Nina mtaji wa laki moja. Je nifanye nini ili niwe napata angalau elfu mbili kwa siku?

☑️☑️☑️☑️☑️ Tunawazarau wale jamaa kuwaona vile Ila niliwahi kaa na jamaa mmoja nyumba ya kupanga kazi yake ndio hio anauza mishikaki ilala stand pale sokoni…mmoja 300 anaingiza faida 30k kwa siku na mwisho wake sa 7 mchana tu kashamaliza…
 
Ahahahahah hataweza ananaibu
 
dar es salaam ,kitunda(ilala v)
Gawa nusu huo mtaji, nusu nyengine weka backup yako, nenda Gongolamboto alfajiri kanunue utumbo kwa 3,500 kilo. Kitunda kilo 5,000.

Tafuta wamama wanaojielewa japo wawili waanzishie biashara ya supu ya utumbo, ukifanikiwa ongeza vijiwe, okota maokoto daily.
 
Uza mifuko, kama upo sehemu iliyochangamka kama sokoni kariakoo. Unanunua kwa jumla unazengeazengea wanunuaji unakata nyuma yao wakinunua bidhaa unawasogezea mifuko. Ya 300,500,1000.
Mkuu mtaji wake ukoje?
 
Reactions: apk
Mkuu mtaji wake ukoje?
Mim nlianza na 2000. Hiyo ni dazeni moja mifuko midogo size ya mwisho.Kwa bei ya kawaida ni kama 150 kila mfuko mmoja ,wewe unauza kwa 200 au mia tatu.unapata faida unaenda kununua ya aina tofauti na size tofauti,ya 300,500,1000,1500,2000 wewe tu kulingana na ubavu wako na soko ulivyoona linaenda.
Unanunua mifuko dazeni kwa jumla inategemea na ukubwa wa mifuko unakaa nyuma ya wateja ,wakianza kununua tu unasogea karibu unakuwa sharp maana mnajikuta mko watu 5 wote mnauza mifuko na mteja ni mmoja 🤣🤣🤣.
DAH MAISHA HAYA!🤣🤔
 
LAKI 1 ni mtaji mkubwa sana japo nimepitia comments zote na sijaona reply ya kumsaidia mtoa uzi.

Angekuwa Singida ningempa ramani. Anunue bundle la waya wa kuku (chicken wire mesh) ya size 1*6 au ¾ af nimwelekeze pa kwenda. Japo n ishu ya msimu lkn ingempa zaidi ya 10k kwa siku.
 
Tusaidie hata sisi Wengine tuko singida piA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…