Nina miaka 27, bado nina ndoto ya kuwa Daktari (Médical Doctor)

Fuata wazo hili.safi sana🤣🤣🤣💺
 

Komaa bhana, inawezekana kabisa.
Soma S.Chand XI&XII Physics. Solve examples tu na NCERT na MCERT. Kazi kwisha huwezi kosa hata C ya Physics plus practicals. Soma vitabu vya T.I.E , sasahivi elimu ya Advance imerahisishwa.

Biology pale kuna Biological sciences, komaa nayo.

Chemistry, sijui kama kuna mtu amemzidi Ngaiza, soma vitabu vyake. Organic Chemistry soma vitabu vyake alafu penda kuelewa mechanisms za organic chemical reactions.

General studies tafuta D tu .

Basic Applied Mathematics pale, hapa nakushauri tafuta wale wanaosoma PCM watakubrush.

Kila kitu kinawezekana ukiamua, narudia ukiamua. WAGMI.
 
Ninachokushauri kwa sasa Jaribu kuanza Kusoma Diploma kama matokeo yako ya Four Yanaruhusu....

Kutokaka na umri wako umekaa sana nyumbani miaka 10 dont think PCB ni chaguo sahihi kusoma after 10 years si nyepesi kiasi hicho unachofikiri
(Its not easy mdogo wangu)

Diploma unaweza kupata nafasi ya kufanya sup na kurudia module (Carry) ila mzee mambo ya NECTA ukianguka umeanguka..

Diploma Anza na CO soma ukimaliza fanya kazi unaweza ukapiga MD hata kama una miaka 40 na ukamaliza Daktari hastaafu ila anapumzika unaweza ukaendelea mpaka Daktari bingwa na kwa sasa Ubingwa umeongezwa miaka ya kustaafu mpaka 65...
 
Mzee Advanve tena PCB kwa Mwaka mmoja simshauri 🤣🤣 atapoteza mda tu
 
Huo umri bado ni mdogo kama kweli una nia ya dhati. Ila inabidi JF nzima tufunge na kuomba ili upite salama kwenye huo muziki wa PCB. Kwa upande mwingine kama ulipata 3 form IV inaelekea ww sio kipanga. Kama vipi endelea kukomaa na hicho unachokifanya kama kinaenda vizuri uwekeze vya kutosha kuliko kulazimisha mambo ya elimu. Miaka 27 pia kuanza kufikira familia ni muhimu.
 
Hahaah Mambo Ya BS na Chand ,understanding Chem, Princple.. Kwa mwaka mmoja tena QT Halafu hajasoma kwa miaka 10

Mzee 🤣🤣🤣 astick na dip tu maana atakachokutana nacho Mungu ndo anajua 😅😅

Sema route ya diploma ndo nzuri ila itabidi aanze certificate.
 
Clinical medicine hakunaga carry
 
Kinacholeta shida form 4 alipiga 3. Yaani matumaini ya huyu dogo kumudu PCB ni madogo sana.
Nilipata Div 1 form four Na PCB nilichomoka kwa uwezo wa Mungu na kama nikiambiwa nirudi kusoma Advance siwezi kubali Miaka 1000😅😅

Kuna mpwa wangu mwaka 2013 alimaliza form four akataka kwenda PCB nikamwambia Nenda Chuo alinishukur baadaye yakumaliza maana wenzake wote walipiga chali halafu wakarudi tena kusoma dip
 
Halaf ndugu mambo ya kufanya mtihan wa form six kama private candidate ogopa kama ukoma,kwenye watu 100 ambao huwa wanatumia hii njia sio chini ya 85 huwa wanafeli yaani wanpata four na zero
 
Hahaah Mambo Ya BS na Chand ,understanding Chem, Princple.. Kwa mwaka mmoja tena QT Halafu hajasoma kwa miaka 10

Mzee 🤣🤣🤣 astick na dip tu maana atakachokutana nacho Mungu ndo anajua 😅😅
Diploma ya Clinical medicine nayo sio mchezo.hata waliopata div II au I inawatesa balaa,wengi Wana sup .na wengene wanasoma mpaka miaka 5 badala ya miaka 3🤣🤣🤣🤣🤣💺.pia ada zipo juu+hostel+chakula,haipungui 3.5M Kwa Mwaka🤣🤣🤣🤣💺
 
Kombi yoyote yenye P iheshimiwe tu. Jamaa yangu alipiga 1.8 pale Tanga Tech na kwenye PCM kanyoosha A tatu. Form six Ilboru akagonga div III. Mwingine one ya 9 form form four ila div 4 form 6. Bahati nzuri wale walikuwa ni vipanga wakaamua kwenda Diploma DIT mambo ya maabara. Walinyoosha vibaya hadi wakamaliza degree zao kwasasa wote wako kwenye green pastures.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…