Nina nia ya kuwa Rais wa Tanzania

Nina nia ya kuwa Rais wa Tanzania

Nina miaka 32, elimu bachelor of science economics population and development chuo mzumbe, kwenye uzi huu ntaelezea maono, mipango na sera niliyonayo juu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Watu wengi wananiuliza unawezaje kugombea na wakati una miaka 32 huku katiba ikitaka mtu awe na miaka 40, na wengine wanasema nina ndoto za alinacha, wengine una matatizo ya akili
Jibu ni kwamba hii movement ina-malengo ya mda mrefu nikimaanisha itachukua mda ili itimie sio jambo la leo au kesho na mimi sina uhusiano wowote na chama cha siasa

PROBLEM STATEMENT
Changamoto kubwa inayoikumba Tanzania na nchi nyingi za Afrika ni kama zifuatazo;-
i) Uwepo wa walipa kodi wachache sababu watu wengi wanajihusisha na informal sekta kwa hiyo wengi hawalipi income tax na kodi nyingine.

ii) Kwa sababu kuna walipakodi wachache imepelekea nchi nyingi kuongeza kodi kwenye vyanzo vilevile na hii imepelekea kuumiza wananchi wengi.

iii) Kiwango cha kodi kinachoongezeka hakiendani na ongezeko kubwa la watu na mahitaji yao hivyo kushindwa kwa serekali kupeleka huduma muhimu za kijamii.

iv) Kwa sababu wigo wa kodi ni mdogo imezilazimu nchi nyingi za africa ikiwemo Tanzania kukopa ili waweze ku-finance budget zao na kuleta changamoto nyingine ya ukuaji mkubwa wa madeni.


SULUHISHO
kujenga viwanda vingi


TANZANIA MODERN ECONOMY OUTLOOK
VISION

  • To become the largest economy in Africa in term of industrial output, gdp, and ppp
MISSION
  • To invest heavily on industrilization as a way of achieving economy supremacy

Kama kisemavyo kichwa cha habari nina nia ya kuwa Rais wa Tanzania, zifuatazo ni njia ntakazotumia kuongeza mapato kupitia viwanda na hatimaye kuondoa umaskini;-
i) Kuzalisha umeme wa megawatts 1,000,000 (gigawatts 1000)
Umeme wa uhakika na bei nafuu ni moja ya msingi muhimu sana wa viwanda, hizi zitachangia kushusha gharama za uzalishaji viwandani.

ii)Kwa miaka 10 serekali itajenga viwanda zaidi ya laki 1 ndio laki moja, na kila kimoja kitaajiri wafanyakazi kiwango cha chini wafanyakazi 500 (wa kiwandani na ofisini) na kuendelea
100,000*500= 50,000,000 (watu million hamsini)


Kutakua na zone saba nchi nzima ambazo zitakua ni kitovu cha viwanda ili kupeleka maendeleo kila mahali ni kama zifuatazo;-
a-Wilaya ya mpanda na uvinza viwanda zaidi ya 20,000
b-Wilaya ya muleba na karagwe viwanda zaidi ya 20,000
c-Wilaya ya kishapu na shinyanga vijijini viwanda zaidi ya 20,000
d-Wilaya ya itigi na manyoni viwanda zaidi ya 20,000
e-Wilaya ya ruangwa na lindi vijijini viwanda zaidi ya 20,000
f-Wilaya ya mwanga na moshi vijijini viwanda zaidi ya 20,000
g-Wilya ya kibaha, chalinze, bagamoyo na mkurunga viwanda zaidi ya 30,000
Kutakua na factories ambazo zinazalisha bidhaa from scratch na sio assembly na vitakuwa ni vya ku-export kwenye soko la dunia
Primary industries

  • Steel
  • Aluminium
  • Leather
  • Plastic
  • Glass
  • Copper cable
  • Battery
Secondary industries
  • Automobile
  • Chipset
  • Home appliances
  • Smartphones
  • Clothes and apparel
  • Aeroplane
  • Pharmaceutical

Minimum wages itakua sh 10,000 na kuendelea kwa mwezi

NINI KIFANYIKE ILI VIWANDA VIWEZE KUDUMU NA KUTEKA SOKO LA DUNIA
Ntaanzisha government agency itakayovipambania viwanda vilivyopo Tanzania ili viteke soko la dunia, na itakua inafanya kazi zifuatazo;-

  • Kutafuta vyanzo vipya vya umeme na kuhakikisha umeme unakua mwingi sana na wa bei nafuu
  • Kuhakikisha viwanda vinapata raw material hili jukumu hataachiwa mwenye kiwanda pekee yake
  • Kuhakikisha viwanda vinapata machine zinazotumika viwandani hili jukumu hataachiwa mwenye kiwanda pekee yake
  • Kuhakikisha viwanda vinapata skilled labour hili jukumu hataachiwa mwenye kiwanda pekee yake
  • Kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa Tanzania zinakua na bei ndogo kwenye soko la dunia ili ziuzike
  • Kuhakikisha bidhaa zinazozalishwa Tanzania zinakua na ubora ili ziuzike kwenye soko la dunia
FAIDA ZA VIWANDA LAKI MOJA KWA NCHI YA TANZANIA
a) Serekali itakuwa na uwezo wa kukusanya moja kwa moja usd billion 100 (Tsh trillion 250,000,000,000,000) kutoka kwenye viwanda tu; hapo sijaongelea sektor nyingine ambazo kupitia multiplier zitaguswa na viwanda indirect na zitaongeza pato la nchi

b) Viwanda Vitakuwa vinamilikiwa na familia tofauti tofauti za wazawa (watanzania), kwa gharama kubwa sana serekali itawapigania kwa nguvu zote wazawa kumiliki viwanda lengo ni uchumi kumilikiwa na wazawa na sio wageni

c) Viwanda vitaondoa sekta ambazo sio rasmi (informal sector)kama wamachinga, wauza mitumba bodaboda n.k sababu wataajiriwa kwenye hivyo viwanda zaidi ya laki 1
Njia ya kuwaondoa wamachinga, wauza mitumba, bodaboda, wapiga debe ni kujenga viwanda vingi ili waajiriwe na wawe na uhakika wa pension wanapofikia miaka 60 na zaidi
Sasa hivi watu wanaojihusisha na sekta ambayo sio rasmi hawana pension au akiba yeyote itakayowasaidia pale watakapokua wazee

d) Nchi ikiwa na viwanda zaidi ya laki 1 hizi squatters na slum zitaondoka tu automatical sababu kutakua na hela ya kuziondoa na watu watakua na kazi za uhakika na hii itaenda sambamba na kupanga kisasa nchi nzima kisasa na nyumba na majengo yatakua na mfumo unao-fanana ili miji yetu ipendeze sio kila mtu anajenga jenga namna anavyotaka

e) Kutakua na wigo mkubwa wa walipa kodi sababu watu wengi watakua wanajihusisha na kazi rasmi

f) Miradi yote mikubwa ya ujenzi itajengwa na kampuni za wazawa; najua hawana uzoefu ila serekali itawawezesha wawe na uzoefu kikubwa ni ela kubakia hapa hapa nchini

g) Gharama za kujenga nyumba zitakua chini sana serekali kushirikiana, na sekta binafsi watajenga nyumba na kuwauzia watu wa hali ya chini na kipato cha kati- kipato cha juu watajenga wenyewe



Karibu tuandike historia mpya ya Tanzania nchi itakayokua na uchumi mkubwa Afrika nzima
Nakuelewa kiasi nikupongeze kwa masomo yako ,kwa umri wako haipaswi kuwa na masomo tena bali uifanye iwe mipango iweke kwenye maandishi isomeke, anza maandalizi kuwa mwanachama wa chama cha siasa kumbuka viongozi wote wa kisiasa ni zao la vyama vya siasa. Hatahivyo napingana na wewe kwenye idadi ya wafanyakazi kwenye kiwanda kimoja idadi hiyo ni kubwa mno kwenye dunia ya sayansi na teknolojia, je umefikiria kuhusu AI? au nafasi ya Robot? ,mengine yote uko vizuri ila nazidi kusisitiza "maono waachie kanisani".
 
Nakuelewa kiasi nikupongeze kwa masomo yako ,kwa umri wako haipaswi kuwa na masomo tena bali uifanye iwe mipango iweke kwenye maandishi isomeke, anza maandalizi kuwa mwanachama wa chama cha siasa kumbuka viongozi wote wa kisiasa ni zao la vyama vya siasa. Hatahivyo napingana na wewe kwenye idadi ya wafanyakazi kwenye kiwanda kimoja idadi hiyo ni kubwa mno kwenye dunia ya sayansi na teknolojia, je umefikiria kuhusu AI? au nafasi ya Robot? ,mengine yote uko vizuri ila nazidi kusisitiza "maono waachie kanisani".
Hiyo idadi sio kubwa hata kidogo ni ya kawaida
Kuna factory zina wanafanyakazi elfu 1000 na zaidi

Na kwenye kiwanda kuna wafanyakazi wa kiwandani, wa ofisini, madereva, wafanyausafi, wapishi n.k
 
Nakuelewa kiasi nikupongeze kwa masomo yako ,kwa umri wako haipaswi kuwa na masomo tena bali uifanye iwe mipango iweke kwenye maandishi isomeke, anza maandalizi kuwa mwanachama wa chama cha siasa kumbuka viongozi wote wa kisiasa ni zao la vyama vya siasa. Hatahivyo napingana na wewe kwenye idadi ya wafanyakazi kwenye kiwanda kimoja idadi hiyo ni kubwa mno kwenye dunia ya sayansi na teknolojia, je umefikiria kuhusu AI? au nafasi ya Robot? ,mengine yote uko vizuri ila nazidi kusisitiza "maono waachie kanisani".
Kitu ambacho hujui ndani ya vyama vya siasa kuna udikteta huwezi kuwa huru kusema mawazo yako mfano ndani ya ccm hakuna anayethubutu kutangaza nia waziwazi sababu utaonekana unampinga Rais aliyepo

Kwa lugha nyingine mfumo wa vyama vya siasa unaua watu wengi sana wenye ndoto kubwa ndo maana wagombea binafsi wanatakiwa kurusiwa
 
Tanzania itakua na uwezo wa kuzalisha megawatts 1,000,000 (gigawatts 1000) za umeme ambao utatumika viwandani na hii itapelekea Tanzania kzalisha bidhaa nyingi za viwandani kwa bei nafuu
 
Huo umeme wa GW 1000 ndio umeme ambao US anazalisha sasa Kwa mwaka, Tanzania hatuna hata GW 2 kwenye gridi ya Taifa,Kwa nchi kama TZ siku ukisikia tuna GW 10 kwenye gridi ya Taifa ujue tumetoka kundi la third word countries, hauko serious wewe
Kama jambo kwako haliwezekani ni kwako kwangu mimi linawezekana
Nigeria ina GW 22+ na bado ni nchi maskini
 
Doh! Kuanza kuchukua hatua ni kukatishwa tamaa ?

Nadhani kuna tatizo sehemu hasa kwenye uelewa wako, Sasa ndugu unakatishwaje tamaa kirahisi namna hii utaweza kusimama kweli kuwa raisi ?
Kusema kuna watu wanajaribu kunikatisha umeme ndo ukweli wenyewe na haina maana kwamba ntakata tamaa wazo la kiwa Rais hakuna aliyenishauri bali ni uamuzi nilioamua pekee yangu na nina matumaini yatatimia
 
Hakuna mtu asieutamani U Rais, but changamoto ni namna ya kufika pale na kukikalia kile kiti safari ni ngumu na mitihani mingi

Ni Sawa na safari ya Wana Israel jangwani kuitafuta nchi ya ahadi
 
Hakuna mtu asieutamani U Rais, but changamoto ni namna ya kufika pale na kukikalia kile kiti safari ni ngumu na mitihani mingi

Ni Sawa na safari ya Wana Israel jangwani kuitafuta nchi ya ahadi
Mimi siutamani urais bali sipendi tu kuona umaskini uliotamalaki sehemu kubwa ya nchi na naona wanaoongoza wanakosa maono ya kututoa kwenye huu umaskini

Kunautofauti mkubwa sana kati anayetaka kutumikia wananchi na anayetamani uongozi
 
WAMACHINGA
Ni-ukweli usiopingika serekali inawachukulia wamachinga kama mzigo na wasiokua na faida sababu;-
  • hawalipi kodi ya moja kwa moja (direct tax)
  • hawamiliki mashine za EFD
  • hawana leseni za biashara
  • wanapanga biashara mbele za maduka ambayo wanalipa kodi
  • wengine wanapanga barabarani na wengine wanatumika na wafanyabiashara kukwepa kodi
  • Wengi sana ni vijana kwahiyo hii nguvu kazi serekali haifaidiki nayo
  • Hawaweki akiba ya uzeeni kupitia mifuko ya akiba na hatari kama hii itapelekea kua na taifa la wazee wengi maskini

Suluhisho sio kuwafukuza kwa kutumia nguvu bali kuwatafutia kazi za uhakika mbadala., Msimamo wangu kuhusu wamachinga ni kama ufuatao;-
  • wasihamishwe maeneo waliyopo kwa kupelekwa huku au kule au kwenye maeneo mapya wabaki maeneo yale yale waliyopo
  • wafuate taratibu zilizowekwa na uongozi wa wamachinga wa eneo husika, na wafuate sheria ndogo ndogo walizojitungia ili usiwe uwanja wa fujo
  • serekali itapambana kujenga viwanda ambavyo vitawaajiri wamachinga na kuwaondoa katika maeneo waliyopo sasa
 
Hongera kwa kuwa na maono hayo, ingawa ni maono madogo sana kwa nafasi ya Urais. Chukua ushauri wa wadau ili uanzia level za chini upate uzoefu. Rais ni taasisi sio mtu so uzoefu unahitajika sana kwani chanamoto wewe umeona moja tu, kiasi kidogo cha kodi na walipaji wachache wa kodi.
 
Mimi siutamani urais bali sipendi tu kuona umaskini uliotamalaki sehemu kubwa ya nchi na naona wanaoongoza wanakosa maono ya kututoa kwenye huu umaskini

Kunautofauti mkubwa sana kati anayetaka kutumikia wananchi na anayetamani uongozi
Kama hutamani urais, ana na vijana wachache wasaidie kwa ujuzi ulionao ili wajikwamue kiuchumi. Pia Famila, Ukoo, Kijiji/Mtaa, Kata, Tarafa n.k
 
Ila unandoto kama zangu,uwa kunaswali linaniumaga sana,kwanini raia wengi ni maskini sana? Yaani kwangu ni kipaumbele ni Barabara za Lami Kila Kata kuunganisha,kilimo kufungua masoko ya kilimo ndani na njee....marufuku kujenga nyumba ya tembe,nyasi wote bati la sivyo uende Burundi.Sitatoka madarakani mpaka miaaka 20 Ili kutekeleza miradi yangu kitaifa.
Unachekesha mkuu
 

Minimum wages itakua sh 2300 (0.90usd) kwa saa na kuendelea kwa wafanyakazi wa viwandani

 
Nina miaka 32, elimu bachelor of science economics population and development chuo mzumbe, kwenye uzi huu ntaelezea maono, mipango na sera niliyonayo juu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Watu wengi wananiuliza unawezaje kugombea na wakati una miaka 32 huku katiba ikitaka mtu awe na miaka 40, na wengine wanasema nina ndoto za alinacha, wengine una matatizo ya akili
Jibu ni kwamba hii movement ina-malengo ya mda mrefu nikimaanisha itachukua mda ili itimie sio jambo la leo au kesho na mimi sina uhusiano wowote na chama cha siasa

PROBLEM STATEMENT
Changamoto kubwa inayoikumba Tanzania na nchi nyingi za Afrika ni kama zifuatazo;-
kushindwa kwa serekali kupeleka huduma muhimu za kijamii.
Oyaa ukipata usinisahau nafiti wizara yeyote au hata ukinieka office ya rais fresh tuh
 
Kama jambo kwako haliwezekani ni kwako kwangu mimi linawezekana
Nigeria ina GW 22+ na bado ni nchi maskini
Hata GW 1 ya uhakika huna then unaongelea 1000 ambayo ni equivalent na capacity ya richest country in the world today, ndoto nzuri lakini be realistic kidogo, na Nigeria with 22GW ndio richest country in Africa, idea nzuri lakini sounds all talk
 
Hata GW 1 ya uhakika huna then unaongelea 1000 ambayo ni equivalent na capacity ya richest country in the world today, ndoto nzuri lakini be realistic kidogo, na Nigeria with 22GW ndio richest country in Africa, idea nzuri lakini sounds all talk
Kama kuna nchi ina GW 1000 kwanini sisi tushindwe
Mkuu usiyaogope sana maisha as long unachowaza hakijavunja sheria yeyote

Wazungu walichofanikiwa ni kuhakikisha wanatuwekea mipaka mingi sana kwenye fikra zetu mara hiki huwezi, kile huwezi., hapana sisi wafrika tunatakiwa tuwe na guts za kusema tunaweza
 
Back
Top Bottom