Nina kijana mdogo ameathirika naishi nae, anagegeda sana vibinti vya watu, nimsaidiaje?

Nina kijana mdogo ameathirika naishi nae, anagegeda sana vibinti vya watu, nimsaidiaje?

We mrudishe kijijini. Utamhurumia mmoja lakini yeye ataua wengi. Usiwe na huruma juu yake tu angalia na anaotaka kuwaangamiza.
huo siyo ushauri mkuu kwani kule kijijini hamana mabinti?cha msingi dogo apelekwe apewe ushauri nasaha msiangalie tuu kua anaambukiza maana uwezo huo hana kwa kua anatumia dawa sema kumshauri kua anapofanya ngono zembe pia anachukua maambukizi mapya kwa hiyo wale virus watakua wengi na watajenga usugu wa dawa muwe mnasoma kabla ya kutoa ushauri unapoathirika ukawa unatumia arvs huwezi muambukiza mtu maana wale wadudu wamelewa wamelala ila sasa ukifanya na ambaye hatumii dawa na ni muathirika apo unachukua maambukizi mapya na pia unapofanya sana kinga inashuka maana kwa umri wa huyo dogo utakuta anapiga bao zaidi ya tatu ...cha msingi apewe elimu ale vizuri aache mawazo ,afanye zoezi,apate mwathirika mwenzie anaetumia dawa afanye ngono kama kawaida bila madhara ataishi miaka mingi sana ....ukimwi siyo ugojwa...........
 
U
Mkuu nina watoto,wangu nilishawaelekeza na wanajua kinachoendelea juu ya huyu kijana wangu mpendwa!!Pale nyumbani sidhani,maana wa kike nilienae bado ni mdogo
Usijidanganye lazima ukae nae chini na uongee nae vizuri akuelewe. Kama yeye hajakuelewa lakini ukaishia kuwaelewesha wanao basi ni kazi bure. Pia haya mambo ya uelewa wa HIV yanaendana na umri.
 
Kwanini huwa mnaeleza mengi kiundani? Nauliza tu kama umeeleza kila kitu ukweli bila kupindisha, akisoma humu unaona itakuwaje kati yako na yeye?

Vizuri kumsaidia ila anatakiwa apate kuona wataalamu wa kumtoa katika hiyo ya kujigundua alizaliwa nayo, hayo ya mazingira kusoma etc hayatamsaidia bali naona ni kama hajali kabisa na pia alishajiachia lolote na liwe.

Mpeleke akasaidiwe kuondokana na yaliyomkuta.
Anaejua undani wa hii habari ni mtoa uzi ....sisi wote ni wasomaji tuu na ku-comment.utajuaje km kuna sehemu kapindisha kidogo ili kupunguza undani wa hili jambo!
 
Nafahamu hawezi kufika huku,lakini naelezea kwa undani kwa sababu sio wote wanaojua kisa hiki
Ni vizuri kuelezea kwa undani kutoa nafasi kwa wanaoshauri,kushauri baada ya kuwa wameelewa kisa kamili.Zamani tulitumia Ukurasa wa "MAONI/MASWALI" wa gazeti la Uhuru,sasa mitandao imeturahisishia

Sawa unajaribu kujitetea naona, Ila mimi bado nasimamia niliyoandika. Hujawahi kuona mitandao mingine pia ilivyo na habari za c&p kutoka JF zinavyosambaa?

Kiukweli umeieleza kama wewe kujifikiria kutoka na picha nzuri ukisomwa, ila unasahau huyo kijana anatakiwa apewe msaada wa kisaikolojia pia na mengineyo haraka sana.

Muhimu ni maisha aliyonayo ambayo hajakubaliana nayo ndio, na kuanza kumsaidia hata hasiposoma kwa nwaka ila awe salama.
 
Mwenywe na ndugu yng ana ngoma ana sambaza balaa natamanigi niwastue wadada anaotembea nao ila nashindwa maana wengi anaotoka nao ni wanafunzi wa sekondari n vyuo
siyo kila unaetembea na mwathirika utaupata kupata hiv ni mpaka usugue kweli kweli patokee mchubuko wote wawili unaweza kusex na mwathirika kama umemwandaa vizuri ukamlainisha na kutokukamia mechi ukatoka salama mkuu..
 
mwenyewe kunadada mmoja huku mtaa najuwa ana gwegwe anagwa tu kama kifulushi cha tigo hapo mzee mwache awape dozi kwa ha vitabu vya mungu vinasema mshahara wa zambi nimauti kwa acha awagawie mauti
Atapita jamaa atamgegeda ataenda kumgegeda na dem wako biashara kwisha, ndo tunavokufa hvo et kunaungua kwa jiran m hakuwez ungua umesahau kuna fenc ya mabua inawatenganisha, damn
 
huo siyo ushauri mkuu kwani kule kijijini hamana mabinti?cha msingi dogo apelekwe apewe ushauri nasaha msiangalie tuu kua anaambukiza maana uwezo huo hana kwa kua anatumia dawa sema kumshauri kua anapofanya ngono zembe pia anachukua maambukizi mapya kwa hiyo wale virus watakua wengi na watajenga usugu wa dawa muwe mnasoma kabla ya kutoa ushauri unapoathirika ukawa unatumia arvs huwezi muambukiza mtu maana wale wadudu wamelewa wamelala ila sasa ukifanya na ambaye hatumii dawa na ni muathirika apo unachukua maambukizi mapya na pia unapofanya sana kinga inashuka maana kwa umri wa huyo dogo utakuta anapiga bao zaidi ya tatu ...cha msingi apewe elimu ale vizuri aache mawazo ,afanye zoezi,apate mwathirika mwenzie anaetumia dawa afanye ngono kama kawaida bila madhara ataishi miaka mingi sana ....ukimwi siyo ugojwa...........
Sio kweli hata ukitumia ARV bado unaambukiza wengine. Ingekuwa huambukizi basi pia watumiaji wasingekufa eventually. ARV inapunguza tu kasi ya virusi kukushambulia wewe ulieathirika
 
Sawa unajaribu kujitetea naona, Ila mimi bado nasimamia niliyoandika. Hujawahi kuona mitandao mingine pia ilivyo na habari za c&p kutoka JF zinavyosambaa?

Kiukweli umeieleza kama wewe kujifikiria kutoka na picha nzuri ukisomwa, ila unasahau huyo kijana anatakiwa apewe msaada wa kisaikolojia pia na mengineyo haraka sana.

Muhimu ni maisha aliyonayo ambayo hajakubaliana nayo ndio, na kuanza kumsaidia hata hasiposoma kwa nwaka ila awe salama.
Basi mkuu!!Kama nimekosea kuwasilisha ujumbe wangu nisamehewe!!Haikuwa nia mbaya kuuliza ili nipate ushauri
 
Msisitize kuhusu matumizi ya condom

Pili hakikisha anatumia dawa zake vizuri, viral load ikiwa ndogo maambukizi hupungua

Tatu mtafutie mshauri nasaha wa kidini na wa afya wambadilishe tabia
 
Anaejua undani wa hii habari ni mtoa uzi ....sisi wote ni wasomaji tuu na ku-comment.utajuaje km kuna sehemu kapindisha kidogo ili kupunguza undani wa hili jambo!

Sababu nimejua kwa nilichosoma tunatofautiana katika mengi binadamu sisi, pia msome jibu lake hapo juu amesemaje mwenyewe.
 
Sio kweli hata ukitumia ARV bado unaambukiza wengine. Ingekuwa huambukizi basi pia watumiaji wasingekufa eventually. ARV inapunguza tu kasi ya virusi kukushambulia wewe ulieathirika
mkuu acha ubishi basi
 
Wakuu Wasalaam
Leo nimekuja tupeane uzoefu na ushauri.Nina bwana mdogo naishi naye.Ana miaka 18 kwenda 19 ni wa kiume.Huyu alikuwa mtoto wa jirani yangu kijijini nilipokulia.Ule ujirani wa kijijini ni kama ndugu tu,sbb huyu bwana mdogo toka anazaliwa mpaka anakua namuona,kila nikienda likizo basi namuona.Maana kwao na kwetu ni uzio wa minyaa tu ndio uliotutenganisha.

Huyu dogo wazazi wake wote walifariki kwa UKIMWI.Bahati mbaya na huyu dogo alizaliwa na maambukizi.Amekuwa hivyo huku akipatiwa dawa kuanzia umri fulani mpaka leo.Kilichonifanya nimchukue na kukaa nae,kuna wakati nirirudi likizo nikakuta dogo amedhoofu sana,sbb ilikuwa ameanza kugoma kutumia vidonge,hii ni baada ya kukua na kupata akili kuwa anatumia vidonge vile sbb ameathirika.

Ilihitaji ushawishi sana kumfanya dogo aendelee kutumia hizi dawa.Maana alikuwa mkubwa na akiwa shule akawa amepata akili kuwa vile vidonge anavyopewa kunywa ni kwa sbb ameathirika.Hakupenda kunywa akisema bora atangulie tu.

Sasa kwa sbb mimi kidogo ananiheshimu jumlisha kuniogopa,wakati wote wa likizo nikamsimamia aendelee kutumia dawa,hatimaye maamuzi ya kuja kuishi naye nilipo.Ameendelea kuwa na afya njema na tulimtafutia VETA baada ya kidato cha nne kutokufanya vizuri,na hii ni kwa sbb ni kama amekata tamaa.Kabla ya hapo darasani alikuwa anafanya vizuri sana kule sekondari.

Sasa bwana mdogo nilianza kustukia kuwa kaanza mahusiano ya kimapenzi.Na hii ni baada ya siku moja kumsikia akiongea kwenye simu asijue kama mimi na wife tupo ndani.Nikajipa zoezi la kutaka kuujua ukweli kupitia simu yake.Nikakuta kweli msg kadhaa toka na kwenda kwa mpenzi wake.

Kifupi dogo kaanza kugegeda,na alivyo HB na afya kuimalika huwezi kujua kuwa ameathirika.Sasa naona hata hapa mtaani kama vibinti vinamshobokea na havijui background yake.Hii inanipa wasiwasi juu ya afya yake na hao anaowagegeda.

Nilijipa siku nikakaa nae,nikampa somo kuwa hayo mambo anatakiwa kuyapa kisogo,atazame kwanza afya yake,lkn pia akumbuke bila kinga atwaangamiza vijana wenzake.Yaani ilikuwa kama nimeharibu.

Dogo akawa anaona kama namnyanyapaa!Anasema yeye pia ana haki ya kuwa na mtu maana umri wa kuwa na mpenzi eti umefika.Mimi kumwambia hivyo eti ni kama namnyanyapaa.Basi akaongea na mambo mengi yaliyonitia uchungu,sbb sikuwa na nia mbaya,bali kumsaidia yeye na hao watakaogegedwa nae.

Mimi bado nataka huyu dogo aachane na mwenendo wa kugegeda,japo nilionana na mshauri mmoja akasema sehemu nyingi huwa wanawatafutia vijana/wenza walioathirika ili wawe pamoja na kujijua kuliko kupeleka kwa wengine.Ila mimi naona umri wa huyu bado kwanza,atulie na kujenga afya.

Toka nimwambie alizila kula siku nzima,siwezi kumkaripia sana sbb ya hali yake.Sipendi aendelee sbb anaweza kuathiri afya yake na wale anaoshirikiana nao.

JF hakiharibiki kitu,kwa mazingira kama hayo,nyie wananzengo wenzangu mngefanyaje?Nifanyaje ili nimsaidie huyu dogo na huyo aliyeanzisha nae mahusiano?Tupeane mawazo.
Kama ana shughuli ya kufanya inayomuingizia pesa,mshawishi ampate mmoja aoe .Itamsaidia kutulia na kuwajibika maana sasa atahamishia nguvu zote kwa mkewe na kutengeneza familia,kama hana shughuli mshauri kwanza apate shughuli ya kumuingizia kipato halafu aoe.
 
Na wewe kalishakupa?

Duh mkuu nitake radhi, mm nakaribia kustafu ajira hapa. Siwezi fanya huo ushenzi, ni mdogo wa mke wa jirani alizaliwa nao sasa ameshavunja ungo na anagawa kwa hawa vijana wa form2,3 na kanajijua hatari sana
 
Back
Top Bottom