Nina nia ya kuwa Rais wa Tanzania

Nani umempa unaibu rais?
 
Asilimia 80 ya mafanikio kwenye biashara yanategemea mjasiriamali asilimia 20 iliyobaki ina nguvu hata kuziua biashara je hiyo asimilia 20 unaijua vizuri inaitwa, the entrepreneur and his her environments yaani mjasiriamali na yanayomzunguka

Hiyo asilimia 20 ndiyo imetufikisha hapa tulipo hivyo vyote ulivyo vitaja haviwezi kufanikiwa bila ufumbuzi wa hii asilimia 20
 
Asilimia 80 ya mafanikio kwenye biashara yanategemea mjasiriamali asilimia 20 ina nguvu hata kuziua biashara je hiyo asimilia 20 unijua vizuri inaitwa, the entrepreneur and his her environments yaani mjasiriamali na yanayomzunguka
Maendeleo ni art hayanaga formula ndo maana karibia kila nchi imefanikiw kinamna yake huwezi copy
Kuna Rais alicopy big result now lakin ilifeli kuna msururu wa sera nyingi mwafrika amecopy na zimefeli

Alichofanikiwa mtu mweupe ni kuhakikisha mwafrika hana huru wa kufikiri mfano una-gold kwanini usitengeneze smelting na refining ya gold nchi kwako ilihali unatumia mabilion kununua ndege

Maendeleo hayana cha asilimia 80 au 20
Utafanikiwa tu siku ukiwa na uhuru wa kufikiri na sio otherwise
 
Napima tu busara yako km kiongozi na rais lazima ukubali kuongelewa sasa km hiv umejaa ukiwa rais utafunga wangapi
Nikiwa Rais
  • Rais hatakua na mamlaka ya kuchagua majaji wa mahakama kuu
  • Rais hatakua na mamlaka ya kuchagua DPP
  • Rais hatakua na mamlaka ya kumchagua mkuu wa tume ya uchaguzi na msajili wa vyama vya siasa
 
Una ndoto kuwa Rais wa nchi 2025 na 2024 huna chama wala hujulikani popote.

Labda kwa kupindua serekali mkuu ila kwenye boksi la kura 2025 sidhani kwa kweli
Kwa huyu wala hawahitaji kwenda maporini kumchimbia dawa
 
I have given you the hints without details, am not closed minded.
Kwa taarifa yako changamoto husababishwa na binadamu kwa makusudi ama kwa kutokujua na mtu binafsi, (an individual), anaweza kujisababishia changamoto kwa uzembe uvivu ujinga, (Lack of knowledge),na kuto kujua,.
In reality though many in our society are short minded and numerous of them find business opportunities
 
KULINDA MIUNDOMBINU YA VIWANDA
Ni ukweli usipopingika Tanzania na nchi nyingi za kiafrika rushwa ni tatizo kubwa sana na ndo moja ya sababu kubwa sana kwa kuwa maskini mfano kuna nchi yenye mafuta mengi Afrika ila refinery zao zote za oil hazifanyi kazi mpaka anakuja mwekezaji binafsi anajenga refinery na bado wanataka tena kumfanyia fitna
Ntafanya mambo yafuatayo kama jitihada za kulinda msingi wa viwanda Tanzania
  • Kuwekeza haswa kwenye tafiti za kuongeza ubora na kupunguza gharama za uzalishaji bidhaa Tanzania
  • Rais kutokuchagua majaji wa mahakama kuu ili mahakama kuwa huru kumshughulikia yeyote yule atakayejaribu kukwamisha jitihada za viwanda na kuvunja sheria sahivi.
  • Dpp kuchaguliwa na wananchi na sio kuteuliwa na Rais hii itampa uhuru wa kufanya kazi zake bila kuingiliwa. Uchumi wa viwanda unahitaji umakini mkubwa sana., DCI, mkuu wa takukuru, kamishna wa kupambana na dawa za kulevya watakua chini ya ofisi ya DPP.
  • Msajili wa vyama vya siasa, mkuu wa tume ya uchaguzi kuchaguliwa na umoja wa vyama vya siasa na sio Rais hii itaepusha kuchaguliwa viongozi ambao wanauwezo mdogo na kuondoa hali ya tume ya uchaguzi kupendelea upande mmoja na hii itaepusha sana vurugu za uchaguzi
 
Kuwekeza kwenye vocational hasa tool engineering hii itasaidia kuzalisha bidhaa za bei ya chini na zenye ubora
 
Kosa kubwa sana kwa nchi za kiafrika ni kutokujenga na kumiliki miundombinu ya viwanda- ni hatari sana miundombinu ya viwanda kumilikiwa na wageni au waekezaji binafsi hawa ni rahisi sana kuihujumu.
 
haujawahi kuwashawishi watoto wenzio wakuchague ukiranja, hata haujawahi kuwa CR wa darasa haujawahi kuwa rais wa chuo, yaani umeshindwa kuwashawishi watoto wenzio wakuchague utaweza kuwashawishi watz 60m? acha bhange
 
haujawahi kuwashawishi watoto wenzio wakuchague ukiranja, hata haujawahi kuwa CR wa darasa haujawahi kuwa rais wa chuo, yaani umeshindwa kuwashawishi watoto wenzio wakuchague utaweza kuwashawishi watz 60m? acha bhange
Ahsante kwa kushiriki na kujikita kwenye personal attack na sio kwenye mada
 
Swala la viwanda afrika limekuwa ni kama slogan tu ya kisiasa wala hamna mikakati yeyote ile ya viwanda tunaamini tukitamka mara kwa mara viwanda basi vitaota kama uyoga
 
Kwenye viwanda kuna nafasi nyingi tu ambazo zinahitaji unskilled labour
Mwl Nyerere alikuwa na maono Kama ya kwako,palikuwa ZZK,UFI, GENERAL TYRE,NMC, NATIONAL PANASONIC, N.K,,,vyote hivyo vimekufa.

NINI KIMESABABISHA VIWANDA VYOTE HIVYO KUFA?
 
Mwl Nyerere alikuwa na maono Kama ya kwako,palikuwa ZZK,UFI, GENERAL TYRE,NMC, NATIONAL PANASONIC, N.K,,,vyote hivyo vimekufa.

NINI KIMESABABISHA VIWANDA VYOTE HIVYO KUFA?View attachment 3089990
  • Corruption and culture of impunity ambayo mpaka leo ipo
  • Hakukua na viwanda vya asili mfano vya kuchakata aluminium, copper, steel, na polymers
  • Serekali haikuwekeza kwenye tafiti za viwanda,
  • Bei ndogo za bidhaa kama zilizokuwa zinazalishwa kutoka abroad
  • Ushindani kutoka viwanda vya nchi nyingine watanzania hawajaandaliwa kushindana
  • Maono ya viwanda alikuwa nayo tu nyerere huku wasaidizi wake wakawa wanachukulia poa
Kwa kumalizia ukiona mradi wa mwendokasi unasua sua huku una monopoly ya route hio summary tosha kwanini viwanda vilikufa
 
Bandiko zuri. Tatizo sio nia yako, mfumo lazima ukuteme tu.

Kuna wazito wananufaika sana na hali ilivyo sasa, hawawezi ruhusu mtu mwenye maono kama wewe ushike madaraka.
 
Bandiko zuri. Tatizo sio nia yako, mfumo lazima ukuteme tu.

Kuna wazito wananufaika sana na hali ilivyo sasa, hawawezi ruhusu mtu mwenye maono kama wewe ushike madaraka.
Hakuna ajuaye kesho
 
Kwanza uwe mwanachama hai wa CCM, jitahidi ugawe chama sehemu mbili A na B, sehemu moja iwe upinzani. Ingia upinzani na utoe hoja zenye mashiko kama ulizotoa, uwe na damu inayofanana na JPM. Chukuwa nchi, pambana na yeyote yule mwenye ufisadi. Hakika utainyoosha nchi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…