Nina millioni 80 nataka ushauri wa biashara

Tafuta mtu ardhi na halmashauri nunua shamba lets say acre 20 gawa viwanja hata 60 weka title deed kwenye viwanja wape halmashauri Wauze watakata commission Yao si unaona tunavyokimbilia halmashauri zikitangaza viwanja
 
Subayi, una haki ya kufikiri unacho fikiria lakini naweza kukuapia mbele ya miungu yote kuwa at the moment crane zenye tani 20 ni nyingi sana, hivyo kazi za kugombania! Na zenye tani 25 sio nyingi sana lakini kazi zipo na hazipumziki! lakini kuanzia tani 30 kwenda juu ni chache na kazi ni nyingi mno mno! Mara iringa, mbeya, dar kwenyewe, tanga, mtwara nk! kazi ni nyingi sana!
Kwa upande fulani nipo kwenye hilo eneo la kibiashara hivyo nafahamu! Kazi zipo nyingi sana, na hata ukitaka kuuza wateja ni wengi mno mno!

Hizi heavy equipment....haziozi, na hata zikiharibika zinatengenezeka na spea zipo! Na kwakuwa ni biashara yako utakuwa unafuatilia kila kitu na hasa service zake!

Pia mkuu, embu fanya risech kidgo...jifanye una kazi ya tani 30, kwa siku tatu na utanataka crane.....ukiipata kwa haraka...mshukuru mungu....vinginevyo utasubir kidgo....na bei yake utakuja kutoa ushuhuda hapa!
 
Wakuu hebu nipeni ushauri wa biashara nimepata hizo pesa hapo juu millioni 80 lakini kila nikichekecha biashara ya kufanya ilipe nakua sioni sasa nimeiona niweke hapa ili nipate mawazo nijue pa kuanzia.Mimi naishi mkoa wa Dar-es-salaam

Wengine tulisoma hii mada hapa chini

Mtaji: 10 Million TZS...

..all the best...........hii mada imenilipa na inaendelea kunilipa, ...kwa kifupi imenitoa!!........nawashukuru wote waliochangia mawazo........
 

Okay tunashukuru kwa kutufumbua macho
 
Mkuu,
Hebu ni PM au nitumie email kwenye samidaenterprises@yahoo.com nikupe picha kubwa sana ya biashara.
Mi ninavyoamini ni vizuri zaidi kupata ushauri wa watu ambao wanafanya biashara na wamefanikiwa katika kile wanachokifanya. Tambua asilimia kubwa ya watu wanamtazamo hasi kuliko wale wenye mtazamo chanya.
Mimi niko Mwanza ila kuna partners Dar, ntakuunganisha nao ili ufike ofisini wakupe picha kubwa ya biashara.
KARIBU...
 
Chukua hizo 30 mil ukafanye nazo biashara hizo Mil 50 ziwekeze upate 10% halafu unakamata mkwanja wako kila baada ya 3 months ambayo itakuwa 1,250,000 ambayo utaitumia ku inject kwenye business au utafungua uwekezaji mdogo mdogo tena.
 
lara 1 bring your advice here on your MKURABITA campaign
 
Last edited by a moderator:
Fanya biashara ya kuhifadhi mazao na kusafirisha ,1. Chukuwa milioni 60 nunuwa mahindi gunia 1000 kwa 30000/= kila gunia =30,000,000/= piya nunuwa gunia 1000 za alizeti kwa 30000/= kwa gunia =30,000,000/= unahifadhi kwa miezi sita hadi february or march unauza mahindi gunia @ 55,000 hjadi 60,000/= mara 1000 unapata 55,000,000/=hadi 60,000,000/= alizeti unakamuwa mafuta kila gunia linatoa wastani wa lita 20 ambazo utauza sh 60,000/= kwa lita 20 mara 1000=60,000,000/= kwenye alizeti uatapata faida ya mashuda ambayo utauzakwa sh 200 kwa kg moja unawezakupata kama 5milioni kwenye mashudu. Jumla ya kipato chako itakuwa 120milioni or 125m. 2. Chukuwa milioni 20 iliyobaki kwenye mtaji wako wa 80 milioni anza biashara ya kusafirisha mazao kwa milioni 20 unaweza leta tani 60 kwa weeki za mahindi ambazo kwa uchache kila tani 30 unaweza pata faida isiopunguwa laki saba hadi 1.5 milioni *2 ni kama 1.4 hadi 3milioni kwa weeki . Kama unahitaji msaada wowote ule kiushauri kuhusu hii biashara unaweza kunitafuta kwa no.0765616178. Kwa yoyote aliyetayari naweza kumpleka kwenye masoko na kumpatiya maelezo na msaada free bila malipo yoyote yale.
 
Last edited by a moderator:

Huu ni Ushauri Mzuri kabisa.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu tafuta shanba walau 50 acres unazoweza pata kwa around 5m chimba kisima kwa around 15m set irrigation system anza kufanya hortculture itakulipa tu

Good idea market yake inapatikana wapi na ni ya uhakika?
 
Kama unakiwanja jenga guest house utapiga hela kama muuza unga! Watu wanabanjuana na kila siku zinavyoendelea kasi ya kubanjuana inakuwa!

Sawa hiyo nimekubali sasa napata idea nzuri,shukran mkuu
 
Tafuta mtu ardhi na halmashauri nunua shamba lets say acre 20 gawa viwanja hata 60 weka title deed kwenye viwanja wape halmashauri Wauze watakata commission Yao si unaona tunavyokimbilia halmashauri zikitangaza viwanja

Kweli hiyo imetulia lakin nasikia kupata title ni issue na inachukua mda sana
 

Excellent idea>>
 
Nashukuru sana kwa mawazo yenu yote ni mazuri lakini ambayo yamenivutia sana na sasa hivi nataka niyafanyie kazi ni ya wilshere kuhusu kuhifadhi mazao ,saragossa kuhusu kujenga guest house and ben van mike kuhusu kununua shamba na kugawa viwanja nitafanya analysis kwa kina na kuja kuimplement mojawapo ambayo itakua best zaidi.
 
Kila la kheri mkuu Uje utupe feedback hata ukikwama humu ndani hutakosa watu wa kukushauri kuhusu title deed kusema kweli ni ishu na Mara nyingi ni urasimu tu wa serikali yetu lakini usife moyo
 
you dont need any new ideas pitia vizuri threads kibao kwenye jukwaa husika utapata unachotaka
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…