashara yako. Jiamini tena waambie watu wewe mtu wa aiina gani, tunahuruma sana watanzania.tutakusaidia
 
Back
Top Bottom