Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
ameshakuja mahakamani na anaendelea kummaliza gaidi mbowe yaani anamuanika maovu yake yote makomandoo wanatoka anabaki aliyelikoroga mbowe jela mlangouko wazi
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
ameshakuja mahakamani na anaendelea kummaliza gaidi mbowe yaani anamuanika maovu yake yote makomandoo wanatoka anabaki aliyelikoroga mbowe jela mlangouko wazi
Mwache aje tu. Sio siri kuwa kipindi kirefu MMEFANYA bidii kubwa kuimaliza CHADEMA lakini Mbowe amekuwa ni kikwazo kikubwa pamoja kuharibu hata 'mali' zake. Utunzi huu wa Afande Ramadhani Kingai ambao ni mwendelezo tu, nao unazidi kupwaya kila uchao.ameshakuja mahakamani na anaendelea kummaliza gaidi mbowe yaani anamuanika maovu yake yote makomandoo wanatoka anabaki aliyelikoroga mbowe jela mlangouko wazi
Mbowe ni sawa na watu wengine hata walinzi anafanana nao wewe ndo unamuona mungu.yaani wewe kumuona kwenye TV tu tayari unamjua vizuri sana MWAMBA MBOWE?
Aise!1. Wakati akitoa ushahidi wake wote Mara kadhaa wakili aliyemuongoza alisita kuendelea kumuuliza na kuanza kuteta chini kwa chini ikionesha Kuna majibu Alitoa nje ya matarajio yao.
2. Kucheleweshwa ushaidi wake kwa siku moja ama kulikuwa na mashaka juu ya ushaidi wake kutoka kwa mawakili wa Serikali au yeye mwenyewe.
3. Amejaribu kutoa kauli za kumtetea Mbowe kuwa pesa alizotumiwa na Mbowe zilikuwa za nauli kwaajili ya kuifikisha walinzi kwa Mbowe na sio za kununua vifaa au vya Ugaidi au malipo ya kufanya Ugaidi.
4. Hoja ya Mbowe kuajiri makomando wanne tu kwaajili ya kukata miti ni kiloja kabisa. Kwamba ilihitaji kuwa na makomando ndio wakate miti.
5. Je, makomando wanne wanawezaje kukata miti na kuchoma vituo vya mafuta Tanzania nzima ni swali gumu kabisa kulielezea.
6. Je, mawakili wanaamini uchomaji vituo vya mafuta na kukata miti ungeweza kuvutia maandamano au kuwatia watu woga na kujifungia ndani? Kama vibomu vya machozi tu na milio ya riasasi watu hujifungia ndani milipuko ya vituo vingevutiaje watanzania kuandamana.
7. Tanzania ina makomando wangapi? Makomando hao wanne wangesaidia vipi Mbowe na elimu yake hao makomando wanne tu kusimamisha nchi isitawalike na kudhibiti makomando zaidi mia watiifu serikalini.
8. Urio lazima aoneshe baada ya kile alichopanga baada ya kuchomà vituo ni vipi Mbowe angepewa nchi na
sio Wanajeshi kuchukua nchi.
9. Je, Urio hajaonesha chochote ambacho kinaonesha kuwa makomando wa Mbowe na yeye walivyojiratibu ualifu na ushahidi waliokuwa nao kama vile kuambiwa silaha walizokuwa nazo.
10. Je, kwanini Urio hakuchagua kusimama na makomando kwa kuweka nguvu kwao ya pesa na hata ajira serikalini upya ili waende kukusanya ushahidi wa ualifu na sio kuwaunganisha kwenye ualifu moja kwa moja.
11. Urio alionesha walijuana na Mbowe tokea 2009. Iweje Sasa Mbowe akate mawasiliano nae tu mara baada ya kumuunganisha na makomando. Yani akaacha kumwamini na kuanza kuwaamini makomando aliokutana nao chini ya mwezi na kuwashirikisha kwenye mipango hatari.
12. Kwanini wapelelezi walimuachia Urio jukumu la kutafuta watu wake mwenyewe na sio kumuandalia kati ya hao watu makachero au kachero moja wapo ili akafanye Kazi na Mbowe ili wapate usibitisho kamili na usio na Shaka.
13. Kwa ushaidi wa Urio mtuhumiwa kamili alikuwa moja tu Mbowe. Hawa wengine ni watuhumiwa aliowafundisha uhalifu na kuwaingiza ni yeye.
14. Urio anakiri pia kujua uadilifu wa watu aliomtafutia Mbowe afanye nao Kazi. Ndio maana akasema alijua wapo kwenye viapo na angewaambia kuhusu kufanya uhalifu wangekataa.
15. Urio pia anakiri pia hao watu aliheshimiana nao na kujuana nao kitambo. Na aliwaalifu wakiona kuna dalili ya uhalifu wamtaarifu. Akawakumbusha kuwa bado wapo kwenye kiapo. Hivyo yeye Kama kiongozi wao hakuwapanga kufanya ualifu. Je kwa mazingira hayo walithubutu vipi kuwa huru kumweleza moja kwa moja kuwa wanaenda kufanya uhalifu bila woga wowote Wala kuwashawishiwa kwake?.
16. Urio anasema hajui maana ya home boy.
17. Urio anaonesha pia kuaminiwa mwanzo na wapelelezi na kuachiwa kuratibu kila kitu. Lakini mwishoni anaonesha kutoaminika tena na kuombwa simu zake zichunguzwe. Maana Kama wangemuamini wasingemnyanganya simu bali wangemuomba namba zake za simu tu ili watafute ushaidi wanaoutaka. Kuchukua simu ni kutafuta ambayo hakuyasema.
18. Kwa kunyanganywa mawasiliano binafsi wakati yeye si mhalifu ilikuwa ni Kama kumtesa Urio kisaikolkjia.
19. Urio anasema amejuana na Mbowe toka mwaka 2009. Toka wakati huo wote hajasema Mbowe kumshirikisha kwenye uhalifu wowote na kunachaguzi nyingi zimepita. Kwanini mwaka 2020 Tena Mbowe anashirikisha watu aliofahamina nao kwa siku chache mno. Chini ya siku 10.
20. Urio amejenga hoja tokea awali kuwa Mbowe alihitaji ukaribu na Urio ili kupata mifumo ya ulinzi na kuwajua wanaoutaka kuhujumu chama kwa kutoa Siri.
Urio akija kesho mahakamani nishitueni. Naona ushaidi wake unaegemea kumuondolea Mbowe shutuma.
Kaingia jeshini akiwa Na form iv akaunga akapata advance diploma ya mambo ya parachute,Take note
1. Anasema aliwasiliana na DCI kuwa Kuna watu wanataka kufanya ugaidi.
Yeye ni kiongozi wa platoon, utaratibu unaelekeza kuwa taarifa zote unazotilia shaka usizipeleke URAIANI, zinatakiwa zipelekwe kitengo Cha usalama jeshini ambacho ndicho chenye jukumu la kufanyia kazi taarifa zote.
Je, ilikuwaje yeye apeleke taarifa URAIANI?
Je, viongozi wake wa 92KJ/Mgulani walitaarifiwa?
Je, number ya DCI aliitoa wapi?
Je, kuna kiongozi wa ngazi yake aliyewahi kumshirikisha na hivyo kupata ushauri Ili apeleke suala la kijeshi URAIANI?
2. Anasema watuhumiwa walifukuzwa kwa utovu wa nidham lkn reference zake zote alizipata kwa admin officer
Je, ndio utaratibu wa kijeshi?
Kama sio utaratibu wa kijeshi aseme ni utaratibu Gani wa kupata taarifa jeshini
Mimi sio mwanasheria
Lakini huyo ni mtuhumiwa mwenzao na hao makomando wengine ila yeye amepewa rushwa either ya kuendelea kubaki kazini Ili atoe ushahidi wa UONGO.
Kosa la kukubali kuwaunganisha wenzake na uhalifu ni kosa kubwa sana. Yeye anatakiwa kuzuia uharifu kabla ya kumtokea.
Inawezekanaje yeye ajue uharibifu utatokea then aruhusu akitegemea nini?
Pia kitendo cha yeye kufanya mawasiliano hayo tu tayari ni KUJIHUSISHA NA SIASA kosa ambalo linamuachisha moja kwa moja na jeshi.
Yaani kifupi
Ushahidi wa URIO umefeli sana/ ni zero
Haya ni matokeo ya elimu. Je, ana elimu Gani na akakubali kulishwa utumbo hivyo?
Lieutenant/ luten kafeli sana.
Sasa unaniuliza mimi ambae siko mahakamani kama wewe?Thibitisha kwanza kama ile bastola ni ya Adamoo au alikutwa nayo. Leteni finger print. Baba acha kuwa mpumbavu. Fikili deeper between lines
Tulieni kwanza ushahidi bado unaendelea kuja.''Askari aliyeiva hawezi kupokea mpangokazi wa Mhalifu na kuuacha hivyo hivyo bila kushauri chochote ambacho kingemtia hatiani mhusika bila kuathiri wengine wasio na hatia. Ni wapi Urio baada ya kupeleka taarifa kwa DCI na Kingai alipoonesha kumwingiza Mbowe mtegoni zaidi ya kumwacha aendelee na mipango yake na yeye kutegemea huruma ya Mbowe kumpigia simu? Komando huyu anayehusudu nguvu pipa na akili Kisoda anamwachia Mhalifu aendelee na uhalifu bila followup wala tailing?''
Wengi wapo jeshini Wana elimu ya hapa na pale na ndio maana magu alishindwa kupeleka huko Mambo ya vyeti feki.Kaingia jeshini akiwa Na form iv akaunga akapata advance diploma ya mambo ya parachute,
mm naomba kueleweshwa hii ya kuingia jeshini ukapata cheo mpaka koplo kisha ukaruka mpaka nyota.
very interesting!!Moshi komando wawili walikamatwa na polisi sita...
Kwa akili yako hayo maelezo yaliyotolewa ndio yanatosha kumtia mtu hatiani kwa ugaidi? Embu tawanya ubongo kidgo alafu ujibuTulieni kwanza ushahidi bado unaendelea kuja.
Haya yote mnayoyajadili hayana muelekeo wa kesi.
Maelezo yalikwishatolewa kwa maandishi.
Hizi mbwembwe za mawakili wa-somy ni vihoja mahakamani tu.
Kwa hiyo hapo wanafanya nini? Kumbe wewe ni Zuzu kiasi hiki? Yaani unadhani Jaji atachukua maelezo kwenye faili la Polisi na kutoa hukumu? Au unadhani Jaji atatumia Committal proceedings kutoa hukumu? Eti yanayotolewa Sasa mahakamani hayana mwelekeo wa kesi? Polisi failure wewe!!!Tulieni kwanza ushahidi bado unaendelea kuja.
Haya yote mnayoyajadili hayana muelekeo wa kesi.
Maelezo yalikwishatolewa kwa maandishi.
Hizi mbwembwe za mawakili wa-somy ni vihoja mahakamani tu.
uthibitiswaji ndo tabuNaona unawapa mbinu za kumkamata Mbowe huko mbeleni....[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Kwa haya maelezo yako nimekwisha kukuelewa/kufahamu uwezo wako wa akili hasa ktk kufikili. Naomba nisiendelee kukujibuSasa unaniuliza mimi ambae siko mahakamani kama wewe?
Mashahidi waliowakamata wameiambia hivyo mahakama na vielelezo vimepokelewa mahakamani kama ushahidi.
Sasa wewe nae unaleta vi-maswali uchwara kwangu?
Sisi wote tuko nje ya mahakama....iacheni mahakama ifanye kazi kwa uhuru.
Kuna kosa kisheria kuhitaji makomandoo?Huoni kuna haja ya kuongeza ulinzi hasa ukizingatia tukio la kupigwa risasi Lisu na wasiojulikana bado kukamatwa?Hebu tafakari kwa kina zaidiNa kwanini Mbowe ahitaji ulinzi wa makomandoo na sio mabaunsa ambao hata yeye anaweza kuwapata maana zamani walikuwa watumishi wake akiwa na Bilicanas?
Je, hao makomandoo wangefanya kazi zipi kwake ambazo zingekuwa mpya tofauti na maisha yake ya siasa zaidi ya miaka ishirini?
Je, wajua komandoo mmoja anaweza kuwa na athali kubwa kwa nchi ambayo raia wengi hawana uelewa wowote wa kivita?