Nina milioni 100 naombeni wazo la biashara


nime kuelewa boss wangu. kuna jamaa kaniambia biashara ya bar haina faida
Sijuwi wewe boss wangu una experience na hiyo biashara?
 
Asante sana ndugu naisi mtaji wangu ni mdogo kuanzisha kitu kikubwa kama hicho. Au we unasemaje?
Huo mtaji ni mkubwa sana, ni suala la wewe kuchagua aina nzuri ya bidhaa.
 
Ndo maana nimekuja kwenu ndugu zangu
kama unayo wazo ya bidhaa niambie ndugu yangu
Mfano: Jaribu kuangalia hapa 👇👇👇
Soneriinternational.com ( Mo huwa anatoa bidhaa zake nyingi hapo).
 
Nimesoma mwanzo mpaka mwisho unapoona hii comment yangu. Idea nzuri isiyo na mambo mengi ni hii hapa.
Itategemea wewe una elimu au uelewa kiasi gani, uzoefu na ni mtu wa aina gani.

Jipe muda miezi kadhaa kujiandaa kila idara
 
Habari Mkuu

Naomba tuongee hii vizur, nashindwa kukuPM

Can you pls PM me
 
Ngoja waje kukupa muongozo na kila la kheri...
 
Tafuta Chaka fungua pharmacy yko Kaa utulie Mambo yatajipa! Au vipi tafuta Chaka fungua duka la spea za Bajaj@pikipiki
Nenda kusanya mazao mkoani lete mjini
 
Tafuta Chaka fungua pharmacy yko Kaa utulie Mambo yatajipa! Au vipi tafuta Chaka fungua duka la spea za Bajaj@pikipiki
Nenda kusanya mazao mkoani lete mjini
Aende na pharmacy.
Atakushukuru sana au
Atafute vibali asafirishe mazao nje ya nchi.
 
Siku hizi nimeishiwa idea za kibiashara kabisa. Kwangu biashara uzaliwa palipo na huitaji. Pasipo huitaji huduma au bidhaa itakubidi utumiw nguvu nyingi kuuza.

Neno langu. Palipo na hatari ndipo palipo na fursa/ uwezekano.

Kwa dar watu wako na capital wako teyari ku compete sokoni so kumbuka kuchagua sahihi.
 
Uwakala mkuu wa mitandao ya simu. Airtel Na vodacom. Hii kwa hela yako mnakuwa wawili na pikipiki mbili kazi yenu ni kuweka flot bank na kuwasambazia mawakala mtaani cash na flot. Hii mkiwa serious inalipa sanaaaa na wala haina stress. Na mkishajulikana kwa mawakala mnapiga kazi kilaini sanaaa......

Mnaanza kazi asubuhi saa 1 mpaka saa 12 jioni...... Mda huu bado unakuwa ni muda mzuriiii kwa usalama wenu na pesa zenu.

Ila hii biashara uzuri wake ununui bidhaa kusema biashara ikikushinda basi utakuwa umepoteza pesa zako au utaanza kumtafuta mtu umuuzie bidhaa kwa bei ya hasara HAPANA!! Biashara ikikushinda pesa yako inakuwa ipo palepale. Kama utakuwa hauna cash basi utakuwa nayo kama flot kwenye simu zako za kazi.

Jaribu hii na wala usikimbilie biashara zenye faida kubwaa kwa misimu ambazo hazina uhakika wa kukuingizia faida mfululizo ndani ya miaka miwili mbele......

Ila hii biashara ukishatengeneza soko ndani ya miezi yako mitatu...... Kinachobakia nikufanya kazi kwa uhakika na faida ya uhakika kila mwezi.

Sent from my Infinix X626 using JamiiForums mobile app
 
Biashara ya pharmacy inalipa sana ukipata location nzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…