Nina mashaka kuwa wasaidizi wa Rais Magufuli wanamdanganya

Nina mashaka kuwa wasaidizi wa Rais Magufuli wanamdanganya

KooZito

JF-Expert Member
Joined
Dec 14, 2020
Posts
397
Reaction score
1,377
Tahadhima kwenu kizazi Cha Covido-19!

Leo akihutubia kijijini kwake Chato katika uzinduzi wa shamba la miti (Silayo Forest) Rais Magufuli alitumia jukwaa hilo kutoa msimamo wa Serikali kuhusu vita kuu dhidi ya janga la Corona.

Pamoja na mambo mengine, Magufuli ameonya Watanzania kujihadhari na chanjo mbalimbali zinazoletwa na "vipepeo weupe" yaani wazungu akisema, "nchi hii ni tajiri sana" akimaanisha weupe hao hawana nia njema na Afrika.

Rais Magufuli ametolea mfano,"kuna nchi moja ililetewa chanjo kwa mabinti wa miaka 14 ili kujikinga na kansa ya kizazi lakini ikaja kugundulika chanjo hiyo iliwafanya wasichana hao wasizae kabisa", wawe wagumba.

Sijui Magufuli amesahau, hakuwepo nchini, au amedanganywa na wasaidizi wangu. Kwa mujibu wa kumbu-kumbu zangu ni kwamba chanjo hiyo ilitolewa kwa watoto wa Kitanzania kati ya Mwaka 2013/14 ikihamasishwa na Wizara ya Afya chini ya udhamini wa USAID.

Kama ni kweli maneno ya Mr. President, basi nchi hiyo ni Tanzania na tujiandaye kwa wimbi kubwa la kinadada wasiozaa, wagumba.

Hofu kubwa kwa wasichana wetu waliochanjwa.
 
Mabeberu hawatupendi kwa sababu nchi yetu ni tajiri sana
Tupo Uchumi wa kati
Au nasema uongo ndugu zanguuuuu
Sio Mitano tena ni milele
Mabeberu wanayajua mavieitee??
Sisi tunatembelea mavieitee

IMG_20210101_160453.jpg
 
Nimejisikia vibaya na aibu pole kwa wataaluma wetu wizara ya afya, kwa kauli ile toka kwa mkuu wetu kuponda chanjo kwa ujumla na lugha ya namna ile. Any way mkubwa hakosei japo sidhani kalishwa na yeyote kauli zile.
 
Rais yupo sahihi,sema hotuba zake hazinaga mpangilio kwahiyo kumwelewa inahitaji uwe unahusianisha tu vitu,hayupo systematic kuhutubia,,
Hata lugha ya kiswahili inamkwaza maana huku Unguja mara zingine anatuacha pabaya labda angekua anatumia kiswahili
 
Nimejisikia vibaya na aibu pole kwa wataaluma wetu wizara ya afya, kwa kauli ile toka kwa mkuu wetu kuponda chanjo kwa ujumla na lugha ya namna ile. Any way mkubwa hakosei japo sidhani kalishwa na yeyote kauli zile.
Chakusikitisha ni majuzi tu kule mkoani Kagera alikuwa na hao hao Wazungu akiwabembeleza waje wawekeze Tanzania. Kuna haja gani ya kuwaita wawekezaji wenye roho mbaya kiasi kile kwenye nchi yetu??

Rais aambiwe ukweli kwamba Duniani tunategemeana. Wewe una madini mimi nina teknolojia na fedha tufanye biashara. Sasa nani atakubali kufanya uwekezaji kwenye nchi ambayo huaminiwi??

Mzee nilimsikia akisema hana mpango wakugombea tena hivyo habembelezi mtu. Ni sawa lkn atuachie nchi yetu ikiwa na mahusiano mazuri na nchi zingine.
 
Hotuba ya leo imeonesha jinsi alivyo empty kichwani, kwani chanjo zote za TB, surua n.k tunazowachanja watoto wetu zimegunduliwa Afrika?

Jamaa ni mtu wa hovyo kabisa, na bila shaka amezungukwa na wajinga watupu wanaomwambia anachotaka kusikia.

Amekomaa kweli na kumwomba Mungu, hajui kuwa huyo Mungu wa kikatoliki aliletwa na mabeberu??
 
MKUBWA HAKOSEI lakini mwanasayansi wa Chemistry wa kiwango cha PhD kwa hili la chanjo amekosea!

Taasisi yetu ya magonjwa ya binadamu NIMR inaweza ikaomba audience na Mwalimu wa Chemistry na kujaribu kumuelewesha.

Leo hii couple ya HIV inazaa HIV free child,leo hii Surua imetokomea pamoja na polio.Science ni pana na tuepuke kuichanganya na siasa.
 
Mabeberu wenyewe kazi yao ni kupambana na Tanzania tu.
Nadharia za wakomunist inferiority complex,

Aache kukua kwenye cocacola,maziwa ya kopo, computer, condoms,madawa ya ARV vyakula nk aje akuuwe kwenye chanjo.

Hawa waliosoma syllabus za zamani zilizopandikizwa chuki dhidi ya weupe tabu kweli kweli.
 
Back
Top Bottom